Tukitumia mfumo huu, hakika tutamaliza ajali za barabarani kwa Siku moja Tu

Tukitumia mfumo huu, hakika tutamaliza ajali za barabarani kwa Siku moja Tu

Umeongelea adhabu kubwa kubwq, lakini unajua hizi ajali nyingi zinatokea kwenye barqbara zipi? Mbona barabara ya dodoma arusha hazitokei hizo ajali? Barabatra hii ya dom arusha ni pana kiasi hata gari 3 zinapishana, na haina mashimo, licha ya uzembe wa baadhi ya madereva barabara zeru kwa kiasi kikubwa zinachangia ajali"
Hizo sio adhabu hapo kuna fidia na faini hizo ni haki kwa waathirika wa ajali. Serikali pia ni mwaathirika namba moja wa ajali, abiria pamoja na watembea kwa miguu bila kusahau wamiliki wa vyombo vya usafiri wote ni waathirika wa ajali.
 
Mauchawi
Ajali za mwaka huu zimetisha. December pekee kwa haraka zaidi ya 100 wamekufa kwenye barabara ya Dar-Arsh-Tarakea. Something must be done.
Mauchawi sometimes hawa wanene wana majambo yao dunia ina upande wa pili ambao sio poa
 
Aina za Uwajibikaji
1). Kwa mtu aliye gongwa na chombo
Mwathirika angelipwa fidia kulingana na viwango vilivyoainishwa (vifo, ulemavu wa kudumu, au majeraha).
Mmiliki wa chombo angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kusababisha ajali hiyo.
Hivi unajua kwanini faini huwa ni realistic na sio kuweka namba ambayo haina uhalisia ? Ni kwam,ba ukiweka vitu ambavyo havilipiki basi havitalipwa au watu kuhonga kidogo ili kupindisha haki..., Pia kumbuka haya mambo yanakuwa na Bima kwahio mwisho wa siku mmiliki yupo covered ila ukileta ubanaji mkubwa katika sekta ambayo UMMA umeshindwa kutoa huduma mwisho wa siku hizo sekta zitakufa.....


Sheria zipo na zifuatwe na katika Usafiri wa UMMA tuboreshe usafiri wa (SGR n.k.) wananchi wapate efficient, affordable alternative sio kuwaachia wabangaizaji (for profit) wanagombania abiria wachache sababu majority can not afford to move from A to B hivyo msimu wa sikukuu ndio kinabakia kipindi cha uchumaji cha hawa watu angalau kulipa mikopo yao...
 
Umezungumzia familia ya MTU akiyekufa ilipwe fidia 200-500 Ila Kwa Kwa aliyepata ulemavu alipwe mil 150-200.


Je umefikiria Kwa kina hapo ukipata ulemavu wa kudumu na ukifa wapi unabidi kulipwa fidia kubwa.?
 
Habari za jioni ndugu na marafiki,
Poleni sana kwa wote mnao endelea kuathirika na ajali zinazo endelea kutokea barabarani.

Hili jambo limelilazimu kukaa chini namimi nitoe mapendekezo yangu ili tuweze kutokomeza ajali zinazo endelea kumaliza ndugu na marafiki zetu.

Lakini kabla ya yote nimeona kwanza nilete pendekezo hili hapa jukwaani ili tuone jinsi ambavyo linaweza kufaa au kutofaa.

Kwanza kabisa naomba kuwasilisha kwamba ajali za barabarani huwa hazitokei kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya uzembe, kutokufuata sheria, na ukosefu wa tahadhari. Vyombo vya usafiri kama magari, mabasi, bodaboda, bajaji, na malori vinaweza kufananishwa na zana hatari kama visu, mapanga, au bunduki. Vyote vinahitaji uangalifu mkubwa ili visisababishe madhara.

Ili kumaliza ajali hizi, naomba kupendekeza mfumo huu madhubuti wa uwajibikaji unaolenga kuhakikisha kila mmiliki wa chombo cha usafiri anawajibika kwa matendo yake, huku akifuata sheria za usalama kwa umakini wa hali ya juu.

