Uchambuzi na upelelezi wa tukio la kifo cha padri Francis uanzie hapa

Uchambuzi na upelelezi wa tukio la kifo cha padri Francis uanzie hapa

Kuna baadhi ya mambo hayawezi kuthibitika kwa macho hadi yajidhihilishe yenyewe!
Kuna wakati tetesi huja na ukweli mwingine kuliko uongo!
Kumbuka kila mwanzo wa jambo huwa ni fikra juu ya jambo hilo!
Kwa hiyo, kwako wewe speculation ndiyo unaona ndiyo njia sahihi ya kupata ukweli, eti? Mimi siwezi kuanza kumhisi vibaya mtu just for the sake la kutafuata ukweli. Kama ukweli utapatikana ni vizuri zaidi, kuliko kuanza kupika hadithi hii na ile na ile tena na ingine na ingine tena.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Hapa ndipo kanisa linapopataka wakati mgumu,lipotezee habari ipite,au lifuatilie ukweli ujulikane lipate aibu?kwa nini hawa jamaa wasiluhusiwe tu kuoa?
Hata wachungaji waliooa wanatafuna wake za watu. rejea kesi za 2018 KKKT Iringa makamu wa askofu na mchungaji aliyerekodiwa ndani ya gari akinyanduana na mwanafunzi wa sekondari. Hata tuliopo kwenye ndoa bado tunamichepuko pembeni
 
Ni chanzo cha uchunguzi
Speculations haziwezi kuwa chanzo cha uchunguzi. Chanzo huwa ni inquiry - kuuliza kilichotokea na jinsi kilivyoanza na hapo ndipo vyanzo vinaweza kusema 'tuliona hivi au vile au tulisikia hivi au vile'. Speculations zinaonyesha tu mambo yale ambayo mara nyingi tunayawaza kichwani mwetu - ya kichawi kichawi na kupiga ramli - huyu kaanguka na ungo, huyu kafanya hivi na mwisho wa siku hakuna kinachotusaidia.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Speculations haziwezi kuwa chanzo cha uchunguzi. Chanzo huwa ni inquiry - kuuliza kilichotokea na jinsi kilivyoanza na hapo ndipo vyanzo vinaweza kusema 'tuliona hivi au vile au tulisikia hivi au vile'. Speculations zinaonyesha tu mambo yale ambayo mara nyingi tunayawaza kichwani mwetu - ya kichawi kichawi na kupiga ramli - huyu kaanguka na ungo, huyu kafanya hivi na mwisho wa siku hakuna kinachotusaidia.
Sasa ushawahi kuona wapi tetesi zinaanza pasipo kuona? Kinachotakiwa ni kuchunguzwa kilichoona na kusemwa kama tetesi
 
Hata wachungaji waliooa wanatafuna wake za watu. rejea kesi za 2018 KKKT Iringa makamu wa askofu na mchungaji aliyerekodiwa ndani ya gari akinyanduana na mwanafunzi wa sekondari. Hata tuliopo kwenye ndoa bado tunamichepuko pembeni
Kwa hiyo heri wasioe?
 
Hayo ni mambo ya mtu binafsi Padre ni binadamu kama binadamu wengine so akijisikia anambato tu swala ni heshima na busara Roman katoliki hutumia kuhandle mambo yake huwezi kulinganisha na mambo ya Konde huko
Askofu Koda alifukuzwa kwa kuwa eti alikuwa member wa secret society.
 
Nani aliye jisifia hakuna mambo ya ajabu ajabu kwenye taasisi za kidini likiwemo Kanisa la Katoliki? Au unataka useme ni Kanisa Katoliki pekee ndilo lenye hayo mambo ya ajabu ajabu?

Na kama ni hivyo basi Gwajima naye ni Mkatoliki! wale Maustaadh wanao walawiti watoto wadogo wa madrasa nao ni Wakatoliki! Wachungaji wote wa Makanisa ya Kipentekoste wanao jihusisha na mapenzi kwa siri na waumini wao, nao ni Wakatoliki!.
 
