Tundu Lissu akamatwa na Polisi akiwa Ngorongoro hotel Wilayani Karatu
Kuna muda mnatetea ujinga na upumbavu hata bila kujishtukia, umeulizwa population inaongezeka Ngorongoro na Loliondo pekee!?, Kwanini hizi kelele ziliibuka kipindi Cha Mwinyi na waarabu na kipindi hiki Cha Samia na waarabu!?,pupolation ya maasai inaongezeka Tanzania tu!?,mbona Kenya hakuna huu upuuzi?,wakati mwingine ni busara kuficha upumbavu wako kuliko kutetea mambo yaliyo nje ya uwezo wako wa kufikiri.
Kuna wakati mnajiona kujua kumbe vichwa vimejaa ujinga. Population aiwezi ata siku MOJA itakua kwa kuringana. Maamuzi yetu ya ndani sio lazma tufuate ya Kenya.
 
Even yourself,you started here as a new member,don't bother na sisi tukinufaika na Forum hii,tujadili hoja iliyopo mezani,acha uoga
SAWA.
Hebu basi turudi mwanzao, ulikoanzia.

Hebu tueleze jinsi swala la 'DP world' lilivyo 'fail' unavyodai wewe?
 
Huyu mwehu wamechelewa sana kumkamata. Ilitakiwa alipoanza tu kuongea hovyo. Siku hiyo hiyo anagtiwa adabu, wengine wote wangetia akili.
Ukweli nikua CHADEMA tunakosea sana kumtanguriza Lissu kwenye mambo ya kitaifa
 
Katibu mkuu wa Chadema mh John Mnyika amesema wamewafuatilia Viongozi wao Waliokamatwa kwenye Vituo mbalimbali vya Polisi Bila Mafanikio

Mnyika ameliomba Jeshi la Polisi liufahamishe Umma walipo Viongozi hao

Ahsanteni
Mimi ni Mtanzania wala sina haja ya kujua wako wapi. Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga, acha wayaoge.
 
As population keep on growing mazingira ya mbugani ambalo wamasai wanaishi na mifugo Yao watagharim future ya mbuga zetu na wanyama,labda kama hujafika maeneo hayo basi huwezi jua uhalisia uliopo
Wengine hawajafika wanabwabwaja tu. Hata kama hawajafika wachukue mfano baadhi ya maeneo nchini miaka ya nyuma maeneo yalikuwa makubwa lakini baada ya miaka mingi kupita na watu kuzaliana maeneo yamebaki madogo.
 
Sasa unadhannnani kashinda katika suala Hilo?unadhan unaweza shindana na serikali smart kama hii inayoongozwa na Malkia Bilkis,Quen of shebah Dr Samia?
Midomo ya Malaya hudondoza Maneno Matamu kama Asali, Refer to JK.Nyerere Viongozi Wenye Tabia za Kimalaya malaya. Ndo Hawa wa sasa na Maneno yenu ndo haya ya Kupambiana.
 
Polisi wanapotezea watu muda tu.
Polisi ni "kifaa" tu kinachotumiwa na mtu anayekitumia.

Kuna umuhimu wa kulitambua hili. Matumaini yangu ni kwamba CHADEMA wanaelewa vizuri maana ya hili, ili waweke mikakati ya kupambana na mtu anayekitumia kifaa hiki isivyostahili.
 
Unahisi unajua sana kuliko wanasheria wao?
Fani ya sheria ni moja ya fani bahari, you can just swim as much as you can at any direction depends on uwezo wako wa ku swim ni unaogelea tuu.

Fani ya sheria haiendeshwi kwa hisia ni vifungu tuu, hivyo sio issues ya kuniuliza kama ninahisi ninajua kuliko wanasheria wao, mwanasheria mkuu wa Chadema ni TL, wakati wa mchakato wa katiba ya Warioba Chadema walisusa. Katiba pendekezwa ilipowasilishwa Bungeni, Chadema wakasema wanapinga, Bunge limeweka utaratibu wa kuwasilisha pingamizi, TL badala ya kuwasilisha pingamizi, alitoa go ahead mchakato uendelee kwa kuwasilisha a go ahead badala ya kuwasilisha pingamizi!. Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Ile Ripoti ya CAG iliyoleta kizaa zaa, JPM aliipokea akala kobiz asiiwasilishe Bungeni, ni mimi nilimtonya Blaza kuwa Je, wajua kikatiba, CAG ana hadhi ya Jaji Mkuu?. Je, wajua ripoti ya CAG ni Zaidi ya Bill?. Je, wajua kwenye ripoti ya GAG, CAG ni zaidi ya Rais ?
Serikali haina wanasheria wa kulijua hilo?.

