TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

Hili jambo naona watu wengi hawalifaham, mmiliki wa gari ya mizigo eg semi ni lazima awe na mashine ya EFD hii mashine hutumika kutoa risiti kwa wateja wake anaowabebea mizigo. Ikitokea unauza gari hata kama ni scrap lazima utoe risiti.
Kwa mizigo ya local huwa na VAT ndani yake. Kuhusu risiti madereva wenyewe wanafaham na wanaelekezwa kila siku wasipakie mizigo kiholela bila idhini ya ofisi.
 
Mkuu haya maelezo yako hapa Wewe unachanganya hisia na sheria.
Cha msingi Wewe ukinunua mzigo wako tafuta sehem kata risiti ya huo mzigo, maana usipofanya hivyo niamin utalia kwa yatakayokukuta. Na utajikuta unalipa hela nyingi kuliko ungekata risiti.
Pale utakaponunulia mzigo jitahidi uwaulize wapi naweza kukata risiti na watakuonesha
 
Sheria ya EFD iko wazi anayetakiwa kutoa receipt ni muuzaji, wajibu wa mnunuzi ni kuidai hiyo fiscal receipt toka kwa muuzaji.

Tuanzie hapo halafu lete hoja yako maana sijakusoma vizuri.
Kwahiyo ukikodi GARI nani anapaswa kutoa risiti mwenye gari au anayesafirisha mzigo? Ww ukipanda basi TIKETI unatoa ww au MWENYE BASI NDIO ANAKUPA RISITI?
 
Hapo muuzaji ni mmiliki wa gari/dereva ambae inatakiwa atoe risiti ya kusafirisha mzigo ampe mkulima
Sheria ya EFD iko wazi anayetakiwa kutoa receipt ni muuzaji, wajibu wa mnunuzi ni kuidai hiyo fiscal receipt toka kwa muuzaji.

Tuanzie hapo halafu lete hoja yako maana sijakusoma vizuri.
 
Elimu imetolewa sana na madereva wanajua hawatakiwi kupakia mzigo wowote ila wanaleta mazoea
Ni chanzo cha rushwa, sidhani kama kila mtu anachajiwa, asipofika bei yao wana mchaji, just common sensr, nenda kariakoo usikie madudu ya TRA walivyokwamisha biashara. Tukubali TZ bado tuna operate kwenye informal economy, ndiyo maana rais wetu mwenye IQ kubwa aliliona jinsi chinga na mama ntilie wanavyochukuliwa vitu vyao na migambo akaleta vitambulisho,
 
Kwahiyo ukikodi GARI nani anapaswa kutoa risiti mwenye gari au anayesafirisha mzigo? Ww ukipanda basi TIKETI unatoa ww au MWENYE BASI NDIO ANAKUPA RISITI?
Watu wengi humu wanaleta hisia sana badala ya kufata sheria. Wanamuonea Huruma kisa kabeba tenga 27 lakini wanasahau Dereva anajua ni Kosa kufanya hivyo.

Wacha walete hisia halafu siku moja wakutane nacho
 
Mimi naona kama kuna wachangiaji huenda kuna jambo hatujalielewa vizuri.

1. Kuna tofauti ya dereva ambaye kazi zake ni kubeba hayo mazao ya kilimo toka mashambani na,
Mfano madereva wa Canters na mafuso ya makabichi toka Lushoto, viazi toka mbeya nyanya toka Moshi au Iringa , matunda toka Mheza n.k

2. Kisha kuna madereva wa masafa marefu waendesha semi trailers ambao wengine huenda kuvuka boda na kwenda nchi jirani .
Hawa mara nyingi husafirisha bidhaa za viwandani nyingine toka ng’ambo (durable goods kwa kiasi fulani) sababu Safari yao huwachukua muda mrefu sometimes.

Sasa aina ya dereva anaeongelewa ni wa aina ya kundi la 2. Hapo juu.

Huyo mara nyingi anapita barabara kuu tu hata watendaji wa vijijini huko ndani hawajui.

Amekutana na wachuuzi wadogowadogo jioni wamemwangukia anunue nyanya zao akawahurumia akanunua, alipowadai risiti wakamwambia hatuijui unaongelea kitu gani huku wakimwangukia anunue bidhaa zao , hapo ungekuwa wewe ungefanyaje?
 
Mkuu ukifanya hivyo magari yatapukutika barabarani. Madereva hawahusiki kwa lolote linalohusiana na matengenezo/tozo au malipo mbalimbali ya gari bali yanamhusu Mmiliki wake.

