Tutafakari pamoja: Waziri Mkenda anaposema wasaidizi wa Rais waliweka kauzibe asimwone mkuu wa nchi, hadhi ya Waziri ipoje kwani?

Kwahiyo anatuambia kwamba amefanya hizo significant changes bila baraka za Baraza la Mawaziri?
 
Narudia tena malipo ni hapa hapa duniani nakumbuka nilipata tabu sana kumpata waziri mkenda ofisini kwake hahahahaaaa.
Ingawake ni β€œ professor β€œ he is not an inspirational minister! Ni mmoja wa mawaziri wanaoweza Kuondolewa Samia akifanya resuffle! Mark my words.
 
Kwa nchi yetu waziri ni formality tu hawana msaada kwa Rais wala nchi wao nikama visemeo (koni) kazi yao ni kupiga kelele na kuiba ela.
 
Ingawake ni β€œ professor β€œ he is not an inspirational minister! Ni mmoja wa mawaziri wanaoweza Kuondolewa Samia akifanya resuffle! Mark my words.
Kwa hiyo Mwenye matatizo ni Mkenda au Saa100?

Hakuna matatizo makubwa kama bosi wako kuwa na uwezo mdogo kiakili,kuliko wewe.

Yule bibi, Kila kitu lazima aambiwe,aulize hawezi kutafakari na kuwaza mwenyewe na kuamua kama Rais,hadi JK amshauri.
 
Serikali Inafarakana Yenyewe Sasa Ndiyo Inaanguka Hivyo, Masuala Ya Mnara Mnafarakana Mpaka
 
Katibu wa Rais hana cheo lakini huyu wa sasa ana nguvu sana
Katibu wa Raisi ndio anayempangia Raisi Ratiba zake. Na watu wakuonana Naye. Baada ya kukubaliana na Raisi au kulifikisha suala lako Kwa Raisi na Raisi kuliafiki.
Kutokana na hilo kuna Makatibu wengine huweka maslahi binafsi katika kutoa hiyo connection iwe Katibu wa Raisi , mawaziri na viongozi wengine. Hujivika cheo cha muhusika katika kutoa connection na mambo yanayo uhusiano nayo.
 
Mi fani yangu uganga wa kienyeji .........najua muda bado kidogo............watanitafuta wenyewe kupitia katibu wangu kama wanataka kurudi kwenye nafasi zao.........wakaendelee kulamba asali
 
Kwa hiyo Waziri hana kabisa mawasiliano na Boss wake, mpaka apitie kwa wasaidizi wa huyo Boss!! Na Boss naye anaonekana yuko busy tu na mambo yake mengine, na wala hana hata muda wa kutenga ili uwasiliana na wasaidizi wake, ili kufahamu kinachondelea huko Wizarani!

Kweli tumepatwa! Na mpaka ifike hiyo 2030, hakika tutashuhudia mauza uza na maajabu mengi tu.
 
Hii nchi kila mwenye nafasi anataka ajionyeshe yeye ni mjuaji na anataka asujudiwe.Hawa jamaa zangu hata tatizo la elimu hawaoni umuhimu wake,wao wanaona sifa kwamba wako karibu na kiongozi.Hili tatizo watanzania wengi wanalo kuona nafasi zao ni kwa ajili ya kutukuzwa.
 
Waziri hakupaswa kuonge hayo hadharani
Waziri hakupaswa kuongea hayo hadharani - hajaiva !
 
 

Attachments

  • v09025g40000cuf23mnog65n745b17cg.mp4
    13.2 MB
Hili jambo inabidi Raisi ilitolee ufafanuzi, Yani Yanga wasiokua na msaada wowote kwa Taifa wanaenda kula pilau na Raisi halafu Waziri mwenye dhamana ya Elimu ya Watanzania anashindwa ??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…