Tusahau kuindoa CCM kupitia ballot box

Tusahau kuindoa CCM kupitia ballot box

Nope,, chama ndio kilishika hatamu, au umesahau,,
Kuna watu walipigania uhuru, wakaupata, wakatengeneza nchi, wakaiita Tanzania, na wakaunda serikali iliyokua chini ya chama,,
Sasa mzee we...
Lakini nchi sio mjini tu.

Na chama hakikuwa mijini peke yake, kilifika kila mahali kikichangiwa na kuwezeshwa na kila kaya hapa Tanzania.
 
Siyo kweli. Halafu unajua wewe unaongea kwa hisia tu. Unajua mimi nilianza form one 1982. Huwezi kuniambia chochote.

..je, ulisoma sekondari ya umma, na mliruhusiwa kuwa viranja bila kuwa uv-ccm?
 
CCM ina miaka 100 mbele
Kama tunabaki na katiba yetu hii hii kauli yako ni sahihi.

Hata wenye mawazo tofauti ndani ya CCM hawana maisha mule..

CCM inabadilika na timu zinajipanga upya bila madhara..sababu dola ndiyo CCM huna la kufanya zaidi ya kukubali yaishe. Kwa mfano CCM ya mwendazake ishakufa, falsafa zake zishazikwa na maisha mapya yanaendelea ndani ya CCM.

CCM si chama cha siasa ndugu zangu bali ni Dola ya Tanzania.

Bila kupigania katiba mpya watanzania- hatuna lolote CCM itatawala itakavyo.
 
..lakini nchi sio mjini tu.

..na chama hakikuwa mijini peke yake, kilifika kila mahali kikichangiwa na kuwezeshwa na kila kaya hapa Tanzania.
Wewe si umeshakiri kila raia alikua ccm, au?

Let it be clear, enzi za mwalimu, watu walikua wanasoma na kupata kazi, ualimu, unesi, upolisi, etc, kulikuwa na uhaba wa wasomi, shule zilikua chache, ilifikia kipindi wahitimu wa la saba wakaanza kupewa kazi, na wakaitwa walimu wa UPE,
Sikuwahi sikia eti mtu kanyimwa kazi kisa hana kadi ya ccm,
Labda una kaushahidi tuone mzee wangu😲
 
..Je, tunakubaliana kuwa Tanu / Ccm ilikuwa taasisi ya umma?
We mzito kuelewa,, chama ndio kiliunda serikali,, elewa msemo wa chama kushika hatamu.

Tatizo wewe ndio unsjichanganya, ngoja nikuweke wazi, nchi ilikua inaongozwa na chama, ambacho ndo kiliunda serikali ambayo iliwajibika kwa chama.
 
Wewe si umeshakiri kila raia alikua ccm, au?.
Let it be clear, enzi za mwalimu, watu walikua wanasoma na kupata kazi, ualimu, unesi, upolisi, etc,, kulikuwa na uhaba wa wasomi, shule zilikua chache,, ilifikia kipindi wahitimu wa la saba wakaanza kupewa kazi, na wakaitwa walimu wa UPE,,
Sikuwahi sikia eti mtu kanyimwa kazi kisa hana kadi ya ccm,
Labda una kaushahidi tuone mzee wangu😲

..kila mtumishi wa umma alikuwa mwana-ccm.

..kila askari polisi, magereza, usalama,jwtz, alikuwa mwana-ccm.

..mpaka hapo bado unabisha kwamba Ccm haikuwa taasisi ya umma?
 
Huu ulevi utatoka siku si nyingi..read where Nebukadrneza ended, Mungu yupo na Mungu si binadamu..maneno yako ni kukufuru baada ya shine ya tumbo.
Nebukednezer alifika hatima yake kama binadamu au viongozi wengine mfano george bush, gorbachev, etc,
 
We mzito kuelewa,, chama ndio kiliunda serikali,, elewa msemo wa chama kushika hatamu..

Sawa.

Kama ni hivyo kwanini unakataa kuwa chama hicho kilikuwa cha umma, na mali na nyenzo zake zote zilikuwa za umma?

..msemo wa chama kushika hatamu ulikuja baadae kidogo, na mimi hoja nilikuwa nimeiweka akiba. Thanks for bringing that up.
 