Blaza akamtonya yule Mkuu wa Mjengo kuwa wagome kuipokea ripoti ya CAG na waheshimiwa wale walivyo mazuzu wakapitisha Azimio la kizuzu la Bunge kuwa Bunge halitapokea ripoti ya CAG, ni mimi ndio niliwatonya kuwa Azimio lao ni la kizuzu Je, Wajua Bunge linaweza kutoa azimio batili? CAG yuko kikatiba. Je, Bunge lina uwezo kutopokea ripoti ya CAG?

Na nikawaambia kitakacho wakuta kama wasipoipokea ripoti ya CAG Je, Wajua Bunge linaweza kuvunjwa Siku 7 Zijazo?. lisipopokea ripoti ya CAG, Bunge linavunjwa kwa mujibu wa Katiba ndipo wakalichomoa Azimio batili lao kimya kimya, wakaipokea ripoti ya CAG!. Kwani hawana wanasheria?.

Mtu akiisha kamatwa na polisi na polisi wakatoa taarifa ya kuwashikilia, utaratibu sio kuita press conference, bali ku file harbeas corpus.

Hii sio mara ya kwanza kwa Chadema kutumia wrong ways ku deal na serious issues Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?

Legal issues zinahitaji legal redress na sio kila kitu ni politics!.
P
 
Anawaachia wenye vihelehele na kutaka misifa ya kijinga
Saa hizi Mbowe yuko kwenye meza ya chakula na familia yake wanaangalia tu wenye vihelehele wanavyohenyeshwa huko polisi.

Ama kweli kila mchuma janga hula na wa kwao.
 
Hili ni bamgo walilobeba polisi wakati wamzuia Lissu asiende Ngorongoro, linasema nini?!

5D40C017-3DFB-49AC-B771-4C3BE55E36D5.png
 
Mkuu Ndo maana Nimekusisitiza sana kusoma "Journal" mbalimbali za Kitaifa na za Kimataifa Sanasana jikite kwenye Journal za Reseaerch pamoja na Statistics Kadhaa utagundua kinachosemwa kwenye siasa hakina UHALISIA zaidi ya kuwapa moyo wananchi ila kwakuwa kaka yako nipo ni jukumu langu kufanya facts check mbalimbali kwako ili nikujengee uwezo wa kupambanua vitu...

Wamasai wanamiliki 'Ngombe wengi huko Kenya alafu hao wamasai ndiyo wenye mifugo mingi kwenye Taifa lenye n'gombe wengi hapa Afrika mashariki na kati wakiwa Tanzania. Hivi hizi ni akili kweli?
FACTS CHECKS....
Nakubaliana na Wewe kabisa kwamba Tanzania Ni Nchi yenye Ng'ombe zaidi Katika East Africa na inakadiriwa kufikia mpaka Milion 33 na pia kwa makadirio kama 24.5 mbuzi na kondoo kama 8milion ikifuatiwa na kenya ambayo yenyewe inakadiriwa kufikia 27miliion ya Ng'ombe....

Sources ya data kutoka (statistics Africa pamoja na nbs) pia unaweza kusoma jarida la LIVESTOCK SECTOR TRANSFORMATION PLAN (LSTP) 2022/23 - 2026/27....lililotolewa na MINISTRY OF LIVESTOCK AND FISHERIES

Sasa mimi Sikuzungumzia Mifugo yote Tanzania Mainland Mkuu naona umenichangany Nilizungumzia mifugo iliyoko Ngorongoro ambayo ni only 1.5% ya mifugo yote iliyopo Tanzania bara ambayo kwa hesabu ya haraka ni kama laki tano hivi...

Differ from Tanzania (ambapo tuna makabila Zaidi ya 120 na makabila ya wafugaji Yanafika makabila zaidi ya 50) na only makabila machache sana sio wafugaji...
kenya wana makabila machache zaidi ya wafugaji na la kwanza likiwa ni kabila la wamasai...
mbali na kuwa wafugaji naendelea kusisitiza kuwa kwa mujibu wa sensa ya kenya bado wamasai wamekuwa ni kabila linalokuwa zaid huko kwao na bado hawahamishwi kwenye Hizo mbuga...
nakupa kidogo statistics ya makabila kwao....

(Wamasai 23 % ,Waluhya 14%,Wajaluo 13%,Wakikuyu 12%,Wakalenjin 12%,Wakamba 11%,Wasomali 8%,Wakisii 6%,Wameru (Meru) 6%,Waturkana 10% e.t.c)
sasa nafikiri kwa hoja hiyo nimeweka wazi na nimeionyesha....

