Uhuru wa maoni uwe na mipaka. Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni uchokozi

Uhuru wa maoni uwe na mipaka. Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni uchokozi

Acheni watu watoe madukuduku yao.

Hofu ya nini kama mnaamini mama yenu anachofanya ni sawa?

Kama mnakubali asifiwe basi pia kubalini asemwe kwa namna yoyote ile.

Mnaumia nini akisemwa?

Kama hamtaki asemwe mwambieni aache kazi arudi Unguja akacheze na wajukuu zake.
Asemwe usiku na mchana hatutaki matusi na ubaguzi wala uchokozi.

Wewe upo nje ya Tanzania halafu ni sukuma gang, tunakufahamu. Ndiyo nyinyi mnaochochea ujinga.
 
Kila mtu ana jambo lake ki maslahi, likiguswa atalalamika...
Jambo la DP World lina maslahi pande tofauti. Kila upande usikilizwe.
Hakuna kuona hawa ni hawa, wale ni wale...
Mkuu hivi umeisoma thd na kuielewa?

Mleta mada hajakataza watu wasitumie uhuru wao wa maoni bali ametaka wakati wa kutoa maoni,watu wasitumie lugha za kuudhi kama vile matusi,kejeli au kashfa ya udini coz hali hiyo inaweza kuleta madhara makubwa sana huko mbeleni.
 
Nani katukana?

Na kejeli kwa viongozi si jinai!

Maneno ya dharau si jinai.

Acheni watu waongee.

Kuwaziba watu midomo ni dalili ya kushindwa hoja.

Na unaposhindwa hoja basi unaanza kutumia maguvu tu.
Hiyo USA na Canada, siyo Tanzania.
 
Acheni watu watoe madukuduku yao.

Hofu ya nini kama mnaamini mama yenu anachofanya ni sawa?

Kama mnakubali asifiwe basi pia kubalini asemwe kwa namna yoyote ile.

Mnaumia nini akisemwa?

Kama hamtaki asemwe mwambieni aache kazi arudi Unguja akacheze na wajukuu zake.
Ona hii punguani,mleta mada ni wapi amekataza watu wasitoe maoni yao? Hivi umeisoma thd au umekurupuka tu kama chafya?
 
Tunazidi kugawanyika.

Yeye anatoa maoni kusimama na kuubariki mkataba.

Lakini hataki kabisa wale wanaopinga mkataba huu, waendelee kuishi.

Yeye ana haki ya kusapoti.
Wengine hawana haki ya kupinga.
Na anadai uhuru umezidi.

Hakulaani, wkt Sheikh Mwaipopo anamponda na kumkashifu Prof. Shivji. Profesa alitweza utu na utanzania wake, hakulaani.

Wengine walipolaani. Hapo anaona washughulikiwe.


Mods, msiunge Uzi huu kwa sababu,

Hoja yangu inaeleza, hii ya walio upande wa ndio, kuanza kusema wasiotaka huu mkataba washughulikiwe kwa njia za wazi na zisizo za wazi.

Tuwaulize, hizo njia zisizo za wazi, ndio zile zisizojulikana. Vifo.

Hatari sana.
Mi nataka kumuwowa huyo Faizafoxy na tuone atakayepinga
 
Mkuu hivi umeisoma thd na kuielewa?

Mleta mada hajakataza watu wasitumie uhuru wao wa maoni bali ametaka wakati wa kutoa maoni,watu wasitumie lugha za kuudhi kama vile matusi,kejeli au kashfa ya udini coz hali hiyo inaweza kuleta madhara makubwa sana huko mbeleni.
Nimemuelewa. Hayo ya lugha ya maudhi yanatokana na kutokueleweka kwa wasemaji..Viongozo wakiwa na lugha moja wataeleweka. Huyu akisema hili na yule lile wananchi wanaona kuna uongo mahali "Watabweka"..
Jambo moja la bandari, bandari wanasema lao, waziri lake,Spika lake, waandishi lao, walioenda Dubai lao, Heeee..!!!!
Kwanini "mbwa asibweke" ...
 
Nimemuelewa. Hayo ya lugha ya maudhi yanatokana na kutokueleweka kwa wasemaji..Viongozo wakiwa na lugha moja wataeleweka. Huyu akisema hili na yule lile wananchi wanaona kuna uongo mahali "Watabweka"..
Jambo moja la bandari, bandari wanasema lao, waziri lake,Spika lake, waandishi lao, walioenda Dubai lao, Heeee..!!!!
Kwanini "mbwa asibweke" ...
Basi sawa,acha hao uliowaita mbwa waendelee kubweka.
 
Sawa kabisa, kila mmoja wetu ana maoni yake, na ni vizuri kwenye maoni tusijumuishe, uweke huyo mwana siasa na alichokifanya ambacho wewe hukioni sawa, ndiyo nguvu ya hoja.

lakini kutukana na kuchochea kwa lugha za maudhi kunajenga au kunabomoa?
Hizo lugha zenye staha ni muhimu sana kwenye kuvuna shamba la bibi. Business as usual
 
Hata hawa jf wenyewe ni wabaguzi na wachochezi, mie nyuzi zangu nyingi tu wamezifuta na wala hazina athari kihivyooooo, ila za wagalatia bwashee, pamoja na kua ni za hatari na za kuuwana bado wameendelea kuziacha na kuzisambaza
Nahisi kitu hapo sio bure
 
Kuna kuchokozwa kwa mwananchi zaidi ya kuambiwa uende Burundi na Wanaokutumikia ?

