True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

Si kuna sehem alisema kua anahisi yawezekana mwanzo alifanyiwa mambo kidogo
Kuna mengine nayajibia kwenye comments na watu hawasomi
Lakini hili la imani lisipewe nguvu sana

Hili zigo la uzembe niko radhi kulibeba
Cha msingi tunaweka kumbukumbu na tunafundisha wengine
 
SEHEMU YA 8:

Kabla sijaendelea mbele kuna kitu nilisahau kukisema, ili kukazia hoja yangu kwamba mtoto sio wangu.
Tunajua kufanana kwa mtoto na mzazi sio lazima lakini je, inawezekana mtoto asifanane na wazazi wote wawili? Yaani hafanani na baba wala mama[emoji1][emoji1][emoji1] hapa nikajua kuna mtu wa tatu ndiye kafanana nae.

Tuendelee tulipoishia, Baada ya kupitia uzi wa Mzee Iringa Native akitafuta wanae na akionesha majuto ya hali ya juu ikaanza kama kunigusa gusa hivi, wakati nasoma ilikuwa 2019 december nikajiambia nitaanza mwaka kwa kuwatafuta hawa watu ili kama vipi niendelee kuhudumia mtoto.
Nikatafuta namba zake maana nilishazifuta kabisa, nikazipata nikampigia
Tukaongea tukaelewana, yaani yeye hanaga mpango na mimi hata nikikaa kimya miaka kibao, nikirudi ananipokea tu
Nikagundua huyu ananipokea ili anipige hela lakini masuala ya mtoto kuna mtu(Baba Mtoto) wanashauriana naye

Kufupisha tu stori baada ya kuwa nimejirudi na sasa nawasiliana nao vizuri nikamwambia nahitaji huyo dogo aje anitembelee nyumbani ili kujenga mazingira ya kujuana na nduguze nikapigwa chenga nyingiii baadae akakubali likizo atakuja kwa muda mfupi, lakini pia nikamwambia anatakiwa afike mpaka kwetu maana babu zake wananidai sana.

Kwa bahati nzuri au mbaya korona ikatuvamia hiyo 2020 mwanzoni, wakafunga shule, haraka nikamwambia kwa kuwa wana likizo ndefu sana naona nimchukie, nilipigwa chenga kali sana nikaambiwa sijui kachukuliwa na nani kwenda wapi sijui
Anyway nilichojua hapa nimekataliwa tu..sasa mimi baba yake nakataliwaje

Tutaendelea
 
Sio sasa ni miaka kadhaa nyuma imeshapita, haya nimekuwa na jeuri ya kuyasema kwa uhuru na amani sasa hivi.
Kwa Kipindi kile sikuwa na uwezo huo, maumivu niliyokuwa nayasikia sio ya kawaida, sasa ndio mfano nikueleze kama hivi halafu uniambie hakuna mwanamke hapo nilikuwa naumia sanaaa ndio sababu sikuwa nasema kwa mtu ilikuwa vita ya mimi na nafsi yangu tu
Yaani nilichokuwa nataka kusikia ni kupendwa (ambako nako sikuwa nikipendwa) nilichokua nataka kusikia kwa watu ni angalau kuitwa mume wa BM nikisikia chochote hata mtu aniulize nasikia mmeachana basi naumia kweli kweli

[emoji1][emoji1][emoji1]Kile kipindi kimeniimarisha sana
[emoji23][emoji23][emoji23] jamani pooleee. Pole sana. Ndo huwa ilivyo. Mapenz ni upofu sikulaumu
 
SEHEMU YA 8:

Kabla sijaendelea mbele kuna kitu nilisahau kukisema, ili kukazia hoja yangu kwamba mtoto sio wangu.
Tunajua kufanana kwa mtoto na mzazi sio lazima lakini je, inawezekana mtoto asifanane na wazazi wote wawili? Yaani hafanani na baba wala mama[emoji1][emoji1][emoji1] hapa nikajua kuna mtu wa tatu ndiye kafanana nae.

Tuendelee tulipoishia, Baada ya kupitia uzi wa Mzee Iringa Native akitafuta wanae na akionesha majuto ya hali ya juu ikaanza kama kunigusa gusa hivi, wakati nasoma ilikuwa 2019 december nikajiambia nitaanza mwaka kwa kuwatafuta hawa watu ili kama vipi niendelee kuhudumia mtoto.
Nikatafuta namba zake maana nilishazifuta kabisa, nikazipata nikampigia
Tukaongea tukaelewana, yaani yeye hanaga mpango na mimi hata nikikaa kimya miaka kibao, nikirudi ananipokea tu
Nikagundua huyu ananipokea ili anipige hela lakini masuala ya mtoto kuna mtu(Baba Mtoto) wanashauriana naye

Kufupisha tu stori baada ya kuwa nimejirudi na sasa nawasiliana nao vizuri nikamwambia nahitaji huyo dogo aje anitembelee nyumbani ili kujenga mazingira ya kujuana na nduguze nikapigwa chenga nyingiii baadae akakubali likizo atakuja kwa muda mfupi, lakini pia nikamwambia anatakiwa afike mpaka kwetu maana babu zake wananidai sana.

