mFuKuZa nDoTo
JF-Expert Member
- Jan 17, 2021
- 492
- 639
- Thread starter
-
- #121
Kuna mengine nayajibia kwenye comments na watu hawasomiSi kuna sehem alisema kua anahisi yawezekana mwanzo alifanyiwa mambo kidogo
[emoji23][emoji23][emoji23] jamani pooleee. Pole sana. Ndo huwa ilivyo. Mapenz ni upofu sikulaumuSio sasa ni miaka kadhaa nyuma imeshapita, haya nimekuwa na jeuri ya kuyasema kwa uhuru na amani sasa hivi.
Kwa Kipindi kile sikuwa na uwezo huo, maumivu niliyokuwa nayasikia sio ya kawaida, sasa ndio mfano nikueleze kama hivi halafu uniambie hakuna mwanamke hapo nilikuwa naumia sanaaa ndio sababu sikuwa nasema kwa mtu ilikuwa vita ya mimi na nafsi yangu tu
Yaani nilichokuwa nataka kusikia ni kupendwa (ambako nako sikuwa nikipendwa) nilichokua nataka kusikia kwa watu ni angalau kuitwa mume wa BM nikisikia chochote hata mtu aniulize nasikia mmeachana basi naumia kweli kweli
[emoji1][emoji1][emoji1]Kile kipindi kimeniimarisha sana
Noma sana, huyu kiumbe alizaliwa maalum (special) kukutesaSEHEMU YA 8:
Kabla sijaendelea mbele kuna kitu nilisahau kukisema, ili kukazia hoja yangu kwamba mtoto sio wangu.
Tunajua kufanana kwa mtoto na mzazi sio lazima lakini je, inawezekana mtoto asifanane na wazazi wote wawili? Yaani hafanani na baba wala mama[emoji1][emoji1][emoji1] hapa nikajua kuna mtu wa tatu ndiye kafanana nae.
Tuendelee tulipoishia, Baada ya kupitia uzi wa Mzee Iringa Native akitafuta wanae na akionesha majuto ya hali ya juu ikaanza kama kunigusa gusa hivi, wakati nasoma ilikuwa 2019 december nikajiambia nitaanza mwaka kwa kuwatafuta hawa watu ili kama vipi niendelee kuhudumia mtoto.
Nikatafuta namba zake maana nilishazifuta kabisa, nikazipata nikampigia
Tukaongea tukaelewana, yaani yeye hanaga mpango na mimi hata nikikaa kimya miaka kibao, nikirudi ananipokea tu
Nikagundua huyu ananipokea ili anipige hela lakini masuala ya mtoto kuna mtu(Baba Mtoto) wanashauriana naye
Kufupisha tu stori baada ya kuwa nimejirudi na sasa nawasiliana nao vizuri nikamwambia nahitaji huyo dogo aje anitembelee nyumbani ili kujenga mazingira ya kujuana na nduguze nikapigwa chenga nyingiii baadae akakubali likizo atakuja kwa muda mfupi, lakini pia nikamwambia anatakiwa afike mpaka kwetu maana babu zake wananidai sana.
Kwa bahati nzuri au mbaya korona ikatuvamia hiyo 2020 mwanzoni, wakafunga shule, haraka nikamwambia kwa kuwa wana likizo ndefu sana naona nimchukie, nilipigwa chenga kali sana nikaambiwa sijui kachukuliwa na nani kwenda wapi sijui
Anyway nilichojua hapa nimekataliwa tu..sasa mimi baba yake nakataliwaje
Tutaendelea
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]Noma sana, huyu kiumbe alizaliwa maalum (special) kukutesa
SEHEMU YA 8:
Kabla sijaendelea mbele kuna kitu nilisahau kukisema, ili kukazia hoja yangu kwamba mtoto sio wangu.
Tunajua kufanana kwa mtoto na mzazi sio lazima lakini je, inawezekana mtoto asifanane na wazazi wote wawili? Yaani hafanani na baba wala mama[emoji1][emoji1][emoji1] hapa nikajua kuna mtu wa tatu ndiye kafanana nae.