1. Uwajibikaji wa Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri
Mmiliki wa chombo cha usafiri alipaswa kubeba jukumu moja kwa moja kwa ajali yoyote inayosababishwa na chombo chake.

Aina za Uwajibikaji
1). Kwa mtu aliye gongwa na chombo
Mwathirika angelipwa fidia kulingana na viwango vilivyoainishwa (vifo, ulemavu wa kudumu, au majeraha).
Mmiliki wa chombo angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kusababisha ajali hiyo.

2). Kwa vyombo vilivyogongana
Kila mmiliki wa chombo angelipa fidia kwa abiria wake.
Kila mmiliki angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kushiriki katika ajali hiyo.

3). Kwa chombo kilichogonga kingine kikiwa kimesimama
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na kwa mwathirika wa chombo kilichokuwa kimesimama.
Pia atalipa faini ya TZS milioni 50 kwa uzembe wake.

4). Kwa chombo kilichogonga kingine kwa nyuma kikiwa kwenye mwendo
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na waathirika wa chombo kingine kilichoharibika.
Faini ya TZS milioni 50 ingelipwa na mwenye chombo kilichogonga.

2. Viwango vya Fidia kwa Waathirika wa Ajali

Ninapendekeza viwango vifuatavyo vya fidia

1). Kwa Vifo: Familia ya aliyefariki ingepokea fidia ya TZS milioni 250 hadi 500.

2). Kwa Ulemavu wa Kudumu: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 150 hadi 200, kulingana na athari za ulemavu wake kwa maisha ya baadaye.

3). Kwa Majeraha ya Kawaida: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 50 hadi 100, kutegemea gharama za matibabu na muda wa kupona.


3. Faini ya Kupata Ajali

Kwa kuwa ajali husababisha madhara makubwa kwa jamii na miundombinu:

Faini ya Lazima: Kila anayepata ajali angelipa TZS milioni 50, bila kujali hali ya ajali (iwe imeua au la, chombo kimeharibika au la).


4. Mfumo wa Bima ya Lazima

Ili kuhakikisha fidia na faini zinalipwa ipasavyo:

1). Kila mmiliki wa chombo angetakiwa kuwa na bima ya dhima kubwa inayoweza kufidia madhara makubwa ya kifedha.

2). Wamiliki wasio na bima inayokidhi viwango wangetozwa faini kubwa au magari yao kufungiwa.


5. Hatua za Nyongeza za Kuzuia Ajali

Ili mfumo huu ufanye kazi kwa ufanisi, hatua zifuatazo zingepaswa kuzingatiwa:

1). Ukaguzi wa Magari: Serikali ingefanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyombo vyote vya usafiri kuhakikisha vinakidhi viwango vya usalama.

2). Elimu ya Usalama Barabarani: Madereva na wamiliki wa vyombo vya usafiri wangeelimishwa kuhusu umuhimu wa kufuata sheria za usalama barabarani.

3). Adhabu Kali kwa Wakiukaji: Madereva na wamiliki wanaopatikana na hatia ya uzembe wanhepatiwa adhabu kali kama kufungiwa leseni au kifungo cha muda.


6. Faida za Mfumo Huu

1). Kuongeza Nidhamu na Uwajibikaji:
Wamiliki wa vyombo vya usafiri wangehakikisha vyombo vyao ni salama, na madereva wangekuwa makini zaidi barabarani.

2). Kupunguza Ajali kwa 100%: Kwa gharama kubwa ya fidia na faini, ajali zingepungua kwa kiwango kikubwa.

3). Kuimarisha Usalama wa Jamii: Barabara zingekuwa salama kwa kila mtumiaji wa barabara.

