Tupeana updates za kuhama kwa Wamachinga
Machinga ni moja ya njia ya kufikisha huduma na bidhaa hasa kwa watu wa kipato cha chini kwa urahisi, haraka na nafuu. Serikali inashindwa ku strategise namna ya kukusanya kodi zitokanazo na bidhaa na huduma wanaenda kuhangaika na machinga wakifikiri ndo wanakwamisha wao kukusanya kodi ya kutosha kutoka kwa wafanyabiashara.

Kimsingi wafanyabiashara wa kiafrika ni wakwepaji wakubwa wa kodi ukilinganisha na wazungu na kuthibiti wamachinga siyo suluhisho la wao kutoendelea kukwepa kodi.

Serikali inatakiwa kubuni njia mbadala za kukusanya kodi kwenye bidhaa na huduma, badala ya kuingilia mifumo ya ufanyaji biashara unaolenga kuwakandamiza wafanyabiashara ndogo ndogo, waliobandikwa jina la wamachinga ambao kimsingi ndo wanasaidia kundi kubwa la watu wa kipato cha chini na kati na kuishia kuwalinda maslahi ya wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa.
 
Hata wasingeunga mkono walipaswa kutekeleza agizo la serikali, sidhani kama viongozi wana nia mbaya na machinga la hasha!

Kinachofanywa ni kuweka mazingira ya miji katika utaratibu wake kwa mujibu wa miongozo ya mipango miji japo bado kasoro zipo nyingi.

Miji ilionekana kuwa michafu muda wote kila mahali, fujo tupu na kuzalisha vibaka, piga picha pale viwanja vya mnazi mmoja yaani ilifikia hatua kupishana ilikuwa shida ni mwendo wa kupigana vikumbo.

Sehemu nyingi zilianza kuwa makazi ya mateja. Mara nyingi unakutana nao wanazurura na kicheni kimoja au betri mbovu kumbe anakula timing ukikosea tu imekula kwako.

Natoa hongera kwa viongozi wetu zoezi hili litapunguza na kuondoa kero hii.

Sehemu kama viwanja vya mnazi mmoja, jangwani na viwanja vingine vinaweza kutengwa kwa siku kadhaa kwa wiki kwa wamachinga kufanya biashara zao.

Pia hata maeneo mengine ya mjini yaliyo wazi kwa utaratibu mzuri au mitaa flani kufungwa siku kadhaa kwa ajiri ya machinga.

Muhimu waendelee kuruhusiwa kutembeza bidhaa zao mitaani.

Ni muhimu vijana waendelee kupata sehemu za kufanya biashara zao.
 
Yaani kuwekewa utaratibu wa biashara ni tatizo?![emoji44]

Btw uongozi wa Machinga mkoa wa Dar umeunga mkono zoezi hilo na wenyewe walikwenda pale Karume kusafisha.....na greda waliomba ofisi ya Mkurugenzi.....

FYI : Ofisi za Wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wanatoa maeneo ya kufanyia biashara....hakuna anyimwaye!

UKWELI UTATUWEKA HURU

#Siempre JMT
Kuwa na wamachinga wengi.
Kipimo cha" ukosefu wa ajira nchini".
sio wote watapata nafasi huko wanapopelekwa.
Wengine wana mikopo.
Kuanza upya pia ni changamoto
 
Huku ndio kuendekeza ujinga, unafahamu serikali ilipoteza mapato kiasi gani kwa kuruhusu machinga kila kona, kariakoo yenyewe ilikua imeshajifia kwani hata wafanyabiashara wa nje waliikimbia kisa msongamano
nchi yako imezalisha ajira kiasi gani?
Usilaumu machinga.
Hakuna anayependa kuwa machinga.
Miaka ya nyumba ilikuwa inajulikana machinga NI kazi ya watu wasiokuwa na elimu.lakini Sasa hivi mpaka went elimu wanaifanya hyo kazi.
 
Ni kweli Machinga walifanya miji kuwa hovyohovyo kwa namna ya ufanyaji wao wa biashara na walipaswa kutikuwa maeneo hayo.

