Tukubabali au tusikubali, Hayati Magufuli alikuwa mkombozi wetu

Tukubabali au tusikubali, Hayati Magufuli alikuwa mkombozi wetu

Je sasa Uhuru wa vyombo vya habari umeongeza nini kwenye pato la wananchi?
je, kuminya uhuru wa vyombo vya habari kuliongeza nini kwenye pato la wananchi? Wananchi kupata habari ni moja ya haki za msingi za taifa lolote.Jiulize bila tv, redio, magazeti maisha yangekuwaje?
 
UU! Umekushibisha uhuru huo,uhuru unaousemea unanisaidia Nini Mimi ninayeumia na mfumuko wa bei za vitu madukani
Kwaiyo magufuli angeenda kuizuia russia isiivamie ukraine? maana icho ndio kilichopandisha bei ya vitu?
 
Ndugu zanguni, hapo nyuma kidogo na sasa kwa uchache baadhi ya watu wamekuwa wakitoa kauli za kubeza kazi nzuri zilizofanywa na JPM kwa kejeli na dhihaka.

Nadhani lengo lao kubwa ni kutaka kufuta Legacy yake. Ukweli ni kwamba, hakuna mtu awaye yote anayeweza kufuta Legacy ya JPM.

Mbaya zaidi ni kwamba,wanapozidi kumbeza JPM na kazi zake ndipo wanapozidi kuumbuka zaidi.
Hapo ni lazima tukubabali kuwa, Mungu yupo upande wa JPM.

Ikumbukwe kwamba:-
1. JPM aliingiza Nchi katika uchumi wa kati katikati ya kipindi cha CORONA, lakini sasa tunaambiwa uchumi umeshuka.

2.Wakati wa JPM, vibaka walitoweka kabisa, lakini sasa wamerudi kwa kasi ya ajabu.

3. Wakati wa JPM, watumishi wa serikali walikuwa na nidhamu na walitekeleza wajibu wao ipasavyo lakini sasa ni balaa tupu. Hata kama ilikuwa nidhamu ya woga kama wanavyosema wengine lakini ilisaidia.

4. Wakati wa JPM, bei za vitu hazijawahi kupanda kiholela holela hivi, lakini sasa kila Mtanzania anajua hali ilivyo huku mtaani. Hali ni mbaya kweli kweli.

5. Wakati wa JPM, Ajali nyingi za kijinga kijinga zilikwisha kabisa lakini sasa zimerudi kwa kasi ya ajabu na kila mtu ni shahidi.

6. Wakati wa JPM, umeme haujawahi kukatikakatika kihuni huni namna hii, lakini sasa kila Mtanzania ni shahidi.

Hayo ni machache tu, yapo mengi mazuri yaliyofanywa na JPM yaliyokuwa msaada kwa Watanzania.

Rai yangu kwa viongozi ni kwamba, fanyeni tathmini ya kina muone mmekosea wapi na mjirekebishe.

Kamwe msihalalishe UDHAIFU wenu kwa kumdhihaki JPM, haitawasaidia isipokuwa mtaharibikiwa zaidi.

Acheni visingizio vya ajabu ajabu, maana sasa kila mnapofeli jambo fulani mnasingizia CORONA kana kwamba CORONA imeanza baada ya JPM kututoka.

Hivi karibuni mmeanza kusingizia vita vya Urusi na Ukraine. Visingizio vingi ni dalili za wazi kabisa za udhaifu wa kiongozi/viongozi.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Kama alikukomboa wewe na Sasa unasugua juu ya mawe basi pole Sana endelea kuomboleza,zamu kwa zamu.
 
Mumfanyie tajiri lolote bila woga hii imekuwa Banana Republic.
Nchi inapaswa kuongozwa kwa katiba, sheria na taratibu na Mtanzania ana haki ya kustawi katika nchi yake kwa juhudi zake akizingatia hayo.
Tuondoleeni roho zenu mbaya nyeusi.
Alikomesha mambo yote ya blaaa blaaa, sasa yamerudi kwa kasi. Ninapenda hii "tajiri kufanyiwa lolote bila woga" sasa mguse tajiri unuke.
 