Mtu anasema eti mbona hifadhi za Kenya awaondolewi? Hivi wanachofanya Kenya ni lazma nasi tufanye hivyo? Hizo Mbuga za Kenya zinayo hadhi kama ya Ngorongoro au na ili mpaka turudi darasani?
Yeah sina maana kwamba tuanze kufikiria kama wanafikiria wakenya au tufanye kama wanavyofanya wakenya ila nna maana ifuatayo kama Hilo swala lilikuwa lina Faida sana kufanya hivyo nafikiri kenya wangeanza kulifanya kwani wao wana Idadi kubwa ya Wamasai kuliko hata idadi tulionayo sisi....

kenya hawana mbuga zenye hadhi ya ngorongoro...
Hivi wewe ndo unasema au mtoto kachezea simu kaandika ulichoandika

Natamani Nikwambie Urudi darasani lakini Hapana wewe ni Mtu mzima mwenzangu Pale unapokosea tunarekebishana tu....

ngoja nikupe report ndogo ya Hifadhi za Taifa za Africa zenye Ubora wa kuwa mbuga bora na maeneo makubwa zaidi ....

kwa Africa inayoshika namba moja mpaka sasa Bado ni serengeti inaukubwa wa eneo la Kilometa za mraba 14,750 ikifuatiwa na Hifadhi ya kruger ya afrika kusini yenye ukubwa wa mraba kilometa 19,485 ikifuatiwa na chobe ya botswana ambayo ina ukubwa wa km za mraba 11700 halafu inafuatiwa na Masai Mara ya kenya Yenye kilomita za mraba 1510 cha ajabu mpaka utafika namba kumi bado hakuna tena Mbuga au hifadhi yoyote ya Africa mashariki.....

Na tunapozungumzia Ubora wa Mbuga au hifadhi hatuzungumzii Ukubwa wa eneo tunazungumzia idadi ya wanyama,Aina ya wanyama sanasana upatikanaji wa Big5,Wonders na baadhi ya Family Au upatikanaji wa species za wanyama mbalimbali....

na ndo maana utaona hapo Yenye ukubwa zaidi ni kruger ila haikuwHi kushika namba moja Africa...

Sasa Kwa Ubora wa Mbuga Ngorongoro haifiki hata kidogo kwa Masai mara ya Kenya....

ambapo sasa Ngorongoro eneo walilopo wanyama ni eneo dogo Tu ambalo ni eneo la crater au Eden ila eneo zima la Ngorongoro ukijumlisha Ngorongoro Crater ukiniuliza kwa ukubwa ni 8292 kilometa za mraba...

Nafikiri umenieleza And thats Why haiitwi Natinal Park inaitwa Ngorongoro Conservation Area...

Ni hasara hipi nchi inapata kuwaondoa watu hao wanao leta madhara kwenye hifadhi ya Ngorongoro?
Mkuu samahani kidogo.kwa hili swali inabidi nikufanyie "sarcastic" kidgo Una miaka Mingapi?????

maana Kama ni mtu mzima ulichoandika kinaenda kinyume na umri wako kama ni Mtoto jitahidi upitie historia za wakubwa waliokutangulia utajifunza mengi...

Mkuu kwanza unajua Maana Ya Ngorongoro Kutoitwa National Park na ikaitwa Conservation Area "ok then nafurahi kukupa Elimu hiyo"

NGOJA NIKUCHAPE SHULE....

Kwanza Ngorongoro Conservation Area ilikuwa established Mwaka 1959 ikiwa ni Jitihada za serikali Kutambua mchango wa Watu wenye Asili ya kutoka mwambao wa mto nile ( Au unaweza waita nilotic people) au kwa sasa wanafahamika kama Wamasai.....

Story Iko hivi Maa-speaking people au maasai walikuwa wakitoka kutoka huko Mwambao wa mto nile wakipits sudani,Ethiopia na nchi zingine kuja Afrika ya Mashariki ili kutafuta Makazi na malisho ya Mifugo yao Mnamo miaka ya 1800s Kwa bahati nzuri walifika sehemu za huko Kaskazini mwa Tanzania ndo wakavumbua Ngorongoro....
japo walipigana ili kuwaondoa watu wa kabila la mbulu ambao wao walikuwa wakulima katika eneo hilo...Wamasai wamekuwa wahifadhi wa eneo hilo Tangi miaka hiyo kwa miaka takribani 250 sasa.....

Sasa Masai wamekuwa ni kivutio katika Ngorongoro na kama kitambulisho cha Mbuga hiyo kwa miaka zaidi ya 200 halafu unakuja unauliza kabisa kwamba Eti
wakiondolewa kuna hasara gani...Wazungu hawaji kuwaona Simba ngorongoro au swala wangetaka wangeenda serengeti au manyara...Wanaenda kuona pia utamaduni wa kimasai ambal pia ni kivutio cha utalii...

Sasa Nataka UJUE kingine hiki kwamba Ngorongoro Haiko chini Ya TANAPA iko chini ya NCA Ngorongoro Conservation Area...
ngoja nikupe key za eneo kuchukua sifa hizo... Yaani kuwa na conservative property ...

kwanza huwa ni Multiple land Uses,Human settlements,Cultiral and historical significant, Geological Features na Management approach

So nakuomba please kama hujaelewa ruksa kuuliza ili usije kuongea vitu usivyovijua tena
 
Back
Top Bottom