UCHAMBUZI: Hoja za NECTA kufuta utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora hazina mantiki kwa 100%

UCHAMBUZI: Hoja za NECTA kufuta utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora hazina mantiki kwa 100%

Wizara hi inaongoza kuaribu hatma za wanafunzi

Kila waziri huwa anakuja na lake kuanzia enzi za mugwai ,mam sita , professor ndalichako ,na SAS huyu wa SAS bwna mkenda ,

Itafika wakti watakuja tu na lingine haswa kwenye mitaala
 
Hakuna haja ya kuwapa mtihani sawa wanafunzi ambao mazingira ya shule, uwezo wao wa uelewa, uwezo wa familia wanazotoka kiuchumi, kiimani, n.k. ni tofauti. Wafute na mitihani shuleni. 😁
 
Mimi nakasirika sana, kwanini shule za kanisa zinafanya vyema kuliko za kata? Shule inaitwa Taifa, performance yake kama Taifa Stars [emoji92], halafu shule inaitwa St. Francis performance yake kama Argentina [emoji1033] mabingwa wa dunia.

Hamjui inaumiza kiasi gani. Afadhali hata UMUGHAKA ana option, either afe yeye au afe Rehema
[emoji4]
 
Hoja zao hazijabeba logic yoyote zaidi wanatufanya tuamini kuna chuki binafsi tu inayoendelea zidi ya shule binafsi.
Halafu preliminary analysis yangu inanionesha kuwa kuna watu wa DINI A WANAFURAHIA MAAUMUZI YA NECTA KUTOWEKA RANKINGS NA DINI B WANAHOJI SANA MAAMUZI YA NECTA ... NGOJA NITENGENEZE HYPOTHESIS
 
Usije kukuta kuna uhusiano na matokeo ya shule za kule Zanzibar, kwa hiyo ukute wanaogopa kumkeresha Madam. Usije kukuta madogo wametaga kichizi na miswaki ya kufa mtu. Sitaki kugusia kule Ruangwa na Kigoma kwa Mpango.

Lakini angalizo ni kwamba mficha maradhi ........
Hiki ulichoandika ndiyo sababu kubwa na ya msingi iliyopelekea walioongoza na waliokuwa wamwisho kutotangazwa.
 
Siku ya leo, Baraza la Taifa la Mitihani Nchini Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne na kufuta utaratibu wa muda mrefu wa kutoa orodha na mtiririko wa ubora wa shule kulingana na kiwango cha ufaulu na pia limefuta utaratibu wa kutangaza wanafunzi bora wa mitihani hiyo. NECTA imetoa sababu kuu mbili za wao kufanya hivyo, ambazo ni;

-Kutangaza shule bora ni kutangaza biashara kwa shule hizo.

-Hakuna usawa baina ya shule moja na nyingine katika mazingira ya utoaji elimu hivyo hawapaswi kushindanishwa.

Kwa kuwa JF ni Kisima cha maarifa na uchambuzi huru, Mimi binafsi hapa hapa nitazipinga hoja zote hizo mbili kwa kuchambua kwa kina hoja kwa hoja.

1. Hoja ya kutangaza biashara
Kwanza kabisa hoja hii imekaa kiupande mmoja, ni hoja ya kibaguzi kwa 100% na kuumiza wasiohusika kwa 100%. It is a double standard decision. Sababu za kibiashara zimewalenga wamiliki wa shule binafsi (zimewabagua) na hapo hapo zinazinyima fursa shule za serikali pasipo sababu (zime wahukumu pasipo kuhusika).

Pili ni hoja ya nusu nusu mno, kwa kuwa NECTA hiyo hiyo ndio imekuwa ikitoa hadharani matokeo yote ya shule moja moja yenye kuakisi ubora wa shule husika, hata kama NECTA haitaweka mtiririko rasmi wa ubora bado mtu yoyote makini (hata asiye makini) anaweza kuchambua na kuonyesha zipi ni shule kumi bora zaidi kulingana na mtiririko wa kimatokeo ulivyo.

