Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu. Magufuli na Lipumba ni wagombea halali

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu. Magufuli na Lipumba ni wagombea halali

Katika siasa hizi hali ni kawaida sana kutoke kwani udhaifu wko ni faida kw wengine lkn bado nawaza sidhani kama ndugu Lissu yuko sahihi sana na haya mapingamizi yake' ngoja niwaze kwa sauti, iwapo anasema fomu za mgombe uraisi magufuli zilihakikiwa mikoani wakat wa kutafuta wadhamini hili sio kosa kwan walio hakiki hizo fomu ni ofisi za Ccm na si NEC hivyo sio kosa kwani sheria za hizo fomu kua halali ziko wazi kw kila mtu hata mie nikitaka kuhakiki ni swala la kufahamu tu kanuni zinasemaje juu ya hizo fomu. Pili picha ktk fomu ni jambo la muhimu sana na kama zilihakikiwa kabla na wasimamizi wa majimbo kila mkoa aliopita haiwez kuwezekana hao wote wasigundue kwamba mwenyekiti wao hajaweka picha ktk fomu zake, tuanze kua tunafikiria zaidi na kwa kina. La mwisho binafsi nimeshuhudia urudishwji wa hizo fomu kwa wagombea wote yaan Lipumba na Magufuli kwa siku hiyo moja ambayo pia ndugu Lissu ndio siku aliyorudisha fomu yake, sasa akisema walirudisha siku ambayo si ya uteuzi nadhani hayuko sahihi au washauri wake wanamlisha matango pori humu kuna uzi ulitoka kwmba siku ya yeye kurudisha fomu aliwekwa chumba cha masubirio kwa muda mrefu ambayo ndo siku hiyi hiyo alisema ndugu magufuli hakumaliza hata nusu saa(30dk) ktk urudishaji wake. Sasa wana JF wenzangu hebu tuanze kua tunawaza na kufikiri zaidi ya tunachoambiwa kwa manufaa ya Taifa letu. Niwe mkweli binafsi nimekuzwa na malezi ya Ccm na mpaka leo kwa matukio ya ccm sikua tayari kuwapa kura yangu kutokana na madudu yao ikiwemo ufisadi na upendeleo lkn hawa wapinzani nao wana kasoro zikiwemo washauri wabovu na mifumo yao ya kiutendaji mfano walitumia miaka mingi kujijenga na kupinga ufisadi kabla ya mwaka 2015 na kweli walifanikiwa na ilikua kweli ccm na viongozi wao kua na maadili mabovu lkn baada ya ccm kucheza na kuamua kuwatoa hao mafisadi ikiwemo Lowasa na wengineo tena dk za mwisho na eti wao upinzani kwa maana ya iliyokua UKAWA kuja kuwakumbatia hao mafisadi na kutaka kutuaminisha wamekua safi JUST BY OVERNIGHT hiyo haikua sawa na hapo ndo walipoteza tena imani kwa baadhi yetu ikiwemo mimi binafsi na washakji zangu ambao hatufuatilii siasa moja kwa moja. Upinzani unatakiwa kuja na hoja za kuendesha inchi yetu na namna gani mipango yao kimaendeleo inavyofanya kazi. Sitaki kuamini CCM ni borq zaidi au hatuwezi kusonga zaidi bila wao kua madarakani HAPANA mabadiliko ni lazima yawepo lkn hao wanaotaka hayo mabadiliko wanatuaminishaje kwamba na wao Upinzani ni watu sahihi?????????!!!!!!!!! Hayo ni mawazo yangu binafsi nami naishi hapa hapa Tanzania na kila siku naona na kusikia kinachiendelea hapa kwetu JMT.
 
Wanazidi kutushangaza!Tungekuwa na Tume Huru, huenda Magu asingekuwa mgombea leo.

Kwa mujibu wa Lissu, Tume ndio iitoa maelezo yanayopingana na sheria, na mgombea uraisi Magufuli, akafuata maelekezo hayo yanayopingana na sheria, maelezo ambayo Lissu yeye alikataa kuyafuata na fomu zake akataka zikahakikiwa na NEC kama sheria inavyoelekeza(alisoma kifungu husika kwa wanahabari).

Swali:Kama Lissu alikuwa wrong,mbona NEC hao hao walikubali kukagua form zake na kuzihakiki kwa maana ya kuhakiki wadhamini wake tofauti na mgombea Magufuli na Lipumba ambao form zao zilihakikiwa huko mikoani na wasimamizi wa majimbo na wakazigonga mihuru badala ya fomu hizo kuhakikiwa na NEC?

Hoja nyingine ya Lissu ni kuhusu siku ya kurudisha fomu ambayo ilikuwa ni jana, na ndio siku ambayo,kwa mujibu wa sheria, ilikuwa ni siku ya uteuzi. Sasa hao wagombea wengine licha ya fomu zao kuhakikiwa na watu wasiostahili kisheria,lakini bado ziliwasilishwa katika siku ambayo haikuwa siku ya uteuzi(kwa maelezo ya Lissu) na hilo,kwa mujibu wa Lissu, pia ni kukiuka sheria ya uchaguzi.

Lissu pia kaweka wazi kuwa kwa mujibu wa sheria,Tume wanaweza kutoa maelekezo, ila sheria hiyo hiyo inatamka kuwa maelezo hayo hayapaswi kuwa kinyume na sheria yenyewe.

All in all,wahusika wamepata funzo tena bila shaka ni funzo kubwa tu hasa kuhusu hizi sheria zetu..

