Tulizeni Mioyo Watanzania: Taifa liko Salama Mikononi mwa Mama Samia Suluhu Hassan
Kuna puppets wanadhani sasa nchi itasambaratika, wasahau. Uzuri ni kuwa nchi yetu iko imara chini ya Samia. Watanzania wengi sana tupo nyuma yake mh. Rais, kwa maombi na ulinzi. RIP MAGUFULI

Nadhani tumekuwa watu wa maruhani na kufikirika tu. Ni akina nani hao maadui wetu tuwafahamu ili tujue kuwakwepa??

Kila siku ooh tuna maadui. Kuweni jasiri muwataje tuwajue - kuepusha kila mtu kudhani ni fulani kumbe sio!! Kama hamuwezi kuwataja mnyamaze. Mnatutia wasiwasi usio na msingi - mnafanya propaganda z kipumbavu!!
 
sijaelewa sisi waTZ na umasikini wetu kuna mtu yupo bize kututisha tena
Mafisiem yanatishana wao kwa wao.punde kila mtu ataanza kutembea na maji yake ya kunywa mkononi.Akijipindua kidogo tu anawekewa sumu! 🤣
 
Nadhani tumekuwa watu wa maruhani na kufikirika tu. Ni akina nani hao maadui wetu tuwafahamu ili tujue kuwakwepa??

Kila siku ooh tuna maadui. Kuweni jasiri muwataje tuwajue - kuepusha kila mtu kudhani ni fulani kumbe sio!! Kama hamuwezi kuwataja mnyamaze. Mnatutia wasiwasi usio na msingi - mnafanya propaganda z kipumbavu!!
madui wetu walishatajwa na Mwalimu Julius K Nyerere miaka ile...ndio tutakaopambana nao siku zote...afe kipa afe beki ushindi ni lazima
 
Lile kundi lenu la watu wasiojulikana sasa ndio limefikia mwisho, boss yuko anatoa mrejesho wa mauaji aliyowaagiza mtekeleze. Siasa chafu sasa na uzalendo uchwara ndani ya hii miezi sita zitakuwa zimesahaulika. Huyo mama ataanzisha kambi yake, nyie Mataga wa lake zone mbaneni mweka hazina awape chenu, maana mmiliki haifahamiki alitoa shilingi ngapi za kuulia watu na yeye ndio katangulia. Tunamshukuru Mungu kwa kusikia kilio chetu na kufanya mabadiliko bila umwagaji wa damu.
Nyie Puppets endeleeni kulelewa huko ubelgiji sisi kazi yetu kila uchaguzi ukifika ni kuwagonga tu maana hamjipangi badala yake mnaendekeza upumbavu kufikiri kila mtu ni msukuma!

Mungu ibariki tz
Mungu mbariki Rais wetu Samia
Mungu ibariki ccm

R. I. P JPM.
 
Yawezekana yupo anayeharibu kututisha na kutaka kutuondoa kwenye mpango kazi muhimu wa kuhakikisha tunakuwa huru kikwelikweli...
Mitano tena ? Vipi waimba mapambio ya kusifu na kuabudu utopolo , sasa mtaenda kuyaimbis sijui wapi ? Mliambiwa muwe na akiba ya maneno hamkusikia , kiko wapi sasa maibilisi wakubwa nyie .
 
Nadhani tumekuwa watu wa maruhani na kufikirika tu. Ni akina nani hao maadui wetu tuwafahamu ili tujue kuwakwepa??

Kila siku ooh tuna maadui. Kuweni jasiri muwataje tuwajue - kuepusha kila mtu kudhani ni fulani kumbe sio!! Kama hamuwezi kuwataja mnyamaze. Mnatutia wasiwasi usio na msingi - mnafanya propaganda z kipumbavu!!
Maadau wetu huwajui kweli?

Piga hesabu kina nani wako kwa akina amsterdam?
 
Mitano tena ? Vipi waimba mapambio ya kusifu na kuabudu utopolo , sasa mtaenda kuyaimbis sijui wapi ? Mliambiwa muwe na akiba ya maneno hamkusikia , kiko wapi sasa maibilisi wakubwa nyie .
mitano tena ni maazimio...hayatetereki
 
Mitano tena ? Vipi waimba mapambio ya kusifu na kuabudu utopolo , sasa mtaenda kuyaimbis sijui wapi ? Mliambiwa muwe na akiba ya maneno hamkusikia , kiko wapi sasa maibilisi wakubwa nyie .
Ccm iko imara safari hii chini ya jemedari mama yetu Samia vipi wewe unahisi kitu gani kimepungua kwa ccm?
 
Tumejipanga kusikia mengi...but our focus remain
Bila shaka.

Lakini kuna mengi pia ya mama kuyazingatia.