Tuendelee tulipoishia, Baada ya kupitia uzi wa Mzee Iringa Native akitafuta wanae na akionesha majuto ya hali ya juu ikaanza kama kunigusa gusa hivi, wakati nasoma ilikuwa 2019 december nikajiambia nitaanza mwaka kwa kuwatafuta hawa watu ili kama vipi niendelee kuhudumia mtoto.
Nikatafuta namba zake maana nilishazifuta kabisa, nikazipata nikampigia
Tukaongea tukaelewana, yaani yeye hanaga mpango na mimi hata nikikaa kimya miaka kibao, nikirudi ananipokea tu
Nikagundua huyu ananipokea ili anipige hela lakini masuala ya mtoto kuna mtu(Baba Mtoto) wanashauriana naye
Kufupisha tu stori baada ya kuwa nimejirudi na sasa nawasiliana nao vizuri nikamwambia nahitaji huyo dogo aje anitembelee nyumbani ili kujenga mazingira ya kujuana na nduguze nikapigwa chenga nyingiii baadae akakubali likizo atakuja kwa muda mfupi, lakini pia nikamwambia anatakiwa afike mpaka kwetu maana babu zake wananidai sana.
Kwa bahati nzuri au mbaya korona ikatuvamia hiyo 2020 mwanzoni, wakafunga shule, haraka nikamwambia kwa kuwa wana likizo ndefu sana naona nimchukie, nilipigwa chenga kali sana nikaambiwa sijui kachukuliwa na nani kwenda wapi sijui
Anyway nilichojua hapa nimekataliwa tu..sasa mimi baba yake nakataliwaje
Tutaendelea
Kuandika si mchezo mzee!! Hawa jamaa wanajitahidi sana kutoa muda wao.Kwanini now watu wa JF mkianza kusimulia kitu mnaweka robo robo??
inakata stimu sana
Kuandika kazi sana, huo moyo anaweza kuwa nao ambaye anafanya biasharaKwanini now watu wa JF mkianza kusimulia kitu mnaweka robo robo??
inakata stimu sana
Inawezekana hii?Hiyo talaka unasajili Rita mchezo umekwisha.
Ndio nenda Rita, nakala yako ya hukumu, kuna fomu utajaza, na ada unalipia. Umemaliza.Inawezekana hii?
Kwahiyo hapo akitumia tu kesi ya madai inamhusu sio?Ndio nenda Rita, nakala yako ya hukumu, kuna fomu utajaza, na ada unalipia. Umemaliza.
ChaiWatu wa Jamii Forum Salaam, Naitwa Mfukuza Ndoto, Nina umri wa katikati ya ujana naishi mkoa fulani kanda ya kati. Basi bwana mnamo mwaka fulani nikiwa na 20+yrs nilitokea kumpenda binti fulani toka nyanda za juu kusini, binti huyo alikuwa mwanafunzi wakati huo katika chuo fulani hapa mjini. Namaanisha alikuja tu kwa ajili ya masomo.
Tukapendana, kwa kawaida huwa nikishaingia kwenye mahusiano huwa nadumu na kutulia ndio maana mpak sasa sina rekodi ya mtoto wa mtu niliyempotezea muda halafu nikamuacha, sina machozi ya mwanamke yeyote yanayoniandama zaidi wote hujutia na hicho ndio nilichokipanga kwenye maisha yangu mwanamke akitaka kupendwa atapendwa ashindwe yeye tu sipendi lawama.
Kabla yake nikiwa mwanafunzi miaka ya 2000's nilipoingia tu kidato cha kwanza nikapendwa na kabinti fulani(Na desturi yangu huheshimu sana hisia za mwanamke, yaani siingii kwenye mahusiano bila mwanamke mwenyewe kuonyesha interest na mimi nami nikiridhika nae anapitishwa. Hapa nazungumzia mapenzi sio ngono kwa maana ya tamaa za mwili, nikitamani kuna sehemu zinajulikana na mabaharia hujipoza maisha yanaendelea
Kwahiyo kwenye maisha yangu nimepitia mahusiano yasiyozidi matatu, acha wale wa kushare nao tu shuka, tukiwataja tutajaza kurasa za Jf.