Yesu hakuanzisha kanisa. Makanisa yapo mengi. Nawaonea huruma sana mnapotumia nguvu kujiaminisha visivyoaminika
Kanisa ni moja, Takatifu na ni perfect maana kichwa chake ni Kristo mwenyewe! Huko kwingine ni huduma binafsi na zinaambatana na ubinafsi wake.

Hakuna uzi unaotenganisha ubinafsi wake na Kanisa. Ndio maana hata huko kwingine wakikomaa wanafikia level walipo TAG! Sijui kama umenielewa!

Kuhusu kuendesha Kanisa labda hulijui Kanisa Katoliki. Sisi waamini ndio kila kitu, shughuli za Kanisa zipo chini ya halmashauri ya walei! Mapato na matumizi vipo chini ya hizo kamati na taarifa za fedha zipo wazi. Kama kuna ubadhirifu kuna utaratibu wa wazi wa kinidhamu hata kama ni paroko.

Hakuna Kanisa linalokusanya mapato mengi kama Kanisa Katoliki na sio kwamba hakuna migogoro mbalimbali! Lakini kwavile si mali binafsi ya mtu yeyote, upo utaratibu wa ku handle hayo.
 
Yesu hakuanzisha kanisa. Makanisa yapo mengi. Nawaonea huruma sana mnapotumia nguvu kujiaminisha visivyoaminika
Yesu hakuanzisha makanisa! Yesu alianzisha Kanisa na alimwambia Petro na juu ya mwamba huu nitajenga KANISA langu! Sasa kajifunze maana ya Kanisa maana wengi mnafikiri kumuamini Kristo tu ndio Kanisa.
 
Kumekuwepo na maneno ya chinichini kwamba anatembea na wanawake.

Hapa ndio pakuanzia
 
Umejishushua hapo hapo Yeye alitoa maagizo Petro akayafanyia kazi,acheni kujimilikisha ukristo huo ni udikteta. Kumuamini Mwenyezi Mungu ndio mpango mzima.
Yesu hakuanzisha makanisa! Yesu alianzisha Kanisa na alimwambia Petro na juu ya mwamba huu nitajenga KANISA langu! Sasa kajifunze maana ya Kanisa maana wengi mnafikiri kumuamini Kristo tu ndio Kanisa.
 
Kwa uzoefu wangu, matumizi mabaya ya pesa (hata kama waumini hawajui hizo pesa zimetoka wapi) na kutembea na wanawake/wake za watu (hata kama waumini wakimwona padri katembelewa na ndugu wa damu wa kike) "ni tuhuma za kawaida sana kwa mapadri".

Sijawahi kuona padri ambaye hana tuhuma kama hizi (awe amefanya au hajafanya) - it doesn't matter. Nina mfano wa padri fulani. Alikuwa na gari linalofanana na gari (Toyota Corolla) la jamaa ambaye alikuwa akifanyakazi Afrika Kusini. Tofauti yake ilikuwa gari la padri lilikuwa na number plate ya njano na plate number nyeusi na la yule mwenye mke lilikuwa na number plate nyeupe na plate number nyekundu. Kwa watu wa kawaida hizi tofauti hazikuwa na maana sana. Walichojali au walichoona wao ni kusema "gari la padri limepaki nyumbani kwa mke wa mtu kwa muda wa wiki moja sasa" na habari hizi zilifika hata kwa Baba Askofu.

Siku moja huyo padri alipita barabara iliyo karibu na nyumba ya huyo bwana, ambaye bado alikuwa likizo na gari lake lilikuwa palepale nyumbani na padri anaendesha hili la kwake. Alipofika karibu na njia inayoenda nyumbani kwa yule bwana, mke wake alikuwepo na watu wengine na alipoona ni padri akamsimamisha. Padri akasimama, lakini hakutoka kwenye gari. Alifungua kioo kumsikiliza huyo mama, ambaye alisema: "Watu wamekuwa wakizusha kuwa gari la padri liko nyumbani kwangu kwa wiki sasa. Mbona anaendesha gari lake hili na lile mbona bado liko pale nyumbani limepaki. Kwani padri ana magari mawili?"

