True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

SEHEMU YA 6:


Pili, haikuwa busara tofauti zetu wawili zimuathiri mtoto, kutengana kwetu ilitosha kabisa kuwa adhabu kwa mtoto tusimuongezee mengine tusingekuwa tunamtendea haki kabisa.



NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI
mtoto ambaye hakuwa wako.

Kuna mzee aliwahi kuniambia kuwa watu "wastaarabu na wapole ndio wanaongoza kulea shahawa zisizo zao".
 
Ni kweli mzee tatizo lilikuwepo nafikiri ndio lilinitibia tatizo unalozungumzia

"A man is monogamous by societal but Polygamous by Nature"

Utakuja kuwa huru kutoka kwenye vifungo vyako siku utakapo gundua kuwa unaisaliti asili ya jinsia yako.
 
"A man is monogamous by societal but Polygamous by Nature"

Utakuja kuwa huru kutoka kwenye vifungo vyako siku utakapo gundua kuwa unaisaliti asili ya jinsia yako.
Lilishaisha likaibua shida nyingine

Yaani ujinga wa mwanamke mmoja unasababisha wengine waishi na mimi kwa tabu sana

Kuna wanawake hapa watashadadia aliyofanya mwenzao hawajui pengine wanawachukia wanaume kwa ushenzi waliofanyiwa bila kujua sababu inaweza kuwa wanawake wenzao

Ogopa kuangukia kwa mwanaume mwenye historia zake huko atokako
 
mtoto ambaye hakuwa wako.

Kuna mzee aliwahi kuniambia kuwa watu "wastaarabu na wapole ndio wanaongoza kulea shahawa zisizo zao".
Sina upole wa namna hiyo
Mashaka juu ya mtoto sio wangu nilishakuwa nayo kitambo, lakini kutumia jina langu inanimilikisha moja kwa moja

Mimi naamini watoto ni baraka, hata ukipata mwanamke huko ametelekezewa mdirect kwangu nitamlea lakini asije kutokea mtu akasema ni mwanae baadae nitajifunzia uchawi kwake
 
mtoto ambaye hakuwa wako.

Kuna mzee aliwahi kuniambia kuwa watu "wastaarabu na wapole ndio wanaongoza kulea shahawa zisizo zao".
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji119][emoji119][emoji119]
 
Sina upole wa namna hiyo
Mashaka juu ya mtoto sio wangu nilishakuwa nayo kitambo, lakini kutumia jina langu inanimilikisha moja kwa moja

Mimi naamini watoto ni baraka, hata ukipata mwanamke huko ametelekezewa mdirect kwangu nitamlea lakini asije kutokea mtu akasema ni mwanae baadae nitajifunzia uchawi kwake
Mkuu tuendelee comment utajibu baadae
 
Ukiona red flags mapema jitahidi kuuzuia moyo wako kuendelea kupokea shida, Fanya kukimbia tena kaa mbali sana na aina hiyo ya mtu.

Wala hakuna sababu ya kujiweka karibu naye ikiwa hata mtoto siyo wako kibaiologia.

Epuka kuwa kimbilio la Waasherati

Kasome Methali 5


image_2021-02-12_043313.png
 
akini kutumia jina langu inanimilikisha moja kwa moja

Kitu ninachotaka nikushauri ewe mwanaume mwenzangu ni kuwa "Women are the Maters when it comes to Manipulation"

Alikfanikiwa kukushika akili kwa kutumia jina lako kwenye jina la mtoto asiye wako, hata amekufanya usahau kuwa DNA haitoweza kusaidia kujua ukweli.
 
Mimi naamini watoto ni baraka, hata ukipata mwanamke huko ametelekezewa mdirect kwangu nitamlea lakini asije kutokea mtu akasema ni mwanae baadae nitajifunzia uchawi kwake
Sina uhakika na unacho kimaanisha hapa.

Utayari wako wa kulea mbegu za wanaume wenzako unaonyesha ni jinsi gani unahitaji msaada wa kuhakikisha unarudi kwenye lengo la kuzaliwa kwako kwenye familia yenu ambalo kimsingi ni kuendeleza uzao wa ukoo wa Mfukuza Ndoto,

Na sasa umeamua kujikita kenye kukuza na kuendeleza mbegu za uzao wa koo nyingine, tena unafanya hivyo kwa kujivunia zaidi.
 