Kwahiyo baada ya kabinti kunipenda hiyo ni pre-form one mpaka tunaanza form one mpaka kidato cha nne tulikuwa wapenzi na shule nzima ilijua hilo lakini cha ajabu hatukuwahi kufanya mapenzi kabisa,
Ilitokea hivyo kwa sababu kuu mbili, kwanza tulikuwa wadogo sana nadhani nilikuwa na miaka 14(kwa mwanaume wakati huo nilikuwa mdogo sana) na yeye alikuwa mdogo zaidi, pili kwa wakati huo mpaka umvue nguo mwanamke ilikuwa shughuli, sio kama sasa katika umri huo kijana anazijua tayari na kama binti tayari anazijua P2.
Kuna wakati nilikuwa naazima mageto ya washkaji tunakutana huko na kabinti basi washkaji wanajua nimemaliza kazi kumbe nimegomewa na mimi ujanja sina sana[emoji1][emoji1] sababu ya tatu sitaitaja lakini ndio kubwa zaidi
Mimi na yule mwanadada tumekuja kuvunjana 'Upya' tukiwa tumeshamaliza form four tumefeli tuko mtaani, kwa kweli yeye na mimi wote tulikuwa wageni wa mambo kwahiyo tulifunguliana
Nayasema haya ionekane namna gani huwa siachi mwanamke nikishaingia nae kwenye mahusiano mpaka yeye aje kuharibu na ajilaumu mwenyewe na akishaharibu hata aje na Fiat (gari za zamani) huwa sibadili msimamo hata aroge vipi, kwa kuwa naamini ukishafanywa mpumbavu mara moja ukasamehe uwezekano wa kuonekana boya ni mkubwa na atakuumiza mara ya pili na zaidi
Kingine naamini wanawake ni wengi, shida ya nini kurudiana na mmoja aliyekuumiza? Sio kweli ile dhana ya kwamba umeandikiwa utaishi nae kumbuka binadamu wawili wawili kama uliandikiwa kuishi na huyo akizingua kuna aliyefanana tena na huyo huyo utampata, na ili tupeane masomo asijeenda kusumbua wengine unamgomea msamaha akienda kwa mwingine hatasumbua labda awe amepinda tu.
Kilichoniachanisha na huyu bikra mwenzangu nikiwa mtaani nimechoka sasa napigwa na maisha kotekote akanifuata jamaa mmoja, ni wale unakuta pale mjini ana sifa ya ukicheche(umalaya)
Zamani ilikuwa kama sifa, kila mji palikuwa na watu sifa yao ni hakuna demu anapindua kwao, na mara nyingi unakuta ni sababu ya maisha mazuri yake au ya familia yake, akishamudu kuwa na kageto na uwezo wa kubadili mavazi kidogo basi mademu wanapishana. Huyu jamaa akaniuliza kama huyo demu ni demu wangu(nafikiri aliambiwa kwa busara akaona asije kuingia anga zangu) basi mimi ile kujivunga eti nampima imani demu nikakataa ili kama atatongozwa akatae mwenyewe
Bwana wee sijakaa sawa demu ananipigia simu ananitukana kwa namba mpya sielewi sababu nini, huku akiwa na wifi zake(dada wa yule jamaa) kuja kufuatilia jamaa keshamtindua dah nikadata maana home kwetu walimjua mpaka dada zangu walimjua alikuwa anafika mpaka home, miaka zaidi ya minne ilikuwa lazima ajulikane. Na pia alipoanza kutoka na huyo jamaa dada zangu walijua ikawa fedheha sana, nikawaza, nikachanganyikiwa kwa aibu sio kwa sababu siwezi kupata mwingine.
Nikapiga moyo konde nikamove on, Mungu si athumani nikaotea kibarua kidogo, aliposikia akaanza kujirudisha.
Sikumtukana, sikumjibu vibaya nikamwangalia tu nikaachana nae mpaka leo ananiona tu mitandaoni.