Kwa kutumia mfumo huu, tungepelekea kuondoka kwa uzembe barabarani, huku tukihakikisha kila anayehusika anawajibika kwa matendo yake. Tungeanza kutekeleza mfumo huu, hakika ajali za barabarani zingekuwa historia ndani ya muda mfupi!
Hizo hela zote ulizotaja serikali ilitakiwa izitumie kupanua miundombinu ya barabara na madaraja ili kuwapa wasafiri highway lanes zisizoingiliana. Walau njia 4 ambazo zimetenganishwa na zege katikati. Mbili za kwenda na mbili za kurudi kisha ungeshangaa rate ya ajali ambavyo zingepungua kwa kasi. Maboresho yanahitajika sababau watumiaji barabara wameongezeka ila serikali ime relax na plan zile zile za kikoloni.

Ajali nyingi za kwetu ni za magari kugongana uso kwa uso kutokana na ufinyu wa barabara na muingiliano wa moja kwa moja.
 
Hili pendekezo ni zuri sana na kwa kweli kwa kiasi kikubwa binafsi naamini linaweza kupunguza ajali hasa zinazotokana na uzembe zikabaki za kawaida

Kila ajali ikitokea huwa nawaza kitu kama hiki. Pengine ajali zinakuwa nyingi kwasababu hakuna uwajibikaji wa moja kwa moja kwa wamiliki na madereva.

Abiria akipata ajali kinachofuata ni kupewa pole ya mdomo tu kana kwamba amejisababishia yeye hata pale ambapo jeshi la polisi linasema ajali imesababishwa na uzembe

Ni muhimu pale ajali inapothibitika kuwa imesababishwa na uzembe wahusika wawajibike kwa kufidia abiria.
Mimi niko pale pale, miundombinu ndio shida. Barabara nyembamba halafu mnapishana bila barrier ndio shida. Mtu ana overtake bila kuona mbele kukitokea kuna gari ghafla kinaumana baaam!!! Head on Head collision. Hii ndio hufanya 90% za ajali.

Hakuna ajali nyingi za mtu kugonga nyuma gari lililoko mbele yake na hata ikitokea impact huwa sio fatal kama ajali za uso kwa uso.

Tizama miaka ya 2000-2015 ajali zilizokuwa zinatokea kipande cha kibaha-ubungo mara basi limegonga na kuua watu, linganisha na hali ya sasa. Yote ni sababu barabara ni pana na imetenganisha watumiaji. Ni nadra sana kusikia ajali sababu nyingi zilikuwa ni head on head collisions.

Jiulize what if Dar-Moshi njia ikawa multi lanes? Wajaribu hilo waone kama watasikia ajali za ajabu ajabu tena. Hakuna cha fine wala fidia suluhisho ni hili.
 
Waasisi wa Tz wamekufa na siri nzito kuhusu hii nchi hususani Ajali za mwisho wa mwaka, mwenge, na watz kuwa na akili fulani hivi iliyolala

Nadhani kuna k2 nyuma ya pazia
 
Bado adhabu aina ya faini siyo suluhisho.

SULUHISHO NI
CONTROL OF TRAFFIC LANES BY ELECTRONIC SENSORS,
Gari zote zisajiliwe electronically using specific road lane sensing technology, ambapo Kila road user (driver) akiingia kwenye gari yeyote atapaswa kuifix driving licence yake kwenyde slot maalumu ya gari anayoitumia.
Wakati wa kutumia Barabara au lanes zake,signs usage zitaku-cross check, ukifanya makosa, zitaku-bill penalty, ukizidisha certain billing mark, utapunguziwa validity of your licence, na pia kadri unavotumia vizuri ikuongezee very little credit marks.
Na pia iweze kukufutia (block) licence Yako.
Hiyo itawapunguzia majukumu traffic hata masaa au maeneo ambayo hawapo.
Inaonekana ni mfumo wa gharama, lakini hata maisha ya watu kupotea plus mishahara na usalama wa traffic ni gharama sana.
Huo itakuwa alternate approach but not the precise one.