Sasa unapowaruhusu madereva kupakia mizigo mbali mbali bila idhini ya mmiliki wa gari hilo litawapelekea baadhi ya madereva kuwa waongo. Mf kuna aina mbili za usafirishaji kwa magari ya mizigo
1. Transit Goods
2. Local Goods
Nizungumzie hiyo ya kwanza dereva anaweza kupakia mzigo toka Bandarini Dar kwenda Rwanda. Wakati wa kurudi atarudi tupu. Sasa basi dereva anaweza kupata mzigo kutoka mpakani kuja Njia Panda ya Nyakanazi lkn mzigo huo utamaliza taratibu za malipo baada ya siku mbili. Dereva anaweza kumdanganya mmiliki wa gari kuwa gari lile limepata hitilafu mpakani wakati wa kurudi kumbe ni uongo.
Dereva yule atapoteza siku kadhaa njiani kwakuwa ameshapata chochote bila kujali kuwa gari lile lilitakiwa lifike mapema na kufanyiwa service kisha kupakia mzigo mwingine wa kwenda DRC.

Hapa mmiliki atalazimika kukodi gari lingine la kubeba ule mzigo ili asipoteze tender yake ile. Sasa basi kwanini TRA wambane dereva anapopakia mzigo wa njiani?? TRA ndiyo wanaokuwa walinzi na wasimamizi wa gari lile linapokuwa mbali na mmiliki. Hivyo basi dereva mara apatapo mzigo wa njiani anapaswa kumtaarifu mmiliki kisha mmiliki akamtengenezea hati ya malipo kisha akamfowardia control no na dereva kufanya malipo halali ya Serikali.

Hapo wote wawili Dereva na Mmiliki watakuwa salama.

Kwa hizi Local Goods ni rahisi kuzi monitor kwani hayana tofauti na mabasi. Kuna mawakala sehemu mbali mbali ndani ya Nchi kulingana na routes zako.
 
Mkuu ndo mana nilisema Wewe unachanganya hisia na sheria . Chunga sana Hili jambo litakukost siku moja
Sasa TRA wakikumata huna risiti utawaambia niliwaonea Huruma wale wa kulima?????? Seriously Kabisa??????? Mkuu step up achana na hisia.
 
Hapa tunazungumzia sheria inavotaka, rushwa hyo ni kesi nyingine sasa. Mmiliki wa gari ametoa gar kwenda lubumbashi na irudi empty, dereva anaanza kupakia nyanya na viazi uyole hii si sawa
 
Mzee hata bidhaa ya buku1 kama hujatoa risit unaadhibiwa alieiba simu na nguo wote si wezi tu?? Sheria haiangalii hvo[emoji28][emoji28]


Hiyo ni kwa ambaye tayari ana vigezo vya kuwa na mashine ya EFD na tayari anayo.

Kumbuka sheria ya EFD inahusu wale wenye mauzo ya kuanzia milioni 10-14 unless uniambia sheria imebadilishwa kwamba kila muuzaji wa thamani yoyote kwa Mwaka hata 1000,000 anatakiwa kuwa na EFD mashine.

Tuwe makini ktk kujadili ili tusipotoshe watu.
 
Hapa sisi hatumuongelei mkulima anayekuuzia tenga mia za nyanya ndo akupe risiti , no Sio jukumu lake hilo
Wewe unaponunua hizo tenga 100 za nyanya kuna watendaji huko vijijini ndo wanakuktaia risiti ya EFD au kuna mageti huko ya kukata risiti.

Kwa hiyo elewa Sio mkulima anayekuuzia tenga mia ndo anatakiwa akupe risiti.
 
Mkuu ndo mana nilisema Wewe unachanganya hisia na sheria . Chunga sana Hili jambo litakukost siku moja
Sasa TRA wakikumata huna risiti utawaambia niliwaonea Huruma wale wa kulima?????? Seriously Kabisa??????? Mkuu step up achana na hisia.


Hapana haitatokea kamwe!

Kwanza nikwambie sheria huwa haiamui moja kwa moja , hakimu au mwamuzi huwa anangalia pia facts around the case!

Dereva ametoka masafa marefu amepigika halali mchana wala usiku, milima na mabonde ni yake, huku kaacha nyumbani hakuna hela wala chakula, Boss wake kamwambia hela nitakumia au utakuta utakaporudi, ikitokea ana akiba amekuta nyanya njiani au mkaa amepakia mnamwambia awape EFD receipt?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…