Tunahitaji mjadala mpana wa kitaifa juu ya timu ya watu inayounda 'Mamlaka za Uteuzi' nchini

Tunahitaji mjadala mpana wa kitaifa juu ya timu ya watu inayounda 'Mamlaka za Uteuzi' nchini

If moderators hamuwezi kumfungia huyu punguani na mada zake za uchochezi?
Kila akijamba ni udini,
Fungieni huyu mpuuzi anayeangalia jina la mtu kujua dini ya mtu.
Hajui kuna jamaa yangu Hamisi Khalfani ni mgalatia na kuna Jesse Joseph ni mjahidina.
Ndugu acha upuuzi.
Najua unatumwa na wenzako wa ndani ya sistim
Kama unataka kila unayepingana nawe afungiwe basi atafungiwa kia mtu humu.

Kwa hiyo mtu akianzisha mada kulaani teuzi zilikzokaa kikanda utataka afungiwe?

Kama mtu akianzisha mada kuhoji teuzi zilizokaa kikabila utataka afungiwe?

Kama mtu akianzisha mada kuhoji teuzi zinazobagua wanawake utataka afungiwe?

Kama hayo yote huwa hamuoni tatizo kwenye mada zinazoyahusu, kwa nini buwa hampendi mada zinazohoji teuzi zilizokaa kidini? —Au mnanufaika na mfumo wa aina hii kwa hiyo hampendi uhojiwe?
 
Mada yako ina uchochezi na ni hatari kwa umoja wa taifa. Umetaja kuhusu dini mbili, lakini umejifanya hujui kuwa nchi hii ins dini zaidi ya hizo, kuna wapagani ambao ni kama theluthi hivi, wahindu, budha, sikh, n.k Je hao nao wakidai uwiano kwa dini zao? Pia hao waislamu kuna sunnni, shia, ismailia, bohora nk. Unaweza kuteua kwa mlengo wa kidini halafu wote wakawa dhehebu moja.

Wakristo ndio usiseme wana madhehebu lukuki kuanzia yake ya kitaasisi kama Catholic, lutheran, anglican na morovian mpaka yale ya mfukoni ambayo ni mali ya mtu mmoja mmoja lakini yanesajiliwa.

Nao wakidai uteuzi kwa uwiano je itawezekana? Kuna makabila 120 maana unaweza kuteua kwa kufuata dini lakini wote wakawa kabila moja.

Je utaweza kulipa kila kabila waziri? Kuna jinsia mawaziri wanaweza kuwa wa hizo dini mbili lakini jinsia moja au unaweza kubalansi jinsia lakini wakawa wa dini na dhehebu moja.

Haya mambo ndiyo yanapelekea kuwa na baraza kubwa la mawaziri kama kule sudan kusini, ambapo nchi ndogo maskini inajitwisha mzivo mkubwa kuhudumia mawaziri lukuki pasipo ulazima.

Rais anateua watu wa kumsaidia kazi kutokana na uwezo wao na mahitaji ya wakati.

Hoja yako kuwa uwaziri ni kipato ni sawa lakini ni kwa yule mtu mhusika sio kipato kwa ajili ya dini yake au kabila lake.


Hoja yako haina mashiko zaidi ya uchochezi na kutaka kumyumbisha Mheshimiwa Rais.
Hizo DINI nyengine hazina athari. Lakini Ukristo na Uislamu ni Kama Simba na Yanga.
 