Huyo ni mmoja kati ya hao watatu
Sasa tuendelee na huyu binti mwanafunzi wa chuo ngazi ya chini ya shahada...huyu nilikutana naye katika ofisi moja ya serikali ambapo alimsindikiza mwenzake na mimi ambaye mimi nilifahamiana nae, baada ya kusalimiana na kukaa wote kwenye benchi kwa muda mrefu tukisubiri huduma tukazoeana(na huyu binti mlengwa) tukabadilishana namba.
Nilipoondoka yule rafiki yake akanitanabaisha kwamba rafiki yake (Binti Mlengwa tumwite BM) anaonyesha namna fulani ya kunikubali/kunipenda/kunizimikia[emoji23][emoji23]sasa kama ilivyo desturi yangu huwa sidharau hisia za mwanamke awe amenipenda au ametamani kushare shuka tu na mimi lazima nimtimizie adhma yake.
Note: Haya hayatokei ikiwa nina mwanamke tayari ninayedumu nae, ni pale napokuwa 'Loose ball' na pia isitafsirike kwamba labda nina mvuto saana hapana hii hutokea kwa yeyote maana wanawake wana sababu nyingi za kupenda mwanaume kama ambavyo wanaume tuna sababu nyingi tu za kuvutiwa na mwanamke.
Tuendelee, nilipopata ujumbe ule nikajua cha kufanya hapa ni kuanza ukaribu tu mwanamke akishakupenda hawezi kukuanza lakini ukimsalimi siku ya kwanza, ukamchatisha bize siku mbili weekend inayofuata ukimtaka appointment atakuja tu hata kama atazuga kidogo, Basi, nikaweka mazingira na uhusiano ukaanza kwa namna hiyo
Mwanzo sikukapenda baadae nikakazoea basi nikakapenda, sijui kalinifanya nini nakiri ndio mwanamke nimewahi kumpenda haijatokea tenaaaaa
Visa vichache vilitokea wakati ule vilifaa kabisa kumuacha sikuviona leo hii ndio nayaona na kujiuliza hivi nilikuwa mimi kweli yule? Mfano kuna wakati nilifuma meseji kwenye simu yake ni dhahiri ilikuwa ya mwanaume na ana mahusiano naye nikafunika kombe mwanaharamu apite
Kuna wakati msanii mmoja alikuja kupiga show kwenye ukumbi fulani sikwenda lakini kuna jamaa akaropoka kwamba alimuona usiku huo huyo binti na kutoka chuoni mpaka mjini ni umbali ambao sio wa kurudi usiku, sasa alilala wapi hicho kiulizo kingine, lakini wakati naoambiwa huyo binti alikuwa club mimi nimeonge nae sana usiku mpaka kwenye saa tano au sita kwa akili yangu ndogo wakati ule sikumuamini jamaa nikafikiri nimemfananisha....maisha yakaendelea
Nilikapenda sana kale kabinti, kuna wakati nilitishia kukaacha kakalia usiku kucha, nikajisemea mwanamke si ndo huyu bwanaaa...nikadumu nae kwa miaka mitatu mpaka anamaliza, kilichonipa imani kwamba mke nimepata ni wakati alipomaliza shule, wanavyuo wengi wakimaliza na mapenzi wanaondoka nayo makwao lakini huyu BM aliendelea "ku-keep in touch" mpaka nikaanza kunenepa, huko huko aliko bado mawasiliano yalikuwa mazuri huku akija kunipikia kila alipopata nafasi
Hata wenzangu waliokuwa na wanawake pale chuoni ambao walishaachana na wapenzi wao waliamini nimependwa haswaaa na mimi ukinipenda nakupenda nataka nini kingine.
Ndio ikawa hivyo, akamaliza akaondoka, akaanza kudai ndoa, basi mi ndo kabisaa naona nimepata mke mwema, nikachukua likizo nikampeleka nyumbani kumtambulisha, kwanza nikaanza kwao kisha kwetu.