Ni sawa na shule ikiwa haifaulishi ukaamua kuibomoa badala ya kubadilisha Management na walimu. Au timu ikiwa na wachezaji wabovu kisha wewe unafukuza kocha wa timu ukitegemea mabadiliko badala ya kusajili upya.
 
Huo itakuwa alternate approach but not the precise one.

Ni sawa na shule ikiwa haifaulishi ukaamua kuibomoa badala ya kubadilisha Management na walimu. Au timu ikiwa na wachezaji wabovu kisha wewe unafukuza kocha wa timu ukitegemea mabadiliko badala ya kusajili upya.

Ushauri wa kupanua na kuboresha miundombinu ndo suluhisho.

Hiyo mbinu ya kuwakamua watu pesa ni mbinu ya kijima hata Magufuli alijaribu ikamletea matokeo hasi .



Maana kuna ajari ambazo zinatokana na barabara (miundombinu)
 
Bado adhabu aina ya faini siyo suluhisho.

SULUHISHO NI
CONTROL OF TRAFFIC LANES BY ELECTRONIC SENSORS,
Gari zote zisajiliwe electronically using specific road lane sensing technology, ambapo Kila road user (driver) akiingia kwenye gari yeyote atapaswa kuifix driving licence yake kwenyde slot maalumu ya gari anayoitumia.
Wakati wa kutumia Barabara au lanes zake,signs usage zitaku-cross check, ukifanya makosa, zitaku-bill penalty, ukizidisha certain billing mark, utapunguziwa validity of your licence, na pia kadri unavotumia vizuri ikuongezee very little credit marks.
Na pia iweze kukufutia (block) licence Yako.
Hiyo itawapunguzia majukumu traffic hata masaa au maeneo ambayo hawapo.
Inaonekana ni mfumo wa gharama, lakini hata maisha ya watu kupotea plus mishahara na usalama wa traffic ni gharama sana.
Mkuu wewe ndiwe ungetakiwa utuletee uzi maana wazo lako ni bora kuliko la mleta uzi
Tunahitaji teknolojia zaidi ili kumaliza changamoto zetu

Ajali, rushwa, umaskini, magonjwa, na mambo mengine kama hayo tunahitaji teknolojia zaidi hili kukabiliana nayo.
 
Ongeza hizi muhimu.

1. Serikali ijenge miundombinu mbadala ya usafiri wa treni kwenda mikoa yote.
Hili litapunguza wingi wa malori, wingi wa magari ya abiria na wingi wa magari binafsi.

2. Barabara za lami ziwe dual carriage way/divided highway, wanaoelekea upande mmoja wawe na barabara yao na sio hizi za sasa zilizotengwa na mstari kati.
Kwa kuanzia ujenzi ufanywe kwanza maeneo ambayo ni hatarishi. (Kama walivyofanya Inyala Mbeya).

3. Kupunguza manual intervention na kukumbatia teknolojia kwa magari na barabara...
 
Habari za jioni ndugu na marafiki,
Poleni sana kwa wote mnao endelea kuathirika na ajali zinazo endelea kutokea barabarani.

Hili jambo limelilazimu kukaa chini namimi nitoe mapendekezo yangu ili tuweze kutokomeza ajali zinazo endelea kumaliza ndugu na marafiki zetu.

Lakini kabla ya yote nimeona kwanza nilete pendekezo hili hapa jukwaani ili tuone jinsi ambavyo linaweza kufaa au kutofaa.

Kwanza kabisa naomba kuwasilisha kwamba ajali za barabarani huwa hazitokei kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya uzembe, kutokufuata sheria, na ukosefu wa tahadhari. Vyombo vya usafiri kama magari, mabasi, bodaboda, bajaji, na malori vinaweza kufananishwa na zana hatari kama visu, mapanga, au bunduki. Vyote vinahitaji uangalifu mkubwa ili visisababishe madhara.

