Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yampitisha Tundu Lissu kuwania Urais kupitia CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yampitisha Tundu Lissu kuwania Urais kupitia CHADEMA

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mhe. Tundu Lissu Kunguruma leo kwenye ofisi za Uchaguzi Dodoma akirejesha Form ya Kugombea Urais wa Tanzania

Updates
----
Tayari Mheshimiwa Tundu Lissu ambaye ni mgombea Urais na makamu wake Salum Mwalim wameshafika kwenye ofisi za tume ya Uchaguzi kwa urejeshaji wa Form

LissuCDM.jpg

UPDATE:-
Tumehifadhiwa kwenye holding room ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi hapa Dodoma kusubiri kuitwa ndani kwa ajili ya uteuzi!

Lissu.JPG

UPDATE:- 9:40
Mgombea wa CCM John Pombe Magufuli hakumali nusu saa kwenye Tume na fomu zake zimepokelewa, akateuliwa na kuondoka. Sisi wengine fomu zetu zinakaguliwa tangu saa sita mchana kwa utaratibu gani wa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge? Upendeleo huu wa nini?
Lissu.JPG

10:13
Kwa ajili ya kusimamia utaratibu wa kisheria, fomu za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA mhe. Tundu Lissu hazikupita kwa Wasimamizi wa Majimbo ya uchaguzi kwa ajili ya zoezi la uhakiki. Zoezi la uhakiki ndio linaloendelea kwa sasa.
Lissu.JPG

UPDATE:- 1:00 Usiku

I'm the only candidate who toured the country, met with actual voters and got their endorsement in person. All other candidates obtained their nominators from NEC registers without having to meet actual voters. Yet I'm the only candidate whose nomination is still under a cloud! - LISSU

Lissu.JPG

1:03 Usiku - NEC
Mgombea mwenza wa CHADEMA, Bw. Salumu Mwalimu akishuhudia zoezi la uhakiki wa fomu za uteuzi za chama hicho. Zoezi hilo linaendelea Ofisi za Tume, Njedengwa, Jijini Dodoma.

nec.JPG

UPDATE: 1:40 - LISSU APITISHWA
Katibu wa tume ya uchaguzi amesema wagombea wa Rais na Naibu Rais kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) wametimiza sifa na masharti ya uteuzi.

Baada ya tamko la katibu, Mwenyekiti amesema tume ya Taifa ya uchaguzi baada ya kujiridhisha kuwa kiti cha Rais na Makamu wa Rais waliopendekezwa na CHADEMA wametimiza masharti tume imewateua ndugu Lissu, Antipas kuwa mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na ndugu Mwalimu, Salum kuwa mgombea wa makamu wa kiti cha Urais wa Tanzania.

nec.JPG


Lissu.JPG

 
Back
Top Bottom