Jodoki Kalimilo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 12,559
- 11,180
Renta bado sijakamilisha mkuu hapa napambana kuimarisha biashara nirudishe mitaji kwanza ndio nikafufue ujenziNa renta umepiga kabisa au bado? Ila kama renta umepiga basi usijali kamanda hapo siku uchumi ukiwa vizuri utakamilisha maana utakuwa unafikiria jambo moja la kueezeka ambalo ndo gumu kwa upande wangu kuliko yote kwani zamani walikuwa wananunua mabati kidogo kidogo wanaweka ndani lakini zama hizi unatakiwa kununua yote hasa haya ya rangi.
Kwahiyo komaa kutafuta ela za kukamilisha mahitaji ya msingi ya familia kujenga kupo tu yaani ukikamilisha mambo madogo madogo ya familia ipo siku utaona kuna hela mkononi inabaki ndo hapo unaanza kufikiria kurudi kwenye ujenzi
Project ya nyumba Kuna muda huwa inapotezewa hata ile shauku ya site visit inapotea kabisa kama umesahau kuna ujenzi baadae unaibuka. Hapo jipange mdogo mdogo ukikaa sawa unaibuka na renta na kuezeka moja kwa moja.Renta bado sijakamilisha mkuu hapa napambana kuimarisha biashara nirudishe mitaji kwanza ndio nikafufue ujenzi
Nashukuru kwa ushauri mkuu hakika umeni-console
Unakuta mtu unakwenda kuangalia kiwanja kila weekend kama unavyokwenda hospital kumuona mgonjwabora ata nyie mna magofu...sie wengine tunaishia kusafisha viwanja tuu
Ujenge ya nini wakati dunia tunapita.Unakuta mtu unakwenda kuangalia kiwanja kila weekend kama unavyokwenda hospital kumuona mgonjwa
Nimepanga mwezi wa kwanza nikavisit site kwa mara nyingine ila natarajia sitaenda mikono mitupu Mungu anijaalieProject ya nyumba Kuna muda huwa inapotezewa hata ile shauku ya site visit inapotea kabisa kama umesahau kuna ujenzi baadae unaibuka. Hapo jipange mdogo mdogo ukikaa sawa unaibuka na renta na kuezeka moja kwa moja.
Pamoja na kwamba finishing ni gharama ila angalau inaweza kufanywa mdogo mdogo, mtihani huwa kwenye kuezeka kwa kuwa ni ela ya mara moja, ukifanikiwa hiyo stage unajipiga kifua kwamba umeshinda kwani hatua zinazofuata hata ukiwa na laki 5 inaweza tafutiwa kazi ya kufanya hata kama kupiga blundering room 2
Pambana mkuu ujenzi ni mgumu hasa kipindi cha kuezeka kuna nguvu ya roho mbaya inakufanya ukate tamaaWakuu habari za muda huu najua mko njema tunaendelea kupata pumzi ya bure na Mungu atubariki
Kama kawaida kuna wakati mtu unapambana na inafika hatua unatamani uwe na kwako uchomoke kwenye mambo za kupanga au tena ukahitaji kujiwekeza kwenye ujenzi kama biashara
Sasa kama ilivyo kawaida kujenga hakujawai kuwa rahisi, baada ya kupiga hesabu zangu nikaona nisimamishe kibanda cha vyumba vitatu na sebure nikiwa na uhakika na biashara yangu kuimarika kiasi kwamba kila mwezi ninaweza kusave 1ml nikaelekeza kwenye ujenzi
Doh! Najuta baada tu ya kuamsha boma upepo wa biashara ukabadirika na nisiweze kunyanyuka mwaka wa pili huu boma limekuwa gofu kila nikipiga ramani hazieleweki.
Je vipi kwako mdau nyumba yako imekamilika au umejiunga katika jumuia ya magofu tz? Unafanyaje kujiondoa katika hali hiyo?
Karibuni
Pambana mkuu kitaeleweka tu hata site visit ni sehemu ya ujenzi kwani inakutia moyo kupata pa kuanzia hata kwa kuona Maendeleo ya wengineNimepanga mwezi wa kwanza nikavisit site kwa mara nyingine ila natarajia sitaenda mikono mitupu Mungu anijaalie
Nakubali mkuu ahsante kwa hamasa sasa hivi nikimuona mwenye nyumba namheshimu sana kuliko mwanzo na nitaendelea kumheshimu na sitomvunjia heshima hata siku mojaPambana mkuu kitaeleweka tu hata site visit ni sehemu ya ujenzi kwani inakutia moyo kupata pa kuanzia hata kwa kuona Maendeleo ya wengine
Kungekuwa hakuna wizi wa vifaa vya ujenzi kama mchanga, mawe, matofali etc Bunge kupa mbinu ya kusogeza ujenzi.Hamna,