Tundu Lissu: Acheni kutunga uongo, mshaurini Rais Samia awataje na kuwakamata walionishambulia

Tundu Lissu: Acheni kutunga uongo, mshaurini Rais Samia awataje na kuwakamata walionishambulia

Shukuran ya punda ni mateke, Lisu siku zote anachoangalia yeye ni tumbo lake na sio wema wa mtu yoyote. Kuhusu waliomshambulia aruhusu dereva wake aje ahojiwe na polisi ili waliomshambulia waweze kukamatwa kama anavyotaka. Angalie njia nyingine ya kutafuta pesa za kumlipa Amsterdam.
Dereva wa Lissu angekufa hao waliomshambulia wasingekamatwa ?
 
huyo mbelgiji wa ikungi akae kwa kutulia huko aliko hana jipya sasa...
 
Ndugu Igu,tuletee chanzo halisi cha taarifa yenyewe ili turned pamoja,kushindwa kufanya hivyo taarifa hiyo una maslshi binafsi nayo.
Kizazi cha nyoka mnamatatizo sana.
Screenshot_20210620-194706.png
 
Siasa za nilipigwa risasi 30 hakuna anaezifatilia aisee Lissu ajipange upya alipata umaarufu kwa siasa za JPM kwa mama ataonekana kituko.
Lissu alikuwa relevant kwenye politics toka 1995 mpaka leo sembuse na awamu ya special groups ?
 
Huyu lissu atapevuka lini,atulie huko ubeligi kwa bwana zake ,huku sisi tuko bize kijenga nchi
 
Kama Sabaya aliweza kuoperate genge la uporaji na utesaji , haitoshangaza kama Mama Samia hajui kwa 100% ni nani haswa aliyeexecute ile assassination attempt kwa kuwa alikuwa sidelined kwenye mambo mengi. Hata kama anajua, hatosema au kufanya kitu, atleast hadharani.

Lissu anahitaji kumove on. Hizo “haki” wala hawezi kupewa tena kwenye plate. Akiwa kawa lawyer mbobezi, nadhani analielewa hili. Ni bora hata kwenda kortini na kupambana huko
 
Kiki at work. Mwendazake keshaondoka. Lissu kama anajiona ana haki aje afungue kesi au afungue huko huko alipo si kuna mahakama za kimataifa
 
Wengine mnaongea kirahisi tu, pigweni nyie marisasi yote labda akili zenu zitakaa sawa, mtaacha kuandika pumba humu. Kifupi serikali ya mama Samia ni serikali inayohitanabaisha ni serikali ya mapatano,maridhiano, Maumivu aliyopitia Lissu ni makubwa na serikali zote za CCM zina deni la risasi zote zile, na sisi wafuasi wa upinzani tunahitaji closure .... haki ipatikane kwanza ndio KAZI IENDELEE...
 
Huyu pungu kweli! Mdomo wake huo unaobwabwaja na kutusi kila mtu hautoshi kutoa ushauri kwa mama eeh🤔!? Dereva waliomficha na Mbowe wake ndio awashauri wajitokeze na kutajana na walipane wenyewe kwa wenyewe! Na kama nchi kwa yote ya hovyo aliyoipakazia nchi yetu na JPM wetu pia tutahitaji 'compensation'!
Kama ni kweli JPM alitaka kumdhuru mbona harudi nchini baada ya Mh. Dr JPM (Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi amen) kuitwa na Muumba wake!?
Waliozaliwa kwenye vigodoro kama huyu utawajua tu. Lugha zao ni chafu na zinakera.
 
Na driver pia tushinikize asaidie uchunguzi
Hili suala linaweza kua rahisi sana endapo kila mhusika atashiriki kwenye uchunguzi.

..I agree with you.

..lakini nadhani hatua ya kwanza ni Raisi kuunda TUME YA KIJAJI YA UCHUNGUZI.

..Tume ya namna hiyo ina mamlaka ya kuita mashahidi na anayekataa wito anakuwa ametenda kosa la jinai.

..lingine ni serikali kuwatumia INTERPOL kumhoji Adam Bakari dereva wa Tundu Lissu huko Ubelgiji alipo na ikilazimu kuomba Polisi wa Ubelgiji wamkamate na kumrejesha nchini.

..Binafsi naamini Watz wengi wanaunga mkono uchunguzi kufanyika na waliohusika kufikishwa mahakamani.
 
Back
Top Bottom