Nakupa machache:

1.Sera ya madini.

Ni lazima serikali isimamie sera mpya ya madini iloweka na iruhusu wawekezaji zaidi wa kigeni kwa makubaliano kwamba hawasafirishi nje makinikia na wawekeze maeneo yanozunguka migodi.

Kuwekeza kwa maana kwamba hawaachi mashimo na umaskini kwenye maeneo hayo.

Pia kuwekeza huko kutawainua wananchi ili nao wajisikie nao ni sehemu ya "Gold Rush" kama ya Ikumbayaga.

Pia JWTZ iendelee na ulinzi wa mgodi wa Mererani Arusha na kudhibiti utoroshaji wa madini ya tanzanite.

2. Sera ya utalii.
Wawekezaji wa utalii walipe kodi kulingana na kipato chao na mashine zile za TRA zitumike ipasavyo. Vijana waongoza watalii nao wawe sehemu ya wajasiriamali na hiyo iwe na ajira rasmi kwa vijana ila watambulike kwa TIN number zao.

3. Mikataba ya uwekezaji kwenye maeneo ya teknolojia na sayansi ipewe kipaumbele kwa makampuni ya nje aqmbayo ya uwezo na utaalam na vifaa ambavyo sisi Tanzania hatunavyo. Lakini kwenye hili fedha wanazolipwa watumishi wa kampuni hizo wakiwa hapa Tanzania zikatwe kodi kabla ya kwenda kwenye akaunti zao huko nje.

4. Kila mtanzania mwenye kuingiza kipato halali alipe kodi. Kodi ndo msingi wa maendeleo ya kila nchi. Kodi ndo hutumika kujenga miundombinu kama barabara, shule na mahospitali.
Serikali yaweza kusema kuanzia sasa kila mtoto anaezaliwa kumbukumbu zake ziwekwe kwenye kanzidata.

Kila kata, manispaaa na wilaya ziwe na kanzidata za wakazi wake na kila nyumba ilipe kodi ya maendeleo. Hizi kodi ndizo zinasaidia kusafisha na kupendezesha miji, barabara za mitaa na usambazaji wa huduma muhimu kama maji.

5. Kuimarisha mahusiano na Kenya na Rwanda ambao ni majirani zetu wazuri. Kenya ni mabepari ambao wamekuwa huko nyuma wakifanya biashara zao bila kuingiliwa. Tuwape ushirikiano khasa kwenye suala la EPA ambalo wao tayari wanashikiana na nchi za Ulaya.
Kuhusu Rwanda, ni katika kuhakikisha biashara kati yetu na wao inayohusu bandari ya Dar na mipakani inaimarishwa kwa kuwekeana viwango rafiki vya kodi ili kuvutia zaidi biashara zao na za kwentu kwao.

Hayo ni machache lakini kuna mengi ntaleta kwa kadri serikali itavyokwenda na "trajectory" ya mtangulizi wa mama Samia.
 
viwanda lazima vitajengwa ...ahadi ipo pale pale

Aliyekuwa anajigamba na viwanda karudisha mpira kwa kipa akiwa hawezi hata kutamka hilo neno viwanda, ndio itakuwa huyu mswahili?
 
Mbona kama umepanic?

Ccm bado iko Ikulu safari hii chini ya mwana mama Samia Suluhu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Ndugu yako mbelgiji ataendelea kuisikia ikulu kupitia twitter ya kigogo.
Vipi muhula mwingine? Daah ule mdomo sahv umeganda tu na barafu
 
Bila shaka.

Lakini kuna mengi pia ya mama kuyazingatia...
Nakuunga mkono katika mara chache sana nifanyavyo hivyo kwenye hizo pointi zako, hapo sasa ndio Richard wa ukweli, na sio zile propaganda mfu sijui za mashoe shine.

Ila hapo unaposema serikali itakavyokwenda na trejoctor ya mtangulizi wake. Sioni kwanini mama abanwe na mambo ya mtangulizi wake, wakati mtangulizi wake alikuwa anajigamba huku akishangiliwa kuwa hapangiwi, na kila zama na kitabu chake.
 
Yawezekana yupo anayeharibu kututisha na kutaka kutuondoa kwenye mpango kazi muhimu wa kuhakikisha tunakuwa huru kikwelikweli....
Unamtishia mama nyau.

Mama ana exposure kuliko nyie wachunga ng'ombe, na kwa taarifa yako tutawakaribisha mabeberu waje wawekeze nchi ipate maendeleo na ile misaada tuliyokuwa tunanyimwa sasa itamwagwa ya kutosha.
 
mifumo ipo na inafanya kazi...style hubadilika...sasa tutawaonesha new style.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Utamuonesha nani wewe Kamongo mliyemwandalia kutawala milele kawatoroka [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom