Tulilalamika sana siasa kuingilia Utendaji. Sasa tumeanza kuvuna matokeo yake

Tulilalamika sana siasa kuingilia Utendaji. Sasa tumeanza kuvuna matokeo yake

Jaribu kutofautisha kufanya kazi kwa sifa au ili uonekane unafanya kazi na kufanya kazi kwa weredi.

Nafasi za Utendaji kama Katibu Mkuu ( Permanent Secretary) ni nafasi nyeti sana.

Mahali tuliporithi mfumo huu (Uingereza) watu hawa hawaondolewi hadi wanapostaafu. Ndo Think Tank wa Mawizara na Inachukua muda mrefu sana kumtengeneza mtu hadi anafikia nafasi hiyo.


Watu hawa ndo wanafanya tafiti kuhusu sera na kushauri kwenye maamuzi makubwa ya kitaifa kwa mamlaka. Wanatakiwa wawe watu wenye competence, integrity, experience na exposure za kutosha. Watu hawa huwa wenye exposure na ndani na nje ya nchi na huwa wanatengenezwa ndani ya Serikali humo humo.

Unapomchukua kijana au mtu kutoka Chama cha Mapinduzi ambaye hajui hata utumishi wa Umma, au katoka tu chuoni au katoka kufanya kazi Chama cha Mapinduzi tu unampa nafasi hiyo ya Katibu Mkuu au DED unadhani kwenye masuala nyeti anayoletewa na anapaswa kufanya analysis kubwa na kufanya maamuzi mazito atafanya maamuzi gani?

Yanayosemwa huko Serikalini yanatisha. Ngoja tukae kimya kuwalinda wenzetu walioko huko.
Tuanzie hapo hapo kwa huyo permanent secretary, nitajie aliyekaa muda mrefu kwa nafasi hiyo na akaja na kitu ambacho tunaweza kusema, "yes pale kuna mtu alikalia kiti hicho" nje ya kutangazwa mikoa mipya. Nitajie walau issues 5 tu with a specific person.

Hilo moja, la pili ni hili, either mtu anafanya kazi kwa hofu au kwa sifa, mwishoni mwa siku mimi kama mwananchi naangalia matokeo, namna gani umefanya sio issue kwangu, "MATOKEO" So hilo la hofu or sifa kwangu sioni kama ni tatizo
 
Tuanzie hapo hapo kwa huyo permanent secretary, nitajie aliyekaa muda mrefu kwa nafasi hiyo na akaja na kitu ambacho tunaweza kusema, "yes pale kuna mtu alikalia kiti hicho" nje ya kutangazwa mikoa mipya. Nitajie walau issues 5 tu with a specific person.

Hilo moja, la pili ni hili, either mtu anafanya kazi kwa hofu au kwa sifa, mwishoni mwa siku mimi kama mwananchi naangalia matokeo, namna gani umefanya sio issue kwangu, "MATOKEO" So hilo la hofu or sifa kwangu sioni kama ni tatizo
Uzi umekuzidi sana akili huu.Sio saizi yako, we endelea na mambo ya Simba ya Yanga.
 
Yalianza kama masikhara ila sasa tuvumilie kuvuna matunda yake.

Kuanguka kwa Tanzania ni suala lililochukua muda kidogo. Tuliopata nafasi ya kuonya, tulionya ili kulikomboa Taifa ila hakuna yaliyofanyika na matokeo yake ndo haya tunayoyaona leo.

Ilianza kwa kuanza kutoa nafasi za utendaji Serikalini za Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri kwa Makada wa Chama cha Mapinduzi.

Tuliopewa macho ya rohoni tulionya kuwa suala hili lilikuwa linaenda kuharibu sehemu nyeti ya Utumishi nchini kwa sababu watu hawa ni watu wanaopaswa kupatikana kwa merit kutokana na kuwa sehemu muhimu ya maamuzi nchini hivyo ni vizuri masuala ya competence, integrity, experience na exposure kuzingatiwa kwenye teuzi zao ila kwa kuwa CCM waliamua kupuuza maoni ya wenye akili walitupuuza kwa maslahi yao ya muda mfupi.

