Tundu Lissu: Tunasikia taarifa watu wanakufa kwa Corona lakini haisemwi wazi. Serikali imerekebisha Sheria inayozuia kupeana taarifa


Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kuukimbia ukweli hakutatusaidia:

Watanzania, Kuukimbia ukweli hakutatusaidia

Heko Lissu hauko peke yako kwenye hili.

Mchana ni mchana haijalishi ni wapumbavu wangapi wangependa kwa kiasi gani kujidanganya kuwa ni usiku.

Koleo na liitwe kwa jina lake kwani koleo siyo kijiko!
 
Kuna watu wakiamka huacha akili zao ndani, Lissu amefika na anaanza kuchimba kaburi lake mwenyewe.
“Whosoever diggeth a pit shall fall therein: and he that rolleth a stone, it will return upon him.” __Proverb 26:27 (Methali 26:27)
#Lissu_Katoa_boko
 
Hiii ndio kazi mtakayo kua nayo mpaka uchaguzi unaisha kazi yenu itakua kutetea upuuz wa Mgombea wenu
 
Huyu jamaa sidhani hata kama atapata muda wa kunadi ilani ya chama,maaana yeye kila kitu kilichoko nchi mwetu ni kibaya,sasa kama kufanya nini ,si angegombea urais huko ubeligiji amabako hakuna madhaifu

Huyu mtu hafai na watanzania inabidi waambuwe ukweli kuwa hili ni garasa,halifai hata kwa bure,mtu amejaa chuki na ubinafsi wa kutupwa ,

Huyu mtu
 
huyu jamaa janja janja nyingi sana mix na kutufokea ndo anaharibu kabisa
 
Lissu bana!!

Anamchukia Magufuli hadi anachukia nchi inayoongozwa na Magufuli. Swala la kusema hali ya Corona nchini inahuzunisha inadhihirisha hilo.

Hivi ukiwa mwanasiasa huwezi kutenganisha kile kilicho maslahi ya nchi na kile kilicho maslahi ya wanasiasa?

Na je ukiwa mwanasiasa huwezi kukubaliana na mwanasiasa mwenzio wa upande tofauti kwenye maslahi ya nchi?

Katika swala la Corona Magufuli kaongoza nchi vyema. Hili huwezi kumwondolea hata kama unamchukia vipi.
 
Nampenda lakini hamna kitu kipya cha kujivunia kutoka kwake
kwani hakuna tofauti kati ya mwanasiasa na mwanasiasa!!!!!!!...
 
Ndugu yangu Tundu Lissu, tunaomba utambue kuwa pamoja na mivutano ya kisiasa tuliyonayo nchini, linapokuja suala la kimataifa ni lazima tuwe wamoja.

Naomba nikuulize katika wale waliokuja kukupokea uwanja wa ndege hakuna hata mmoja aliyevaa taulo la usoni, je umewahi kusikia kuna mtu kafa kwa korona.

Juzi ulikuwa kwenye mkutano mkuu wa chadema na umati wa wajumbe. .Je umewahi kusikia kuna mtu anaugua korona?

Siku iliyofuata ulikuwa kwenye mkutano mkuu wa ACT. Ulipokelewa vizuri kwa shangwe na kukumbatiwa...je kuna mtu umesikia ana korona?

Ni ukosefu wa uzalendo kuituhumu nchi eti watu wanakufa na korona na takwimu zinafichwa tena kwenye vyombo vya kimataifa na cha jirani yetu ambaye ni hasimu wetu wa kiuchumi....ni ukosefu wa uzalendo kwa nchi, ni uhaini mkubwa.

Tena wewe ilitakiwa ukae karantini siku za kutosha maana umezurura sana nchi zenye korona. Usije ukatuletea korona la kibeberu hapa.

Wewe unayemshukuru Mungu amekuponya na mauti, ndiye huyo huyo aliyetuponya na Korona. Usimdhihaki Mwenyezi Mungu...

Hili limeniuzi sana

Wajumbe oyee
 
Huyo jamaa ni country pumpkin!

Tena boga la kiangazi.


Anawataka watanzania wachukue tahadhari ambazo yeye na chama chake hatuoni wakizichukua.

1.Hajakaa "eda" ya siku 14 inayotakiwa na wataalamu pindi aliporejea.

2.Mapokezi yake hayakuzingatia social distancing wala hakuna barakoa.

3.Vikao vya chama chake hakukua na barakoa wala social distancing and likely hata mikono hawakunawa.

4.Jana kule ACT kaenda wanashikana mikono na kubambiana bila tahadhari yoyote.


Huyo jamaa yenu ilifaa aungane na dereva wake kwenye matibabu ya "saikolojia" pengine moto bado ni mdogo kichwani.
 
Huyu kichwa atakuwa alikiacha ubelgiji. Kweli nchi iwe na corona kwa kiwango anachoongelea halafu wanachadema waendelee kukutana bila tahadhari yoyote!
 
Huu mtego wa Covid 19 amenasa.
Watu wa karibu wangemchomoa chezeni na wapiga kura mbona hamtuelewi? Kweli Lockdown na social distance kwa chinga?

Second mistake
 
Jamani jamani kama kuna corona kiasi hicho Lissu si angeanza kuvaa barakoa kuanzia siku alipofika hadi alipohudhulia mkutano mkuu wa kumteua kuwa mgombea urais daah.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…