Uchaguzi 2020 Tundu Lissu atua Katoro - Geita kwa kishindo

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu atua Katoro - Geita kwa kishindo

Wakati kesho tukijiandaa kwa mkutano mkubwa Katoro, muda huu Tundu Lissu ametua hapa na umati mkubwa umejitokeza kumsindikiza.

Kwa hakika lipo la kujifunza kwa watu wa CCM. Msijifanye hamuoni kinachoendelea!

Video: Katoro Geita
View attachment 1578469
Huyu ndiyo tunayemtaka atuongoze kwa haki uhuru na maendeleo ya kweli kwa watu wote
 
Umeshafungua hiyo video hapo juu mkoani geita inakopatikana wilaya ya chato?

Huwezi kulinganisha mikutano ya mpayujaji Lissu na ya Rais JPM, wala Makamu Samia, wala PM Majaliwa, huu ndio ukweli mchungu kwa cdm na wale mnaomchukia JPM na Serikali yake.
 
Wana weweseka ,walisha tamba Miaka 5 na mamiradi wakati Raia wana taabika.Hata walio patwa na Majanga hawakusaidiwa zaidi ya kusimangwa na kudhihakiwa.

Baada ya uchaguzi 28/10/2020 wembe ni ule ule hakuna nafasi ya ule upuuzi wa kuendeleza mikutano ya hadhara ya kisiasa isiyo na tija yeyote. Kaa ukijua hilo.
 
Huwezi kulinganisha mikutano ya mpayujaji Lissu na ya Rais JPM, wala Makamu Samia, wala PM Majaliwa, huu ndio ukweli mchungu kwa cdm na wale mnaomchukia JPM na Serikali yake.

Unaandika nadharia tu kutoka Kichwani kwako kwa kusukumwa na unacho kijua ,ukiambiwa ithibitishe uropokaji hauwezi.Mzee wako anaisoma tu Ilani ya Chadema na ku'copy and paste.
 
Baada ya uchaguzi 28/10/2020 wembe ni ule ule hakuna nafasi ya ule upuuzi wa kuendeleza mikutano ya hadhara ya kisiasa isiyo na tija yeyote. Kaa ukijua hilo.

Tunajua mmezoea kuvunja Sheria hata zile mlizo zipitisha wenyewe Bungeni ma CCM ,ni kawaida yenu ila ni ajabu na haifai kwa Chama cha Siasa na wana Chama kushabikia uvunjwaji wa Sheria za Nchi.

Tunapo sema CCM haifai tuna maanisha ..
 
Hata huoni Tena ya Leo funga kazi hizo picha kama za nchi ya Burkina Faso angalia na usikikize wasindikizaji lugha wanayoongea hata haieleweki Ni ya wapi.Hongera Sana Kitengo Cha uchakachuaji picha Cha Chadema.Mumetisha leo
😂😂😂😂 poleee mataga!!! Naona mmeumia sana shujaaa wa Mungu kukubaliwa kwa kishindo na wana Geita eeh????

Tulieni tu, tuliwaambia mtajua hamjui mwaka huu


Lissu ndo Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025. Mtake msitake
 
Tunapo sena Lissu ni kibaraka na adui wa Taifa hili la Tanzania tunamaanisha hivyo pia.

Sawa ,ndio sababu mlijitahidi kumuua lakini Mungu akalikataa hilo kwa Mkono wake akamuepusha na Mauti.Hichi kisingizio cha kumtuhumu Mtu kuwa ni kibaraka hata ANC ya wakati huo iliitumia hii Sababu yenye nia ovu na kuwa nyanyasa Raia wengine walio kuwa wakiwakosoa..
 
