Uchaguzi 2020 Tundu Lissu (CHADEMA), aomba mdahalo na Dkt. Pombe Magufuli (CCM)

Kuna tofauti kubwa kati mdahalo wa urais na mipasho..... Kama alikua hajui Magufuli ni mtu wa kazi zaidi ya maneno na sasa anafanya kampeni ya kisayansi

Wewe utakuwa ni mwenye ile hotel pale Mwenge.. Si bure.
 
Sisi tunataka kusikia sera na sio mashindano ya midahalo. Kwanza anatakiwa ajue Magufuli anafanya mambo mawili makubwa kwa wakati mmoja kuendesha nchi kama rais na kuendelea na kampeni na mambo yote kaweza kuyamudu vizuri sana. Chadema mwambieni mgombea wenu asimpotezee muda jemedari
 
Sasa kama ni kujinadi kuzunguka si kwatosha?

Na kama ni sera mgombea wa CCM ameishaziongelea?

Na Tundu Lissu nae si bado azunguka?

Sasa midahalo ya ni?

Kwani kinachohofiwa kwenye mdahalo ni nini? Mbona mnahangaika hivi? Mnaelewa hapo kuwa mtu wenu hamuwezi Lissu kwa hoja, sasa mnajaribu kufunikafunika.
 
Huyu mgombea wetu hana adabu kabisa sijui kalelewa na mzazi mmoja? Wanachadema wenzangu nisaidieni kunielewesha juu ya mgombea wetu lissu, kwani mdahalo ndo utampa kura? Akafanye midahalo na Robert Amsterdam,
Mbona mnamficha magufuli kama msukule?
Mwacheni apambane na wanaume wenzie.
Kuongoza nchi sio mashindano ya urembo wala vijembe.
Amepata mshindani kwani alitamba sana miaka mitano akifokafoka na kutukana.
Mleteni hadharani apambane
 
Anatapatapa sasa ameshindwa kuwa win watz! Hatuhitajj mdahalo sisi bali tunataka utuambie umefanya nini na utafanya nini tukikupa kura zetu! Hatuko kwenye mashindano ya mdahalo!

Amefanya nini Kwani amewahi kuwa Rais, ni vema kuwepo na mdahalo ili kuhojiwa namna wanavokusudia kuiongoza hii nchi aliyekuwepo madarakani pia atwambie kama anakusufia kuendeleza ukandamizaji wa haki na uhuru wa wananchi kwa kuendelea kutunga sheria za kutubana au tutegemee nini na huyo a,baye hajawahi kutawala atwambie anataka kufanya kipi tofauti na aliyetawala na mkakati wake ni upi. Mdahalo ndo njia pekee ya kuelewa maono ya kila mgombea.
 
Naunga mkono mdahalo huu, na kwa nyongeza naomba uendeshwe kwa lugha ya kiingereza ili dunia nzima ielewe.!!!
 
Lengo la mdahalo ni nini?
Kama ni utendaji wote tunajua kwa sasa JPM hana mpinzan

Sisi hatutaki kuchagua Rais wa nchi yetu kwa mazoea tunataka mdahalo tuweze kujuwa tofauti ya maono yao hatutaki kuwa na kiongozi ambaye hatujuwe atatupeleka wapi hii miaka 5 ijayo
 

Binafsi nafikiri Lissu ni mzuri. Ila nafikiri wewe unataka kuwajaza watu ujinga ili waamini Lissu na Magufuli wote hawajui Kiingereza.
 
Hahaha Mdahalo tena? Leo hata Mseven alijua alitoa hotuba kwa lugha tatu, Kizinza, Kiswahili na kiingereza. Nakila alipoongea Kiingereza alisisitiza kutafsiri.
 
Unadhani Urais ni midahalo??

Wenzetu wanafanya midahalo huo urais wa kupewa kificho kwa watu wasio nasifa sasa basi tunaanza na mdahalo wa urahisi halafu na wengine wote watakuwa wanafanyiwa interview katika nafasi kubwa tena zinakuwa wazi kama wanavofanya kenya tusiendelee kuongozwa na watu wasikuwa na uwezo hata wakujieleza matokeo yake kuogopa kwenda kukutana na marais wenzako kwa kisingizio cha kubana matumizi
 
Mimi na wewe ni watu wa kawaida sana.

Hata Tundu Lissu ni mtu wa kawaida sana ukiondoa sifa yake ya ugombea uraisi.

Uchaguzi ukiisha atateremka atatulia.

Tundu Lissu ana kitu chaitwa "personal hatred" kwa JPM na hiyo iko wazi.
Waswahili tunsema kikulacho ki-nguoni mwako. Jamaa hajafungua akili kuangalia kwa kina kujua ni nani aliyetaka kumuua. Yeye anaamini kuwa ni Magufuli tu ndiye aliyetaka kumuua bila kujua kuwa Magufuli kwa position yake kama rais alikuwa na njia nyingi sana za kumhandle. Kibaya ni kwamba, ile kurupuka ya kulaumu serikali ilivuruga sana nguvu za serikali kufuatilia jambo hilo. Tunasahau kuwa miaka ya nyuma kidogo Dr. Mwakyembe naye alikumbana na kadhia ya kufuatiliwa na baadaye kulishwa sumu.
 
Binafsi nafikiri Lissu ni mzuri. Ila nafikiri wewe unataka kuwajaza watu ujinga ili waamini Lissu na Magufuli wote hawajui Kiingereza.
Inawezekana na wewe hujui kiingereza; unaweza kujua kuasiliana kwa kiingereza bila kukijua vizuri kama Lissu na Magufuli walivyo.
 
Ikishakuwa serikali ya majungu hayo ndiyo matokeo yake.

Kuna sheria kanuni na taratibu zilizotungwa kutoka kwenye katiba.

Sio kufanya kazi kwa hisia. Hata kama hupendi jambo lakini unabanwa kisheria ni wajibu wako kutekeleza.

Huu upuuzi ndiyo tunausikia eti mkichagua upinzani hampelekewi maendeleo.

Sasa sijui ukishachagua upinzani unakuwa nchi nyingine.
 
Jamani mtasababisha mtu apatwe stroku hivi wewe mtu hawezi kuongea hata sentesi mbili za Kiingereza leo ndio umpe mdahalo ? .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…