Tundu Lissu: Walionipiga risasi ni Kikosi Kazi cha Ofisi ya Rais chini ya Mkuu wa TISS, Balozi Kipilimba

Tundu Lissu: Walionipiga risasi ni Kikosi Kazi cha Ofisi ya Rais chini ya Mkuu wa TISS, Balozi Kipilimba

Lissu anatafuta legitimacy ya kuendelea kuishi ubelgiji na hakuna lingine hapo.

Kila siku story ya risasi, watu tulikwisha achana na huo ukurasa.

Kuna wengi walidhurika na wapo wanasonga na maisha yao bila hofu.

Hapa tatizo liko kwa kina Maria Sarungi na Fyatu karume wanao host hiyo the space na kumfanya mwenyekiti kila siku.

Mnatuchosha bhana!

Lissu na Lema ni kama nyuki daima sio wa kukumbatiwa.

Lisu alidhurika lazima aseme ukweli wa kilichomkuta, ww ulidhurika wapi? Hamna sababu ya kukalia kimya watu waovu ambao bado wapo, ww uliyefaidika na uovu ule ni haki yako kukaa kimya. Na hakuna mtu anakulazimisha usikilize huko space maana kuna ukweli unaokuumiza.
 
Anata apate kauli thabiti kwamba atakuwa salama akirejea nchini.
Huyu muacheni aendelee kuishi huko huko, ambako anaenjoy kuporomosha kejeli kwa Rais Samia. Maana akirudi hata kama atakufa kwa malaria wanaharakati watasema ameuliwa na Serikali.

Athari za risasi 16 zimekwenda mpaka kwenye saikolojia. Aendelee na matibabu tu, asirudi
 
Vita ya ulaya inayosababisha bei ya mafuta na unga wa ngano kupanda Bei Tanzania.



Endelea na dhihaka hayajakufikia. Subiria siku yakikufika ndio utajua ukweli upoje. Hata Sabaya leo analia kuwa Polisi walimshambulia walipomkamata kule dar.

Hakuna dhihaka hapa ni ukweli mchungu. Unauhakika gani sijafikwa na hayo mambo? Ama unafikiri kufikwa na dhahama ni kupigwa risasi tu? Tunachokataa ni kutumia madhila yako kukugeuza kuwa tapeli la Kisiasa na kuhatarisha hatima ya roho za mamiloni ya wafuasi wako.

Hawa matapeli wa kisiasa wameandamanisha wafuasi wao mara kadhaa na wakawaingiza kwenye kushindana na vyombo vya dola. Wafuasi wao wengine wakafa(Mawazo), wengine vilema mpaka kesho.etc. Wao from no where wakaja na biashara ya kubadili gia angani. EL waliye mpaka kila uchafu wa kifisadi na Watanzania wakawamini hivyo. Wakageuka tena wakawa waimba mapambio ya kumpigia kampeni awe Rais wetu.

So kwangu mimi na amini na hakuna wa kunibadilisha kwamba TL, Mbowe, Lema na waaina zao ndani ya CDM with exception of JJ Nyika maana alimpinga EL na sera ya kubadili gia angani, they are paying for huo uovu woo unaoitwa kubadili gia angani. Na kama hawaja tubu bado wataulipia sana tu huko mbeleni hizi ni rasharasha tu masika itawanyea vilivyo.
 
Lisu anatukanaaaa alafu akimaliza anaenda kupanda Dreamliner ya Magufuli.

Shame upon him na mme wake amsterdam

Wewe una shida eti dreamliner ya Magufuri. Magufuri alikuwa na uwezo gani wa kununua dreamliner? Ndege zipo Chini ya serikali na sio za Magufuri. Zinanunuliwa kwa Kodi ya wwananchi.Kwa hivyo Kikwete aliyejenga UDOM au Nyerere UDSM Ni za kwao?.

Kwa akili Kama zako ndio maana Waziri mkuu aliwadanganya Magufuri yupo hai kumbe amekufa maana aliona hauna hadhi ya kuambiwa ukweli. Shame on you too.
 
Waliompa taarifa Lissu kuhusu hali ya mwendazake ndio waliompa taarifa kuhusu kikosi kazi kilichomshambulia.

Wewe huoni tayari goli lemehamishwa. Ndio maana nawaita hawa wakimbizi wa Kisiasa wa CDM they are a batch of fools.
 
Kati ya jambo la hovyo Sana ambalo the state wamefanya hadi leo ni kuruhusu nchi itawaliwe na chama kimoja KWA MUDA mrefu Sana!!!Tusimlaumu jpm !jpm alipewa jukumu la kulinda chama ambacho kilishapoteza mvuto ndio màana ilikuwa ni lazima atumie nyenzo haramu kama POLISI na Tiss kwenye siasa za kibabe!!!chanzo chake ndio hayo mauaji hayo na marisasi!!!!The state ingejiandaa KWA KUANDAA chama mbadala tangu mwaka 2010 Baada ya uchaguzi wa kikwete ule!!hata kama si Chadema Basi hata NCCR MAGEUZI TU!!HATA TLP AU CUF Wangeandaa mtu mzalendo hata huyo jpm akagombee HUKO na kushinda asingeua wala kutwaa Sana Sana angepambana na mafisadi tu!!!MIMI NITAENDELEA KUWALAUMU THE STATE KWA UZEMBE WAO NA KUKOSA MAONO YA KESHO!!!MARAISI WA CCM WANATUMIA NGUVU NYINGI KUPAMBANA NA UPINZANI ILI KULINDA CHAMA KULIKO KUPAMBANA NA MAENDELEO!!!NA HII ITAKUJA KULETA MACHAFUKO HUKO MBELENI NA TAIFA LITAPATA WAASI NA TUTAGAWANYIKA KWA UZEMBE WETU SISI WENYEWE!!

