Ufugaji Mbuzi wa kienyeji (Asili) kibiashara

Ufugaji Mbuzi wa kienyeji (Asili) kibiashara

Nawasalimuni kwa jina la Mungu. naomba niwapongezeni sana nyote ktk kujenga mawazo ya kutaka kuingia ktk miradi kama hii ya ufugaji. Mimi ni mfugaji wa Mbuzi na nina fuga Mbuzi kwa muda mrefu, niwaombeni kitu ufugaji ni mzuri na una faida na changamoto zake, kikubwa ni kukubali kujifunza na kujijengea umakini ktk ukaguzi na usimamizi wa mifugo yako. Kwa aliyepo Dar namkaribisha kwangu aje tujifunze pamoja na tugawene ujuzi kwa pamoja. Kwa anae anaza kufuga nakuomba sana usinunuwe mbegu kwanza kabla hujapita kwetu wafugaji tulio kutangulia ujifunze vitu halafu ndio uingize Mbegu shambani kwako. Karibuni kwa maswali mbali mba;li nipo hapa tutasaidiana kwa kadiri Mungu atakavyo tujaalia.
Ndugu zangu wenzetu wa MBOGO RANCHESE wameanza kuuza mbuzi wa mbegu wakiwa ni cross ya Boer na Isiolo/Galla, naweka na number yao hapa naomba muwasiliane naoe mjipatie Mbegu zilizo bora kabisa. 0767 803 520, Mbogo Ranchese naomba muwasiliane nao mjipatie Mbuzi kwaajili ya mbegu kuboresha mashamba yenu.
Hii Mbogo iko mooa gani
 
Nafurahi kujumuika nanyi wafugaji wenzangu! Mm nafuga Mbuzi, maeneo ya Msowero - Kilosa, Morogoro! Changamoto kubwa niliyoipata ni kuingizwa chaka na Wafugaji/Wamasai walioniuzia mbegu wakisema inazaa Mapacha.
Haikuwa kweli. Kinyume cha hapo sijutii kuwa Mfugaji
Pole sana ndugu kwa hii chanagamoto naomba nikushauri kitu, ktk ufugaji wako unapotafuta Mbegu ya mapacha uwe unajuitahidi kutafuta na kuona kabisa Mbuzi mwenye watoto mapacha na kama ikiwezekana akuuzie na watoto wake kabisa itakusaidia kuwa na uhakika ktk hilo hitaji lako. Mimi huwa naitumia hiyo njia ktk kujihakikisha kama namhitaji huyo Mfugo, ila kwangu mimi kipaumbele ni Mbuzi kuzaa sio lazima mapacha ikitokea namshukuru Mungu nasonga, kipaumbele ni kuwa na majike bora yenye kunipatia matokeo bora, Barikiwa sana ktk ufugaji huu.
 
Bei iliyochangamka
Hapo ni pair ama
Cross breed nao vipi
Cross wanauzwa na Mbogo mara ya mwisho aliweka lak 3.5 kama sijakosea mkuu, ila ukiingia kwenye page yao wameweka na bei kabisa hao ni F1 na wameweka ni cross ya Mbuzi yupi na yupi ili kukusaidia kufanya maamuzi ya kipi kina kufaa.
 
Cross wanauzwa na Mbogo mara ya mwisho aliweka lak 3.5 kama sijakosea mkuu, ila ukiingia kwenye page yao wameweka na bei kabisa hao ni F1 na wameweka ni cross ya Mbuzi yupi na yupi ili kukusaidia kufanya maamuzi ya kipi kina kufaa.
Nimeangalia Instagram page yao, hata maswali hawajibu
Ngoja nitafute namba zao
 
Nawasalimuni kwa jina la Mungu, naomba niwataarifu kuna mwenzetu mmoja analeta Mbuzi majike ya Mubende kutoka karagwe na jana tumewapokea Mbuzi 100 kwajili ya wafugaji ambao waliagiza. nawakaribisha sana .
 
Hongereni wakuu kwa kufuga,ukiachana na uzoefu, ushauri wangu kwenu ni kuwatumia wataamu wa mifugo (vets) kama sehemu ya input ktk biashara zenu
 
Nikisoma Uzi kama huu nashangaa sana kwamba wizara ya kilimo na taasisi zinazohusika na mambo haya ya mifugo wanafanya Nini? Kwa Nini pasiwepo mkakati WA makusudi kuboresha mbegu za kienyeji ili kuongeza tija?
 
Back
Top Bottom