Tulilalamika sana siasa kuingilia Utendaji. Sasa tumeanza kuvuna matokeo yake

Tulilalamika sana siasa kuingilia Utendaji. Sasa tumeanza kuvuna matokeo yake

Tatizo lilianza kwenye utawala wa Magufuli.
I hate that devil
Imagine wote waliofeli kwenye kura za maoni za ubunge CCM 2015 aliwapa nafasi za kiutendaji serikalini
Tuweni wakweli, enzi za Magufuli watendaji wa serikali walikua wakifanya kazi, waziri wa maji kwamfano, enzi za Magufuli kweli alikomesha mgao wa maji, wa umeme as well; hospital ukienda una uhakika wa kuhudumiwa, hata kama dawa zilikua hazitoshelezi but kuna kazi ilikua inafanyika. Tutamkaumu Magufuli kwasababu ya chuki zetu but the guy showed the way and he made a lot of transformation in our government and it's organs. RIP JPM
 
Tuweni wakweli, enzi za Magufuli watendaji wa serikali walikua wakifanya kazi, waziri wa maji kwamfano, enzi za Magufuli kweli alikomesha mgao wa maji, wa umeme as well; hospital ukienda una uhakika wa kuhudumiwa, hata kama dawa zilikua hazitoshelezi but kuna kazi ilikua inafanyika. Tutamkaumu Magufuli kwasababu ya chuki zetu but the guy showed the way and he made a lot of transformation in our government and it's organs. RIP JPM
Kabisa 🙏👍
 
Walio ndani ya CCM wenye kutaka Katiba mpya ni wengi kuliko wasioitaka,

TUNDU Lissu aanze tu, watamalizia wengine.
 
Walio ndani ya CCM wenye kutaka Katiba mpya ni wengi kuliko wasioitaka,

TUNDU Lissu aanze tu, watamalizia wengine.
Tusimpe mzigo huu Tundu Lissu tu. Watanzania wote tunapaswa kuidai Katiba Mpya kwa nguvu zote maana hapo ndipo ulipo mzizi wa kupona kwetu kama Taifa
 
Tusimpe mzigo huu Tundu Lissu tu. Watanzania wote tunapaswa kuidai Katiba Mpya kwa nguvu zote maana hapo ndipo ulipo mzizi wa kupona kwetu kama Taifa
Ni Kweli,

Watanganyika walipenda uhuru, lakini ilihitajika Nyerere na wenzie kuongoza njia,

Likewise kwenye Katiba mpya watu committed Wana mchango mkubwa.
 
Yalianza kama masikhara ila sasa tuvumilie kuvuna matunda yake.

Kuanguka kwa Tanzania ni suala lililochukua muda kidogo. Tuliopata nafasi ya kuonya, tulionya ili kulikomboa Taifa ila hakuna yaliyofanyika na matokeo yake ndo haya tunayoyaona leo.

Ilianza kwa kuanza kutoa nafasi za utendaji Serikalini za Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri kwa Makada wa Chama cha Mapinduzi.

Tuliopewa macho ya rohoni tulionya kuwa suala hili lilikuwa linaenda kuharibu sehemu nyeti ya Utumishi nchini kwa sababu watu hawa ni watu wanaopaswa kupatikana kwa merit kutokana na kuwa sehemu muhimu ya maamuzi nchini hivyo ni vizuri masuala ya competence, integrity na experience kuzingatiwa kwenye teuzi zao ila kwa kuwa CCM waliamua kupuuza maoni ya wenye akili walitupuuza kwa maslahi yao ya muda mfupi.

Haikuishia hapo. Siasa ikaingia hadi kwenye majeshi na vyombo vya Ulinzi. Kubadilishwa kwa Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa zaidi ya mara 4 ndani ya miaka 3 ni kielelezo kingine kuwa Siasa ilianza kuingia huko.

Kupandishwa vyeo kwa maofisa wa Polisi wanaoonekana kuzungumza mbele ya vyombo vya habari masuala yanayowafurahisha wanasiasa nako kuliendelea kuonesha kwa namna gani siasa imeingia kwenye vyombo vyetu hivi.

Matokeo ya haya:
1. Sasa Tanzania imepoteza nafasi yake ya kuwa Think Tank na Main determinant wa Siasa za Maziwa Makuu. Nafasi hii wamechukua Rwanda na Uganda baada ya kufanikiwa kupenyeza mamluki wengi kwenye mfumo wa Tanzania. Sasa Rasmi Rwanda anaenda kuichukua Mashariki ya Congo.

