TFF yapokea barua ya Malalamiko ya Yanga dhidi ya Feisal

TFF yapokea barua ya Malalamiko ya Yanga dhidi ya Feisal

Mkuu upande uliosimama wewe ndio upande unaotoa hoja za kishabiki na sio mpira

Club kubwa haiwezi kuendeshwa kihuni kama vile eti kwakua tu huwezi kubali kila kitu.

Kubisha ni mwanzo wa kuruhusu maarifa mapya lakini sio kila ubishi unatija

Nakupa mfano swala la mkataba wa GSM walioingia na TFF uliona namna Club ya Simba ilivyosimamia msimamo wake ambao ulikuwa supported na sheria mpaka TFF wenyewe wakagundua wamefanya makosa?

Niambie katika yale madai yenu ya kuilaumu TFF ni wapi mlikuwa na hoja zaidi ya malalamiko yasio na tija??
Mkuu, nakushangaa kwa haya unayoongea. Sipendi nirejee sakata la Morrison na ushahidi wa wazi jinsi TFF ilivyohusika kuhujumu mfumo wa usajili. SIPENDI KUBISHANA MRADI TUNAVUTIA KILA MTU UPANDE WAKE.

Jibu jepesi kwako ni hili, soka la Tanzania sote tunalijua. Ushawishi wa Simba na Yanga TFF sote tunajua. Hoja unayilalamikia wewe ni ya ufinyu wa uelewa. Yanga wameandika malalamiko yao rasmi kwa CHOMBO KINACHOHUSIKA KUSIKILIZA MALALAMIKO HAYO, wewe unapinga.

Swali kwako: ungetaka wapeleke wapi malalamiko hayo kama wanadhani mwajiriwa wao amekiuka mkataba wake?

Swali jingine: unafahamu kuwa ili kufika CAF na FIFA ni lazima shauri lako kwanza lisikilizwe na chama cha soka cha nchi husika ambaye ndiye msimamizi wa mikataba yote ya wachezaji wa nchi husika?
 
Hiyo TFF iliyomlinda Hersi na Manara kwenye ile kesi yao ya kuropoka siku ya Mwananchi, mpaka leo wako kimya hawajalitolea maamuzi lile suala...
 
Sasa nyinyi utopolo si Amna Imani na tff nendeni uko mkapate aki au shida ni mwiko uko nyuma
Mbumbumbu FC, tunaanzia kwanza TFF ili asipotenda haki tuende mbele. Kama hamuelewi jambo si mumuulize Rage awaelewesheni. Mnajidhalilisha kwa hoja zenu mandazi
 
Kama mnaheshimu utaratibu kwanini mlikuwa walalamishi kwenye swala la Kisinda kuenguliwa baada ya kukiuka utaratibu na baadaye mkaanza kusema TFF inachuki dhidi ya Yanga?

Kwanini ishu ya kufungiwa Manara ambayo ipo kiutaratibu hamkukubaliana nayo na kuitpia lawama TFF kuwa inachuki dhidi ya Yanga?

Leo hii kwenye ishu ya Feisal kwasababu wewe ndio inakusaidia, unaona TFF ni utaratibu?
Haya unayo yasema uliyatoa wapi? kiongozi gani alitamka haya,?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Yanaanza maneno maneno ka yale ya Morisson kipindi kilee

Tuwekeeni mkataba wake na timu tuusome --- mikataba mingi ni ya siri
Naomba nioneshe mkataba uliowazi kati ya mchezaji & club anayochezea hapa bongo..!
 
Nimesema jana hapa. Yanga wameumizwa sana na hili jambo, ni kama bado wamepigwa na butwaa. Hawajui hata hatma yao hasa katika mashindano ya Afrika itakuwaje bila huyu dogo kuwepo.

Cha msingi, waachane naye, waimarishe timu yao ya wanasheria na watoe mikataba stahiki kwa wachezaji wao. Yanga inaharibiwa na siasa na kujiweka karibu na wanasiasa, hili litaendelea kuwasumbua sana katika kujenga club ya kisasa.
[emoji23][emoji23][emoji2772]! Mashindano ya Africa unamtegemea Feisal? Acha masikhara mkuu.. Hapo viongozi wanaendeshwa kwa mihemko tu ya mashabiki ila Feisal hata akiondoka bado Yanga itabaki na ubora ule ule...! Feisal ni mashabiki / media tu ndio zinamjaza( Kuonekana mchezaji wa kiwango hicho) ila kiuhalisia ni mchezaji wa kawaida tu...
 
