Ujio wa DR Congo EAC: Kiburi cha Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki sasa kimefika mwisho

Matadi, Boma na Banana Ile ni mialo tu... Hakuna biashara wala sophisticated machine za kufanya kuweza kuhimili biashara ndani ya Congo. Hiyo Matadi ambayo ndio kubwa kabisa anategemea transhipment from Angola.
Mualo na unachukua ocean going ships!?
 
Unaeleza mini kwani watanzania south Sudan na kongo tumezubaa? Huelewi unachoongea.Uko sifuri

Tanzania tumekamata kongo kuliko member yeyote wa EAC EAC kibiashara sababu ya position yetu

Anyway nisimwage mtama kwenye kuku wengi sababu na mimi nina biashara kongo
Wafanyabiashara wanaofanya biasharaa kongo wananielewa vizuri wawe wanafanya biashara ndogo au kubwa wananielewa barabara
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza
Naomba ufute hiyo kauli kusema watanzania tumezubaa kupiga pesa kongo au Sudan kusini

Hujiulizi kwa nini Tanzania tulipeleka majeshi south Sudan na kongo

Niishie hapo
 
Sasa unavyosema kuna wababe wa kivita tu? Ukweli ni kuwa kiburi cha Tz kama Darling wa EAC kimefika mwisho. Nategemea kuona sasa EAC inapiga hatua.
 
Sasa unavyosema kuna wababe wa kivita tu? Ukweli ni kuwa kiburi cha Tz kama Darling wa EAC kimefika mwisho. Nategemea kuona sasa EAC inapiga hatua.
Njaa tu imewashinda kuidhibiti huko kwenu Kenya, sasa mtaweza kupambana na hao waasi wa Congo?.

Pia Alshaab wanawapapasa wajisikiavyo, sasa hiyo nguvu ya kuwekeza Congo huku mkipambana na waasi inatoka wapi?.

Tanzania ndio nchi pekee inayoamua EAC iwepo au isiwepo maana ina kura ya Veto. Hivyo bado wote mnaitegemea Tz kwa kila kitu ili kudumisha uwepo wa EAC. Mengine ni maneno tu
 
Congo kuna waasi gani wa maana? Wale ni bandits tu wanaotafuta ugali.
 
We nyang'au nenda kanunue Sasa ardhi kongo uone hata kama utailika bado Tanzania atabaki ni baba tu
 
We nyang'au nenda kanunue Sasa ardhi kongo uone hata kama utailika bado Tanzania atabaki ni baba tu
Jipe moyo, enzi za TZ kubembelezwa zimeisha. Hata makao makuu ya EAC yanaweza hamishwa
 
Sisi ni kama Russia ni vitendo tu
 
na wewe kwa kweli, yaani dr congo amtishe tanzania!!??!! hata karwanda tu hakababaisi. ndio ni likubwa lakini halina mipango iliyonyooka. hamna kitu hilo
 
Hali ya kisiasa na kiusalama ni mwiba kwa Drc, huku Tz inajivunia hali nzuri kwenye hayo maeneo mawili.
Ishu ya usalama wa DRC kwa sasa ni wanyang'anyi tu. Hakuna kitisho cha maana cha usalama. Ni wanyang'anyi wanaotafuta ugali. Na pia DRc ni kubwa sana. Kuna sehemu nyingi hakuna hao bandits.
 
na wewe kwa kweli, yaani dr congo amtishe tanzania!!??!! hata karwanda tu hakababaisi. ndio ni likubwa lakini halina mipango iliyonyooka. hamna kitu hilo
Lakini inapotential kubwa. Itakuwa na say kubwa sana jinsi mambo ya EAC yanavyoenda. Ina ardhi kubwa, watu wengi na rasilimali nyingi. Ikisema ikikataa kitu impact yake ni kubwa, kama ambavyo Tanzania ilikuwa. Akikubali ushirika wa ardhi kwa members wa EAC, hata Tz akikataa hakutakuwa na madhara, zaidizaidi ni Tz ndiye atapata hasara.
 
Ishu ya usalama wa DRC kwa sasa ni wanyang'anyi tu. Hakuna kitisho cha maana cha usalama. Ni wanyang'anyi wanaotafuta ugali. Na pia DRc ni kubwa sana. Kuna sehemu nyingi hakuna hao bandits.
Hao unaowaita wewe wanyang'anyi ndio wameifanya kuwa na idadi kubwa ya wakimbizi kwenye eneo la maziwa makuu.

Na ndio hao wanaohatarisha hata shughuli za kiuchumi na kibiashara huko (rejea kutekwa kwa madereva wa malori).

Ndio hao hao wanaohusika na vitendo vya ubakaji na mauaji kwa raia huko kwenye eneo la Drc mashariki.

Kama unaona hilo ni tatizo 'dogo' tu, Sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…