Haikuishia hapo. Siasa ikaingia hadi kwenye majeshi na vyombo vya Ulinzi. Kubadilishwa kwa Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa zaidi ya mara 4 ndani ya miaka 3 ni kielelezo kingine kuwa Siasa ilianza kuingia huko.

Kupandishwa vyeo kwa maofisa wa Polisi wanaoonekana kuzungumza mbele ya vyombo vya habari masuala yanayowafurahisha wanasiasa nako kuliendelea kuonesha kwa namna gani siasa imeingia kwenye vyombo vyetu hivi.

Matokeo ya haya:
1. Sasa Tanzania imepoteza nafasi yake ya kuwa Think Tank na Main determinant wa Siasa za Maziwa Makuu. Nafasi hii wamechukua Rwanda na Uganda baada ya kufanikiwa kupenyeza mamluki wengi kwenye mfumo wa Tanzania. Sasa Rasmi Rwanda anaenda kuichukua Mashariki ya Congo.

2. Mfumo wa Maamuzi wa Tanzania umeshakuwa fully penetrated na Majasusi wa Bahima Empire. Inasemwa sehemu nyeti zote zimeshakuwa Penetrated. Hadi sasa Naibu PM wa TZ ni product wa Bahima Empire. Na onasemwa BOT, Hazina, Mipango kote wamejaa wao.

3. JWTZ kuanza kuwa Jeshi la Kisiasa na kupoteza nafasi yake kama Jeshi Bora na linaloheshimika Afrika Mashariki. Jeshi hili saivi limekuwa Jeshi la Maonesho, kupenda sifa badala ya Jeshi la Mikakati na Mipango Kabambe. Kichapo walichokipata huko Congo hadi saivi Malawi wameamua kuondoka ni kielelezo tosha.

4. Kukwama kwa mipango kabambe ya maendeleo ya Taifa. Hii ni kwa sababu nafasi za DED, KM na RAS zimeshikwa na makada wa Chama cha Mapinduzi ambao wao kazi yao ni kuangalia uhai wa Chama cha Mapinduzi ila sio mustakabali mzuri wa Taifa letu kwa miaka mingi ijayo. Watu hawa hawawezi kufanya analysis ya masuala ya msingi zaidi ya kuangalia siasa na Chama chao ambacho wanaamini bila hicho wasingekuwepo hapo.

Kwenye haya maamuzi mengi sasa yamekuwa yakifanywa kwa mtazamo wa kisiasa na sio kwa ajili ya kuijenga Tanzania imara Kiuchumi na Kimaisha kwa miaka mingi ijayo.


5. Kuibuka kwa watu ambao kazi yao ni kuwalamba miguu Viongozi na Kuwasifia huku wakilipwa fedha ambazo ni kodi za wananchi. Watu hawa wanaharibu vijana kwa kuwaonesha kuwa maisha ni kuwa Chawa na inawezekana usijishughulishe na kufanya kazi kwa bidii ila ukawa chawa wa kiongozi na maisha yakaenda.

6. Kuendelea kushuka kwa kiwango kikubwa na cha kutisha masuala ya Utawala Bora na Utawala wa Sheria. Hili linapelekea wananchi wenye mawazo tofauti kutekwa, kuuwawa na wengine kupotezwa bila hatua zozote kuchukuliwa.

Matukio ya Soka, Ben Saanane, Mzee Kibao na Sativa ni mfano mdogo tu wa wapi tumefika kama Taifa.

Poleni sana Watanzania.

Kilaaniwe CHAMA CHA MAPINDUZI.

Tupambane kufa na kupona tupate KATIBA MPYA.
Nyumbu wa Chadomo Huwa mnajijaza upepo sana sijui Kwa nini 😁😁

Ndio maana mnapuuzwa na Nchi inazidi kusonga.

Hao uliowataja wanakuja hapa Tanzania siku sio nyingi kupata miongozo au hujui?
 
Hi nayo huaga ni style ya watu kukwepa uwajibikaji, jibu maswali ili niendelee na U Simba na Yanga
Swali lako lina akisi upeo wako wa kufikiri. Nitajipotezea muda kukujibu.