Lakini la msingi pia, tusisahau nao ni Watanzania wana haki zao kama Watanzania kwenye hii keki ya Taifa... Mh Rais na viongozi wake baadala ya kuwafurumusha tu, ungeanza kuandaliwa utaratibu mzuri kwa kuwashirikisha wahusika wenyewe na watalaam wa mipango miji na watendaji wengiene wa Serikali kuangalia namna bora ya kuwapanga na kuwa control nao kama Watanzania waweze kupata ugali wao wa kila siku..

Mamlaka zilipaswa zifanye sensa ya wamachinga katika kila eneo na kuangalia eneo gani la wazi karibu na eneo walilokuwa wanaweza kutosha kwa idadi yao na nyongeza...
Mfano wale wa Kariakoo wangepelekwa wote eneo fulani Kigamboni pakaitwa Kariakoo Machinga area na huduma zote zikawekwa hapo na Kariakoo yote machinga wakatolewa wakapelekwa hapo.... Wale machinga wote wa Manzese liangaliwe eneo labda mabibo au mburahati eneo kubwa (sio kama pale big brother) wakawekwa huko, Pale Mbezi pia na kwingineko Dar es salaam na mikoani ifanyike hivyo...

Hili pia lisiishie kwa wamachinga tu bali lifanyike hata kwa wenye showrooms za magari, wauza used za magari wote Dar es Salaam wawekwe sehemu moja na ilipaswa watafutiwe eneo kubwa sana la wazi waende huko na Serikali iweke miundo mbinu pamoja na kuwajengea godowns watakazokuwa wanalipia hela na serikali kukusanya mapato..

Serikali pia sasa ipige Marufuku maduka yote yatakayokuwa sehemu rasmi kama Kariakoo, Manzese nk kutouza bidhaa feki baadala yake zianze kuuzwa bidhaa original kutoka kwa manufacturer wanaotambulika na sio wahuni wachina hapa TBS na wengine wafanye kazi yao.. Bidhaa feki, second hand na used waachiwe machinga kwenye hizo designed areas..

Ikumbukwe kila mwaka vijana wetu wengi wanamaliza kwenye mavyuo na shule mbalimbali na hatuna uwezo wa kuwapa ajira hata 20% yao matokeo yake walio wengi wanazagaa mtaani kujitafutia, tusipowaandalia utaratibu na kuwawekea mazingira safi hawa vijana na wao waweze kujitafutia huko mbele tutapata janga ambalo hakuna atakayeweza kulidhibiti (hii ndio inawakuta SA)...

Tukumbuke kuwa elimu yetu bado duni na inaleta mtaani wahitimu feki aka duni wengi wao ambao masikini ya Mungu uwezo wa kifikiri ni mdogo kufanya makubwa vs elimu zao kwa wengi wao inabidi tu wafanye shughuli ndogo ndogo mitaani nao waweze kuishi...
Elimu nayo iboreshwe tupate wahitimu strong wenye uwezo wa kusurvive nje na ndani kwa kufanya mambo makuwa hata kama ni wizi basi wakisasa mkubwa ( mfano Nigerians)...
 
Kwahiyo unaona wamachinga ndo vibaka acha dharau. Graduate wangapi wako mtaani na hawajaitwa vibaka.
We jamaa graduate ndio kipimo cha ubinadamu ?
Kila kitu reference ni graduatuate, hatuwezi jadili jambo kuzingatia misingi ya ubinadamu?
Mbona kwenye human right, basic need, maslow highlack of need hawajajaduli kwa misingi ya graduate. Hicho kipaumbele cha graduate kinatoka wapi, mnajipa ukuu na daraja ambalo hata walionzisha elimu hawana.
Jadili katika misingi ya utu wa mwanadamu awe mtoto mkubwa,mzee, kinana,mwanamke mwanaume, mzungu,mweusu,mwarabu au mchina wite ni sawa na wanamahitaji sawa.
 
Back
Top Bottom