Kama upinzani wakitaka mwamko wa maandamano nchi nzima, hapo katoro ndio sehemu ya kuanzia mji mdogo lakini unaamsha sana... Mji uliojaa matukio ya kila namna.
===
Hawa watu sio waongeaji sana japo wanavitendo hatari nakumbuka miaka ya nyuma walishawahi kubomoa kituo cha polisi.. Yaani wanaume wanabomoa na kuchoma magari yale yanayokamatagwa na askari wakati huo askari wanarusha mabomu ya machozi, cha ajabu wanawake walikuwa wanawaletea wanaume maji ya kunawa ili waendelee na uharibifu..chanzo cha vurugu hizi ni kwamba polisi wamemshikilia mama mmoja aliyekuwa anadaiwa mchawi.
=
=
.
Tukumbuke miaka ya nyuma sakata la waislamu na wakirsto kuchinjana kisa walalamikiana suala la kuchinja mifugo machinjioni lilianzia hapo.
Waislamu walichoma bible na wakristo walichoma Quran hadharani.. Tukio lilipelekea mchungaji kuchinjwa na waislamu huku wakristo wakimalizia hasira zao kwa kubomoa maduka ya waislamu.
.
Hapo ni mpakani mwa wilaya ya chato na geita vijijini hapo nyuma ikiwa mpakani mwa kagera na mwanza..
.
Kiufupi katoro ni mji wa kuogopa sana tena sana tu.
.
Way back kwa Mara ya kwanza nilihudhuria mkutano wa chadema 2009 uchaguzi wa marudio Hapo katoro jimboni busanda. ndio Mara ya kwanza nilimuona Tundu Lissu alikuwa kavaa t.shirt ya chadema na kofia zile za miti huku kashika tablet Mkononi.Nakumbuka Finiasi magesa mgombea wa Chadema alishinda lakini akamuuzia ubunge bi Lolensia bukwimba wa CCM.
=
.
Siku moja nitarudi huko.
Msalimie lissu mleta mada mwambie finiasi magesa alitulaza nje kisa kufuatilia matokeo yake.
..
Hongera katoro hongera Lissu.
We unaona sifaa kukitokea machafuko. We unafikiri yakitokea utajificha na familia yako kwenye keyboard ya Computer au ya simu. Embu muwe mnashirikisha ubongo kabla ya kukaa kuandika ushabiki wa uvunjifu wa amani.
 
Wakati kesho tukijiandaa kwa mkutano mkubwa Katoro, muda huu Tundu Lissu ametua hapa na umati mkubwa umejitokeza kumsindikiza.

Kwa hakika lipo la kujifunza kwa watu wa CCM. Msijifanye hamuoni kinachoendelea!

Video: Katoro Geita
View attachment 1578469
View attachment 1578537View attachment 1578539View attachment 1578540View attachment 1578541View attachment 1578542View attachment 1578543View attachment 1578544
View attachment 1578469
Chadema hii sasa sifa! Khaaa!!!
 
Sawa ,ndio sababu mlijitahidi kumuua lakini Mungu akalikataa hilo kwa Mkono wake akamuepusha na Mauti.Hichi kisingizio cha kumtuhumu Mtu kuwa ni kibaraka hata ANC ya wakati huo iliitumia hii Sababu yenye nia ovu na kuwa nyanyasa Raia wengine walio kuwa wakiwakosoa..

Mungu kamfundisha Lissu kuona kionjo cha madhila ya wale aliokuwa anawashawishi kupambana na vyombo vya dola na wakadhurika na kupoteza maisha. Msmidanganye Lissu mwambine ukweli ili apone. Ziko damu bado zinamlilia za wale alio wahadaa tena bado hazija nyamaza, ukweli mchungu huu.
 
We unaona sifaa kukitokea machafuko. We unafikiri yakitokea utajificha na familia yako kwenye keyboard ya Computer au ya simu. Embu muwe mnashirikisha ubongo kabla ya kukaa kuandika ushabiki wa uvunjifu wa amani.
Kikubwa ni Haki
 
Hata huoni Tena ya Leo funga kazi hizo picha kama za nchi ya Burkina Faso angalia na usikikize wasindikizaji lugha wanayoongea hata haieleweki Ni ya wapi.Hongera Sana Kitengo Cha uchakachuaji picha Cha Chadema.Mumetisha leo
Kwahiyo lissu alikuwa Burkina faso leo. Tafuta panadol umeze
 
Back
Top Bottom