Nyumbani kwetu walimpenda sana, she was hard working na mrembo kiasi, tukiwa hapo nyumbani nafasi za ajira zikatoka akaajiriwa mkoa fulani kanda ya magharibi
Wakati nampeleka nyumbani ilikuwa mnamo August ya mwaka huo, kufika December ndio picha picha zilipoanza...
.....Wacha nichukue mapumziko....leo ndio nimeona ugumu wa kuandika...wale wazee wa itaendelea hawafanyi kwa makusudi inawalazimu kupumzika
Will Be Back!!!
Samahani mkuu naomba unisaidie unaangalia nn ili kujua mtt ni wako au umepigwa ikitokea hujafanana nae? Maana naona umelisema juu juu, utakua umenisaidia sana mkuu.SEHEMU YA 5:
Mwenendo mzima wa BM, Mwenendo mzima wa ujauzito wake na mwenendo mzima wa kujifungua kwake na ushirikishwaji wangu kwake mpaka hapo ulishanipa mashaka sana
Kama mtoto ni wangu kwanini mambo yote haya yanatokea? Kama nilihudumia ujauzito mwanzo mwisho hasira zao/zake juu yangu zinatoka wapi? Bado haitoshi kunifanya baba wa mtoto? Iwe nimetoa mahari au sijatoa madhali sikukaa mbali na mimba kwanini nitengwe hivi?
Anyway wakati wa ujauzito nilijua labda hasira za mimba sasa mbona mambo yanaendelea mpaka baada ya kujifungua?
Taa nyekundu ikazidi kuangaza ndani ya ubongo wangu, isisahaulike stress ziliendelea kuniandama vilivyo, watu wangu wa karibu, ndugu na jamaa wakashangazwa na mabadiliko..lakini kwa mbaali nikaanza kuzisikia roumours kwa watu wakisema hali hii imepelekewa na kuachwa kwangu na mwanamke huyo, watu walijuaje? Nikaanza kunote kitu kwamba inawezekana yeye ndio anayasema haya kwa watu. Hali ilikuwa mbaya sana, najifungia ndani tu kama siko kazini. Huko ndani ni mimi na mitungi tu.
Kwa mara ya kwanza ni wakati huu sikupata usingizi, nilikuwa naweza kukaa macho tu tangu giza linaingia mpaka linapotea siku ya pili. Sikuutamani usiku tena, ni angalau mchana ningekutana na watu nikapoteza mawazo lakini giza likiingia nikabaki peke yangu ilikuwa ni mawazo mwanzo mwisho, mimi na mawazo, mawazo na mimi.
Ikafikia kipindi nikafreeze nikakaa kimya nikakubali matokeo, kwamba hapa sina changu tena. Kilichobaki ikawa kupambana kurudi katika hali yangu ya kawaida. Nilipambana sana mpaka angalau nikawa sawa kidogo.
Mwaka ukaisha, bila mawasiliano yoyote as if kule sina damu yangu, yaani hata simu ya bahati mbaya haikuwepo hapo nikaamini kuna mwenye mtoto anahudumia
Siku moja akanitumia meseji anasema nyumbani kwao wanataka kujua hatima yangu na yeye maana pako kimya tu. Nikapiga akili ya haraka nikaona huo ni mtego, kwao wanasubiri mimi niseme simtaki binti yao ili ionekane mimi ndio nilimuacha na kama kuna madai kwao nisidai, mimi nikamjibu hatima yetu alishaiamua yeye BM hapo kinachofanyika ni kunitega tu.
Kuna kitu akasema sasa kukaa kwako kimya ni kama namfunga yeye(maana yake ni iwapo anataka kuolewa kwingine nitoe go ahead) hapo nikajihakikishia huyu ana mtu mwingine sasa anataka kuolewa
Nikamjibu sijamfunga kama anataka kuolewa anaweza kuolewa tu maan mimi sidai kitu kwao biashara imeisha na kiukweli sikumhitaji tena hata bure.
Akauliza kimtego na mtoto je, nikamjibu nimewapa zawadi, akasema atawaambia yote hayo. Tukamaliza hivyo
Ikumbukwe ni mwaka sasa sijawahi kumuona huyo mtoto, sio mimi wala wazazi wangu.