SEHEMU YA 7:


Talaka ikatolewa baada ya siku 45, maisha yakaendelea na mwanamke huyu mwingine, nikahisi kuutua mzigo maana wakati alipokuwa ananibembeleza turudiane nikigoma anasema yeye ndo mke hata nifanyeje, ananitumia na picha ya cheti cha ndoa
Ikawa inaniudhi sana, kwamba mtu hakutaki lakini anataka tu kukukwamisha hasa kwa wivu tu kwa mwanamke mwenzie, hili la kunikwamisha kweli lilikuwa linaniwazisha mimi umri unaenda nahitaji kupikiwa kufuliwa na kuitwa baba lakini kuna mtu tu yuko somewhere ameamua kushikilia maisha yako
Nilikuwa naogopa sana kama nitashinda kesi yangu ya madai ya talaka ningefangaje na yeye najua hanitaki anataka kukwamisha tu na akishajua sasa sina cha kufanya tena ndio angeninyoosha vilivyo.

Lakini kwa kufaulu kwangu kumshinda mahakamani na talaka kutolewa sasa nikajiona maisha yanasogea kwa ahueni ya hali ya juu
Hapa ikaibuka changamoto nyingine, yule mwanamke niliyempata akawa ana-miss fire mara kwa mara, nina hamu na mtoto na kila akidaka ngoma inatokea kusikojulikana
Hapa ilifuata stori ambayo haina umuhimu sana katika mjadala huu lakini kwa ufupi ndio nikajua yoote ya tangu kabla na mpaka nilipoletewa zawadi nikazikataa, yote yalielezewa lakini sikuyatilia maanani kwa kuwa sikwenda huko physically nilisimuliwa tu.

Hapa sasa nikiwa na akili zangu timamu nikaanza kuishi nae kwa tahadhari sana, kuna wakati akanitumia akaunti ya benki anasema ni kwa ajili ya mtoto nikipata chochote niwe natuma huko, yaani amekaa amepanga mwenyewe akaamua kufanya hivyo bila kujadili na mimi, bila kujua kama kuna akaunti nyingine au vipi
Nilimjibu kwa ufupi tu "Watoto hawalelewi hivyo" hakujibu chochote tena
Nilishapigwa pesa ya kulea mimba sikuwa tayari kupigwa mara nyingine.
Tangu hapo kuna baadhi ya matukio alihitaji nichangie chochote basi hata kama ni elfu kumi tu aliipata kwa mbinde mno, sikumuamini tena.

Nataka hii stori imalizike haraka...
Niseme tu mimi ni muoga sana wa kutelekeza mtoto, hili sikutaka kabisa lije linitokee, so mpaka hapo bado nafsi yangu haikuridhika kwamba yule sio mwanangu, kuna wakati nikikaa akili inaniambia ni mwanangu.
Kikapita kitambo kidogo sina mawasiliano nao, nae kama kawaida akanyamaza tu.
Kimyaa, zaidi ya mwaka.

Kwahiyo mwaka 2019 mwishoni nikiwa humu nikapitia uzi wa mzee Iringa Native
Niliusoma kwa makini sana, ukanigusa, nikajihisi yanakwenda kunikuta hayo, ni uzi uliokuja kupigilia msumari ile dhana yangu ya kutokuwa na rekodi ya kukataa mtoto

Watu wanaweza kufikiri kwanini pamoja na yote hayo bado kuna wakati niliamini mtoto ni wangu, kuna vitu vingi pengine kwa kuruka makusudi au kwa kuvisahau viliendelea ambavyo vilikuwa vinanirudisha kwenye mstari sometimes.

Kuna wakati nikawa nahisi huenda ni kichaa cha mwanamke tu wacha nijishushe kwa faida ya mtoto mfano tukiwa poa namuuliza hivi mambo unayofanya mbona ni kama mimi sio baba wa huyo mtoto? Anajibu kama humtaki sema na akikua nitamwambia ulimkataa, acha kufikiria vitu usivyo na uhakika navyo?[emoji2307][emoji2307] Katika mazingira haya narudi tena kujaribu kuwa karibu na mtoto.

