Tukutane tunaomiliki magofu kwa ajili ya kufarijiana

Na renta umepiga kabisa au bado? Ila kama renta umepiga basi usijali kamanda hapo siku uchumi ukiwa vizuri utakamilisha maana utakuwa unafikiria jambo moja la kueezeka ambalo ndo gumu kwa upande wangu kuliko yote kwani zamani walikuwa wananunua mabati kidogo kidogo wanaweka ndani lakini zama hizi unatakiwa kununua yote hasa haya ya rangi.

Kwahiyo komaa kutafuta ela za kukamilisha mahitaji ya msingi ya familia kujenga kupo tu yaani ukikamilisha mambo madogo madogo ya familia ipo siku utaona kuna hela mkononi inabaki ndo hapo unaanza kufikiria kurudi kwenye ujenzi
 
Renta bado sijakamilisha mkuu hapa napambana kuimarisha biashara nirudishe mitaji kwanza ndio nikafufue ujenzi

Nashukuru kwa ushauri mkuu hakika umeni-console
 
Renta bado sijakamilisha mkuu hapa napambana kuimarisha biashara nirudishe mitaji kwanza ndio nikafufue ujenzi

Nashukuru kwa ushauri mkuu hakika umeni-console
Project ya nyumba Kuna muda huwa inapotezewa hata ile shauku ya site visit inapotea kabisa kama umesahau kuna ujenzi baadae unaibuka. Hapo jipange mdogo mdogo ukikaa sawa unaibuka na renta na kuezeka moja kwa moja.

Pamoja na kwamba finishing ni gharama ila angalau inaweza kufanywa mdogo mdogo, mtihani huwa kwenye kuezeka kwa kuwa ni ela ya mara moja, ukifanikiwa hiyo stage unajipiga kifua kwamba umeshinda kwani hatua zinazofuata hata ukiwa na laki 5 inaweza tafutiwa kazi ya kufanya hata kama kupiga blundering room 2
 
Nimepanga mwezi wa kwanza nikavisit site kwa mara nyingine ila natarajia sitaenda mikono mitupu Mungu anijaalie
 
Ujenge ya nini wakati dunia tunapita.
Ila kujenga sii mchezo bwana alafu kuna fala mmoja humu anasema kuwa na nyumba na gari sio mafanikio...shenz type
Labda tumuulize yeye kwake mafanikio ni kuwa na nini?
 
Hapa kama kuna dalali anaweza pata connection ya kupiga pesa .....!!
 
Pambana mkuu ujenzi ni mgumu hasa kipindi cha kuezeka kuna nguvu ya roho mbaya inakufanya ukate tamaa

USSR
 
Pambana mkuu kitaeleweka tu hata site visit ni sehemu ya ujenzi kwani inakutia moyo kupata pa kuanzia hata kwa kuona Maendeleo ya wengine
Nakubali mkuu ahsante kwa hamasa sasa hivi nikimuona mwenye nyumba namheshimu sana kuliko mwanzo na nitaendelea kumheshimu na sitomvunjia heshima hata siku moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…