Ili kumaliza ajali hizi, naomba kupendekeza mfumo huu madhubuti wa uwajibikaji unaolenga kuhakikisha kila mmiliki wa chombo cha usafiri anawajibika kwa matendo yake, huku akifuata sheria za usalama kwa umakini wa hali ya juu.

1. Uwajibikaji wa Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri
Mmiliki wa chombo cha usafiri alipaswa kubeba jukumu moja kwa moja kwa ajali yoyote inayosababishwa na chombo chake.

Aina za Uwajibikaji
1). Kwa mtu aliye gongwa na chombo
Mwathirika angelipwa fidia kulingana na viwango vilivyoainishwa (vifo, ulemavu wa kudumu, au majeraha).
Mmiliki wa chombo angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kusababisha ajali hiyo.

2). Kwa vyombo vilivyogongana
Kila mmiliki wa chombo angelipa fidia kwa abiria wake.
Kila mmiliki angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kushiriki katika ajali hiyo.

3). Kwa chombo kilichogonga kingine kikiwa kimesimama
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na kwa mwathirika wa chombo kilichokuwa kimesimama.
Pia atalipa faini ya TZS milioni 50 kwa uzembe wake.

4). Kwa chombo kilichogonga kingine kwa nyuma kikiwa kwenye mwendo
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na waathirika wa chombo kingine kilichoharibika.
Faini ya TZS milioni 50 ingelipwa na mwenye chombo kilichogonga.

2. Viwango vya Fidia kwa Waathirika wa Ajali

Ninapendekeza viwango vifuatavyo vya fidia

1). Kwa Vifo: Familia ya aliyefariki ingepokea fidia ya TZS milioni 250 hadi 500.

2). Kwa Ulemavu wa Kudumu: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 150 hadi 200, kulingana na athari za ulemavu wake kwa maisha ya baadaye.

3). Kwa Majeraha ya Kawaida: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 50 hadi 100, kutegemea gharama za matibabu na muda wa kupona.


3. Faini ya Kupata Ajali

Kwa kuwa ajali husababisha madhara makubwa kwa jamii na miundombinu:

Faini ya Lazima: Kila anayepata ajali angelipa TZS milioni 50, bila kujali hali ya ajali (iwe imeua au la, chombo kimeharibika au la).


4. Mfumo wa Bima ya Lazima

Ili kuhakikisha fidia na faini zinalipwa ipasavyo:

1). Kila mmiliki wa chombo angetakiwa kuwa na bima ya dhima kubwa inayoweza kufidia madhara makubwa ya kifedha.

2). Wamiliki wasio na bima inayokidhi viwango wangetozwa faini kubwa au magari yao kufungiwa.


5. Hatua za Nyongeza za Kuzuia Ajali

Ili mfumo huu ufanye kazi kwa ufanisi, hatua zifuatazo zingepaswa kuzingatiwa:

1). Ukaguzi wa Magari: Serikali ingefanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyombo vyote vya usafiri kuhakikisha vinakidhi viwango vya usalama.

2). Elimu ya Usalama Barabarani: Madereva na wamiliki wa vyombo vya usafiri wangeelimishwa kuhusu umuhimu wa kufuata sheria za usalama barabarani.

3). Adhabu Kali kwa Wakiukaji: Madereva na wamiliki wanaopatikana na hatia ya uzembe wanhepatiwa adhabu kali kama kufungiwa leseni au kifungo cha muda.


6. Faida za Mfumo Huu

1). Kuongeza Nidhamu na Uwajibikaji:
Wamiliki wa vyombo vya usafiri wangehakikisha vyombo vyao ni salama, na madereva wangekuwa makini zaidi barabarani.

2). Kupunguza Ajali kwa 100%: Kwa gharama kubwa ya fidia na faini, ajali zingepungua kwa kiwango kikubwa.

3). Kuimarisha Usalama wa Jamii: Barabara zingekuwa salama kwa kila mtumiaji wa barabara.