Kwahiyo uzi wa Iringa Native ukaamsha ari mpya maana nilikaa kimya kitambo sana ukizingatia tayari nilikuwa na mtoto ambaye ukimtazama huulizi, hata ukimuacha mtaani japo ni mdogo sana lakini watamleta kwangu... Sikuwa na munkari tena na watoto wenye mashaka mashaka ..
Nikapanga kumtafuta tena..

NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI
 
SEHEMU YA 7:


Talaka ikatolewa baada ya siku 45, maisha yakaendelea na mwanamke huyu mwingine, nikahisi kuutua mzigo maana wakati alipokuwa ananibembeleza turudiane nikigoma anasema yeye ndo mke hata nifanyeje, ananitumia na picha ya cheti cha ndoa
Ikawa inaniudhi sana, kwamba mtu hakutaki lakini anataka tu kukukwamisha hasa kwa wivu tu kwa mwanamke mwenzie, hili la kunikwamisha kweli lilikuwa linaniwazisha mimi umri unaenda nahitaji kupikiwa kufuliwa na kuitwa baba lakini kuna mtu tu yuko somewhere ameamua kushikilia maisha yako
Nilikuwa naogopa sana kama nitashinda kesi yangu ya madai ya talaka ningefangaje na yeye najua hanitaki anataka kukwamisha tu na akishajua sasa sina cha kufanya tena ndio angeninyoosha vilivyo.

Lakini kwa kufaulu kwangu kumshinda mahakamani na talaka kutolewa sasa nikajiona maisha yanasogea kwa ahueni ya hali ya juu
Hapa ikaibuka changamoto nyingine, yule mwanamke niliyempata akawa ana-miss fire mara kwa mara, nina hamu na mtoto na kila akidaka ngoma inatokea kusikojulikana
Hapa ilifuata stori ambayo haina umuhimu sana katika mjadala huu lakini kwa ufupi ndio nikajua yoote ya tangu kabla na mpaka nilipoletewa zawadi nikazikataa, yote yalielezewa lakini sikuyatilia maanani kwa kuwa sikwenda huko physically nilisimuliwa tu.

Hapa sasa nikiwa na akili zangu timamu nikaanza kuishi nae kwa tahadhari sana, kuna wakati akanitumia akaunti ya benki anasema ni kwa ajili ya mtoto nikipata chochote niwe natuma huko, yaani amekaa amepanga mwenyewe akaamua kufanya hivyo bila kujadili na mimi, bila kujua kama kuna akaunti nyingine au vipi
Nilimjibu kwa ufupi tu "Watoto hawalelewi hivyo" hakujibu chochote tena
Nilishapigwa pesa ya kulea mimba sikuwa tayari kupigwa mara nyingine.
Tangu hapo kuna baadhi ya matukio alihitaji nichangie chochote basi hata kama ni elfu kumi tu aliipata kwa mbinde mno, sikumuamini tena.

Nataka hii stori imalizike haraka...
Niseme tu mimi ni muoga sana wa kutelekeza mtoto, hili sikutaka kabisa lije linitokee, so mpaka hapo bado nafsi yangu haikuridhika kwamba yule sio mwanangu, kuna wakati nikikaa akili inaniambia ni mwanangu.
Kikapita kitambo kidogo sina mawasiliano nao, nae kama kawaida akanyamaza tu.
Kimyaa, zaidi ya mwaka.

Kwahiyo mwaka 2019 mwishoni nikiwa humu nikapitia uzi wa mzee Iringa Native
Niliusoma kwa makini sana, ukanigusa, nikajihisi yanakwenda kunikuta hayo, ni uzi uliokuja kupigilia msumari ile dhana yangu ya kutokuwa na rekodi ya kukataa mtoto

Watu wanaweza kufikiri kwanini pamoja na yote hayo bado kuna wakati niliamini mtoto ni wangu, kuna vitu vingi pengine kwa kuruka makusudi au kwa kuvisahau viliendelea ambavyo vilikuwa vinanirudisha kwenye mstari sometimes.