#3 eti mama anataka nidhamu ya moyoni sio ya woga....
Hahaha! Kabla JPM watu tulikuwa tunaingia kazini(hospitali) na mkoba umejaa dripu, ganzi, mabomba ya sindano, dawa na kadi za wajawazito na kuuza mchana kweupe, ni JPM era nilishuhudia dawa maarufu "pawasefu" ikiletwa kwenye kiti ya MSD ngazi ya zahanati!(nidhamu ya moyoni hiyo) sasa hivi taratiiibu wameanza tena nimeona wajawazito wanatumia photocopy za kadi za kliniki nikawaza "neema" umerudi kwa manesi wenzangu ila bahati mbaya nilishaondoka huko nipo zangu mgodini Ikumbayaga tunatorosha tu dhahabi bila tozo....mitano tena kwa SSH!
 
Alikuwa mkombozi wako ww na family yako na watu wako, kwangu mimi alikuwa mnyang'anyi! Alikuwa katili, alikuwa dhulumati! Kwangu mimi na family yangu na ukoo wangu na ndugu na jamaa zangu wote walikuwa waathirika wa magufuli, nili furahi alipolala yooo na ninasema am happy now Mimi na family na ukoo wangu na ndugu zangu na jamaa zangu wote we are so happy now.
Mimi mwenyewe nilifurahi sana. alijifanya anajua,kumbe mbwiga tuu
 
Alikuwa Rais mwenye akili nyingi kuwahi kutokea.

Yani Rais ambae hadanganyiki hovyohovyo.
Rasi anaejiamini, rais anae fuatilia maagizoyake, rais anae fanya ziara za kushtukiza,ambae mbali na taarifa anazopewa na wasaidiziwake yeye mwenyewe anauwezo wa kuzichambua na kupata ukweli.

Kikubwa zaidi hakuwa muoga, na hakutaka kuyumbishwa na matajiri na mabeberu.

Aliweza kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati bila kupanda ndege kwenda ulaya.

Ndio maana watanzania wote walimuamini sana sana sana.

Viongozi acheni kumpiga vijembe magu, pigeni kazi tuwapime kwa jinsi mnavyo tuhudumia, acheni wivu.
 
Kila nafsi itakiri ni swala la muda tu.RiP Jembe
We ngoja tu, tutaelewana tu. Uzuri ni kwamba, kila wakijaribu kupindisha ukweli juu ya JPM, baada ya siku mbili tatu wanaumbuka.

Wameshasahau kipindi ambapo magari na Mabenki yalipokuwa yakitekwa na kuporwa mchana kweupe.
 
Matendo yake asilimia 80% yalikuwa ni ujambazi na utapeli kwa nchi hii mfano;1.Kuzima BUNGE laivu huo ni ujambazi,2.Kufuta mikutano ya kisiasa wakati akiendelea na siasa miaka yote mitano huo ni ujambazi,3.Kumpiga TUNDU LISSU risasi,kumnyima matibabu na kumvua ubunge,4.Kumwondoa CAG kabla ya muda kisa tu amegusa kwenye 1.5 trilioni huo ni utapeli na ujambazi,5.Kubariki uchaguzi 2019 wa Serikali za mitaa kuwa wa chama kimoja huo ni ujambazi,6.Kuchafua uchaguzi wa Octoba 2020 huo ni ujambazi,7.Kuwaaminisha wananchi mbumbumbu kama wewe kuwa tuliibiwa sana wakati muda wote alikuwa kwenye kundi la waizi ccm huo ni ujambazi,8.Kusema Tanzania hakuna korona wakati dunia nzima ikiathirika na korona huo ni ujambazi,9.Kujenga Chato kuwa IKULU na Jiji kwao alikozaliwa yeye huo ni ujambazi, na mwisho 10.Kupendelea teuzi nyingi kutoka Kanda ya Ziwa kwao anakotokea huo ni ujambazi.
Umesahau mengine,
Kujenga Ikulu Dodoma huo ni ujambazi, kudhibiti ajali za kijinga kijinga huo ni ujambazi, kutokomeza vibaka waliokuwa wametapakaa mitaani huo ni ujambazi, kuiingiza Nchi katika uchumi wa kati huo ni ujambazi, kuleta nidhamu ya watumishi wa umma huo ni ujambazi nk.
 
Hili Lina tija Gani? Yaani serikali kuhamia Dodoma ni mafanikio? Au ni gharama tu kwa raia maskini?