Ni vizuri nikuache uendelee kuwa na upeo huo huo mdogo maana sio wote wanaojaliwa kuwa na akili
 
Nyumbu wa Chadomo Huwa mnajijaza upepo sana sijui Kwa nini 😁😁

Ndio maana mnapuuzwa na Nchi inazidi kusonga.

Hao uliowataja wanakuja hapa Tanzania siku sio nyingi kupata miongozo au hujui?
Unadhani nchi zinazoanguka huwa hazisongi mbele?
 
Mfano wa Zilizokuwa zinasonga zikaanguka ni upi? Ili tujuie huo kuelewa wako.
Unahitaji mfano gani zaidi ya hiyo Congo iliyoelezewa hapo kwenye sehemu ya uzi?

Au hujui kuanguka kwa Congo kumetokana na njia hii hii mnayoenda nayo CCM leo hii?
 
Swali lako lina akisi upeo wako wa kufikiri. Nitajipotezea muda kukujibu.

Ni vizuri nikuache uendelee kuwa na upeo huo huo mdogo maana sio wote wanaojaliwa kuwa na akili
Bro; jibu swali. Nitajie huyo unaesema think tank alikaa muda mrefu na akaja na kitu cha maana cha kukumbukwa to-date, acha kukwepa mjadara kwa point dhaifu eti upeo. Hili ni jukwaa la majadiriano, umeanzisha uzi kubali kujibu maswali yetu tusio kua na upeo mkubwa. Biashara ya nyie kusoma na kudukua mambo ya Ulaya (kama ulivotolea mfano wa Uingereza) usilete huku, hata sisi tunayajua hayo ya Ulaya. My point is, umetolea mfano wa Uingereza and may be na sisi tuli adopt but tuli adopt mfumo na sio utendaji. Uingereza bunge several times limemuondoa mtawala madarakani, mifano ipo mingi, bunge kama hilo hilo hata hapa tumeli copy but je, bunge letu lina meno kama la Uingereza?
Turudi kwenye maada, lete mfano bro. Nina umri wa mtu mzima so kumbukumbu za nchi yangu ninazo za kutosha since enzi za Mwalimu nipo duniani
 
Wewe hata mumeo akishindwa kusimamisha akupande utamlaumu Magufuli
Jadili hoja.
Huu ujinga wa makada kupewa nafasi nyeti za utendaji kwa sababu ya uchawa na kusifu watawala ulikomaa kipindi cha magufuli.
Magufuli kaasisi mambo mengi sana ya hovyo
 
Huyo CDF mwenyewe anawaogopa wanasiasa kama sio CDF.

Yanayosemwa kumuhusu sio mazuri. Ajirekebishe na asimame kwenye nafasi yake kama CDF na sio kupelekeshwa pelekeshwa na wanasiasa. Aangalie wenzake kina Twalipo, Mwamunyange, Mabeyo na Mboma walivyokuwaga.

Pia Majenerali wamekuwa watu wa kujali maslahi na sio kuboresha jeshi letu. Jeshi letu halipaswi kupoteza nafasi yake kama Jeshi Bora zaidi katika kipindi chake.
Mabeyo ndo alikuwa wa ovyo kabisa wakati wa jpm
Alikuwa anafanya siasa za ccm waziwazi kabisa.
 
Swala la Bahima lisitujengee kuhisiana vibaya, watu wote wa wilaya ya Karagwe Wana asili ya kitusi, hivyo ni Bahima, waha wa kigoma wamechanganyika nusu ni Bahima nusu ni wengine, Ngala pia ni mchanganyiko. Je hao wote sio watanzania? Wafukuzwe?

Makabila ya mipakani Yana mchanganyiko mkubwa na watu wa nchi jirani
Karagwe majority ni wanyambo
Wanyarwanda walihamia kama wakimbizi miaka ya 1950's walipochinjana kwa mara ya kwanza...
Halafu acheni kusema watusi,Rwanda kuna watusi na wahutu lakini wote wanaongea lugha moja...kinyarwanda
 
Kuna hii staili ya ccm ya bora liende inaigharimu sana nchi. Rushwa, uzembe na kutowajibika imekuwa staili mpya ya utawala ya ccm ...na wananchi kama walishakata tamaa wamebaki kuangalia tu.
 
Back
Top Bottom