Kuna wakati nikawa nahisi huenda ni kichaa cha mwanamke tu wacha nijishushe kwa faida ya mtoto mfano tukiwa poa namuuliza hivi mambo unayofanya mbona ni kama mimi sio baba wa huyo mtoto? Anajibu kama humtaki sema na akikua nitamwambia ulimkataa, acha kufikiria vitu usivyo na uhakika navyo?[emoji2307][emoji2307] Katika mazingira haya narudi tena kujaribu kuwa karibu na mtoto.

Kwahiyo uzi wa Iringa Native ukaamsha ari mpya maana nilikaa kimya kitambo sana ukizingatia tayari nilikuwa na mtoto ambaye ukimtazama huulizi, hata ukimuacha mtaani japo ni mdogo sana lakini watamleta kwangu... Sikuwa na munkari tena na watoto wenye mashaka mashaka ..
Nikapanga kumtafuta tena..

NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI
Duh!! Mambo yanazidi kupamba moto!! Nafwatilia kwa ukaribu kabisa...
 
  • Thanks
Reactions: T11
SEHEMU YA 6:

Wakati tukiendelea kuweka kumbukumbu lazima kuna kitu mfuatiliaji aki-note, kwamba huyu bidada yeye hanaga shida na mimi wakati wote, nikikaa kimya nae anakaa kimya jambo ambalo sio rahisi kwa wazazi, kuna mambo hupelekea kuwasiliana, ukizingatia mtoto anaishi naye yeye kwahiyo kuna kuumwa, kuna mipango mbalimbali juu ya mtoto na kuna kumuunganisha mtoto na baba, kwa maana kwamba labda kupiga simu niongee na mtoto au asikie sauti yangu
Au nikipiga basi ampasie niongee nae, hayo yametokea mara chache san. Hakukuwa na sababu ya kunitenganisha na mtoto ikiwa sijawahi kuwa na ugomvi nae juu yake, hata yeye mwanamke hakuna ugomvi hasa tumewahi kuingia kiasi cha kupelekea umbali wa mtoto na mimi.
Kwahiyo naweza kususa nikakaa hata miaka nae akatulia tu, ni mara moja tu amewahi kunianza, wakati alipotaka turudiane.

Basi bwana tuendelee na soga letu lilipoishia, siku aliyoomba msamaha akaondoka akijua yameisha, nakumbuka nilimpa tu kihela fulani kidogo kumsaidia nauli maana alikuja kwa kushtukiza na sikuwa na kitu, nacho nilimpa tu sababu ya mtoto sio sababu yake, najua alijiandaa na safari. Siku zote pamoja na kuona kuna vitu haviko sawa sikupunguza love kwa mtoto.
Alipoondoka akafika mkoani kwake ananitumia vimeseji sijui mbona sijamtakia safari njema au mbona sijampigia kuuliza kama amefika, mi nikala bati tu
Hayakuwa mambo ya kuisha kirahisi namna hiyo na mimi nilishaingia kwenye mahusiano mapya, as i said before nikishakuwa na mtu tayari basi ni huyo huyo huwa siyumbi wala kurudi nyuma
Mungu fundi bwana, mwanamke niliyekuwa nae kwenye mahusiano wakafahamiana, kuna mazingira yalipelekea wakafahamiana akili yangu ikanituma huyu ananirudia ili aharibu tu mahusiano ya sasa kimsingi hanipendi nikimrudia nitafurahi na show.
Nikabaki na msimamo wangu.

Akaendelea kuwa karibu akaona sielekei kibra akaamua kupotezea kama kawaida yake.
Lakini hiyo hali bado ikawa hainifurahishi mimi,
Kwanza katika maisha yangu niwe hai au nimekufa sikupenda kuwa na rekodi ya kukataa mtoto, maana huku mtaani watu wasioelewa nilisikia chini chini wakidhani nimemkataa mtoto,
Pili, haikuwa busara tofauti zetu wawili zimuathiri mtoto, kutengana kwetu ilitosha kabisa kuwa adhabu kwa mtoto tusimuongezee mengine tusingekuwa tunamtendea haki kabisa.
Yaani awe wangu asiwe wangu sikutaka aishi kwa upweke wa kutomjua baba ni bora hata ningekuwepo kivuli ili hata akijua ukubwani haitamuathiri kisaikolojia atakuwa ameshapita stage muhimu zilizohitaji masikio yake kusikia Baba/Mama.
Kitu tu pekee sikuwa nafanya kwa ajili yacho ni kwamba eti nikimkataa kuna siku atakuwa mtu gani sijui atashindwa kunisaidia. Mimi imani yangu ni kwamba mzazi anatakiwa kumsaidia mtoto sio mtoto amsaidie mzazi kwahiyo hata awe rais na asinisaidie hayo ni juu yake, sipangi kuwa fukara.
Ni umasikini ndio unafanya watua waogope eti ukimkataa utakuja kukwama.
Sasa mimi nimeamua kumkataa awe wangu asiwe wangu alaumiane na mama yake.