Kwa bahati nzuri au mbaya korona ikatuvamia hiyo 2020 mwanzoni, wakafunga shule, haraka nikamwambia kwa kuwa wana likizo ndefu sana naona nimchukie, nilipigwa chenga kali sana nikaambiwa sijui kachukuliwa na nani kwenda wapi sijui
Anyway nilichojua hapa nimekataliwa tu..sasa mimi baba yake nakataliwaje

Tutaendelea
Noma sana, huyu kiumbe alizaliwa maalum (special) kukutesa
 
SEHEMU YA 8:

Kabla sijaendelea mbele kuna kitu nilisahau kukisema, ili kukazia hoja yangu kwamba mtoto sio wangu.
Tunajua kufanana kwa mtoto na mzazi sio lazima lakini je, inawezekana mtoto asifanane na wazazi wote wawili? Yaani hafanani na baba wala mama[emoji1][emoji1][emoji1] hapa nikajua kuna mtu wa tatu ndiye kafanana nae.

Tuendelee tulipoishia, Baada ya kupitia uzi wa Mzee Iringa Native akitafuta wanae na akionesha majuto ya hali ya juu ikaanza kama kunigusa gusa hivi, wakati nasoma ilikuwa 2019 december nikajiambia nitaanza mwaka kwa kuwatafuta hawa watu ili kama vipi niendelee kuhudumia mtoto.
Nikatafuta namba zake maana nilishazifuta kabisa, nikazipata nikampigia
Tukaongea tukaelewana, yaani yeye hanaga mpango na mimi hata nikikaa kimya miaka kibao, nikirudi ananipokea tu
Nikagundua huyu ananipokea ili anipige hela lakini masuala ya mtoto kuna mtu(Baba Mtoto) wanashauriana naye

Kufupisha tu stori baada ya kuwa nimejirudi na sasa nawasiliana nao vizuri nikamwambia nahitaji huyo dogo aje anitembelee nyumbani ili kujenga mazingira ya kujuana na nduguze nikapigwa chenga nyingiii baadae akakubali likizo atakuja kwa muda mfupi, lakini pia nikamwambia anatakiwa afike mpaka kwetu maana babu zake wananidai sana.

Kwa bahati nzuri au mbaya korona ikatuvamia hiyo 2020 mwanzoni, wakafunga shule, haraka nikamwambia kwa kuwa wana likizo ndefu sana naona nimchukie, nilipigwa chenga kali sana nikaambiwa sijui kachukuliwa na nani kwenda wapi sijui
Anyway nilichojua hapa nimekataliwa tu..sasa mimi baba yake nakataliwaje

Tutaendelea

Kwanini now watu wa JF mkianza kusimulia kitu mnaweka robo robo??

inakata stimu sana
 
SEHEMU YA MWISHO:


Naona niifupishe maana japo lengo halikuwa kuomba ushauri lakini naona kuna haja ya kuomba ushauri baada sasa ya kujivua rasmi.
Mwaka jana baada ya kupigwa chenga kwa lugha nyingi mara bibi yake amemchukua mara sijui yuko wapi nikakausha, siku moja nikampa somo zito juu ya umuhimu wa mtoto kuwajua nduguze ikiwemo kuwajua babu na bibi yake wa upande wangu, na kweli wazee walikuwa wananidai sana kwamba kama anatumia jina langu maana yake ni wangu kwahiyo wanataka awapelekee wamjumlishe kati ya wajukuu zao maana hawajamtilia maanani bado kati ya wajukuu walionao.
Hapo akakubali na akasema bwanaee kamchukue mi nimechoka
Nikamuuliza amechoka nini akasema amechoka kupiga chenga.
Inavyoonekana upande wao ni kama walikuwa wanakaza, nikimdai ilikuwa lazima aombe kwao wamkubalie sasa akawa amechoka huku namdai kule mpaka awaombe, kweli nikapanga weekend moja nimchukue lakini kutokana na shughuli zangu nikashindwa nikamwambia akipata muda ampeleke home mwenyewe.

Huyu BM sasa alikuwa amehama mkoa ule amehamia mkoa ambao wazazi wangu wapo ingawa wilaya tofauti, kwahiyo kutoka alipo mpaka kwetu ni masaa machache tu. Akakubali atampeleka akipata muda.

