Pre GE2025 Tundu Lissu: Hatutasusia Uchaguzi, tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya Umma, sio bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi

Pre GE2025 Tundu Lissu: Hatutasusia Uchaguzi, tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya Umma, sio bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa Tundu Lissu akizungumza wakati wa mkutano kati ya CHADEMA na Jukwaa la Wahariri (TEF) unaofanyika siku ya Jumapili Machi 2, 2025 Makao Makuu ya CHADEMA, Dar es Salaam

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"Sasa shida iko wapi? Kwanini kila tume inayoteuliwa (Ikiwamo Tume ya Jaji Warioba) inasema tufanye mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi? Huu mfumo wa uchaguzi una shida gani hasa? Na hii shida hii ndiyo inayoelezea sababu ya bila mabadiliko hakuna uchaguzi."

"Hiyo shida ndiyo tunayosema isipotatuliwa hakutakuwa na uchaguzi. Mheshimiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, lugha yangu ilikuwa bayana kabisa, tumesema siyo hatutasusia uchaguzi, tutazuia uchaguzi, lugha siyo kususia uchaguzi lugha ni kuzuia uchaguzi, na tumesema tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya umma, tutawaalika Watanzania wahakikishe uchaguzi huu haufanyiki."

"Bila mabadiliko hakuna uchaguzi na siyo bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi, hiyo siyo lugha yetu, lugha yetu ni bila mabadiliko uchaguzi hautafanyika, ndiyo lengo letu. Sasa ni kwanini, hii lugha mbona kali sana, ni kwanini? Mfumo wetu wa uchaguzi una shida gani? na kwanini wazee waliopendekeza ubadilishwe kwanini walipendekeza hivyo? Una shida gani? Shida ya kwanza kabisa, mfumo wetu wa uchaguzi ni mfumo wa Rais, ambao unadhibitiwa kutoka juu mpaka chini ya Rais na mnafahamu Rais wa nchi hii ni Mwenyekiti wa CCM, na Marais wa CCM wametumia udhibiti wao wa mfumo wa uchaguzi kuhakikisha kwamba CCM inabaki madarakani kwa njia zozote, nyingi haramu"

 
Wewe kaa kando usiburi mabadilko. Hauna ubavu wa kuziua uchaguzi hata wa jimbo Moja tu!

Wenzanko walioingia maridhiano walikuwa wanawaza kama wewe ila walichagua njia ya amani !

Mmesahau Kikwete alijitolea kuleta katiba mpya angalau ilikuwa inaleta mabadiliko, mkata zaidi Kisha mkaikosa jumla!

Kaja mwamba akasema katiba si kipaumbele chake hakuna aliyeinua hata kope!
 
Wewe kaa kando usiburi mabadilko. Hauna ubavu wa kuziua uchaguzi hata wa jimbo Moja tu!

Wenzanko walioingia maridhiano walikuwa wanawaza kama wewe ila walichagua njia ya amani !

Mmesahau Kikwete alijitolea kuleta katiba mpya angalau ilikuwa inaleta mabadiliko, mkata zaidi Kisha mkaikosa jumla!

Kaja mwamba akasema katiba si kipaumbele chake hakuna aliyeinua hata kope!
Nawewe kaa kando usubiri uone uchaguzi unavyozuiwa usilete hadithi zako,Huyo Mwamba wako yuko wapi sasa?Mbona alipingwa waziwazi mpaka Presha ikapanda akafa akazikwa?
 
Wewe kaa kando usiburi mabadilko. Hauna ubavu wa kuziua uchaguzi hata wa jimbo Moja tu!

Wenzanko walioingia maridhiano walikuwa wanawaza kama wewe ila walichagua njia ya amani !

Mmesahau Kikwete alijitolea kuleta katiba mpya angalau ilikuwa inaleta mabadiliko, mkata zaidi Kisha mkaikosa jumla!

Kaja mwamba akasema katiba si kipaumbele chake hakuna aliyeinua hata kope!
Maridhiano huku mnaendeleza kuua na kuteka wapinzani mixer kupora uchaguzi!...No Way
 
Sasa huo "Umma" ukikataa au ukishindwa kuzuia huo uchaguzi, Bado CHADEMA itashiriki?
 
Lisu yuko sahihi bila mabadiliko kupiga kura ni kazi bure. Mfumo uliopo umepelekea watanzania wengi kukosa haki yao kikatiba ya kupiga kura. Wengi hawaendi kupiga kura kwa sababu wanasema nanukuu "hata nikipga kura ni kazi bure wakishamuweka wanaemtaka hata nisipompgia watampitisha tu"
Ni vema tubadili mfumo wa uchaguzi kwanza ndipo tuingie kwenye uchaguzi ili anaeshinda awe ameshinda kihalali.
pia chadema wanapaswa wachukue madhaifu ya mpinzani wao kama agenda ya kuja nayo kwa wananchi.
Bila kusahau suala la kero za muungano. Natumaini mambo yatakuwa mazuri na mabadiliko ni lazima yatatokea maana kila mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi yake moyon mwake hafurahii haya yanayoendelea na anatamani mabadiliko
 
Tundu Lissu asiwategemee sana Watanzania katika hilo ajitahidi awe na options nyingi kuliendea hilo.

Watanzania wengi hawaaminiki ni vigeugeu na ni wepesi kuwa manipulated.
Aanze kwa kufungua kesi ya kikatiba mahakama kuu, kuzuia uchaguzi na kupambania baadhi ya kipengele viwekwe sawa.
 
Lisu yuko sahihi bila mabadiliko kupiga kura ni kazi bure. Mfumo uliopo umepelekea watanzania wengi kukosa haki yao kikatiba ya kupiga kura. Wengi hawaendi kupiga kura kwa sababu wanasema nanukuu "hata nikipga kura ni kazi bure wakishamuweka wanaemtaka hata nisipompgia watampitisha tu"
Ni vema tubadili mfumo wa uchaguzi kwanza ndipo tuingie kwenye uchaguzi ili anaeshinda awe ameshinda kihalali.
pia chadema wanapaswa wachukue madhaifu ya mpinzani wao kama agenda ya kuja nayo kwa wananchi.
Bila kusahau suala la kero za muungano. Natumaini mambo yatakuwa mazuri na mabadiliko ni lazima yatatokea maana kila mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi yake moyon mwake hafurahii haya yanayoendelea na anatamani mabadiliko
Asante.
Umeandika kisomi zaidi
 
Back
Top Bottom