Wakuu wakumbuke kwamba tangu mtoto akiwa na mwaka mmoja hajakaa sio na baba tu bali hata mama yake, mwanzo alisingizia kwenda kujiendeleza kielimu lakini hata baada ya kumaliza bado mtoto aliendelea kubaki kwa bibi. Nikawa najiuliza ni kwamba huyu sio mama bora au kuna kitu anamkimbiza mtoto huko?
Nalo lilikuwa linaniudhi sana kila wakati tunapokuwa tuko poa nilijaribu kumsisitiza akae na mtoto haiwezekani mtoto akose mapenzi ya baba akose na ya mama pia halafu wazazi wote wawili wapo zao tu town wanadunda tena vijana kabisa.

Yeye udhaifu wake ni mmoja tu ambao pia unaniongezea mashaka juu ya ubaba wa mtoto huyo, ukiacha lile la kukaa kimya napokaa kimya lakini kuna la maamuzi.
Mwanzo yeye ndio aliita jina la mtoto kibabe tu, yaani yeye ndio aliamua mtoto aitwe nani utafikiri mtoto hana baba au baba mwenyewe sijulikani kwao. Yaani kama tulikutana tu njiani.
Pia hili la mtoto kukaa kwa bibi alinijulisha lakini akiwa ameshaamua, yeye akiamua hata umshauri vipi tayari ana maamuzi yake akanijulisha tu kwamba anapeleka mtoto kwa bibi ili akajiendeleze
Kwa mara nyingine maamuzi yangu juu ya mwanangu yakabaki kama kivuli, baba jina tu msemaji yupo.

Kwahiyo wakati alipoomba msamaha nikagoma alipoamua kukaa kimya maisha mengine yakaendelea, sasa kaumri kangu kalikuwa kanasogea nimeshaishi kibachela kwa kitambo(maana huyu BM sijawahi kuishi naye tulivurugana mwanzo tu wa ndoa) nikaanza michakato ya kuvunja ndoa ya kwanza ili nifunge ya pili.
Mwanamke ninayemuoa nae anamjua, kwanza akaona ni aibu kwake lakini pia ule wivu tu wa asili kwamba ulichokikataa wenzako wanakitafuta. Nafikiri akapanga lazima turudiane au aharibu tu, akaanza kutumia watu wa karibu wanipe somo huku akiwajaza uongo nikagoma.
Akahamia kwa wadogo zangu, wale maselasela akawa anawatumia vocha wanaona yeeess shemeji si ndo huyu, wale wa kike anawatia maneno ati huyu mwanamke wa sasa ndio aliharibu ndoa yake, kwamba ni bora nirudiane nae kwa kuwa tuna mtoto tayari kuliko kuanza upya na mtu mwingine, mara tulishafanya mambo ya kimaendeleoa sijui tuna kiwanja wapi na wapi sijui wakati si kweli.
Wanawake ni rahisi kumuelewa mwanamke mwenzao wakanivagaa, nikawatia mkwara wakaniacha.
Kwa upande wa wazazi akashindwa maana ukiacha la kutoa mimba lakini kuna wakati mzee wangu aliwahi kuumwa taabani pamoja na kumjulisha alipiga simu tu mara moja kwa kumlazimisha asije akaonekana vibayaa hakurudia tena
Kwahiyo kwa wazazi alishajijengea picha mbaya.

