Hatukubali tafiti za kipuuzi dhidi ya waafrika maarufu
Wakajifanyie na wao huko kwao
Unajua kubisha humu jf haisaidii kanisa wala mtu..
Ni kuposti BBC na kukanusha hata kwenye website zao, radio zao nk
 
Utafiti wao wa Uebert Angel uliishia wapi?

Wafanye tafiti watoe na mrejesho sio kupoteana tena
Kwanza sio utafiti, ni uchunguzi,
Pili, wewe ulitaka wafanuaje baada ya kutoa ripoti yao kama waandishi wa habari?
 
Ni kweli haya makanisa yanayoibuka kila siku na watu kujiita manabii na mitume, kuna mengi nyuma ya pazia
Na wewe usiwe kama BBC, ungoje mtu afe useme alikuwa mbakaji. Sema sasa hivi ni mtume na nabii gani ameficha mengi nyuma ya pazia.
Mtaje na utaje aliyoficha ili vyombo vya sheria viokoe mapema.
 
Mbona kama ushahidi hauna nguvu, mtu yoyote anaweza kuzungumza.

N.B MIMI SI MFUASI WA TB JOSHUA
Hata mi naona kama ulivyoona wewe...tena wazungu ndio wanatoa ushahid huo!.. yan mzungu kabisaa ukam lock up for 20 years mtu mweusi,seriously???
 
Na wewe usiwe kama BBC, ungoje mtu afe useme alikuwa mbakaji. Sema sasa hivi ni mtume na nabii gani ameficha mengi nyuma ya pazia.
Mtaje na utaje aliyoficha ili vyombo vya sheria viokoe mapema.
Kabisaaa walikua wapi hawa..? Mbona hawakum expose b4 wasubir mpaka afe??? Au kuna maslah wamedhurumiana???
 
Na wewe usiwe kama BBC, ungoje mtu afe useme alikuwa mbakaji. Sema sasa hivi ni mtume na nabii gani ameficha mengi nyuma ya pazia.
Mtaje na utaje aliyoficha ili vyombo vya sheria viokoe mapema.
Inahitaji uchunguzi kufikia hitimisho ndo maana nimetia shaka hayo mazungumzo yaloletwa na BBC.

Nasema kuna mengi nyuma ya pazia kulingana na ibada zenyewe zinavyoendeshwa, kuyajua yahitaji uchunguzi wa kina
 


Kwanini wasichunguze hawa manabii ambao hawajafa badala ya mtu ambaye hawezi kujitetea
 
1. Wanaoshuhudia madhila na utapeli ni walioukuwa watumishi na wanafunzi wa TB Joshua mwenyewe na kanisa lake, sio watu baki. Mmojwapo ni watu waliokuwa karibu kabisa naye kama mtu namba mbili baada ya TB Joshua.

2. Kwenye baadhi ya sehemu za clips zilizorekodiwa na kanisa hilo na ambazo ni public zilizotumiwa na BBC TB Joshua anaonyeshwa akifanya mambo ya ajabu mbele ya hadhara kama kupiga watu makofi kama sehemu ya huduma!

3. TB Joshua alikuwa akiishi kwenye jumba mfano wa gereza na kundi kubwa la wanaoitwa "disciples" wanafunzi wake, wengi wakiwa wanawake vijana na vigori, walivyokuwa wanapatikana anajua yeye mwenyewe ila mmoja wa wahojiwa anasema alipewa na kazi na TB Joshua ya kuleta wanafunzi wa kike mabikira. Watu kuzuiliwa kama wako kifungoni na viongozi wa cults sio jambo jipya, mifano ni mingi sana kuanzia kwa jirani zetu hapa Kenya katika kisa cha Shakahola, huko kwingine duniani wamewahi kuwepo kina Jim Jones wa people's temple, David Koresh wa Waco n.k

4. Hakuna mgogoro wowote ndani ya kanisa la SCOAN unaohusishwa na waathirika hawa walioamua kusema yaliyokiwa yanatendeka nyuma ya pazia, hivyo huwezi kusema hata ni watu wenye nia ovu ya kulimega hilo kanisa na kuanzisha lao.

5. BBC wanasema waandishi wao walirushiwa risasi na walinzi wa kanisa hilo walipokuwa wanachukua video. Kanisa lolote linaloweza kufikia kiwango hichi cha kujificha kutoka waandishi wa habari ni taa nyekundu.

6.Ni kweli jengo la kanisa la TB Joshua liliwahi kuanguka na kuua mamia ya watu kwa sababu ya kutofuata taratibu sahihi za ujenzi na TB Joshua akasema kulikuwa na ndege ndogo iliyokuwa ikizunguka katika jengo hilo iliyopelekea kuporomoka na kwamba pia lilikuwa na jaribio la mauaji dhidi yake. Hata hivyo Ushahidi wa wazi ni kwamba taratibu nyingi za ujenzi wa jengo hilo zilikiukwa lakini kwa sababu matapeli wa kidini kama yeye wamekuwa na nguvu na ushawishi mkubwa sana katika serikali za Africa hakuna hatua yoyote aliyochukuliwa.

7. BBC wamefanya uandishi wa kiuchunguzi "investigative journalism" sio utafiti "research" au forensic investigation ambayo sasa inapaswa kufanywa na polisi kuthibitisha zaidi yaliyoletewa hadharani na BBC. Yani kazi kubwa iliyofanywa na BBC ni kuwasikiliza waathirika takribani 30 kutoka sehemu mbalimbali, kuhakikisha hawajapanga "conspire" kusema walichosema, kuoanisha wanachosema"corroboration" na kisha kuwapa fursa kanisa la SCOAN la TB Joshua kuzungumzia tuhuma hizo ambapo walikataa kuwapa ushirikiano wowote.

Kazi ya ushahidi mwingine unaodaiwa na baadhi ya member hapa jukwaani kama ushahidi wa video wa watu wakibakwa ni suala la forensic investigation na mahakamani kama polisi wa Nigeria wataamua kufuatilia kesi hiyo. BBC wamefanya kazi yao uandishi wa kiuchunguzi kwa weledi mkubwa na wamemaliza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…