Sasa mwaka jana mwishoni akataka mtoto ahame alipo ambapo ni karibu na mimi ahamie kwake, na mimi ndio nilipendekeza hivyo baada ya kumdai sana kwanini hataki kukaa na mtoto, sio vizuri mtoto ana wazazi wote vijana tu halafu anakaa na mama mdogo sijui. Nimamwambia kufika mwisho wa mwaka jana asipomchukua namchukua hata kwa nguvu hapo akaogopa
Yeye hoja yake ni mtoto hawezi kukaa na mwanamke mwingine nikamwambia ntampeleka kwa bibi yake bado ana nguvu za kumlea, akaogopa akasema atakaa naye yeye. Kwa kuwa mimi ndio nilikuwa karibu na anapoishi mtoto akaniomba nifuatilie uhamisho shuleni, kweli nikafuatilia mtoto akatangulia uhamisho ukafuata..
Kabla sijakamilisha uhamisho akaanza visababu eti mtoto hataki kuishi huko aliko anataka abaki, nikamwambia amdanganye kama anaenda kusalimia tu atarudi, akakomaa nikamwambia hataki tu kukaa na mtoto ikabidi akomae akae nae.

Sijakaa sawa akaanza visababu ooh shule aliyopo sio nzuri imekaa pabaya kwa sababu kutoka nyumbani mpaka shule inabidi avuke barabara anahofia atagongwa nikamwambia watoto wengine wanavukaje akasema huyu mgeni nikamwambia atazoea kama wenzie. Akakosa cha kusema
Akaibuka na hoja nyingine hii shule hawajui kufundisha nikamwambia mhamishie shule nyingine akasema anataka shule fulani ina gari la kuchukua na kurudisha watoto kwahiyo tutakuwa tume-solve tatizo la hatari ya kugongwa na magari lakini pia atapata elimu nzuri halafu anataka mtoto ajue kizungu.

Hapa wafuatiliaji wafahamu kwamba pamekuwa na mjadala kabla mimi na huyo mwanamke juu ya namna ya kuwapatia elimu watoto, Tangu siku za nyuma nilishamwambia si kwa kukosa pesa au kwa kutojua umuhimu wa elimu lakini mimi binafsi sipendelei mtoto asome boarding katika ngazi ya shule hizi za chini iwe awali au shule ya msingi, sitaki mtoto asome shule za kishua hata kama sio boarding katika ngazi hizi za elimu
Nikitoa hoja kwamba mtoto atasoma changanyikeni huku chini halafu atasoma shule hizo za kishua ukubwani kama ni kizungu hakihitaji mtu kuanzia awali anaweza kukijua vizuri kabisa hata akikutana nacho chuo tu hata asipoenda chuo anaweza kujua kizungu.
Nikampa mfano wa wasanii wetu hawa wengine hata form four hawajafika lakini kwa kujua wanahitaji kujitanua kimataifa walijifunza na wanazungumza vizuri tu

Kwahiyo suala la kizungu halihitaji miaka bali nia na nilimueleza sio kwa mtoto wake tu bali watoto wangu wote watasoma kwa utaratibu huo.

Pamoja na hoja zangu zote hakuelewa, kama nilivyosema kabla yeye akiamua ameamua, habari ya ubaba haina maana kwake.
Juzi tumebishana sana nikamwambia mbona sasa ubaba wangu uko kwenye suala la hela tu lakini sina maamuzi yeyote ina maana hiyo mimba ulijitia mwenyewe? Akanijibu ndio maana unaambiwa mtoto ni wa mwanamke

Shuuubamiiiit!!!! Nikapanda jazba nikamwambia sababu ya mimi kila mara kujishusha ni kwa sababu mtoto anatumia jina langu bila hivyo nisingekuwa na habari, anachotakiwa kufanya ni kubadili hilo jina hatakuja kunisikia tena
Akaniuliza kwahiyo nakataa mtoto? Kwa mara ya kwanza nikamjibu ndio namkataa fanya nilivyokwambia sitakusumbua tena, akajibu sawa.
Nikakata simu, baadae nikapiga kuna jambo sikumalizana nae, hakupokea tena.

Hapa unajiuliza kama ningekuwa baba wa mtoto mbona nikisusa hajishughulishi yaani ni fasta tu anakata mawasiliano?

Nikajiambia sitajihusisha tena na huyo mtoto.
Kwahiyo wadau wa jamii forum kwa heshima na taadhima napenda kusema NIMEAMUA RASMI KUMKATAA MTOTO, wakati nafikiria kuandika huu uzi nilijawa na hofu nitasimangwa kwa kukataa mtoto, nilijipanga hasa kushawishi nieleweke kwanini nakataa mtoto, kwa bahati nzuri kabla sijamaliza uzi wananzengo wote wanaelewa kwanini nakataa na wengine wametambua kabisa namna gani nilibambikwa tu.
Kwahiyo kazi yangu imekuwa nyepesi.