Nikaenda baraza la kata, akaitwa kwa simu ili kuchelewesha mambo akataja tarehe ya mbali ili kukwamisha mchongo, tarehe ilivyofika alikuja likizo kimya kimya siku namkumbusha kesho yake ndo anaondoka hakusema kama anaondoka akasema tu atakuja barazani, kesho akapanda zake basi akayeya(Angejua baraza halivunji ndoa linasuluhisha tu pengine angekuja tungeyamaliza, napo ni kama ningechemka hoja zote za kumuacha)

Alipoondoka mwanaume nikaliambia baraza lichukue hatua.
Baraza likaipeleka mahakamani(mahakama ya mwanzo), kule akalimwa wito/ summmons ya kimahakama. Akaahidi atakuja.

Hapo akaona mambo yamekuwa ya moto akanipigia kunichimba mkwara eti naongea na mwanasheria wangu juu ya hili[emoji23]kwanza najua hawezi kuwa na mwanasheria pili kama alitafuta mwanasheria inawezekana wanasheria wana zile "Sema ukweli wote tujue tunatoboaje" kama madaktari tu ili utibike kirahisi sema ukweli nilipita kavu mahali fulani sasa naona ute ute(joking)
Inavyoonekana mwanasheria alipopewa ukweli akamwambia tu ukweli kwamba hatoboi.
Akahamia kwa ndugu zake, siku moja nimekaa naona namba mpya, jamaa ananipigia anasema ni mjomba wake(kwa muda mfupi niliodumu kwa amani naye kuna ndugu sikuwafahamu) kumuuliza shida yake anasema anaomba tukutane tuyazungumze haya, nikamwambia imeshafika mahakamani tutazungumza huko, akarudishiwa jibu lake.

Pumbavu sana hao wakati napambania penzi langu niliwashtakia sana wakanitosa leo wanaibukia hata nisiowafahamu
Kwa upande wa yule shangazi inawezekana alitosa kuingilia maana walitakiwa kuyaweka sawa wakati nawalalamikia sasa yamefika pabaya wataingiaje.
Alichofanya hakuja, sio kwa kukaa kimya ila kwa kutafuta visababu.
Akasema anakuja nimtumie nauli nikataka kugoma mahakama ikanishauri nimtumie asije kuifanya kama sababu, nikawa tayari kumtumia. Nikamuelekeza njia ambayo akiitumia atatumia nauli ndogo akagoma anasema huko barabara mbaya anataka azungukie mbali apite Dar sijui

Wasichokijua wafuatiliaji kuhusu BM ni mpenda pesa, ndio maana huwa nahisi mtoto sio wangu ila ananipiga hela tu.

Ile kunipangia njia ya kupita na tunajua njia hiyo ilishawekwa lami mwanzo mwisho yeye anasema mbaya nikafura kwa hasira nikaenda mahakamani nikamwambia Hakimu aifute nitajua cha kufanya.
Yule hakimu abarikiwe huko aliko akasema usifanye hivyo atakusumbua baadae, mradi ameshasaini summons sisi tutasikiliza upande mmoja.

Na kweli kwanza mlolongo ukapungua nikasikilizwa mimi talaka ikaandika
Nikaambiwa nisubiri siku 45 za rufaa nifuate hati ya talaka.

Sheffer95


NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI
Nashuka na uziiiii nasubiri episode ya 7
 
  • Thanks
Reactions: T11
Sina upole wa namna hiyo
Mashaka juu ya mtoto sio wangu nilishakuwa nayo kitambo, lakini kutumia jina langu inanimilikisha moja kwa moja

Mimi naamini watoto ni baraka, hata ukipata mwanamke huko ametelekezewa mdirect kwangu nitamlea lakini asije kutokea mtu akasema ni mwanae baadae nitajifunzia uchawi kwake
Sio uchawi tuuu.. ni kumlima gharama za hatari ulizomlea mtoto.. ili aruke
 
  • Thanks
Reactions: T11
SEHEMU YA 7:


Talaka ikatolewa baada ya siku 45, maisha yakaendelea na mwanamke huyu mwingine, nikahisi kuutua mzigo maana wakati alipokuwa ananibembeleza turudiane nikigoma anasema yeye ndo mke hata nifanyeje, ananitumia na picha ya cheti cha ndoa
Ikawa inaniudhi sana, kwamba mtu hakutaki lakini anataka tu kukukwamisha hasa kwa wivu tu kwa mwanamke mwenzie, hili la kunikwamisha kweli lilikuwa linaniwazisha mimi umri unaenda nahitaji kupikiwa kufuliwa na kuitwa baba lakini kuna mtu tu yuko somewhere ameamua kushikilia maisha yako
Nilikuwa naogopa sana kama nitashinda kesi yangu ya madai ya talaka ningefangaje na yeye najua hanitaki anataka kukwamisha tu na akishajua sasa sina cha kufanya tena ndio angeninyoosha vilivyo.