Na katika hili, mtu au taasisi tofauti (vikiwemo vyombo vya habari) vinaweza kuja na uchambuzi wenye kukinzana na kuzaa upotoshaji. Kifupi tu, NECTA imejivua jukumu lake na sasa inakwenda kuruhusu mtu au taasisi yoyote kujitangazia ubora wake kimatokeo, hata kama ni kwa upotoshaji. Na tutegemee matangazo ya kibiashara (yenye chembechembe za upotoshaji) kwa kwa kutumia matokeo ya NECTA yakichipuka na kuongezeka maradufu. Mwisho katika hili, NECTA haipaswi kukwepa kuteketeleza majukumu yake, kisa tu inaogopa kivuli cha kuonekana inatangazia biashara shule bora. Vipi kama shule hizo 10 bora ningekuwa ni shule za serikali tu?

2. Hoja ya mazingira yasiyolingana katika utoaji elimu hapa nchini
Nadhani huenda hii ni hoja ya kipumbavu kupita maelezo kuwahi kutolewa na NECTA. Kwanza kabisa kuweka hoja sawa, sote yanapaswa kufahamu kuwa, NECTA haiwajibiki popote katika kutengeneza, kuboresha au kuyapima mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania, hivyo hawapaswi kuyasemea chochote mazingira hayo maana sio jukumu lao.

Pili NECTA wanawajibika kuandaa, kusimamia, kusahihisha na kutoa matokeo ya mitihani. Kama NECTA wanaona na kuamini kuwa mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania hayako sawa baina shule na shule na yanaathiri matokeo yao, ni kwanini waandae mitihani mmoja kwa wote au usahihishaji na utoaji wa alama za ufaulu uwe sawa?

Kwanini suala la utofauti wa mazingira baina ya shule moja na nyingine liwe ni hoja wakati wa kutangaza ubora wa shule tu, lakini isiwe ni hoja ya msingi wakati wa kutunga mitihani, kusahihisha na kuweka alama za ufaulu?
Naungana na wewe 100% naona umepiga kwenye mshono.....
 
NECTA, wangetumia hya matokeo kama njia ya kutafuta suluhu kwa Shule za Serikali, yaani ni sababu zipi zinapelekea Shule za Serikali kufanya vibaya. Mfano; 2.upungufu wa walimu(siasa imeshaingilia kati hili suala kiongozi). 2.Vifaa vya kujifunzia yaani vitabu n.k,
3.makazi ya walimu. licha ya walimu kuwa ni wachache, hawakai jirani na maeneo ya kazi kutokana uhaba wa Nyumba.
4. Masilahi duni. Mishahara ya walimu ni kidogo hii hupelekea walimu kufanya kazi kwa ufanisi mdogo.
Hivyo: necta ingetumia haya matokea kuboresha/kurekebisha mapungufu yalioko kwenye Shule za public na sio kuogopa kutoa matokea kwa ranking za Shule.
 
Hivi developed country huwa Zina asses vipi matokeo any one with experience
 
Ndo maana huwezi kuwaweka sawa katika kupanga list ,ndo kafuta ni hatua na tangu mwanzo walikuwa wanajua kwamba hawatokuwa sawa Kwa zile wanasoma mazingira tofauti
Kwanini wasingetungiwa mitihani tofauti kama issue ni mazingira kutofanana? Kama issue ni mazingira basi wangezitenga kulingana na mazingira wwkatangaza top ten kwa kila kundi mfano private school, government special school na hizi nyingine
 
Kwanini wasingetungiwa mitihani tofauti kama issue ni mazingira kutofanana? Kama issue ni mazingira basi wangezitenga kulingana na mazingira wwkatangaza top ten kwa kila kundi mfano private school, government special school na hizi nyingine
Labda wawatungie tofauti angalau.
 
Wapo sahihi... Top 10 inakusaidia nini wewe mlalahoi, huwezi kupeleka watoto wako Feza boys, wakati hata michango tu ya shule ya kata huwezi kutoa
 
Ila Tanzania tunaburuzwaa haswaa, haya mambo ya kubadirishiwa utaratbu kwa hoja hoja dhaifu ni kukoseana Adabu sana
 
Wizara hi inaongoza kuaribu hatma za wanafunzi

Kila waziri huwa anakuja na lake kuanzia enzi za mugwai ,mam sita , professor ndalichako ,na SAS huyu wa SAS bwna mkenda ,