Hivi hiyo pesa ingepelekwa kwenye bajeti ya maendeleo ya kilimo ambayo huwa inatekelezwa chini ya 20% unadhani tungekuwa wapi sahivi kma sio uchumi wa kati juu??

Kuna mambo ya kumsifia ila sio kuhamia dodoma hiko means nothing.....

Afu unasema eti Bwawa La Nyerere limeshindIkana toka uhuru? Kwani kusambaza umeme wa gesi uliwezekana tangia uhuru? Maana kama shida ilikua ni umeme tu mbona hamtoi credit kwa Kinyerezi 1 and 2 ambayo ni Miradi ilianza na Jk?

Unafiki unawasaidia nini?
Yawezekana ulikuwa bado hujazaliwa, wakati wa huyo jk ndipo umeme ulipokuwa unakatika karibu kila dakika kadhaa, lakini hali hiyo ya kipuuzi ilidhibitiwa na JPM.
Sasa hali inarudi kule kule.
 
Ndugu zanguni, hapo nyuma kidogo na sasa kwa uchache baadhi ya watu wamekuwa wakitoa kauli za kubeza kazi nzuri zilizofanywa na JPM kwa kejeli na dhihaka.

Nadhani lengo lao kubwa ni kutaka kufuta Legacy yake. Ukweli ni kwamba, hakuna mtu awaye yote anayeweza kufuta Legacy ya JPM.

Mbaya zaidi ni kwamba,wanapozidi kumbeza JPM na kazi zake ndipo wanapozidi kuumbuka zaidi.
Hapo ni lazima tukubabali kuwa, Mungu yupo upande wa JPM.

Ikumbukwe kwamba:-
1. JPM aliingiza Nchi katika uchumi wa kati katikati ya kipindi cha CORONA, lakini sasa tunaambiwa uchumi umeshuka.

2.Wakati wa JPM, vibaka walitoweka kabisa, lakini sasa wamerudi kwa kasi ya ajabu.

3. Wakati wa JPM, watumishi wa serikali walikuwa na nidhamu na walitekeleza wajibu wao ipasavyo lakini sasa ni balaa tupu. Hata kama ilikuwa nidhamu ya woga kama wanavyosema wengine lakini ilisaidia.

4. Wakati wa JPM, bei za vitu hazijawahi kupanda kiholela holela hivi, lakini sasa kila Mtanzania anajua hali ilivyo huku mtaani. Hali ni mbaya kweli kweli.

5. Wakati wa JPM, Ajali nyingi za kijinga kijinga zilikwisha kabisa lakini sasa zimerudi kwa kasi ya ajabu na kila mtu ni shahidi.

6. Wakati wa JPM, umeme haujawahi kukatikakatika kihuni huni namna hii, lakini sasa kila Mtanzania ni shahidi.

Hayo ni machache tu, yapo mengi mazuri yaliyofanywa na JPM yaliyokuwa msaada kwa Watanzania.

Rai yangu kwa viongozi ni kwamba, fanyeni tathmini ya kina muone mmekosea wapi na mjirekebishe.

Kamwe msihalalishe UDHAIFU wenu kwa kumdhihaki JPM, haitawasaidia isipokuwa mtaharibikiwa zaidi.

Acheni visingizio vya ajabu ajabu, maana sasa kila mnapofeli jambo fulani mnasingizia CORONA kana kwamba CORONA imeanza baada ya JPM kututoka.

Hivi karibuni mmeanza kusingizia vita vya Urusi na Ukraine. Visingizio vingi ni dalili za wazi kabisa za udhaifu wa kiongozi/viongozi.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Daaah ni kweli mkuu,ukiangalia jinsi mambo yanavoenda, magufuli alikua jembe

Ila tufanyaje sasa?tunajifanya kupinga tu kwa roho ngumu ili tuonekane wagumu ila kwa sasa tunapigwa kila kona

😀😃😀😃😀
 
Kwaiyo magufuli angeenda kuizuia russia isiivamie ukraine? maana icho ndio kilichopandisha bei ya vitu?
Muda mwingine tuwe tunafikiri mambo kiyakinifu.
Vita vya Russia na Ukraine vimeanza juzi hapa wakati huo bei za vitu zilikuwa zimeshapanda tayari.
 
Back
Top Bottom