Lakini kwa kufaulu kwangu kumshinda mahakamani na talaka kutolewa sasa nikajiona maisha yanasogea kwa ahueni ya hali ya juu
Hapa ikaibuka changamoto nyingine, yule mwanamke niliyempata akawa ana-miss fire mara kwa mara, nina hamu na mtoto na kila akidaka ngoma inatokea kusikojulikana
Hapa ilifuata stori ambayo haina umuhimu sana katika mjadala huu lakini kwa ufupi ndio nikajua yoote ya tangu kabla na mpaka nilipoletewa zawadi nikazikataa, yote yalielezewa lakini sikuyatilia maanani kwa kuwa sikwenda huko physically nilisimuliwa tu.

Hapa sasa nikiwa na akili zangu timamu nikaanza kuishi nae kwa tahadhari sana, kuna wakati akanitumia akaunti ya benki anasema ni kwa ajili ya mtoto nikipata chochote niwe natuma huko, yaani amekaa amepanga mwenyewe akaamua kufanya hivyo bila kujadili na mimi, bila kujua kama kuna akaunti nyingine au vipi
Nilimjibu kwa ufupi tu "Watoto hawalelewi hivyo" hakujibu chochote tena
Nilishapigwa pesa ya kulea mimba sikuwa tayari kupigwa mara nyingine.
Tangu hapo kuna baadhi ya matukio alihitaji nichangie chochote basi hata kama ni elfu kumi tu aliipata kwa mbinde mno, sikumuamini tena.

Nataka hii stori imalizike haraka...
Niseme tu mimi ni muoga sana wa kutelekeza mtoto, hili sikutaka kabisa lije linitokee, so mpaka hapo bado nafsi yangu haikuridhika kwamba yule sio mwanangu, kuna wakati nikikaa akili inaniambia ni mwanangu.
Kikapita kitambo kidogo sina mawasiliano nao, nae kama kawaida akanyamaza tu.
Kimyaa, zaidi ya mwaka.

Kwahiyo mwaka 2019 mwishoni nikiwa humu nikapitia uzi wa mzee Iringa Native
Niliusoma kwa makini sana, ukanigusa, nikajihisi yanakwenda kunikuta hayo, ni uzi uliokuja kupigilia msumari ile dhana yangu ya kutokuwa na rekodi ya kukataa mtoto

Watu wanaweza kufikiri kwanini pamoja na yote hayo bado kuna wakati niliamini mtoto ni wangu, kuna vitu vingi pengine kwa kuruka makusudi au kwa kuvisahau viliendelea ambavyo vilikuwa vinanirudisha kwenye mstari sometimes.

Kuna wakati nikawa nahisi huenda ni kichaa cha mwanamke tu wacha nijishushe kwa faida ya mtoto mfano tukiwa poa namuuliza hivi mambo unayofanya mbona ni kama mimi sio baba wa huyo mtoto? Anajibu kama humtaki sema na akikua nitamwambia ulimkataa, acha kufikiria vitu usivyo na uhakika navyo?[emoji2307][emoji2307] Katika mazingira haya narudi tena kujaribu kuwa karibu na mtoto.

Kwahiyo uzi wa Iringa Native ukaamsha ari mpya maana nilikaa kimya kitambo sana ukizingatia tayari nilikuwa na mtoto ambaye ukimtazama huulizi, hata ukimuacha mtaani japo ni mdogo sana lakini watamleta kwangu... Sikuwa na munkari tena na watoto wenye mashaka mashaka ..
Nikapanga kumtafuta tena..

NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI
sijutii kuufuatilia huu uzi, nikiwa mkubwa ntautoa na wangu coz unafanana na huu 4 sure..
 
  • Thanks
Reactions: T11
Hayo nayo yataka moyo mkii..ila kitanda hichoo hakizai kharaaam..😄😄
 
  • Thanks
Reactions: T11
Back
Top Bottom