2. Mfumo wa Maamuzi wa Tanzania umeshakuwa fully penetrated na Majasusi wa Bahima Empire. Inasemwa sehemu nyeti zote zimeshakuwa Penetrated. Hadi sasa Naibu PM wa TZ ni product wa Bahima Empire. Na onasemwa BOT, Hazina, Mipango kote wamejaa wao.

3. JWTZ kuanza kuwa Jeshi la Kisiasa na kupoteza nafasi yake kama Jeshi Bora na linaloheshimika Afrika Mashariki. Jeshi hili saivi limekuwa Jeshi la Maonesho, kupenda sifa badala ya Jeshi la Mikakati na Mipango Kabambe. Kichapo walichokipata huko Congo hadi saivi Malawi wameamua kuondoka ni kielelezo tosha.

4. Kukwama kwa mipango kabambe ya maendeleo ya Taifa. Hii ni kwa sababu nafasi za DED, KM na RAS zimeshikwa na makada wa Chama cha Mapinduzi ambao wao kazi yao ni kuangalia uhai wa Chama cha Mapinduzi ila sio mustakabali mzuri wa Taifa letu kwa miaka mingi ijayo. Watu hawa hawawezi kufanya analysis ya masuala ya msingi zaidi ya kuangalia siasa na Chama chao ambacho wanaamini bila hicho wasingekuwepo hapo.

5. Kuibuka kwa watu ambao kazi yao ni kuwalamba miguu Viongozi na Kuwasifia huku wakilipwa fedha ambazo ni kodi za wananchi. Watu hawa wanaharibu vijana kwa kuwaonesha kuwa maisha ni kuwa Chawa na inawezekana usijishughulishe na kufanya kazi kwa bidii ila ukawa chawa wa kiongozi na maisha yakaenda.

Kwenye haya maamuzi mengi sasa yamekuwa yakifanywa kwa mtazamo wa kisiasa na sio kwa ajili ya kuijenga Tanzania imara Kiuchumi na Kimaisha kwa miaka mingi ijayo.


6. Kuendelea kushuka kwa kiwango kikubwa na cha kutisha masuala ya Utawala Bora na Utawala wa Sheria. Hili linapelekea wananchi wenye mawazo tofauti kutekwa, kuuwawa na wengine kupotezwa bila hatua zozote kuchukuliwa.

Matukio ya Soka, Ben Saanane, Mzee Kibao na Sativa ni mfano mdogo tu wa wapi tumefika kama Taifa.

Poleni sana Watanzania.

Kilaaniwe CHAMA CHA MAPINDUZI.

Tupambane kufa na kupona tupate KATIBA MPYA.
 

Attachments

  • IMG-20250128-WA0054.jpg
    IMG-20250128-WA0054.jpg
    142.5 KB · Views: 1
Udhaifu mmojawapo wa CCM ni kupenda kusifiwa na kutokuwa na mechanism ya kupata wanachama. Wanasombasomba tu. Ndio maana hata wahamiaji haram kwa kutambua hilo wakiingia tu nchini wanajiunga na CCM na kuanza kuwa machawa. Matokeo yake wanapatiwa nafasi na wanapanda hadi ngazi za maamuzi.
CCM ilo ndo lilikua anguko la CCM walitumia chama cha Mapinduzi kama Kinga ukiwa muhamiaji haramu unakadi unageuka kua mtanzania ni aibu sana
 
Nadhani yalianza wakati wa Nyerere. I wonder how a devil can hate another:ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN::ALIENALIENALIENALIENALIEN:
Hata siasa maofisini zilianzishwa na Mwalimu hadi kukawa na ofisi za chama. Mwanzoni ofisi hizo makazini ziliongozwa na wafanyakazi wa ngazi za chini. Baadaye wakuu wa idara na mashirika walichoka kuitwa na chama kuhojiwa na kupewa maelekezo na chama wakaingia wenyewe kwenye uongozi wa chama. Hapo ndipo mambo yakanoga.
 
Mkuu umeongea point kubwa sana, this country has damaged beyond repair. Kingine cha kukuongezea hapo ni mfumo ya Auditing umeingiliwa na siasa. Hakuna cha maana kinachofanyika ndio maana fedha zinaliwa na bado uozo unaowekwa hadharani ni sehemu ndogo sana.
Kuanzia kwa Mdhibiti mpaka bunge hakuna mwenye time
 
Udhaifu mmojawapo wa CCM ni kupenda kusifiwa na kutokuwa na mechanism ya kupata wanachama. Wanasombasomba tu. Ndio maana hata wahamiaji haram kwa kutambua hilo wakiingia tu nchini wanajiunga na CCM na kuanza kuwa machawa. Matokeo yake wanapatiwa nafasi na wanapanda hadi ngazi za maamuzi.
Duh!!!
 
Back
Top Bottom