K

Kiongozi kuna mambo bado hujayachambua kwa kina... MIMI SIO MDINI ila naandika kile kilichopo katika jamii yetu kwa sasa...
1. Wanafunzi wengi waliopo shule za kata niwa dini ya Kiislamu.... kwa shule za binafsi asilimia kubwa ni wakristo... ( tafakari hapo kiongozi)
2. Idadi kubwa ya vijana wakike na kiume waliopo mtaani niwadini ya kiislamu... matokeo yake Vijana wa kike wanazalishwa wengi wao wakiwa shuleni au mtaani ili hali hawana mafanikio yoyote ya kiuchumi kuweza kujikwamua au kuwapeleka shule nzuri watoto... wanaishia shule za kata....
3. Hata huku kwenye roots ya elimu kuanzia elimu msingi na vyuo, walimu wengi staff niwa kristo.
4. Kibaya zaidi hata hao wachache iwe ni walimu, madaktari etc huwa hawana misimamo mikali ya imani iwe kuangalia eti huyu mkristo au muislam ( big up Mama Samia chagua kwa kuangalia utendaji wa mtu)
5. Mfano Mazingira ninayoishi, majirani zangu kila siku visomo na mambo mengine ya ushirikina... kiongozi haya yana athiri sana... elimu ya vijana mashuleni.
6. Fuatilia mashuleni haswa msingi na sekondari kila siku watoto wanadondoka mashetani 100% niwa wanafunzi wa kike wa dini ya Kiislamu... hii ina athiri sana elimu ya watoto....
Kwa ufupi kiongozi elimu ndio kila kitu... pamoja na utendaji wa mtu. Naamini watu hao wapo kwa dini zote mbili... ila ukweli ni kuwa wakristo mpaka sasa wanaongoza kwa wasomi....
Note: Shule nyingi za wakoloni ( zilikuwa zipo kikristo zaidi) viongozi wako mfano Mzee Makamba alisoma shule za mission.... lakini mzee makamba sio mdini... Kiongozi Achana na Mawazo ya Udini angalia utendaji wa mtu anafaa mpe kazi hafai achana naye. ACHA UDINI.
Hizi takwimu za Pemba, Bagamoyo na Tanga tu
 
Mkuu usituletee udini hapa ,tunacho taka ni kwamba mtu ateuliwe bila kujali ,dini,ukabila jinsia ,chamsingi awe ana uwezo na nafasi husika, mbona nafasi kubwa za juu kitaifa zipo KWA ndugu zetu na wakiristu hawajapiga kelele,huko Zanzibar vipi mbona wakiristu hawalalamiki ali Hali Hili ni taifa moja , tutolee udini hapa
Wakristu wa Zanzibar hawafiki hata asilimia moja. Ndio maana hawalalamiki. Kwasababu wanapewa kikubwa kuliko wanachostahili.
 
Mwacheni mama achape kazi usimpangie cha kufanya au mnataka siku akasirike naye aropoke "mimi sipangiwi" msilete mambo ya udini na ukabila mama anaangalia uwezo wa mtu sio dini wala kabila.

Mbona huko katika uongozi mmejaa wakristo na waislam ila taifa tupo wengine ni Budha lakini hatujawai lalamika.
 
Muulize Jasusi Evarist Chahali kuhusu idadi ya waislamu na Wakiristu nchini na ishu ya imbalance katika teuzi hizi zinazoinvolve watu wa dini hizi—Alikuwa, anafanyia PhD suala hili.

By the way, huwezi kujua idadi ya Waislamu na Wakiristo nchini bila sensa

Sensa ninayoifahamu mimi iliyokuwa na kipengele cha dini za watu ni sensa ya mwaka 1954 iliyoonyesha Waislamu ni wengi zaidi.

Kwa sasa ni vigumu kujua idadi ya waislamu na wakiristo nchini mpaka labda ingekuwepo sensa inayoangalia kipengele hicho!
Najua hata wewe unaujua wingi wa wakristo, kwa huku Tanganyika hata bila kumuuliza huyo Mganga njaa Chahari, Wakristo ni wengi.Kule visiwani waislam ni wengi kuliko wakristo sikatai.Ila tunapozungumzia Tanzania (Tanganyika + Zanzibar) ndo tutahitaji hiyo sensa unayoizungumzia.

