Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Sijaletewa malalamiko yoyote kuhusu chochote " As far as I'm concerned" sina chochote cha kufanya nje ya ratiba yangu

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Sijaletewa malalamiko yoyote kuhusu chochote " As far as I'm concerned" sina chochote cha kufanya nje ya ratiba yangu

dikteta2020

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2018
Posts
595
Reaction score
3,991
Yupo Arusha anaongea na waandishi muda huu na huo ndiyo ujumbe wake kwa tume. Malalamiko hayapelekwi CHADEMA wala Twitter bali anapelekewa yeye.

Tundu Lissu amesema kuwa yeye ndiye aliyesaini hati ya maadili ya tume na lolote linalomhusu yeye kuhusu maadili ya uchaguzi ni lazima apelekewe yeye kwa maandishi.

Lissu amesema kuwa anasikia tu huko mitandaoni kuwa vyama vya NRA na CCM vimepeleka malalamiko dhidi yake kwa tume ya uchaguzi kuwa anakiuka maadili ya uchaguzi ambayo aliyasaini.

Hivyo basi amesema mpaka leo asubuhi hajapelekewa malalamiko yoyote kimaandishi yakimhusu kutoka tume hivyo anaendelea na ratiba yake kama ilivyopangwa na tume.

=======
Mgombea urais kupitia tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu amesema,

“Nikichaguliwa kuwa Rais nitaunda Serikali ya Chadema kwasababu ya Katiba inavyosema. Kama kutakuwa na uhitaji itabidi tubadilishe Katiba kwanza, na moja ya maazimio ya Chadema ikishinda Uchaguzi Mkuu ndani ya siku 100 tutaanzisha mchakato wa Katiba mpya.”Tundu Lissu

“Bob Amsterdam ni Mawakili wangu, wanashughulika na maswala yangu yote yakisheria ya ndani na nje ya Nchi. Kama Tume imeandikiwa barua basi Mawakili wangu wamekuwa wakitimiza wajibu wao, Kama nilivyosema uchaguzi mkuu hatutaki mchezo, na Chadema lazima tushinde uchaguzi huu.”TL

1601458286471.png
 
Sawa, lkn utafungiwa kufanya kampeni na hakuna kitu utafanya, utaikosesha chadema kura inazozihitaji ili iweze hata kupata ruzuku zetu na kukulipia wewe na familia yako.

Low IQ!
 
Sawa, lkn utafungiwa kufanya kampeni na hakuna kitu utafanya, utaikosesha chadema kura inazozihitaji ili iweze hata kupata ruzuku zetu na kukulipia wewe na familia yako.

Low IQ!

Jambo la msingi ni kufuata sheria, kanuni na taratibu, kama tume wamekosea ni sawa kuwafuata wao. Suala la kufungiwa kama sheria haijafuatwa ni batili.
 
Yupo Arusha anaongea na waandishi muda huu na huo ndiyo ujumbe wake kwa tume. Malalamiko hayapelekwi Chadema wala Twitter bali anapelekewa yeye.
By the time yanamfikia masaa 72 yatakuwa yameisha
 
Sawa, lkn utafungiwa kufanya kampeni na hakuna kitu utafanya, utaikosesha chadema kura inazozihitaji ili iweze hata kupata ruzuku zetu na kukulipia wewe na familia yako.

Low IQ!

Hawatafanya hivyo nje ya utaratibu...!!

Yaani mnaanza na kurudi kulekule...

Ooh, huyo hatarudi Tanzania....!.

Ooh, huyo akifika JKINA tu anaelekea Segerea...!

Ooh, huyo Mbowe hatakubali agombee....!!

Ooh, huyo hatapewa fomu za ugombea na tume....!!

Ooh, anawekewa pingamizi, amevunja maadili ya viongozi wa umma...

Ooh, huyo hapitishwi na NEC ana kesi Mahakamani.....!!

Ooh, huyo hana pesa za kampeni, hatafika popote....!!

Sasa mmerekodi santuri nyingine kwa "producer", Dr Wilson Mahera Mkurugenzi wa uchaguzi - NEC yenye wimbo wenye beat za hovyo usio na radha kusikiliza masikioni wa...

"... Anakiuka ama kuvunja kanuni katika kampeni zake...."

Haya, ngoja tuone mwisho wenu. Obviously, ni uleule tu....KULEGEA..!!
 
Sawa, lkn utafungiwa kufanya kampeni na hakuna kitu utafanya, utaikosesha chadema kura inazozihitaji ili iweze hata kupata ruzuku zetu na kukulipia wewe na familia yako.

Low IQ!
Sasa kama hana hiyo barua ya wito, ataendaje huko na atasema ni nini kilichompeleka? Je akiambiwa hawajamwita atasemaje?
Yeye aendelee na majukumu yake, akipata huo wito, basi ataushughulikia.
 
Sasa kama hana hhiyo barua ya wito, ataendaje huko na atasema ni nini kilichompeleka? Je akiambiwa hawajamwita atasemaje?
Yeye aendelee na majukumu yake, akipata huo wito, basi ataushughulikia.


Kusomea sheria ni zaidi ya hapo, unaandika kama mtoto wa miaka 12, hili somo la sheria nina uhakika huwa hamlielewi, vinginevyo msingekuwa mnareason kama watoto, ...
 
Hii inaitwa upper cut, unakula ya chembe kisa kidevu lazima ukae, nchi inaendeshwa kwa kanuni na sheria, siyo maagizo tu
 
Hawatafanya hivyo nje ya utaratibu...!!

Yaani mnaanza na kurudi kulekule...

Ooh, huyo hatarudi Tanzania....!.

Ooh, huyo akifika JKINA tu anaelekea Segerea...!

Ooh, huyo Mbowe hatakubali agombee....!!

Ooh, huyo hatapewa fomu za ugombea na tume....!!

Ooh, anawekewa pingamizi, amevunja maadili ya viongozi wa umma...

Ooh, huyo hapitishwi na NEC ana kesi Mahakamani.....!!

Ooh, huyo hana pesa za kampeni, hatafika popote....!!

Sasa mmerekodi santuri nyingine kwa "producer", Dr Wilson Mahera Mkurugenzi wa uchaguzi - NEC yenye wimbo wenye beat za hovyo usio na radha kusikiliza masikioni wa...

"... Anakiuka ama kuvunja kanuni katika kampeni zake...."

Haya, ngoja tuone mwisho wenu. Obviously, ni uleule tu....KULEGEA..!!
Wamebakia kusema hata akishinda hatangazwi..... akitangazwa watakuja kusema hamalizi miaka 5.
 
Jamani mwenye kujua Lissu atakuwa maeneo gani hapa Arusha anijulishe. Leo nipo free, nataka nikamsikilize.
 
Back
Top Bottom