Baada ya kusema hivyo na wale watu baada ya kuona kuwa kumbe lile gari si la padri, wakamwomba radhi, wakisema "hatujakutendea haki hata kidogo, tusamehe padri". Padri alisema tu "endeleeni na ujinga wenu kama unawasaidia" na akaondoka.

Mapadri wamisionari wanatunzwa na shirika lao na parokiani huwa si 'mabwana fedha'. Parokia nyingi za mjini kama Dar es Salaam, kila parokia ina kamati ya fedha na kuna mhasibu wa parokia ambaye siyo padri. Sasa hizo pesa anazoweza kula anazipata kutoka wapi na kwa nani au ni kamati ya fedha iliidhinisha ili azichukue? Na nijuavyo kamati ya fedha inaidhinisha kwa matumizi ya mradi fulani na padri yeye anakuwepo kama mshauri, lakini mambo yote yanafanywa na viongozi wa kamati ya fedha kwa kushirikiana na kamati zingine - mfano kamati ya ujenzi etc.

Hapa najaribu kuona tu namna waumini wanavyoweza kumshusisha padri fulani na matumizi mabaya ya pesa hata bila kujua undani wa matumizi yenyewe. Kwa shirika kama la Wamisionari wa Afrika, paroko anakuwa ni msimamizi tu wa parokia, lakini anakuwa na mapadri wengine wawili anaofanya nao kazi na wote ni sawa hakuna mdogo wala mkubwa. Kwenye nyumba ya mapadri (community ya hao mapadri watatu), kuna pia mkuu wa nyumba na bursar (wale mapadri wengine wawili ambao siyo paroko - mmoja anakuwa mkuu wa nyumba na mwingine anakuwa anaangalia masilahi yao (bursar) kwa mfuko unaotoka shirikani.

Na kwa vile wote watatu wamepangwa kwenye parokia hiyo uamuzi wa uendeshaji wa parokia lazima uridhiwe na mapadri wote wanaofanyakazi pale. Hapa ndipo ninapoona ugumu wa kufuja hela za parokia. Na kwa baadhi ya parokia (kwa vile mapadri wa shirika wanakaa watatu na wote wanatoka mataifa tofauti), kuna baadhi ya mapadri kulingana na huko wanakotoka wana utajiri kwa mfano wale wanaotoka kwenye familia tajiri - familia zao zinaendelea kuwa'support' kwa hali na mali wanapokuwa huku Afrika. Namfahamu padri mmoja kijana alikuwa akitokea Ireland - alipata pesa za urithi - kutoka familia moja tajiri ambayo iliandika 'will' kwamba watakapofariki mali yao yote itakuwa ni kwa ajili ya huyo Fr.

Huyu alikuwa based Afrika Kusini (ninamfahamu) maana ni schoolmate na kwa utaratibu wa Shirika la Wamisionari wa Afrika mali yote anayopata padri fulani ni mali yake binafsi (ingawa anashauriwa kuitumia vizuri na ikiwezekana aweze kuwasaidia wenzake ambao hawana mali au wanatoka familia masikini kadiri atakavyoona yeye).

Hapa juu nimependa kueleza tu namna padri anavyoweza kuwa na shtuma ambazo kimsingi hazina basis. Lakini natambua pia binadamu tuna upungufu wetu na kama shtuma za waumini ni genuine - mimi ni nani wa kusema padri alikuwa hachukui wake za watu au hakutumia vibaya pesa za parokia? Ila nimetaka tu tuwe na caution!
You have spoken the truth. Nimekuwa na Missionaries of Africa kwa miaka 4 now. Shirika lina wapatia allowance, transport, food and medications.
 
Kulikuwa na shida ya maji mpaka aingie kutazama? Je, ni lazima kuingia kwenye tank kujua halina maji? Je, alikuwa analifanyia ukarabati au usafi? Hakuna wafanyakazi wa kufanya hilo hasa ukizingatia ni Juma Kuu?

Walijuaje kama alikuwa ndani ya tank, je alianza kuharibika na kutoa harufu?

Huenda kaamua kujiua, kaingia mwenyewe ndani ya tanki...hilo lawezekana pia
 
Vipi kama viongozi wake wameamua kumzima baada ya kuona anaichafua parokia na kanisa kwa ujumla!!
 
Back
Top Bottom