Tumepoteza kijana huko Houston, Texas. RIP Humphrey Magwira

Wewe vipi umekaa Tz miaka yako yote unaweza kutoa $20,000 bila kujiandaa?!

Ilitakiwa walimalize wao kama wao tu kwenye umoja wao wanaoishi huko....Tz na US kiuchumi hatulingani hata kidogo,kama ningekuwa US usd 100k au 200k ingekuwa kitu kidogo sana achilia mbali hizo usd 20,000......Huo ndiyo ukweri.

US wameendelea kitambo sana ,nina imani hata kwenye mambo ya bima wapo advanced sana ,kama huku TZ kuna bima ambazo zinagharamia misiba,vp kuhusu marekani walioendelea zaidi ya miaka 200 iliyopita?
 
Misiba tunachangia kila mahali kwenye jamii ya Watanzania. Kuchangia msiba haina maana mfiwa kashindwa kuubeba.
Na kuhusu wewe ungekuwa US 100k au 200k isingekuwa shida unajipa moyo tu. Hapo Tz Ulipo wapo wenzio hio 100k au 200k USD sio issue. Haihitaji uwe USA. Hata huko USA wapo Wabongo kibao hizo 100k USD sio big deal
 
Ni mtoto wa Lissu?
 
Hili la kusafirisha mwili linawahusu Watanzania waliopo Marekani.

Hata Wachaga msiba ukiwa Dar wanachangishana wachaga wa Dar, wale waliopo Moshi wanasubili kuzika tu.

Hata mimi binafsi kijijini kwetu ukitokea msiba unaotuhusu sisi wa Dar ndio tunawezesha pesa ya kuendesha ule msiba, sanda, sanduku na ng'ombe mmoja wa mboga.

Kwahili kuna tatizo kwenye jumuiya za Watanzania USA, ukiwaona walivyompokea mama Samia New York utadhani ni watu wa maana kumbe mipumbavu mingi misaka fursa ikiongozwa na yule Dada Mamuya.
 

Unaleta ubishi usio na kichwa wala miguu ,nimekwambia uchumi wa usa na tz ni tofauti sana means kipato cha mtu mmoja mmoja wa marekani ni kikubwa compare na kipato cha tz,sisi huku tunaishi chini ya usd 1,sijasema watu wasichange ,nimesema ilo la michango wangemaliza kwenye jumuiya yao ya huko huko sio mpaka iende gofund wachangiwe na dunia nzima,wangemaliza kwenye whatsapp group zao tu.

Kazi unayofanya wewe hapa TZ ungekuwa hiyo hiyo unaifanya marekani ungekuwa mbali sana,usingekuwa unatembelea kibiriti wala usingekuwa na pagale,hata kwenye nchi ya mwisho kwa umasikini pia kuna mabilionea na pia hata kwenye nchi tajiri pia kuna masikini ila wakipima per capital income hapo ndipo utaona utofauti.
 
Hakuna sehemu niliposema mzungu nimesema mweupe, Duniani kuna mtu mweusi na mweupe tu hao wahindi wekundu hawana tofauti ki rangi na John Deep
Hiyo categorization yako ni yako binafsi kwa umeamua wewe iwe hivyo. Ila wengine wote tunajua kama ulivyoeleweshwa na wachangiaji hapo juu white means mzungu then kuna hizo races nyingine
 
Dogo aligongana na mtu mweupe, mtu mweupe akatoka kwenye gari yake akaja kwa dogo na kumpiga risasi sita, mtu mweupe amekamatwa na amefunguliwa kesi ya mauaji. Sasa sijui ni ubaguzi au bhange tu za mtu mweupe
Mweupe gani msenge tu M mexico huyo fala ugangstar wa kishamba tu.
Unaua mtu kisa mmegongana?
Si angeenda benki angalau achukue pesa.
Atapigwa mvua miaka 200 na akitoka atakuta 200 ingine inamngoja.
Us hawachekagi na kima
 
Huyo atanyongwa kwa sheria kali za Texas yani ukiwa na murder case ukahukumiwa huponi Texas. Ila jamaa kwenye picha insonekana ana influence na madawa ndo maana kaua bila kujali.
 
Pamoja na hayo yote bado natamani kuishi US hata leo. Sema tu ndio hivyo sina uwezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…