Hiyo sensa ya 1954 unayoizungumzia wewe, haiwezi kutoa uhalisia wa maisha ya Sasa kwasababu ilikuwa ni kabla ya uhuru, na kipindi kile dini ya kiarabu(Islamic) ilikuwa imetawala sana tofauti na wakati huu.
 
I'm trying to make the same argument on appointments that always seem to tilt in favour of one group (based on religion affiliation), I am trying to show them that whenever appointments are made in bulk, there has never been a single time when people from religion X are more in numbers than people of religion Y.
So my argument is, is it true that there are no enough people from religion X who have all qualifications required as compared to people of religion Y?

And why there has always been an observable pattern where people of religion X are always in a margin of about (20-25)% when a bulk appointment is done? —This has been true in the DASes, RASes, RCs, DCc, Ambassadors, DEDs, Ministers, Executive Secretaries and so on!

The argument that the number of people of religion X having qualifications is low to warrant a fair representation is futile because, There are thousands of their graduates coming out f universitiea every year.

When Nyerere was retiring in 1985 he said, he has successfully decreased the gap of education imbalance between Muslims and Christians, and he said that when he makes appointments, he no longer worry about having few people from Muslims conmunity, Now the question is, if by 1985 the education gap has been decreased significantly, then why on earth in 2021 we still see a large gap on appointments between Muslims and Christians where by the latter taking a lionshare of those? —Something is smelling fishy here!
So, are you saying that a Muslim president is prejudiced against Muslims?
 
Shida ya waislamu huana haya wanapopewa mamlaka makubwa kama hivyo. Huyu Mama sio kama hajui anajua vyema msuguano uliopo baina ya imani hizi, ila basi tuu kapuuzia kwasababu anazozijua yeye mwenyewe. Hivi kweli ndio hakuna waislamu wa kutosha wenye elimu na ujuzi wa kuwekwa ngazi ya utawala wa katibu mkuu walau kufanya ile ratio iwiyana walau kwa 40% hadi 50%. Basi tuu ufedhuli wa wenye mamlaka na dharau. Ndio mwisho yanatokea ya Mozambique halafu mnasema wamekosa ustahamilivu.
kwamba mlifikiri akiwa rais basi atapendelea upande fulani?
nadhani mna miss concept ya urais.
ni taasisi na hafanyi maamuzi mwenyewe.. majina yanapita vetting.. ambayo ime comprise mashirika ya ulinzi, na ya kiraia.
kama vetting cometee hamuitaki. andamana wafute
 
Labda tujiulize ni bias za makusudi au ni za kimazingira. Maana distribution ya dini au kabila huwa hazina usawa katika kila level. Let's assume umechukua list ya watanzania wote wenye PHD, distribution yao itakuwaje? Unaweza ukakuta katika hao probably Wahaya ni 10%, lakini population ya wahaya Tanzania sio 10% ya watanzania wote, au pengine ukakuta 70% ya hao ni wa dini fulani wakati hiyo dini doesnt not represent 70% ya watanzania.

Haya mambo ni complicated sana, hakuna majibu rahisi kwa sababu hakuna data pia.
Nimekuelewa vizuri hadi natamani mleta uzi akuelewe pia. Kwa kuongezea ,katika distribution let's say ya wenye PhD wakiwa categorized kwa dini je hizo PhD na uzoefu zinakidhi nafasi husika???Maana swala la dini ni very minor compared to technical experience and expertise in the required field , sijui kama mleta uzi amezingatia hayo!

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Hao 20 percent Muslims bado kuna watu wanamuona mama mdini.

Walitaka Muslim ikiwezekana wawe 1 percent I guess.

Hii nchi ngumu sana
Hapa mdini ni wewe. Bila shaka hata wateuliwa waislamu 60% hautaridhika.

Mbona mpaka sasa teuzi zinazolalamikiwa na kupigwa mawe sana ni za Phillip, Dotto, Lameck na huyu Thobias aliyetenguliwa. Wanaoshambulia ni wamisheni na waislamu na hamna mtu anayesema wakina Fatma wanawakosoa kwa sababu sio waislamu!