TAMATISHO:
Kama nilivyosema hapo juu sikuwa na mpango wa kuomba ushauri lakini nimepata wazo la kuomba ushauri wenu wa kisheria juu ya haya;

1) CHETI CHA NDOA: Mahakama ilitoa talaka, nina hati ya talaka lakini kiutaratibu cheti cha ndoa kinabaki kwa mwenye ndoa, ni hati tu inajulisha ndoa imevunjika
Sasa mwenzangu nilipomjulisha nimeshavunja ndoa afuate hati yake ya talaka ikibidi achane kile cheti akajibu kwa nyodo hawezi kuchana kinamsaidia kwenye mambo mengi ikiwemo kuombea stahiki fulani fulani kazini
Lakini pia kilimsaidia kuhama mkoa mmoja kwenda mwingine, na kwa mbwembwe anakutumia na kapicha ka cheti whatsapp
Jambo hili linanikera naona ananitumia kwa faida yake je, naweza kumchukulia hatua za kisheria kwa kutumia cheti ambacho ndoa yake haipo? Hata nisipomchukulia hatua hawezi kuja kusumbua kughushi masuala yoyote hapo baadae wakati shuhuda nikiwa sipo?

2) JINA: Huyu mwanadada siku zote ni jeuri najua nimemwambia abadili jina la huyo mtoto kuondoa jina langu, na mimi sitaki tena atumie jina langu.
Nikibaini bado anatumia nimchukulie hatua gani kisheria?

MWISHO

NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI!
 
Kutumia cheti cha ndoa ambayo imeshavunjwa kujipatia manufaa hapo kuna elements za jinai.

Kwenye issue ya kusajili talaka Rita, ni bora ukatafuta mwanasheria aliye karibu nawe akusaidie.
 
Ni kweli , mi na mwana anapitia hayo kipindi hichi story zinafanana kwenye swala la mtoto na tabia ya demu wake (japo wote wapo mkoa mmoja) anakamuliwa tu matumizi bora we unauhakika wa kipato...naye mwanzoni alikuwa na machale sahv ndo kapotea kabisa hashikiki..

Naona story yako umenikumbusha mwana, Inahuzunisha Sana !
 
Cha
Watu wa Jamii Forum Salaam, Naitwa Mfukuza Ndoto, Nina umri wa katikati ya ujana naishi mkoa fulani kanda ya kati. Basi bwana mnamo mwaka fulani nikiwa na 20+yrs nilitokea kumpenda binti fulani toka nyanda za juu kusini, binti huyo alikuwa mwanafunzi wakati huo katika chuo fulani hapa mjini. Namaanisha alikuja tu kwa ajili ya masomo.
Tukapendana, kwa kawaida huwa nikishaingia kwenye mahusiano huwa nadumu na kutulia ndio maana mpak sasa sina rekodi ya mtoto wa mtu niliyempotezea muda halafu nikamuacha, sina machozi ya mwanamke yeyote yanayoniandama zaidi wote hujutia na hicho ndio nilichokipanga kwenye maisha yangu mwanamke akitaka kupendwa atapendwa ashindwe yeye tu sipendi lawama.
Kabla yake nikiwa mwanafunzi miaka ya 2000's nilipoingia tu kidato cha kwanza nikapendwa na kabinti fulani(Na desturi yangu huheshimu sana hisia za mwanamke, yaani siingii kwenye mahusiano bila mwanamke mwenyewe kuonyesha interest na mimi nami nikiridhika nae anapitishwa. Hapa nazungumzia mapenzi sio ngono kwa maana ya tamaa za mwili, nikitamani kuna sehemu zinajulikana na mabaharia hujipoza maisha yanaendelea
Kwahiyo kwenye maisha yangu nimepitia mahusiano yasiyozidi matatu, acha wale wa kushare nao tu shuka, tukiwataja tutajaza kurasa za Jf.
Kwahiyo baada ya kabinti kunipenda hiyo ni pre-form one mpaka tunaanza form one mpaka kidato cha nne tulikuwa wapenzi na shule nzima ilijua hilo lakini cha ajabu hatukuwahi kufanya mapenzi kabisa,
Ilitokea hivyo kwa sababu kuu mbili, kwanza tulikuwa wadogo sana nadhani nilikuwa na miaka 14(kwa mwanaume wakati huo nilikuwa mdogo sana) na yeye alikuwa mdogo zaidi, pili kwa wakati huo mpaka umvue nguo mwanamke ilikuwa shughuli, sio kama sasa katika umri huo kijana anazijua tayari na kama binti tayari anazijua P2.
Kuna wakati nilikuwa naazima mageto ya washkaji tunakutana huko na kabinti basi washkaji wanajua nimemaliza kazi kumbe nimegomewa na mimi ujanja sina sana[emoji1][emoji1] sababu ya tatu sitaitaja lakini ndio kubwa zaidi
Mimi na yule mwanadada tumekuja kuvunjana 'Upya' tukiwa tumeshamaliza form four tumefeli tuko mtaani, kwa kweli yeye na mimi wote tulikuwa wageni wa mambo kwahiyo tulifunguliana

