Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Nani alikuambia pesa ya kibongo inasevika!? Ukiiweka tu kesho,unapewa taarifa za kuumwa kwa ndg yako au Mtoto wa ndg yako,na unatakiwa mchango!!
Sasa si bora kusaidia ndugu yako kuliko kuweka pesa kwenye passport usiyojua utaitumia lini?
 
Hivi ulishawahi kusikia marekani au ulaya raia zao wanahangaika na passport?.
Kabla sijakujibu labda uniambie Mmarekani akija Tanzania anafuata nini na wewe unapoenda huko Marekani unafuata nini?
 
Upumbavu mtupu!
Viongozi wenu wa nchi niwa hovyo kabisa
 
Awamu hii tutashughudia mengi ya ajabu sasa zile ridhiki za papo kwa papo tutashindwa,unampata sponsor wa kukupa maisha na muda ni ukuta utakuta unapoteza maana passport huna!passport ni haki yetu sio fadhila za serikali na nchi nyingi ni bure kuipata hasa ombi la kwanza.
 
Hawa nyau kuna siku watasema sisi ambao hatuna magari hatutakiwi kuwa na leseni.

Sifahamu utaratibu kwa nchi nyingine upo vipi juu ya passport ila huu wa lazima uwe na safari haupo sawa. Kuna watu wanatafuta kazi au scholarship na zote hizo wanaitaji passport ID ndio uwe kuwa sehemu ya ombi lako kufanyiwa kazi. Sasa sijui wanasaidia vipi watu wa aina hii!!! Ni kweli hawa maboss wa uhamiaji hawawezi kujiuswali jepesi kama ilo na kujijibu then watengeneze sera ya maana au wanafanya makusudi tu.
 
Pia atambue anaikosesha serikali mapato yake kwa sababu Applicant hajatoa dhumuni la safari au ametoa sababu ambayo Uhamiaji hawakubaliani nalo.
 
Kuna familia moja ya kishua dada yao mkubwa aliolewa na Mzungu na waliishii Ulaya. Baada ya miaka mingi yule dada alipata saratani. Walimuuguza mpaka mauti yalimfika. Mzungu aliamua mke wake anazikwa Ulaya ili watoto na wajukuu waone kaburi kila wakimkumbuka. Alipiga simu akawaambia anatuma mwaliko wenye passport waende kuomba visa ya kwenda msibani.

Familia nzima hakuna aliyekua na passport kasoro chizi wao mmoja aliyeshindikana. Katika mihangaiko yake alipata pass akaiweka ndani. Siku walizopewa zilikua chache sana ku ku process pass. Mchizi alikua mwanafamilia pekee aliyepata viza na kukwaa pipa kwenda kwenye mazishi ya sister wao.
 
Kuna familia moja ya kisua dada yao mkubwa aliolewa na Mzungu na waliishii Ulaya. Baada ya miaka mingi yule dada alipata saratani. Walimuuguza mpaka mauti yalimfika. Mzungu aliamua mke wake anazikwa Ulaya ili watoto na wajukuu waone kaburi kila wakimkumbuka. Alipiga simu akawaambia anatuma mwaliko wenye passport waende kuomba visa ya kwenda msibani.

Familia nzima hakuna aliyekua na passport kasoro chizi wao mmoja aliyeshindikana. Katika mihangaiko yake alipata pass akaiweka ndani. Siku walizopewa zilikua chache sana ku ku process pass. Mchizi alikua mwanafamilia pekee aliyepata viza na kukwaa pipa kwenda kwenye mazishi ya sister wao.
Alirudi?
 
Back
Top Bottom