True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

...47
Nilitazama ile njia ya kwenda kisimani, nilishtuka kumwona paka mkubwa mweusi akinikata jicho baya mno.
Sijawahi ona paka kubwa kama hili, niliwaza huku nikiyakwepa macho yake mabaya kama ya bundi, ama ndo huyu anaekamata kuku? nilipo mtupia tena macho sikuamini, yule paka hakuwepo na badala yake bonge la bundi alikua pale ananitizama!
Nilishindwa kuvumilia, nilitimua mbio ndani kwangu nikafunga mlango na kukaa kitandani, jamani yaani uchawi njenje? Hapana bwana mie kesho lazima nirudi nyumbani, niliwaza huku hofu ikiwa imenikumba.
Muda kidogo majira ya kama saa 8 mchana alikuja yunge mkubwa akiwa na kisufuria kidogo alichokuwa amekijaza viazi vitamu na maziwa mgando!
Mbona umejifungia jua kali hivi? Aliuliza yunge.
Hiki kijiji chenu mie sikiwezi, naona kesho niende nyumbani tu, huku kutishana mie sipendi kabisa, nilimwambia.
Yunge: Nani kakutisha mchumba?
Nilimsimulia kila kitu, vituko vya bibi na babu mpaka kile cha paka na bundi.
Yunge: mhh! Kabla hujamwona bundi, hukushirikiana kitu na yunge mdogo?
 
...13
Basi tuliingia ndani ya slopu ile, nikaingia chumbani huku babu akiningoja pale sebleni, nilichukua elfu 60 ndani ya begi na kurudi nayo sebleni ambapo nilimkuta babu amengoja kwa hamu, nilimkabidhi akafurahi sana,
Kubyala kwa wiza (kuzaa kuzuri sana) alisema babu huku azificha fedha zili ndani ya puzo (bukta kubwa) alokuwa amevaa kwa ndani,
Usimwambie bibi yako kama umenipa mzigo, sawa mzee mwenzangu?
Alitahadhalisha babu, nikamwambia wala asijali, kwani bibi yeye nmempa masukari na maunga ya ngano kutoka kwa mama mkwe wake (mama yangu) hivyo simwambii chochote bibi,
Sawa pumzika kijana wangu, kesho ntakusimulia ntakayoyasikia huko kwenye tukio, alisema babu, kisha akaondoka,
Nilitoka nje kumuaga bibi kwamba nataka nipumzike, kwani nilitaka pia kuhakikisha kama babu ameondoka ili bibi naye nimpe mzgo wake,
Kweli babu alikua ameelekea senta kwenye tukio la fisi kuiba mtoto mapema tu,
Nilirudi ndani ya slop na kuchukua 50 elfu nikamkabidhi bibi na kumwambia, 30 imetoka kwa baba na 20 kwa mama.
Antonnia Tayukwa njooni
 
Tuendelee
Saa 11 nafika kijijini pale tunaona watu wamejazana uwanjani, nikajua pale kuna boli linatembea, nikawaza, hapa ndo penyewe sasa, basi tukiwa pale senta, (tupaite isonda sio jina rasmi) tukamwona binti kabeba ndoo ya maji, tulimsalimia kisha tukamwuliza kwa mzee bhuhabi ni wapi? Yule binti akastuka, akanitazama kisha akauliza ahabhalogi gete? (kwa wale wachawi?) sikujibu, tukatazamana na wale wakimbiza daladala, walikuwa wawili, mmoja alibeba mizigo, mwingine alinibeba mimi! Basi yule binti alituelekeza kisha tukashika njia kuelekea kwa babu, tulifika pale ikiwa saa 12 kasoro dkika 6. Tulipokelewa na bibi ambae alionekana kuchangamka sana, huku nikiwa na aibu na hofu iliyotokana na kuambiwa ninapokwenda ni wachawi wa kupindukia, nilitamani wale daladala waondoke mapema ili kukwepa aibu ile, kwani kila tukikutanisha macho tu, nilihisi wananiogopa hata mimi, duh! Nakweli licha ya bibi kuwasihi wale waendesha daladala wasubiri apike haraka msosi waligoma na kuaga wakaondoka....!
Hii ni chai,saa moja jioni kuku hajarufi bandani,saa moja jioni anaenda mashineni kusaga,mwezi december saa moja ni giza sana huko
 
WAJUAJI WAKIJA WATAKUULUZA

Mpaka sasa huyu bwana hajafikisha masaa 24 hapo ugenini kwa Babu yake kifupi alifika saa 12 na mpaka Sasa n saa nane mchana lakini sasa

👉Ameshajua kuku huwa wanakaa WAP mchana?
👉Kaonana na msichana jion nayeye akiwa mgen lakin usiku alimfungulia geto?
👉Saa 11 asubuh unasindika mtu ambae hujui kwao n wap na vp heshima yako kwenye mji husika ipoje?
👉Inakuaje we n mgen tena mjukuu ulipewa jina lababu alafu wote wanakuacha walijua we n mgen bila hata chakula Cha mchana?
👉Hukuwah kulala na msichana Ila mpaka sasa umeshalala nae na bado una shauku ya kupata mwingine.(mkojo wa kwanza kutoka kwa Mara ya kwanza huwa unakuchukua akili kwa aliyekukojolesha)
👉Unapata ujasiri gani kutoa nguo zako na shuka la Bibi yako liende kwenye mji usioufahamu ili Hali ulishataadhirishwa na Mambo ya ushirikina?
👉Muda n mchache Mambo n mengi.



Jamani achen mihemko hapa tupite Kama kuburudika na kuongeza kitu kichwan tusiwe serious Sana.
 
Back
Top Bottom