Mipaka ipo wapi ya Maoni - Ukiachia vitu subjectlve ndio viwe viashiria vya kuzibana midomo mwisho wa siku vinatumika kuziba watu midomo..

Kama watu wanavuka uhuru wa kuongoza kwa kukanyaga makubaliano na kubadilisha chochote inapokuwa convenient kwao sio wao watakaoleta maafa bali ni hao wanaondesha hii nchi kwa matakwa yao binafsi......

Naona kuna rungu la kuziba watu midomo lililotumika kuwaziba kina Ndugai (walivyosema tukiamka tutakuta tumeuzwa) au yule mfanyakazi wa TRC aliyelalamika kuhusu Tozo linataka kuendelea / kuanza kutumika

Tuambie ukweli tu, things are falling apart.... Na ukichekelea unapoambiwa unaupiga mwingi vumilia au jibu ni kwanini unalikoroga unapoambiwa unaharibu... (Heri muonesha Kero kuliko mnafiki anayekupaka mafuta kwa mgongo wa Chupa)
 
Haakuna shaka yoyote, kwa sasa hivi tunaona Watanzania wengi, wanaojiita wasomi, wanaojiita mawakili wakitowa maoni yao kwa lugha ambazo ni za kuudhi, kukebehi, kukejeli mapa kutusi.

Haya yanayoendelea si maoni tena bali ni vunjifu wa amani uliokusudiwa. Uhuru wa maoni ni lazima uwe na mipaka.

Mtu anajiita mwanasheria msomi au wakili msomi , mwanasiasa, anasimama kwenye majukwaa ya habari na kurusha matangazo yaliyojaa chuki kuwa nchi inauzwa, au bandari inauzwa, Wazanzibari waniuza nchi. Na cha kushangaza sana waziri wa habari amekaa kimya. Waziri wa sheria amekaa kimya. Waziri wa mambo ya ndani amekaa kimya, waziri wa ulinzi amekaa kimya.

Nashauri, vyombo vya habari vyote vinavyorusha matangazo ya chuki vichukuliwe hatua kali za kisheria. Wale wote wanaosimama majukwaani na kufanya uchokozi wa makusudi wachukuliwe hatua za kisheria.

Mpaka sisi tuliozowea mitandao ya kijamii tunawashangaa moderators wapo kimya, watu wanaporusha matusi na kejeli mpaka kwa Rais na mawaziri wake. Hivi hatuyaoni? Au tunapenda huu uchokozi uendelee mpaka uzae madhara?

Kuuwasha moto ni kwepesi sana, kazi inakuja katika kuuzima.

Mimi nadhani wale wote wanaodai nchi imeuzwa waende mahakamani au kwa wao kupeleka madai au serikali iwaite mahakamani waje kuonesha nchi imeuzwa wapi na kwa lipi zaidi?

Nahisi kuna watu wapo nyuma ya pazia amabao wanadhani labda yataishia kiwepesi wepesi yakiachiwa yaendelee. Sasa hivi tayari chuki za wazi zinajionesha kati ya Wasio EWaisslam na Waislam, wasio Waarabu na Waarabu, Wabara na Wazanzibari. watu wa pwani na wasio wa pwani.

Hivi hayo yote kweli yamesababishwa na makubaliano ya Dubai na Tanzania yaliyopitishwa bungeni au kuna yanayoendelea nyuma ya pazia ambayo hatuyaelewi?

Tunaionmba serikali ichukuwe hatua za dhati, kila anaerusha au kuongea chuki akajieleze kwa ushahi wa hayo ayasemayo, kama hana ushahidi aseme ukweli ni na nani yupo nyuma yake anaemlipa au kumchochea kufanya hivyo.

Serikali itumie mbinu za kawaida na zisizo za kawaida za kiusalama ili kulinda raia wa nchi hii kujiingiza katika chuki na migogoro isiyo ya lazima. Huu ni mtego wa panya watania waliokuwemo na wasiokuwemo.

Naamini katika uwazi na ukweli na naamini katika uhuru wa maoni na habari, lakini kila uhuru ni lazima uwe na mipaka yake. Naona au Tanzania hatuna mipaka ya kujielezza maoni yetu aukama tunayo ama hatuijuwi au tunaiwachiie makusudi mipaka inavukwa?

Serikali, hususa Waziri wa habari, Nape Nnauye tueleze tupo bado ndani ya mipaka ya sheria au tumekiuka? Kama bado upo ndani ya mipaka ya sheria za uhuru wa maoni, tunaomba shertia zikafanyiwe ukarabati. Ili tuwe nchi yenhe kuheshimu utowaji mapni yetu uwe wa kuheshimiana.

Wewe kama hupendi nilichosema au kufanya mimi nifahamisheni usinitukane.

Moderators wa JF tunaomba majukwa haya siasa na habari mchanganyiko yapewe kipa umbele ili yasiwe ni chimbuko la maafa.
Kwa sasa asilimia kubwa wananchi ni wenye hasira kali, kwa sababu wakubwa hawawasikilizi
 
Back
Top Bottom