Itafika wakti watakuja tu na lingine haswa kwenye mitaala
Nyie hamjui yaliyoko katika shule za private waulizeni walimu watawaambia yanayotendeka huko
Watoto weny wanatunika kuingia pesa lakini hawapati kile kinachotakiwa zaidi ya kukariri
1. Umeshawahi kuona syllabus ya mwaka mzima inamalizwa kufundishwa kwa miezi mitatu
Kwa madai ya kufanya revision miezi iliyobaki
Na hyo revision ni kukaririsha naswaki ya nyuma yaliyowahi kutolewa na baraza la mitihani .Sasa ulimoeleka mtoto shule akafanye revision na kujibu maswaoi au apate Maarifa yatakoyomsaidia katika maisha yake ya baadae

2 njia za ufundishaji za kumshurikisha mwanafunzi hazipo
Ndio maana ya kupata product isiyoweza kujitegemea kwa chochote
.application ya kile wanachofundishwa hakuna katika maisha Yao kabisa
Watoto wanatoka wa A lakini hakuna kitu WANAWEZA wakati syllabus yetu ikifuatwa vizuri na njia za ufundishaji zinazotakiwa mbona mtoto anaweza kumaliza form four na akawa
Fundi umeme
Fundi fridge nk

3. Wizi wa mitihani , angalia walimu wanavyooambana kuwapa majibu watoto .hiyo yote ni kwa sababu ya kuhakikisha kuwa shule yake inafanya vizuri unapata wanafunzi wengi
Wakuu wa shule pamoja na walimu wanapambana kwa njia yoyote Ile kuhakikisha wanawapa majibu watoto
Mitihani hii walimu wanapambana kutoa mitihani kwa watoto ilimradi tu shule yake ionekane imefaulu
Angalia primary schools walimu wanashikwa choini wanatoa majibu kwa watoto
.binafsi nashukuru sana kwa maamuzi ya baraza la mitihani
Kabla ya kuandika chochote fanta utafiti huko mashuleni
Mimi nimeacha kufundisha private school mwaka Jana lakini nimefanya kazi huko kw miaka kumi najua sana
 
Kwanini wasingetungiwa mitihani tofauti kama issue ni mazingira kutofanana? Kama issue ni mazingira basi wangezitenga kulingana na mazingira wwkatangaza top ten kwa kila kundi mfano private school, government special school na hizi nyingine
Hoja ya mazingira ni ya kipuuzi, kuna mwanafunzi kutoka shule ya sekondari ya kata na hata wanafunzi wengi kutoka familia maskini huwa wanaongoza kama best students...........hawa mbona mazingira hayajawaathiri? hapa kinachofichwa ni shule za upande uleee kuonekana kuwa na ufaulu hafifu miaka nenda rudi.​
 
Pili ni hoja ya nusu nusu mno, kwa kuwa NECTA hiyo hiyo ndio imekuwa ikitoa hadharani matokeo yote ya shule moja moja yenye kuakisi ubora wa shule husika, hata kama NECTA haitaweka mtiririko rasmi wa ubora bado mtu yoyote makini (hata asiye makini) anaweza kuchambua na kuonyesha zipi ni shule kumi bora zaidi kulingana na mtiririko wa kimatokeo ulivyo.
Hivi ndivyo walivyofanya NECTA. Kama kuna uchambuzi unaweza kufanywa lkn NECTA wamejitoa. Uchambuzi wowote utakuwa sahihi ikiwa utafuata vigezo. Sioni tatizo hapo.
 
Ilichokifanya serikali ni kana kwamba haitaki ushindani na kwa lugha ingine ni kwamba imekataa kujifunza. Hakuna maajabu yeyote zaidi ya kuweka walimu competent kwenye shule za kata na kuwa finance vizuri. Watoto watafaulu tu, mbona Kibaha inafaulisha, ilboru kama kawaida.

Kuna mahali serikali inafanya uzembe na dawa sio kuficha ukweli kwamba inafanya uzembe. Wekeni walimu bora na muwalipe vizuri muone kama wanafunzi hawatafanya vizuri. Shule haina vyoo walimu wana lindi la madeni mtaani sababu mshahara finyu unategemea elimu inakuwaje bora. Mwalimu hana utulivu wa akili kwanini asimalizie hasira kwa mwanafunzi kumpiga stiki za visigino.