Kwa kutumia mfumo huu, tungepelekea kuondoka kwa uzembe barabarani, huku tukihakikisha kila anayehusika anawajibika kwa matendo yake. Tungeanza kutekeleza mfumo huu, hakika ajali za barabarani zingekuwa historia ndani ya muda mfupi!
highways kama dar iringa
Au dar Ars ziwe double roads, mbona Namibia wameweza?
Hii itakuwa ndio muarobaini.
 
Ajali zinaweza kupunguzwa kwa Polisi kusimamia Sheria na sio kwa utozaji wa viwango.
Tatizo ni rushwa wanazopewa polisi na mahakama.
 
Siku moja nipo safarini kutokea jijini basi nililppapnda lipo mbio mbio kaa kawaida. Tukafika kwenye kona flani hivi kabla ya kuingia mkoa, dereva wa basi akawa anaovateki Lori ghafla yaani ile ghafla tunaona mbele Kuna Lori jingine ikabidi dereva wa basi arudi kushoto ghafla na kujibamiza kwenye kile Lori. Bahati kwa dereva wa basi ni kwamba dereva wa Lori hakuwa Mtanzania hivyo basi likawekwa kwenye namna ambayo walivyo kuja kupima wakasema Lori limegonga basi....DHULMA
Haya mambo yanapimikaje ili aliyesababisha alipe na kweli iwe halali amefanya adhabu?
 
Habari za jioni ndugu na marafiki,
Poleni sana kwa wote mnao endelea kuathirika na ajali zinazo endelea kutokea barabarani.

Hili jambo limelilazimu kukaa chini namimi nitoe mapendekezo yangu ili tuweze kutokomeza ajali zinazo endelea kumaliza ndugu na marafiki zetu.

Lakini kabla ya yote nimeona kwanza nilete pendekezo hili hapa jukwaani ili tuone jinsi ambavyo linaweza kufaa au kutofaa.

Kwanza kabisa naomba kuwasilisha kwamba ajali za barabarani huwa hazitokei kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya uzembe, kutokufuata sheria, na ukosefu wa tahadhari. Vyombo vya usafiri kama magari, mabasi, bodaboda, bajaji, na malori vinaweza kufananishwa na zana hatari kama visu, mapanga, au bunduki. Vyote vinahitaji uangalifu mkubwa ili visisababishe madhara.

Ili kumaliza ajali hizi, naomba kupendekeza mfumo huu madhubuti wa uwajibikaji unaolenga kuhakikisha kila mmiliki wa chombo cha usafiri anawajibika kwa matendo yake, huku akifuata sheria za usalama kwa umakini wa hali ya juu.

1. Uwajibikaji wa Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri
Mmiliki wa chombo cha usafiri alipaswa kubeba jukumu moja kwa moja kwa ajali yoyote inayosababishwa na chombo chake.

Aina za Uwajibikaji
1). Kwa mtu aliye gongwa na chombo
Mwathirika angelipwa fidia kulingana na viwango vilivyoainishwa (vifo, ulemavu wa kudumu, au majeraha).
Mmiliki wa chombo angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kusababisha ajali hiyo.

2). Kwa vyombo vilivyogongana
Kila mmiliki wa chombo angelipa fidia kwa abiria wake.
Kila mmiliki angelipa faini ya TZS milioni 50 kwa kushiriki katika ajali hiyo.

3). Kwa chombo kilichogonga kingine kikiwa kimesimama
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na kwa mwathirika wa chombo kilichokuwa kimesimama.
Pia atalipa faini ya TZS milioni 50 kwa uzembe wake.

4). Kwa chombo kilichogonga kingine kwa nyuma kikiwa kwenye mwendo
Mmiliki wa chombo kilichogonga angelipa fidia kwa abiria wake na waathirika wa chombo kingine kilichoharibika.
Faini ya TZS milioni 50 ingelipwa na mwenye chombo kilichogonga.

2. Viwango vya Fidia kwa Waathirika wa Ajali

Ninapendekeza viwango vifuatavyo vya fidia

1). Kwa Vifo: Familia ya aliyefariki ingepokea fidia ya TZS milioni 250 hadi 500.