CCM ni chama kikubwa, lakini kubwa jinga, na kiko hadi leo madarakani kwa uoga wa wananchi. Maana kama ni wizi wa kura wanaufanya waziwazi maana hawana uwezo tena wa kushinda uchaguzi. Hivyo tukiacha uoga CCM itazikwa kaburi moja na KANU ya Kenya. Machafuko tu ndio njia ya kurejesha heshima ya box la kura.
Mjinga hawezi kukutawala kaka
 
Sawa.

Kama ni hivyo kwanini unakataa kuwa chama hicho kilikuwa cha umma, na mali na nyenzo zake zote zilikuwa za umma?

..msemo wa chama kushika hatamu ulikuja baadae kidogo, na mimi hoja nilikuwa nimeiweka akiba. Thanks for bringing that up.
Nimeshagundua tunapochengana,, kwani wewe unadhani umma ni nini?
 
Sasa kuwa kiranja na kudai mali ya ccm wapi na wapi?

..nimejaribu kueleza ni jinsi Ccm ilivyokuwa imefungamanishwa na maisha ya kila Mtanzania, ili kukazia hoja yangu kwamba kilikuwa chama cha umma.

..manaake wewe ulikuwa unadai Ccm inawahusu watu fulani tu, waliokuwa mjini, na haikuwahusu Watanzania wote, na haswa wale wa " uswekeni. "
 
Wakoloni weusi wameharibu na kufuja sana nchi za Africa baada ya mkolini mzungu kuondoka. Wamefanya mataifa yetu kama wana haki miliki nayo.
..ilianzishwa 1954 tukapata uhuru 1961. Kwa hiyo ni miaka 7.

..kinachonishangaza ni Muingereza kuwa na utu kuliko hawa Watanzania wenzetu wa Ccm.

..kwa mfano, kulifanyika uchaguzi mwaka 1958 na Muingereza hakuengua mgombea hata mmoja wa Tanu.

..Sasa fast forward mpaka uchaguzi wa 2019 na 2020 ambako Tume ya Uchaguzi chini ya Ccm iliengua maelfu ya wagombea wa upinzani.

..Je, ni lazima uwe Ccm li utendewe haki na uwe huru hapa Tanzania?

..Mazingira hayo ndio yanayonifanya nisionee fahari Uhuru na nchi yetu.
 
Unjani sabuwona
Kwa hali niliyoiona jana pale Dodoma kamwe ccm haiwezi kutokana madaraka kwa kutumia ballot box hawa watu wamejipanga kweli kweli kila kitu ni Chao.

Hapa nielewe sijamaanisha itumike violence hapana let make sure that katiba mpya inapatikana soon as possible ili mambo yasiaribike .

Kila kitu kipo kwao polisi ni wao, mahakamani ni wao, timu za mpira wa miguu ni wao and each and everything ni wao this is too much wakuu.

CCM wamehodhi kila kitu mambo yote ni wao vijana wengi vyuoni katika vijana kumi 8 ni ccm mmoja hana chama na mmoja ni upinzani CHADEMA au Act.

Wapinzani mtoke humu mitandaoni sio kupiga kelele mitandaoni fikiria mwananchi wa chini kabisa huko maganzo au nanjilinji ndani ndani huko haijui twitter wala jamiiForum yeye au wao hauwezi kuwaambia chochote kuhusu ccm, ccm ni wao na wo ni ccm.

Nchi haiongozwi kwa kutumia space au club house tu tujitokeze barabarani kutaka katiba mpya.

Join with me kwa maandamano ya amani mpaka ikulu siku ya jumamosi kushinikizwa kwa katiba mpya. Maandamano yataanzia posta kwenye mnara wa askari mpaka magogoni ikulu. Kula, kunywa na matibabu ni juu yangu.

Shalom.

Upinzani hawapo bungeni na Wala hawajapewa uwanja sawa wa kisiasa. Unakataza watu wasifanye siasa miaka Saba, halafu bado unawalaumu? Be srious.
 
Kwa nini serikali yako inasajili vyama visivyo na ofisi??
Sasa tunarudi kwetu hapa. CHADEMA ilianzishwa 1992 mpaka leo 2022 ni miaka 30 hawana ofisi. Je, hizi ndizo siasa za kutaka kuongoza nchi!?
 
Kuna watu watakupinga, ila ukweli ni huo hasa. Ila hapo kwenye kutoka barabarani hapo watakaoteseka ni familia yako kukutibisha.

CCM wamekuaminusha kuandama ni kosa na ukiandama utauawa. A shithole country.
 
Back
Top Bottom