Nayasema haya ionekane namna gani huwa siachi mwanamke nikishaingia nae kwenye mahusiano mpaka yeye aje kuharibu na ajilaumu mwenyewe na akishaharibu hata aje na Fiat (gari za zamani) huwa sibadili msimamo hata aroge vipi, kwa kuwa naamini ukishafanywa mpumbavu mara moja ukasamehe uwezekano wa kuonekana boya ni mkubwa na atakuumiza mara ya pili na zaidi
Kingine naamini wanawake ni wengi, shida ya nini kurudiana na mmoja aliyekuumiza? Sio kweli ile dhana ya kwamba umeandikiwa utaishi nae kumbuka binadamu wawili wawili kama uliandikiwa kuishi na huyo akizingua kuna aliyefanana tena na huyo huyo utampata, na ili tupeane masomo asijeenda kusumbua wengine unamgomea msamaha akienda kwa mwingine hatasumbua labda awe amepinda tu.

Kilichoniachanisha na huyu bikra mwenzangu nikiwa mtaani nimechoka sasa napigwa na maisha kotekote akanifuata jamaa mmoja, ni wale unakuta pale mjini ana sifa ya ukicheche(umalaya)
Zamani ilikuwa kama sifa, kila mji palikuwa na watu sifa yao ni hakuna demu anapindua kwao, na mara nyingi unakuta ni sababu ya maisha mazuri yake au ya familia yake, akishamudu kuwa na kageto na uwezo wa kubadili mavazi kidogo basi mademu wanapishana. Huyu jamaa akaniuliza kama huyo demu ni demu wangu(nafikiri aliambiwa kwa busara akaona asije kuingia anga zangu) basi mimi ile kujivunga eti nampima imani demu nikakataa ili kama atatongozwa akatae mwenyewe

Bwana wee sijakaa sawa demu ananipigia simu ananitukana kwa namba mpya sielewi sababu nini, huku akiwa na wifi zake(dada wa yule jamaa) kuja kufuatilia jamaa keshamtindua dah nikadata maana home kwetu walimjua mpaka dada zangu walimjua alikuwa anafika mpaka home, miaka zaidi ya minne ilikuwa lazima ajulikane. Na pia alipoanza kutoka na huyo jamaa dada zangu walijua ikawa fedheha sana, nikawaza, nikachanganyikiwa kwa aibu sio kwa sababu siwezi kupata mwingine.
Nikapiga moyo konde nikamove on, Mungu si athumani nikaotea kibarua kidogo, aliposikia akaanza kujirudisha.
Sikumtukana, sikumjibu vibaya nikamwangalia tu nikaachana nae mpaka leo ananiona tu mitandaoni.
Huyo ni mmoja kati ya hao watatu

Sasa tuendelee na huyu binti mwanafunzi wa chuo ngazi ya chini ya shahada...huyu nilikutana naye katika ofisi moja ya serikali ambapo alimsindikiza mwenzake na mimi ambaye mimi nilifahamiana nae, baada ya kusalimiana na kukaa wote kwenye benchi kwa muda mrefu tukisubiri huduma tukazoeana(na huyu binti mlengwa) tukabadilishana namba.
Nilipoondoka yule rafiki yake akanitanabaisha kwamba rafiki yake (Binti Mlengwa tumwite BM) anaonyesha namna fulani ya kunikubali/kunipenda/kunizimikia[emoji23][emoji23]sasa kama ilivyo desturi yangu huwa sidharau hisia za mwanamke awe amenipenda au ametamani kushare shuka tu na mimi lazima nimtimizie adhma yake.
Note: Haya hayatokei ikiwa nina mwanamke tayari ninayedumu nae, ni pale napokuwa 'Loose ball' na pia isitafsirike kwamba labda nina mvuto saana hapana hii hutokea kwa yeyote maana wanawake wana sababu nyingi za kupenda mwanaume kama ambavyo wanaume tuna sababu nyingi tu za kuvutiwa na mwanamke.