Cha ajabu,wao katika kujibu, hawatufafanulii zaidi ya kusema tu wametupilia mbali na kwamba majibu yatatolewa kwa muweka pingamizi kwa maandishi.
Acha ulofa
 
Kinyago uchonge mwenyewe then kikutishe? Mabeberu wenye mdoli wanazodolewa mchana kweupe sembuse hicho kikaragosi chao?
Wengine eti Mh. Raisi uso kwa uso na....! Bulldozer ukikutana nalo uso kwa uso sijui kama watapata hata picha ya kuambatanisha kwenye simulizi ama ushahidi.
Usiwe shabiki ongea ukweli watendaji wamezingua,wawe wanafanyia kazi mishahara yao wamewaingiza chaka wagombea na sio magufuli tu wote,sema aliweka pingamizi kwa magufuli ili kuleta mtikisiko
 
Kumekuchaaaa.....

Panaitwa Njendengwa....ilipo TUME HURU YA UCHAGUZI.....
 
Hatuwezi kutumia akili za kichaa kuongoza nchi, huyo huyo kasema tume inaweza kuwapa mamlaka wasimamizi, bado tena anasema sio harali,
Pili kuhusu picha
Naomba unipe tafasiri ya
pasport size?
full size na?
half size?
Medium size?
Big size
Je maana yake ni lazima uangalie mbele au ni kipimo cha ukubwa wa picha?

Kuhusu kuangalia mbele ni masharti ya taasisi au hitaji husika na sio kiwango cha ukubwa wa picha. Na ndo maana tunasema tundu ni kichaa ila bado mnamshangilia tu. Alisema magufuli katoa rushwa ya laki moja bado mkashangilia. Nyie ni mazuzu tu.

Ukitaka kujua tundu anamuogopa magufuri, toka jana usiku anatafuta makosa ya magufuli tu siku nzima na nadhani hajalala.
Hivi kama tundu in kichaa maguu atakuwa nani? Hii tume ni shida
 
Mkurugenzi wa Uchaguzi: Tume ya uchaguzi baada ya kupokea pingamizi dhidi ya wagombea hao, imewataarifu wawekewa pingamizi mapema iwezekanavyo na wahusika wamewasilisha utetezi wao.

Pingamizi dhidi ya mgombea wa CUF kwamba hakurudisha fomu kwa mujibu wa masharti yaliwekwa na sheria, tume baada ya kupitia sababu za pingamizi pamoja na utetezi uliotolewa imejiridhisha, Professa Ibrahim Haruna Lipumba amerejesha fomu zake kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya tume ya taifa ya uchaguzi hivyo tume ya taifa ya uchaguzi imejiridhisha pingamizi halina msingi na imelitupilia mbali. Professa Ibrahim Lipumba anaendelea kuwa mgombea halali wa kiti cha Rais kupitia chama cha CUF.

Pingamizi dhidi ya mgombea wa CCM

  1. Mleta pingamizi anadai kwamba, mgombea Urais kwa tiketi ya CCM hakuambatanisha picha kwenye fomu ya uteuzi.
  2. Hakurudisha fomu ya uteuzi kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na sheria
Tume baada ya kupitia sababu za pingamizi zote mbili kwa pamoja na utetezi uliotolewa imejiridhisha kuwa, Dr. John Magufuli, Mgombea wa kiti cha Rais kupitia chama cha mapinduzi amerejesha fomu zake ambazo zimeambatanishwa pamoja na picha kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya tume ya Taifa ya uchaguzi, hivyo tume ya Taifa ya uchaguzi imejiridhisha kwamba pingamizi hizo hazina msingi wa kisheria na imezitupilia mbali kwa maana hiyo, Dr. Magufuli anaendelea kuwa mgombea halali wa kiti cha Rais kupitia chama cha Mapinduzi CCM.

Kwa mujibu wa kanuni ya 39 kanuni ndogo sita ya kanuni za uchaguzi wa Rais na wabunge za mwaka 2020, sababu za uamuzi huu wa tume watapewa kwa maandishi, aliyeweka na aliyewekewa pingamizi, kwa msingi wa uamuzi huu, vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu wa kiti cha Rais na makamu wa Rais vinabaki kuwa 15.

Imetolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi


View attachment 1549104
View attachment 1549105

View attachment 1549098
Lieu anachekesha.
Tume aiteue Magu. Leo hii anataka imuite. Hizi ni dalili kuwa katiba yetu ni mbovu. Chadema hawataki kusikia ila time itamtangaza meko mchana kweupe
 
Wale watu wana elimu kubwa kuliko ya Tundu Lisu huwezi walinganisha na kichaa huyo anayeona marofa wengi kisha anawadanganya
Tundu lisu hajawahi shinda kesi kwa uhalali zaidi ya kuwahonga mahakimu
Na ndo maana kipindi cha kikwete aliwadhalau sana mahakimu.
Hakuna cha elimu wala nn, ile tume haina Uhuru wowote, ushahidi ni jinsi wakurugenzi makada walivyoondoa wagombea wa upinzani kihuni.
 
majibu ya pingamizi za magufuli yako wapi ?
Yako NEC ulitaka waKuletee nyumbani kwako?

Halafu wewe unamwamini Lisu fomu Ina Hadi sehemu ya kubandika picha unaamini kweli kuwa picha haulikubandikwa?

Lisu anatafita kiki kwenye media kwa.kila hali hata kwa kutunga vitu vidogo vya uongo
 
Back
Top Bottom