Mnakotaka kutupeleka siko.

Amandla...
 
Ukiondoa waislamu na wakiristo, hao wa dini nyingine ni wachache sana nchini, by the way hata nao wakiwa included serikalini haina shida tena ni jambo zuri tu.

Hata hivyo hoja yako haiwezi kuwa kigezo cha kufanya teuzi ambazo kiajabu sana zinalalia mno upande mmoja mpaka inaraise alarm
Nafikiri ili hii hoja iwe na mashiko
Uje na analysis ya kuthibitisha hio imbalance
Mfano uteuzi wa jana tuweke column ya dini afu tutafute ratio

Vinginevyo hizi zinabaki kuwa ni hisia
 
Ukitaka kulijua hilo vizuri anzia CHEKECHEA KABSA baadae njoo sekondari, baadae njoo vyuo vikuu then chukuo orodha ya wagombea wa nyazifa mbalimbali hasa ubunge na udiwani kupitia ccm kwa kila jimbo au kata nadhani utapata jibu sahihi. Labda kama ungesema ipo haja ya kufanya juhuudi za makusudi kabsa kupendelea upande flani kwani inaonekana dhaili unataka kumeza upande mwingine, lkn kumshutumu MTEUZI kuwa anapendelea upande mwingine unamwonea bure, na hii iko hivyo hata kabla ya uhuru, ukitaka kujua hilo chukua takwimu za watumishi wa serikali kabla ya uhuru na uanze kuwachambua then lete mrejesho.
 
Umesema vizuri kuwa nchi hii ni ya watu wote, sasa inakuwaje teuzi nyingi huwa zinalalia kwa watu wa dini moja kwa margin kubwa mno wakati shule tunazosoma ni zilezile na watu wenye vigezo vyote wanapatikana katika dini zote kubwa nchini—Je hii ni bahati mbaya au kuna watu huwa wanahakikisha hilo litokee kwa sababu zao za udini?
Mbona Zanzibar husemi waislamu wamependelewa mana ndo wamejaa huko?.
Ushasikia mkristo analaumu?.
 
Nimekuelewa vizuri hadi natamani mleta uzi akuelewe pia. Kwa kuongezea ,katika distribution let's say ya wenye PhD wakiwa categorized kwa dini je hizo PhD na uzoefu zinakidhi nafasi husika???Maana swala la dini ni very minor compared to technical experience and expertise in the required field , sijui kama mleta uzi amezingatia hayo!

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
Mimi nadhani watu wazingatie deliverables.

Kumpa mtu kazi kwa sababu ya dini yake ni udini, kumnyima mtu kazi kwa sababu ya dini yake pia ni udini.

Mtu akianza kuchukua pesa za shirika au wizara kwenda kufanya mambo ya kidini, hapo ndio tuanze kumletea shida. Hata Magu, kuteua watu wa kanda yake haikuwa shida. Tatizo ni alipoanza kupelekea vitu kwao ambavyo namna pekee vinaweza kwenda ni kwasababu yeye ni Rais. Hapo ndio tabu ipo.

Kumuambia Rais balance dini, mimi nawaza how do you do that practically? Maana ukiwaambia wasaidizi nipeni composition fulani ya kidini, tayari unakuwa umeleta udini.
 
So what ,tumekubali kwamba Zanzibar na tanganyika ni taifa moja so nao wajiandae ipo siku mkiristu atakua mkuu wa nchi TOKA bara na mikoa yote itakua nusu KWA nusu Kama ambavyo tz kwamba bila ukabila ,dini jinsia kiongozi twampenda
Wakristu wa Zanzibar hawafiki hata asilimia moja. Ndio maana hawalalamiki. Kwasababu wanapewa kikubwa kuliko wanachostahili.
 
Back
Top Bottom