Tuendelee, nilipopata ujumbe ule nikajua cha kufanya hapa ni kuanza ukaribu tu mwanamke akishakupenda hawezi kukuanza lakini ukimsalimi siku ya kwanza, ukamchatisha bize siku mbili weekend inayofuata ukimtaka appointment atakuja tu hata kama atazuga kidogo, Basi, nikaweka mazingira na uhusiano ukaanza kwa namna hiyo

Mwanzo sikukapenda baadae nikakazoea basi nikakapenda, sijui kalinifanya nini nakiri ndio mwanamke nimewahi kumpenda haijatokea tenaaaaa

Visa vichache vilitokea wakati ule vilifaa kabisa kumuacha sikuviona leo hii ndio nayaona na kujiuliza hivi nilikuwa mimi kweli yule? Mfano kuna wakati nilifuma meseji kwenye simu yake ni dhahiri ilikuwa ya mwanaume na ana mahusiano naye nikafunika kombe mwanaharamu apite
Kuna wakati msanii mmoja alikuja kupiga show kwenye ukumbi fulani sikwenda lakini kuna jamaa akaropoka kwamba alimuona usiku huo huyo binti na kutoka chuoni mpaka mjini ni umbali ambao sio wa kurudi usiku, sasa alilala wapi hicho kiulizo kingine, lakini wakati naoambiwa huyo binti alikuwa club mimi nimeonge nae sana usiku mpaka kwenye saa tano au sita kwa akili yangu ndogo wakati ule sikumuamini jamaa nikafikiri nimemfananisha....maisha yakaendelea

Nilikapenda sana kale kabinti, kuna wakati nilitishia kukaacha kakalia usiku kucha, nikajisemea mwanamke si ndo huyu bwanaaa...nikadumu nae kwa miaka mitatu mpaka anamaliza, kilichonipa imani kwamba mke nimepata ni wakati alipomaliza shule, wanavyuo wengi wakimaliza na mapenzi wanaondoka nayo makwao lakini huyu BM aliendelea "ku-keep in touch" mpaka nikaanza kunenepa, huko huko aliko bado mawasiliano yalikuwa mazuri huku akija kunipikia kila alipopata nafasi
Hata wenzangu waliokuwa na wanawake pale chuoni ambao walishaachana na wapenzi wao waliamini nimependwa haswaaa na mimi ukinipenda nakupenda nataka nini kingine.

Ndio ikawa hivyo, akamaliza akaondoka, akaanza kudai ndoa, basi mi ndo kabisaa naona nimepata mke mwema, nikachukua likizo nikampeleka nyumbani kumtambulisha, kwanza nikaanza kwao kisha kwetu.
Nyumbani kwetu walimpenda sana, she was hard working na mrembo kiasi, tukiwa hapo nyumbani nafasi za ajira zikatoka akaajiriwa mkoa fulani kanda ya magharibi
Wakati nampeleka nyumbani ilikuwa mnamo August ya mwaka huo, kufika December ndio picha picha zilipoanza...


.....Wacha nichukue mapumziko....leo ndio nimeona ugumu wa kuandika...wale wazee wa itaendelea hawafanyi kwa makusudi inawalazimu kupumzika

Will Be Back!!!
Chai
 
SEHEMU YA 5:

Mwenendo mzima wa BM, Mwenendo mzima wa ujauzito wake na mwenendo mzima wa kujifungua kwake na ushirikishwaji wangu kwake mpaka hapo ulishanipa mashaka sana
Kama mtoto ni wangu kwanini mambo yote haya yanatokea? Kama nilihudumia ujauzito mwanzo mwisho hasira zao/zake juu yangu zinatoka wapi? Bado haitoshi kunifanya baba wa mtoto? Iwe nimetoa mahari au sijatoa madhali sikukaa mbali na mimba kwanini nitengwe hivi?
Anyway wakati wa ujauzito nilijua labda hasira za mimba sasa mbona mambo yanaendelea mpaka baada ya kujifungua?
Taa nyekundu ikazidi kuangaza ndani ya ubongo wangu, isisahaulike stress ziliendelea kuniandama vilivyo, watu wangu wa karibu, ndugu na jamaa wakashangazwa na mabadiliko..lakini kwa mbaali nikaanza kuzisikia roumours kwa watu wakisema hali hii imepelekewa na kuachwa kwangu na mwanamke huyo, watu walijuaje? Nikaanza kunote kitu kwamba inawezekana yeye ndio anayasema haya kwa watu. Hali ilikuwa mbaya sana, najifungia ndani tu kama siko kazini. Huko ndani ni mimi na mitungi tu.
Kwa mara ya kwanza ni wakati huu sikupata usingizi, nilikuwa naweza kukaa macho tu tangu giza linaingia mpaka linapotea siku ya pili. Sikuutamani usiku tena, ni angalau mchana ningekutana na watu nikapoteza mawazo lakini giza likiingia nikabaki peke yangu ilikuwa ni mawazo mwanzo mwisho, mimi na mawazo, mawazo na mimi.