[emoji23][emoji23][emoji2772]! Mashindano ya Africa unamtegemea Feisal? Acha masikhara mkuu.. Hapo viongozi wanaendeshwa kwa mihemko tu ya mashabiki ila Feisal hata akiondoka bado Yanga itabaki na ubora ule ule...! Feisal ni mashabiki / media tu ndio zinamjaza( Kuonekana mchezaji wa kiwango hicho) ila kiuhalisia ni mchezaji wa kawaida tu...
Ni mchezaji wa kawaida ni kweli ila alikuwa na umuhimu wake mkubwa pale Yanga.
 
Ni jambo zuri kukaa meza moja ili haki ipatikane kwa pande zote mbili. Ingekuwa Yanga ndiyo imevunja mkataba kama alivyofanya huyo Feisal; naamini kelele zingekuwa ni nyingi sana.

Hivyo sioni sababu ya watu kulalamika, na wakati huo mkataba uliingiwa kati ya Yanga na Feisal! Sasa nongwa iko wapi kwa mwajiri kumshtaki mwajiriwa wake kama ameona kuna mambo hayakobsawa kwenye mkata waliongia?


Ingekuwa Feisal ndiyo kaishtaki Yanga kwa kukiuka vipengele vya mkataba wao, mngekuwa upande wa Yanga, au bado mngeegemea kwa Feisal?
 
Mkuu, nakushangaa kwa haya unayoongea. Sipendi nirejee sakata la Morrison na ushahidi wa wazi jinsi TFF ilivyohusika kuhujumu mfumo wa usajili. SIPENDI KUBISHANA MRADI TUNAVUTIA KILA MTU UPANDE WAKE.

Jibu jepesi kwako ni hili, soka la Tanzania sote tunalijua. Ushawishi wa Simba na Yanga TFF sote tunajua. Hoja unayilalamikia wewe ni ya ufinyu wa uelewa. Yanga wameandika malalamiko yao rasmi kwa CHOMBO KINACHOHUSIKA KUSIKILIZA MALALAMIKO HAYO, wewe unapinga.

Swali kwako: ungetaka wapeleke wapi malalamiko hayo kama wanadhani mwajiriwa wao amekiuka mkataba wake?

Swali jingine: unafahamu kuwa ili kufika CAF na FIFA ni lazima shauri lako kwanza lisikilizwe na chama cha soka cha nchi husika ambaye ndiye msimamizi wa mikataba yote ya wachezaji wa nchi husika?
Hilo la Morrison bora umechagua kuliacha maana humo mliumbuliwa sana na usiihukumu TFF kwa hilo maana hatua ya mwisho swala hilo limeamuliwa na CAS

Na CAS ni chombo huru kilicho jui ya TFF otherwise uijumuishe nayo kama ni idara inayoichukia Yanga pia.

Hilo la Morrison limeisha...

Sijakataa Yanga kuandika malamiko kwa TFF

Naomba uelewe hilo kwanza

Mimi nahoji tu kivipi chombo hiki ambacho uongozi wa Yanga uliweka mashaka na kusema hauna imani na TFF hii?

Usinipe majibu kuwa huo ni utaratibu, kwasababu kuna mambo mengi ya kiutaratibu ambayo yapo kisheria na TFF iliwataka myafanye lakini mmekuwa mkipingana nayo kwa kusema hamna imani na TFF

Na mifano ipo

Nafahamu kuwa ili ufike CAF au FIFA ni lazima uwe umepita TFF

Namimi nakuuliza swali hapo

Unaelewa kuwa swala la Morrison lilianzia TFF huko huko ambapo hamna imani napo na liliamuliwa kuwa Yanga ndio wenye makosa na mwisho mkalipeleka CAS ambapo majibu yalikuja vile vile?
 
Mbumbumbu FC, tunaanzia kwanza TFF ili asipotenda haki tuende mbele. Kama hamuelewi jambo si mumuulize Rage awaelewesheni. Mnajidhalilisha kwa hoja zenu mandazi
Kwenda si mnawakataaga wanatuhujumu muende sasa
 
TFF Kwa kushirikiana na utopolo ni kama wamepanga kumkomoa feitoto ndio maana wamepanga tarehe ya karibu huku wakijua feitoto yupo nje ya nchi lakini wajiandae kupata pigo takatifu kwanza hata yanga wakishinda feitoto ataenda cad huku akiomba kibali fifa Cha kutafuta timu ya kuchezea kulinda kiwango chale wakati shauri lake linasikilizwa so ajabu akaibukia Simba
 
Sasa mimi swali langu ni moja,je kama yanga atashinda kesi hii na feisal akatakiwa kurudi yanga JE ATACHEZA KWA MOYO MMOJA AU NDO ATAJIVUNJA KILA MECHI??.

Nadhani ni heri kumuacha mtu mzima akishaamua aende zake.

Huwezi kumlazimisha mtu mzima,akiamua lake ndo kashaamua hivyo.
 
Utopolo wakishindwa hii kesi watakimbilia kumroga kijana wa watu
 
Back
Top Bottom