Wenzenu private wanalipa 1.5 to 2M na wanahakikisha bonus zipo kwa matokeo mazuri zaidi. Utakosaje motisha wakati unajua ukizalisha A's swala la uongozi wa shule kukuzawadia gari na hela ni jambo la kawaida.
 
Siku ya leo, Baraza la Taifa la Mitihani Nchini Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne na kufuta utaratibu wa muda mrefu wa kutoa orodha na mtiririko wa ubora wa shule kulingana na kiwango cha ufaulu na pia limefuta utaratibu wa kutangaza wanafunzi bora wa mitihani hiyo. NECTA imetoa sababu kuu mbili za wao kufanya hivyo, ambazo ni;

-Kutangaza shule bora ni kutangaza biashara kwa shule hizo.

-Hakuna usawa baina ya shule moja na nyingine katika mazingira ya utoaji elimu hivyo hawapaswi kushindanishwa.

Kwa kuwa JF ni Kisima cha maarifa na uchambuzi huru, Mimi binafsi hapa hapa nitazipinga hoja zote hizo mbili kwa kuchambua kwa kina hoja kwa hoja.

1. Hoja ya kutangaza biashara
Kwanza kabisa hoja hii imekaa kiupande mmoja, ni hoja ya kibaguzi kwa 100% na kuumiza wasiohusika kwa 100%. It is a double standard decision. Sababu za kibiashara zimewalenga wamiliki wa shule binafsi (zimewabagua) na hapo hapo zinazinyima fursa shule za serikali pasipo sababu (zime wahukumu pasipo kuhusika).

Pili ni hoja ya nusu nusu mno, kwa kuwa NECTA hiyo hiyo ndio imekuwa ikitoa hadharani matokeo yote ya shule moja moja yenye kuakisi ubora wa shule husika, hata kama NECTA haitaweka mtiririko rasmi wa ubora bado mtu yoyote makini (hata asiye makini) anaweza kuchambua na kuonyesha zipi ni shule kumi bora zaidi kulingana na mtiririko wa kimatokeo ulivyo.

Na katika hili, mtu au taasisi tofauti (vikiwemo vyombo vya habari) vinaweza kuja na uchambuzi wenye kukinzana na kuzaa upotoshaji. Kifupi tu, NECTA imejivua jukumu lake na sasa inakwenda kuruhusu mtu au taasisi yoyote kujitangazia ubora wake kimatokeo, hata kama ni kwa upotoshaji. Na tutegemee matangazo ya kibiashara (yenye chembechembe za upotoshaji) kwa kwa kutumia matokeo ya NECTA yakichipuka na kuongezeka maradufu. Mwisho katika hili, NECTA haipaswi kukwepa kuteketeleza majukumu yake, kisa tu inaogopa kivuli cha kuonekana inatangazia biashara shule bora. Vipi kama shule hizo 10 bora ningekuwa ni shule za serikali tu?

2. Hoja ya mazingira yasiyolingana katika utoaji elimu hapa nchini
Nadhani huenda hii ni hoja ya kipumbavu kupita maelezo kuwahi kutolewa na NECTA. Kwanza kabisa kuweka hoja sawa, sote yanapaswa kufahamu kuwa, NECTA haiwajibiki popote katika kutengeneza, kuboresha au kuyapima mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania, hivyo hawapaswi kuyasemea chochote mazingira hayo maana sio jukumu lao.

Pili NECTA wanawajibika kuandaa, kusimamia, kusahihisha na kutoa matokeo ya mitihani. Kama NECTA wanaona na kuamini kuwa mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania hayako sawa baina shule na shule na yanaathiri matokeo yao, ni kwanini waandae mitihani mmoja kwa wote au usahihishaji na utoaji wa alama za ufaulu uwe sawa?

Kwanini suala la utofauti wa mazingira baina ya shule moja na nyingine liwe ni hoja wakati wa kutangaza ubora wa shule tu, lakini isiwe ni hoja ya msingi wakati wa kutunga mitihani, kusahihisha na kuweka alama za ufaulu?
Unataka watangaze shule bora na wanafunzi bora hao wanafunzi bora wakimaliza elimu zao ajira utawapa wewe?
 
Back
Top Bottom