Toka mwanzo nimesema ya kuwa CHADEMA kila siku inaendelea kujipotezea sifa kwa Aina ya watu wanao Wategemea
Tundu Lissu leo katika Mahojiano yake na KTN anakiri kuwa Tanzania hali ya corona ni mbaya jambo ambalo sio kweli tena anakiri mbele ya Taifa Ambalo siku zote limekua likijaribu kutuchafua katika sura ya Dunia.
Tundu Lissu anailaumu serikal kuwa inaficha Taarifa za janga la corona na kusema kuwa serikali haijachukua hatua na kusema kipindi hiki cha Corona mpaka kufikia uchaguzi hali itakua Mbaya Sana.
Vip wao kama chadema hawato endesha kampeni? Ili kuokoa Wafuas wao wengi kama wanajua kuelekea kampen Hali itakua mbaya?
Kwanini anayasema haya wakati yeye alipotoka ubelgij hakuvaa mask kujikinga wala hawakutoa ushauri wowote wa tahadhari.
Pia Tundu Lissu anasema watanzania hatuchukui Tahadhari yoyote ya kuachiana nafasi vipi kwao CHADEMA hizo nafasi wao Wana achiana?, au wao hawaugui corona?
Na vipi wao kama viongozi mbona hata siku moja hawaamrishi wafuasi wao kuachiana nafasi bali wanawaamrisha Tena kwa Nguvu nyingi Wakusanyike.
Tundu Lissu kumbuka unavyozidi kuichafua nchi hata ukiwa Rais jua tu utakua na kazi mbili, moja kuisafisha na nyingine kuikuza kiuchumi kazi ambayo itakua ngumu kwako.
Naomba Wanasiasa tuwe makini sana wakati huu wa kampeni heshima ya Tanzania ni muhimu sana kuliko kitu chochote,
tuache kuropoka tuongee.