Ikafikia kipindi nikafreeze nikakaa kimya nikakubali matokeo, kwamba hapa sina changu tena. Kilichobaki ikawa kupambana kurudi katika hali yangu ya kawaida. Nilipambana sana mpaka angalau nikawa sawa kidogo.
Mwaka ukaisha, bila mawasiliano yoyote as if kule sina damu yangu, yaani hata simu ya bahati mbaya haikuwepo hapo nikaamini kuna mwenye mtoto anahudumia
Siku moja akanitumia meseji anasema nyumbani kwao wanataka kujua hatima yangu na yeye maana pako kimya tu. Nikapiga akili ya haraka nikaona huo ni mtego, kwao wanasubiri mimi niseme simtaki binti yao ili ionekane mimi ndio nilimuacha na kama kuna madai kwao nisidai, mimi nikamjibu hatima yetu alishaiamua yeye BM hapo kinachofanyika ni kunitega tu.
Kuna kitu akasema sasa kukaa kwako kimya ni kama namfunga yeye(maana yake ni iwapo anataka kuolewa kwingine nitoe go ahead) hapo nikajihakikishia huyu ana mtu mwingine sasa anataka kuolewa
Nikamjibu sijamfunga kama anataka kuolewa anaweza kuolewa tu maan mimi sidai kitu kwao biashara imeisha na kiukweli sikumhitaji tena hata bure.
Akauliza kimtego na mtoto je, nikamjibu nimewapa zawadi, akasema atawaambia yote hayo. Tukamaliza hivyo
Ikumbukwe ni mwaka sasa sijawahi kumuona huyo mtoto, sio mimi wala wazazi wangu.
Kiutaratibu baada ya kujifungua alitakiwa amlete kwangu nimuone, kisha awapelekee babu zake, kama mimi na yeye tulikuwa na matatizo angewapelekea hata wazee wangu, hakufanya hivyo. Na kwao wanaona sawa wala hawakujihangaisha kumshauri juu ya hilo.

Siku tuliyoongea hayo nikafuta na namba zake moja kwa moja, miaka ikakatika nikaja kusikia alipeleka kijijini mtoto akiwa na mwaka mmoja yeye akarudi shule, nikawaza sana huyu mwanamke wa aina gani? Mtoto wa mwaka mmoja kumpeleka kijijini kisa shule mbona shule zipo tu si angesubiri? Sikujali nikaachana nao

Ikawa mwaka wa kwanza, wa pili na wa tatu, mtoto alishakuwa na miaka minne namsikia tu. Mimi nikaendelea na mambo mengine. Nikaanza kusikia kwa watu wa karibu vitu ambavyo ni kama kuna kitu huwa wanaongea nae kinachofanana na kurudiana na huyo mwanadada. Kuna jamaa yangu mlevi siku moja alilewa katika stori akasema utarudiana tu na mama fulani? Yaani BM nikamwambia kwa mapito aliyonipitisha haitawezekana
Akasema tutaona mtoto atawaunganisha tu, kusema kweli mtoto bado nilikuwa namhitaji sio mama yake .

Watu waliamini kweli naweza kumrudia sababu walijua nampenda sana sina ujanja, hata yeye alijua hivyo. Inasemekana hata alipoenda shule alijua mimi sina ujanja wa kumove on atanikuta tu, anakuja kumaliza shule anaanza harakati anakuta mimi nilishapambisha mapenzi kwingine.

Anyway baada ya kuanza kusikia kwa watu vitu vinavyofanana na kurudiana nikaanza kujiandaa kisaikolojia nilijua ni yeye tu anayasema haya. Kweli bwana siku moja akanitumia meseji yuko njiani anataka tuje tuonane, nikamwambia kuna tatizo gani? Akasema tutaongea akifika.
Nikamwambia haiwezekani akasema tuache tofauti zetu bhana turudiane tutunze mtoto. Halafu anaongea kirahisi tu kwa kuwa alijua mimi ni wake tu nampenda sana. Hakujua mambo yalibadilika kutoka mapenzi mpaka chuki.
Mpaka wakati huoa alikuwa ndio binadamu namchukia kuliko wote, yeye hakujua hilo
Kiukweli nilimgomea.

Alipofika akapitiliza chuo alichokuwa anasoma akadai anafuata cheti chake, mimi nikajiuliza huyu cheti alishachukua ni cheti gani amefuata? Nikanyamaza
Jioni hiyo ananipigia simu anajichekesha chekesha kisha akanipa mama mmoja niongee nae, nikaongea nao kidogo nikakata.

Huyu mama tangu akiwa anasoma walikuwa wanaitana mama wa hiyari, huyu mama ilifikia hatua akihitaji kitu ananipigia mimi niko mjini yeye bush namuagizia.
Kuna dhana nyingi zinatembea hapa, inawezekana huyu mama ndio aliwezesha mchongo mzima wa mimi kukamatika kirahisi, na sasa baada ya akili yangu kurudi sawa kwa kuona sielewi tena somo basi BM alirudi kujieleza ili mama afanye mambo tena..hizi ni dhana tu sina hakika ila zenye mantiki mbele ya safari.
Yaani ni kwamba BM alinipenda, alipofika miji ya watu akazuzuka hakunitaka tena, lakini kule nasikia alikuja kuachwa kwa fedheha ndio akanikumbuka mimi wakati tayari nimeshabumburuka nateleza tu kama kambale[emoji1][emoji1][emoji1]
Kuhusu mtoto hata kama sio wangu alijua ntaamini tu maana jina anatumia langu.

