Tundu Lissu: Aliyeongoza Kikosi cha wauaji walioagizwa kuniua ni Paul Makonda, ndio maana Marekani ilimzuia

Tundu Lissu: Aliyeongoza Kikosi cha wauaji walioagizwa kuniua ni Paul Makonda, ndio maana Marekani ilimzuia

Ni hatari sana watu wajinga kujihusisha na siasa, hawa hua na kauli mbaya, wachonganishi, wapambe na hutumia mamlaka vibaya kwa kuua na kukamata/kuteka ovyo maana hawana hoja.

Nashauri siasa iwe marufuku kwa watu aina ya Makonda, Msukuma na wengineo hawajui chochote huko wanaharibu Nchi.
 
Kwa huo ufisadi aliofanya na hao wawekezaji asingefunguliwa mashtaka mahakamani na serikali ili makosa yake yathibitike kisheria badala ya kuuawa?
Kwa swali kama hili inaonyesha wewe ujui ufisadi wa kibeberu ...kwanza aliye kuambia mafisadi ya kibeberu yanashitakiwa nchini ni nani ? Kesi ya mtoto wa chui kuipeleka kwa mama chui tena mwenye njaa.
 


Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara Tundu Lissu amezungumza hayo mbele ya wanahabari leo, Jumatano Septemba 25.2024, jijini Dar es Salaam

Kiongozi wa kikosi cha mauaji dhidi yangu mwaka 2017 alikuwa Paul Makonda. Aliwaongoza wauwaji walionipigia risasi 36 Dodoma.” - Tundu Lissu

View attachment 3106495

"Shambulio dhidi yangu (shambulio la Tundu Lissu kupigwa risasi) limetokea katikati ya majengo ya serikali wanayokaa Mawaziri, Naibu Spika Tulika akson kwa wakati ule (sasa ni Spika wa Bunge), Waziri Harrison Mwakyembe (aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo), Waziri wa Nishati wa wakati ule yeye alikuwa anakaaa juu na mimi nilikuwa nakaa chini" -Lissu

Pia soma:

- Kupigwa risasi kwa Tundu Lissu: Kampuni ya simu ya Tigo yadaiwa ilivujisha mawasiliano yake kwa mamlaka

"Katika majenho ambayo yana ulinzi na yanakaa wakubwa (viongozi wa juu/waandamizi) eneo hilo lilikuwa sio tu lina ulinzi masaa 24 bali lilikuwa vilevile na kamera za CCTV, na kama mtakumbuka baada ya shamhulio hilo aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma alikuwa anaitwa 'Mroto' alitangaza kuwa Polisi walikua wamepata ile picha za hiyo CCTV kamera iliyokuwa inatazama ile parking lot ambayo nilikuwa nimeshambuliwa" -Lissu


PIA SOMA
- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali
View attachment 3106568

Itafahamika tu
 
Moja ya maneno yaliyonishutua ni Lissu kusema vijana wawili waliomshambulia kwa risasi wanawajua na watawataja.

Kingine ni pale aliposema siku ile anashambuliwa. Makonda alikuwa Afican Dreams(kama sikose hii ni hoteli iliyoko Dodoma).

Mungu fundi sana.
 
Chadema akili hamna kama wewe unaweza kubishana hata na lissu pale atakapo sema ukweli ? Mbona lissu anajipendekeza kutaka kwenda kwenye kaburi la jpm kuhiji ....ulishajiuliza way? Lissu anaujua ukweli wote juu ya kupigwa kwake risasi.
Kawaambia serikali ilete wachunguzi huru imekataa sasa wewe unasema nini.
 
Nimeamini usemi unaosema hakuna marefu yasiyo na mwisho.wanaojifanya wasiojulikana watajulikana waziwazi.maana mahakama za huko uingereza Samia hawezi kuwapigia simu majaji kuwapa maelekezo ya kupindisha haki.kama anaubavu ajichanganye kuwapigia majaji wa ulaya aone kesi atakazofunguliwa.
 
Moja ya maneno yaliyonishutua ni Lissu kusema vijana wawili waliomshambulia kwa risasi wanawajua na watawataja.

Kingine ni pale aliposema siku ile anashambuliwa Makonda alikuwa Afican Dreams(kama sikose hii ni hoteli iliyoko Dodoma).

Mungu fundi sana.
Awataje kwa majina hao Watu waliompiga risasi ili tuwajue, asifiche utambulisho wao.
 
Back
Top Bottom