Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Ngoja nimtafute kijana type ya Muro na nimpe camera afanye kazi kwa traffic wa Rufiji mliomkamata mchepuko wangu na kumtongoza.
 
Kwanza askari huwa hawschukuliwi hatua za kisheria bali wanachukuliwa hatua za kijeshii, ambazo ni siri.
 
Rushwa inaanzia juu huko kwa vigogo

Ova
Mrangi kweli Dula ni Abdala lakini anayekula mihela mpaka wajawazito wakajifungua chini au wengine wakafa kwa kukosa mia tano ya paracetamol na hawa wazee wa buku buku, wapewe onyo kali basi kuwafukuzisha ni mbaya sana tuanze na mapapaa wakinyooshwa hawa vidagaa watakwisha mfano umeona
Kisa cha wale KURUNA Congo?
 
Ukweli ukisemwa Rushwa ni mfumo rasmi nchini mwetu. Tunakwenda kupata huduma huku tunajipanga kutoa rushwa. Hata kama huduma ni haki yetu.
 
Sasa wanajuaje kilichopokelewa kama ni fedha
 
Askari wengi wapenda rushwa wakikutana na mtu ambae hutaki kutoa rushwa basi ata kutreat kama muhaini kwanza anakusimamisha kwamba umepita na taa nyekundu na kukwambia anakuandikia faini kwa kosa hilo

Akiona umemwambia sawa niandikie atabadilika na kukwambia ngoja nikukague na nikikukuta na makosa hata matatu nakuandikia yote na kosa unalokuwa umefanya ni kukubali hyo faini moja linazaa yote hayo yani mateso hawa jamaa na wao wakitolewa chambo hvyo basi wawe wanajifunza sio wote tunapenda kutoatoa hzo rushwa
 
Kawaida hujenga mazoea kama hapo kwenye video clip....
Rushwa ianzie kudhibitiwa kuanzia chini hadi juu
 
Hakuna udhibitisho walicho kuwa wanapokea ni fedha au ni karatasi.
tusihqngaike na vidagaa....tunapaswa kukodelea macho RUSHWA zinazo liangamiza taifa sio buku ya maji.
Ahaaaa Eti karatasi. Za nini mkuu? Huko kwingine wanawezi shindwa kesi hiyo, lakini kijeshi ndo basi tena. Kazi imeishia hapo.
 
Mengine ni aibu sawa tu na kufumaniwa
Hawa wakipelekwa mahakamani watachomoa mkuu. Nani ana ushahidi kuwa hicho walichopewa ni pesa na kwamba wamepewa kama RUSHWA? Watapoteza muda bure kuwapeleka mahakamani.
 
Lakini si wanamgawia na yeye?
 

Kosa lao ni kupokea rushwa hadharani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…