Kiutaratibu baada ya kujifungua alitakiwa amlete kwangu nimuone, kisha awapelekee babu zake, kama mimi na yeye tulikuwa na matatizo angewapelekea hata wazee wangu, hakufanya hivyo. Na kwao wanaona sawa wala hawakujihangaisha kumshauri juu ya hilo.
Siku tuliyoongea hayo nikafuta na namba zake moja kwa moja, miaka ikakatika nikaja kusikia alipeleka kijijini mtoto akiwa na mwaka mmoja yeye akarudi shule, nikawaza sana huyu mwanamke wa aina gani? Mtoto wa mwaka mmoja kumpeleka kijijini kisa shule mbona shule zipo tu si angesubiri? Sikujali nikaachana nao
Ikawa mwaka wa kwanza, wa pili na wa tatu, mtoto alishakuwa na miaka minne namsikia tu. Mimi nikaendelea na mambo mengine. Nikaanza kusikia kwa watu wa karibu vitu ambavyo ni kama kuna kitu huwa wanaongea nae kinachofanana na kurudiana na huyo mwanadada. Kuna jamaa yangu mlevi siku moja alilewa katika stori akasema utarudiana tu na mama fulani? Yaani BM nikamwambia kwa mapito aliyonipitisha haitawezekana
Akasema tutaona mtoto atawaunganisha tu, kusema kweli mtoto bado nilikuwa namhitaji sio mama yake .
Watu waliamini kweli naweza kumrudia sababu walijua nampenda sana sina ujanja, hata yeye alijua hivyo. Inasemekana hata alipoenda shule alijua mimi sina ujanja wa kumove on atanikuta tu, anakuja kumaliza shule anaanza harakati anakuta mimi nilishapambisha mapenzi kwingine.
Anyway baada ya kuanza kusikia kwa watu vitu vinavyofanana na kurudiana nikaanza kujiandaa kisaikolojia nilijua ni yeye tu anayasema haya. Kweli bwana siku moja akanitumia meseji yuko njiani anataka tuje tuonane, nikamwambia kuna tatizo gani? Akasema tutaongea akifika.
Nikamwambia haiwezekani akasema tuache tofauti zetu bhana turudiane tutunze mtoto. Halafu anaongea kirahisi tu kwa kuwa alijua mimi ni wake tu nampenda sana. Hakujua mambo yalibadilika kutoka mapenzi mpaka chuki.
Mpaka wakati huoa alikuwa ndio binadamu namchukia kuliko wote, yeye hakujua hilo
Kiukweli nilimgomea.
Alipofika akapitiliza chuo alichokuwa anasoma akadai anafuata cheti chake, mimi nikajiuliza huyu cheti alishachukua ni cheti gani amefuata? Nikanyamaza
Jioni hiyo ananipigia simu anajichekesha chekesha kisha akanipa mama mmoja niongee nae, nikaongea nao kidogo nikakata.
Huyu mama tangu akiwa anasoma walikuwa wanaitana mama wa hiyari, huyu mama ilifikia hatua akihitaji kitu ananipigia mimi niko mjini yeye bush namuagizia.
Kuna dhana nyingi zinatembea hapa, inawezekana huyu mama ndio aliwezesha mchongo mzima wa mimi kukamatika kirahisi, na sasa baada ya akili yangu kurudi sawa kwa kuona sielewi tena somo basi BM alirudi kujieleza ili mama afanye mambo tena..hizi ni dhana tu sina hakika ila zenye mantiki mbele ya safari.
Yaani ni kwamba BM alinipenda, alipofika miji ya watu akazuzuka hakunitaka tena, lakini kule nasikia alikuja kuachwa kwa fedheha ndio akanikumbuka mimi wakati tayari nimeshabumburuka nateleza tu kama kambale[emoji1][emoji1][emoji1]
Kuhusu mtoto hata kama sio wangu alijua ntaamini tu maana jina anatumia langu.
