Tuliambiwa Mawakili wa kesi ya Mbowe ni wa kujitolea, kulikoni tena wanataka pesa?

Mmmmm upigaji pesa mwingine huo

Jibu hoja ya mleta mada
Hatumchangii Mbowe pesa, kwa kuwa hana pesa au kwa sababu mawakili wanahitaji pesa, tunachanga ili kuwakera, kama tulivyo wakera zile za ile hukumu ya kuhusu Aquiline!
 
Unadhani ukijitolea hauli nyumbani, ada ya watoto, kodi, nk vinafutika acha ujinga
 
Mmmmm upigaji pesa mwingine huo

Jibu hoja ya mleta mada
Pesa ya kujitolea ni kama sadaka kanisani au msikitini, watu wanatoa kwa hiyari yao na ni Kiherehere kikubwa kwa watu wa nje wasiohusika kuzifuatilia.
 
CDM siku hizi wanatumua "gofundme" tena organizer ni mtu binafsi!
Mtoa mada ona aibu basi, hata kama una chuki na CDM.
CDM wakitaka tuchange watatoa press.
 
Kwani wamekuambia wanataka kiasi gani,wamejitolea ndiyo maana hamna specific amount,kuchanga si lazima kama hutaki unaweza nyamaza usicomment -ve kuwakatisha Tamaaa wanaochanga
 
Ahsante kwa kunisaidia kupata link... nime donate $100 sikua najua hii kitu.
 
Mmmmm upigaji pesa mwingine huo

Jibu hoja ya mleta mada
Damu ya Tundu lissu bado itakulilia hadi nawe ukatike. Sitasahau namna ulivyohamasisha shambulio lile... JIWE keshalipia gharama yake bado wewe!
 
Kuhoji ni upambavu nyie mnavyohoji kila siku ni wapumbav? Akili za Bavicha bana.
Naona ulikuwa kimya siku hizi umerudi tuikumiss sana aaah!! Magu acha tu sisi wengine tunapambana kujitibu na madhila yale
 
Ahsante kwa kunisaidia kupata link... nime donate $100 sikua najua hii kitu.
Duh, safi sana! Wanadhani kuwa wafanyavyo ndio ku discourage watu kuchangia kumbe ndio wanasambaza habari zaidi kwa watu wema.
Kuna wanaccm kadhaa nimewajua na wamechangia.
 
Kama mawakili wa serikali wanatumia Kodi zetu tunazolimwa kila mahali,tukiwachangia akina Kibatala Kuna kosa gani?
Kwa juhudi na commitment waliyoionesha mpaka Sasa wanastahili mchango wangu! Kiroho safi kabisa nitachanga,Asante Kwa taarifa maana nilikuwa sijui!
 
Ni nani alikuomba mchango wewe mchawi
 
Nimeangalia $100,000 kwa siku ya leo ni shilingi ngapi ni zaidi ya Milioni 230.

Hii milioni 230 hapo itachangwa na watakaopendezwa ambao wengi ni chadema. Lakini kama wao kwa uchache wao wanalenga pesa hiyo ikatokea waTanzania kwa umoja wetu tukalenga pesa hiyo hiyo ili kutengeneza madawati na madarasa tunayolalamika hayatoshi tutakua tunakosea?

Siku hizi unasikia Taasisi ABC kutoka China imetoa msaada wa matundu ya choo sita. Matundu ya choo zamani ilikua wananchi tunaenda kuchimba wenyewe lakini siku hizi tundu linakuja kwa msaada.

Haya matukio yanatuonyesha sisi kama taifa tumefikia wapi.
 
Kwani inalazimishwa? Kama hutaki tupishe tuwachangie mpambanaji wetu
 
Kama Kuna watu wanalipwa laki 5 Kila siku iweje Hawa wasipate chochote?
 
Kama mnaona vibaya watu kuwachangia si mfute hiyo kesi yenu feki ili hoja ya uchangiaji ife kama ndicho kinachowakondesha.

Mlivyompiga Lissu risasi pia mliumia alipochangiwa na hata kipindi kile yule mungu wenu aliyekufa alipowabambikia kesi feki pale Kisutu pia walipochangiwa mkaumia vile vile. Siku yenu yaja.
 
Wabambikaji mtafute sehemu nyingine ya kumbana Mbowe lakini sio pesa maana tunazo na tutachanga kuliko mahitaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…