Alipotoka huko moja kwa moja akataka tuonane, mizimu ya kwetu ikacheza kama Pele nikagoma[emoji23][emoji23][emoji23](mimi niligoma tu kwa sababu zangu kumbe ningekubali nilikuwa nakwisha, haya niliyajua baadae)
Sababu ya kugoma nilimwambia wewe mtu wa ajabu una mtoto miaka minne sijawahi kumuona na unaona kawaida tu badala yake unataka tuonane mimi na wewe.
Akanibembeleza sana nikamwambia kama unataka kuonana na mimi uje na mtoto, maana yangu nataka kumuona mtoto sio wewe, akakubali
Safari hii hakuwa jeuri sana kila kitu anakubali tu.

Kesho yake akaja na mtoto sikutaka kuonana naye nyumbani kwangu nilimwita tu somewhere(Mizimu iliendelea kucheza part yake[emoji1][emoji1]nasikia ningempeleka home nilikuwa narudi kulekulee kwenye kukamatwa) Baada ya miaka minne ndio wanandoa wanakutana[emoji2307]
Naita wanandoa kwa sababu hatukuwa tumevunja ndoa kisheria lakini kimsingi hakukuwa na ndoa.
Akaja na zawadi fulani za vijijini ni aina ya chakula sitaitaja ilikuwa kwenye kapu.
Kuhusu kwanini tumeonana hapo na sio kwangu kuna namna nilimpiga kiswahili.

Baada ya kutulia umakini wangu wote ulikuwa kwa mtoto, nikamtazamaa, kusema kweli hakuna nilichofanana nae hata kimoja, wakati nakuja kuonana naye nilishaongea na bi mkubwa akasema ukiona hamfanani angalia kitu fulani, kweli wazazi ni wazazi aisee, ndio maana BM n wazazi wake walikimbiza mtoto walijua wazazi wangi wakimuona tu watajua wamepigw au hawajapigwa.
Sisi vijana unaweza kubambikiwa mtoto, sio mama yako, akimshika mtoto tu anajua kila kitu na ndio ilikuwa maana nzima ya kupeleka mtoto kwa babu na bibi zake tangu enzi na ndio sababu kupigana hakukuwepo sana hata ukipigwa ujue wamekutunzia siri kwa sababu maalum sio kwamba hawajajua.

Nilimcheki yule dogo hakufanana na mimi, nikajipa imani wacha nisimhukumu, mradi mama yake anasema mtoto ni wangu acha niwe mtulivu nikiamini kufanana sio ishu sana, basi bwana baada ya stori mbili tatu nikaona mtu anaenda kwa magoti ananiomba nimsamehe ulikuwa ujana utoto tu kama vipi tumalize tofauti zetu tulee mtoto.

Hapa utajiuliza ulikuwa utoto tu upi? Kunijibu dry? Kunitoroshea mtoto? Kunichukulia poapoa? Hapana hapa unapata jibu kwamba utoto wenyewe ulikuwa kupigisha nje. Na sasa kaachwa
Nilimwangalia tu sikumjibu nikamuinua, akajua yameisha si sinaga ujanja kwake.
Tukaendelea na maongezi baadae tukaagana, akataka kunipa ile zawadi kikapuni nikagoma[emoji23][emoji23][emoji23] mizimu ilichukua nafasi yake tena, sijui kwanini mwanzo ilinitelekeza, kuna sababu nilimpa ikabidi arudishe kwa dada yake

Inasemekana ningepokea ile zawadi sasa ndio nilikuwa namalizwa kabisa, sijui ni kweli maana haya naambiwa tu baadae kabisa tena na mtu mwingine kabisa sema mi sio mtu wa maimani inawezekana aliyasema kwa interest zake tu maana nae nina stori nae


Tunaendelea kuweka kumbukumbu


NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI!
Samahani mkuu naomba unisaidie unaangalia nn ili kujua mtt ni wako au umepigwa ikitokea hujafanana nae? Maana naona umelisema juu juu, utakua umenisaidia sana mkuu.
 
Kutumia cheti cha ndoa ambayo imeshavunjwa kujipatia manufaa hapo kuna elements za jinai.

Kwenye issue ya kusajili talaka Rita, ni bora ukatafuta mwanasheria aliye karibu nawe akusaidie.
Asante
 
Back
Top Bottom