Alipotoka huko moja kwa moja akataka tuonane, mizimu ya kwetu ikacheza kama Pele nikagoma[emoji23][emoji23][emoji23](mimi niligoma tu kwa sababu zangu kumbe ningekubali nilikuwa nakwisha, haya niliyajua baadae)
Sababu ya kugoma nilimwambia wewe mtu wa ajabu una mtoto miaka minne sijawahi kumuona na unaona kawaida tu badala yake unataka tuonane mimi na wewe.
Akanibembeleza sana nikamwambia kama unataka kuonana na mimi uje na mtoto, maana yangu nataka kumuona mtoto sio wewe, akakubali
Safari hii hakuwa jeuri sana kila kitu anakubali tu.
Kesho yake akaja na mtoto sikutaka kuonana naye nyumbani kwangu nilimwita tu somewhere(Mizimu iliendelea kucheza part yake[emoji1][emoji1]nasikia ningempeleka home nilikuwa narudi kulekulee kwenye kukamatwa) Baada ya miaka minne ndio wanandoa wanakutana[emoji2307]
Naita wanandoa kwa sababu hatukuwa tumevunja ndoa kisheria lakini kimsingi hakukuwa na ndoa.
Akaja na zawadi fulani za vijijini ni aina ya chakula sitaitaja ilikuwa kwenye kapu.
Kuhusu kwanini tumeonana hapo na sio kwangu kuna namna nilimpiga kiswahili.
Baada ya kutulia umakini wangu wote ulikuwa kwa mtoto, nikamtazamaa, kusema kweli hakuna nilichofanana nae hata kimoja, wakati nakuja kuonana naye nilishaongea na bi mkubwa akasema ukiona hamfanani angalia kitu fulani, kweli wazazi ni wazazi aisee, ndio maana BM n wazazi wake walikimbiza mtoto walijua wazazi wangi wakimuona tu watajua wamepigw au hawajapigwa.
Sisi vijana unaweza kubambikiwa mtoto, sio mama yako, akimshika mtoto tu anajua kila kitu na ndio ilikuwa maana nzima ya kupeleka mtoto kwa babu na bibi zake tangu enzi na ndio sababu kupigana hakukuwepo sana hata ukipigwa ujue wamekutunzia siri kwa sababu maalum sio kwamba hawajajua.
Nilimcheki yule dogo hakufanana na mimi, nikajipa imani wacha nisimhukumu, mradi mama yake anasema mtoto ni wangu acha niwe mtulivu nikiamini kufanana sio ishu sana, basi bwana baada ya stori mbili tatu nikaona mtu anaenda kwa magoti ananiomba nimsamehe ulikuwa ujana utoto tu kama vipi tumalize tofauti zetu tulee mtoto.
Hapa utajiuliza ulikuwa utoto tu upi? Kunijibu dry? Kunitoroshea mtoto? Kunichukulia poapoa? Hapana hapa unapata jibu kwamba utoto wenyewe ulikuwa kupigisha nje. Na sasa kaachwa
Nilimwangalia tu sikumjibu nikamuinua, akajua yameisha si sinaga ujanja kwake.
Tukaendelea na maongezi baadae tukaagana, akataka kunipa ile zawadi kikapuni nikagoma[emoji23][emoji23][emoji23] mizimu ilichukua nafasi yake tena, sijui kwanini mwanzo ilinitelekeza, kuna sababu nilimpa ikabidi arudishe kwa dada yake
Inasemekana ningepokea ile zawadi sasa ndio nilikuwa namalizwa kabisa, sijui ni kweli maana haya naambiwa tu baadae kabisa tena na mtu mwingine kabisa sema mi sio mtu wa maimani inawezekana aliyasema kwa interest zake tu maana nae nina stori nae
Tunaendelea kuweka kumbukumbu
NIMEAMUA KUMKATAA MTOTO RASMI!
AsanteKutumia cheti cha ndoa ambayo imeshavunjwa kujipatia manufaa hapo kuna elements za jinai.
Kwenye issue ya kusajili talaka Rita, ni bora ukatafuta mwanasheria aliye karibu nawe akusaidie.