2). Kwa Ulemavu wa Kudumu: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 150 hadi 200, kulingana na athari za ulemavu wake kwa maisha ya baadaye.

3). Kwa Majeraha ya Kawaida: Mwathirika angepokea fidia ya TZS milioni 50 hadi 100, kutegemea gharama za matibabu na muda wa kupona.


3. Faini ya Kupata Ajali

Kwa kuwa ajali husababisha madhara makubwa kwa jamii na miundombinu:

Faini ya Lazima: Kila anayepata ajali angelipa TZS milioni 50, bila kujali hali ya ajali (iwe imeua au la, chombo kimeharibika au la).


4. Mfumo wa Bima ya Lazima

Ili kuhakikisha fidia na faini zinalipwa ipasavyo:

1). Kila mmiliki wa chombo angetakiwa kuwa na bima ya dhima kubwa inayoweza kufidia madhara makubwa ya kifedha.

2). Wamiliki wasio na bima inayokidhi viwango wangetozwa faini kubwa au magari yao kufungiwa.


5. Hatua za Nyongeza za Kuzuia Ajali

Ili mfumo huu ufanye kazi kwa ufanisi, hatua zifuatazo zingepaswa kuzingatiwa:

1). Ukaguzi wa Magari: Serikali ingefanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyombo vyote vya usafiri kuhakikisha vinakidhi viwango vya usalama.

2). Elimu ya Usalama Barabarani: Madereva na wamiliki wa vyombo vya usafiri wangeelimishwa kuhusu umuhimu wa kufuata sheria za usalama barabarani.

3). Adhabu Kali kwa Wakiukaji: Madereva na wamiliki wanaopatikana na hatia ya uzembe wanhepatiwa adhabu kali kama kufungiwa leseni au kifungo cha muda.


6. Faida za Mfumo Huu

1). Kuongeza Nidhamu na Uwajibikaji:
Wamiliki wa vyombo vya usafiri wangehakikisha vyombo vyao ni salama, na madereva wangekuwa makini zaidi barabarani.

2). Kupunguza Ajali kwa 100%: Kwa gharama kubwa ya fidia na faini, ajali zingepungua kwa kiwango kikubwa.

3). Kuimarisha Usalama wa Jamii: Barabara zingekuwa salama kwa kila mtumiaji wa barabara.

Kwa kutumia mfumo huu, tungepelekea kuondoka kwa uzembe barabarani, huku tukihakikisha kila anayehusika anawajibika kwa matendo yake. Tungeanza kutekeleza mfumo huu, hakika ajali za barabarani zingekuwa historia ndani ya muda mfupi!
Mapendekezo yako hayana uhalisia na hayatekelezeki!

Je serikali ipate adhabu gani kwa ubovu wa barabara na kujenga barabara zisizo na viwango?
 
Mnajadili ajali, mnalaumu madereva sijui wamiliki mnatoa mapendekezo blablabla... kumbe ni mwisho wa mwaka watu wanafunga hesabu. Wanasiasa wanafungua njia za madaraka mwakani.
 
Ushauri wa kupanua na kuboresha miundombinu ndo suluhisho.

Hiyo mbinu ya kuwakamua watu pesa ni mbinu ya kijima hata Magufuli alijaribu ikamletea matokeo hasi .



Maana kuna ajari ambazo zinatokana na barabara (miundombinu)
Eeh wanafikiri ku impose heavy fines and penalties ndio suluhu. Watazalisha mianya mipya ya rushwa tu. Hamna mtu atafanya ujinga wa kulipa laki na nusu ilihali kuna option ya kuhonga elfu 20 akaenda zake na safari.

Ajali ziko centred kwenye miundombinu mibovu na finyu. Unakwepa shimo ghafla unajikuta umevaana na mwenzio anayekuja usoni mwako.
 
Back
Top Bottom