Good observation. Greta mind
 
Tundu Lissu aweke mezani ulinzi anaoutaka tuuelewe. Maana this is too much demanding.

Labda anataka awe protected kama Marais wastaafu maana apart of protection ya Rais na viongozi wengine wakuu, Watanzania wengine hatulindwi

Mkuu kuweka hadharani kwa kila mtu haiwezi kuwa sahihi.

Hata hivyo si kweli kuwa hakuna watanzania wengine wakiwamo wa kawaida tu wanaolindwa from time to time.

Ni kwa mujibu wa sheria watu wanaohisi kutishiwa usalama wao kulindwa.

Ombi la Lissu halina upya zaidi ya kuwa liliwahi kupuuzwa siku za nyuma.
 
Atakuwa tapeli maana aliomba/aliombewa asaidiwe kwani ameshindwa kupata stahiki zake. Wako wenye uhitaji wakati huu ambapo yeye hahitaji tena kufanyiwa upasuaji/ matibabu. Kwa nini hizo fedha za matibabu azichukue tena yeye asisaidie wenye uhitaji kama alivyosaidiwa?
Kama matibabu hayajesha asipewe
 
Tundu Lissu aweke mezani ulinzi anaoutaka tuuelewe. Maana this is too much demanding.

Labda anataka awe protected kama Marais wastaafu maana apart of protection ya Rais na viongozi wengine wakuu, Watanzania wengine hatulindwi

Anataka TISS waondoe operation eliminate Lissu. Maana kumbuka aliibiwa passport ujerumani.
 
Kama ni kweli kuna "kikosi kazi" basi kama amri hiyo amri ya "Eliminate" Lissu haijatenguliwa bado, ajichunge.

Nani wa kuifuta?
Ndio maana kumbe amekuwa akimuomba Rais Mh Mama Samia Suluhu atoe japo tamko tu. Inaonekana hali si nzuri sana.

Mungu atulinde watanzaia.

Mungu Mbariki Rais Samia
 
Alafu unaweza hisi tangia apigwe risasi akuwai kurudi Tanzania,kumbe alirudi na akatembea nchi nzima kufanya kampeni tena huku akuchimba mikwara.
Ni kweli kabisa, tena alirudi kipindi ambacho anayedai mtesi wake Magufuli alikuwa bado yuko hai na bado akiwa rais.

Kama hakuogopa kurudi awamu ya mtesi wake, anaogopa nini kurudi awamu ya aliyemwona kwa amani Nairobi na Ubelgiji?
 
Kati ya jambo la hovyo Sana ambalo the state wamefanya hadi leo ni kuruhusu nchi itawaliwe na chama kimoja KWA MUDA mrefu Sana!!!Tusimlaumu jpm !jpm alipewa jukumu la kulinda chama ambacho kilishapoteza mvuto ndio màana ilikuwa ni lazima atumie nyenzo haramu kama POLISI na Tiss kwenye siasa za kibabe!!!chanzo chake ndio hayo mauaji hayo na marisasi!!!!The state ingejiandaa KWA KUANDAA chama mbadala tangu mwaka 2010 Baada ya uchaguzi wa kikwete ule!!hata kama si Chadema Basi hata NCCR MAGEUZI TU!!HATA TLP AU CUF Wangeandaa mtu mzalendo hata huyo jpm akagombee HUKO na kushinda asingeua wala kutwaa Sana Sana angepambana na mafisadi tu!!!MIMI NITAENDELEA KUWALAUMU THE STATE KWA UZEMBE WAO NA KUKOSA MAONO YA KESHO!!!MARAISI WA CCM WANATUMIA NGUVU NYINGI KUPAMBANA NA UPINZANI ILI KULINDA CHAMA KULIKO KUPAMBANA NA MAENDELEO!!!NA HII ITAKUJA KULETA MACHAFUKO HUKO MBELENI NA TAIFA LITAPATA WAASI NA TUTAGAWANYIKA KWA UZEMBE WETU SISI WENYEWE!!

Nimewahi kusema sana kuhusu hili kuwa mifumo ya nchi hii itaendelea kuwa mibovu iwapo ccm itaendelea kukaa madarakani kwa shuruti. Unakuta nguvu ya kupambana na upinzani inakuwa kubwa kwani ccm sio chama cha kizazi hiki. Ni vyema CCM wakubali kukaa pembeni kwa heshima ili watu waonje ladha mpya, kisha kama ni kurejea irejee ikiwa na sura mpya.
 
Hajaweka wazi nini haswa hoja yake. Ni kama mtu mwenye wasiwasi usiokwisha kwa vigezo vya mwanzoni mwa maongezi haya.

Inaweza kuwa ni muendelezo wa siasa za mitandaoni, hataki kutoka midomoni mwa watu kirahisi hivyo inambidi aongee hata kama anachokiongea ukikipima hakina undani sana.
Wewe upo huku mtandaoni ni Nyani au Mtu?
 
Back
Top Bottom