TRA inazalisha mabilionea wengi kupitia wafanyakazi wake

Walipoleta mambo ya EFD yameleta rushwa kubwa sana kwenye hiyo taasisi maana wanawatishia wateja kwa faini kubwa mtu akitoa nusu anaachiwa hao jamaa wanazoa rushwa yaani makusanyo ya Wafanyakazi kwa rushwa kwa mkoa mmoja yanaweza yasitofautiane na mapato ya Mkoa wahuni wanazoa rushwa aisee na hawajaanza jana wala juzi na pia yule aliyenyooka na kulipa Kodi stahiki anachukiwa na kutengenezewa zengwe lolote...
 
Sio watu wote wezi wapo wasioiba kabisa ila % kubwa ni wezi ndio maana wanafunikwa na wachache wasio wezi..
 
Very true
 
Wamentandika Offense ya kukosa EFD machine Ofisini, Number inasoma 3m

Nimeenda TRA afisa ananiambia nipe 500k nifute mzigo wote...

or else nikutolee control number yako ukalipie.

Mimi ni nani niache kumpa 500k yake nipite zangu hiviiii...

Kwann wasiwe ma bilionea mtu anaingiza 500k na zaidi kwa siku kwa desk Job... to Hell T R A
 
mkuu mbongo ukimwajiri sehemu yoyote lazima atengeneze mazingira yakuiba tuu.
Niliwahi kufanya kazi na dada mmoja dukani Mbeya(Mwanjelwa) alikua aibi aisee alikua na hofu ya Mungu sana yaani mfanyakazi alilifanya Duka kama lake hasara hapendi kusikia alikuja kuolewa na Eng mmoja huko huko kusini...nimefanya kazi na vijana wengi nina uzoefu nao ndio maana huyo kabaki kama mfano..
 
Ukweli usemwe.... nina rafiki yangu tumehu
itimu wote chuo.. mm nilisomea faculty X yeye alisomea mambo ya Pesa.. mimi niliwah kupa job.. yeye kaka kama miaka mitatu tu mtaa.. sasa yaye ni mwaka w pili kazini saivi jamaa ana usafiri af anapost mashamba ya mpunga tu... mimi mwaka wa 6 huu kazin hata usafiri sifikirii
 
Aisee.....
Tanzania yetu....
Tanzania yetu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…