Ujumbe wa Afande Sele akimlilia Hayati Magufuli

Ujumbe wa Afande Sele akimlilia Hayati Magufuli

Kwa hali hii mmmhh
 

Attachments

  • 1507072_afandesele.jpg
    1507072_afandesele.jpg
    23.8 KB · Views: 1
Historia ya kizazi chetu na ya babu zetu ni tofauti wao walikuwa na tamaduni zao na Sisi tumekuta tamaduni zetu kwa hiyo naamini nilichikiona au kukikuta hayo mambo kwamba tumeletewa ndio tusiamini siungi mkono hoja na china kutokuwa na dini hainizuii mimi kuamini ninachikiamini.
Sasa wewe unamaendeleo kuwazidi wachina na wakorea
 
Afande amemlaumu sana Mungu kwa kutuonea waAfrica.

Ameshauri watanzania na waAfrica kuachana na dini za wazungu tuamini mizimu yetu na jua.

Amesema hayo akishangaa kwa nini Mungu aliyepewa kipaumbele na JPM ameshindwa kumlinda na husda za wazungu mpaka wakafanikiwa kumuondoa.

Kumbe kitu cha Moro ni matata kweri kweri kwa ukali kuliko hata kile cha Arusha!
 
Napenda kuwapa pole kutokana na msiba wa kiongozi wetu.

baada ya Magufuli kufariki imesambaa voice clip iliyotoka kwa Afande Sele akilalamika kuhusu kifo chake akafika mbali zaidi na kutoa lugha za kumtukana Mungu. jambo hili limeonekana kuibua hisia nzito na hasira juu ya afande sele, mpaka watu wengine wameanza kulazimisha jeshi la polisi kumchukulia hatua kwa kosa la kumtukana Mungu.

Kwanza naomba niweke wazi kuwa mimi ni mkristo mwenye imani ya kipentekoste ingawa sisali mara kwa mara, naamini uwepo wa Mungu na ninamjua kwa sehemu.

Binafsi sioni sababu ya kuanza kumshambulia Afande Sele kwa alichosema maana ametoa uhalisia uliopo ndani yake sio mnafiki na mimi napenda watu hawa hata biblia imekataza kuwa mnafiki. Katika taifa kama Tanzania lenye uhuru wa maoni ingawa haikuwa hivyo kwa miaka hii ya karibuni labda kama hali itabadilika Afande sele hajafanya kosa lolote kutoa maoni yake kuhusu huyu tunayemuita Mungu.

Ni vyema tukaelewa kuwa sio lazima kila mtu aamini kuwa Mungu yupo na wanaoamini wana uhuru wa kumuabudu Mungu wanayemtaka ndio maana kuna miungu mingi, dini nyingi na ibada tofautitofauti. Sio lazima kila kinachosemwa na mtu kituridhishe au tukikatae vingine hatuna budi kuvikubali ili kuelewa mtazamo na msimamo wetu juu ya yule tunayemuamini kuwa ni Mungu. Mbona watu hawakutaka washirika wa midahalo ya waislamu na wakristo kuwa dini ya kweli na mungu wa kweli kipindi cha sheikh Mazinge wachukuliwe hatua maana sio kila wakati waliongea vizuri kuhusu upande pinzani.

Binafsi naona swala hili kuwa ni vita nyenye wahusika wawili tu MUNGU na afande sele, aliyetangaza vita ni afande sele kinachobaki ni uamuzi wa MUNGU kuamua kukaa kimya au kuingia vitani, wengine tukae kimya hatuwezi kumtetea MUNGU nafasi yetu ni kuangalia na kujifunza ili kujenga imani zetu. Serikali ina mambo mengi ya kufanya isipoteze nguvu kwa Afande Sele.

Ni jukumu la MUNGU kujitetea na kudhihirisha kuwa anafanya kazi na ana nguvu sio mwanadamu kumtetea Mungu. rejea kisa cha gideoni kwenye biblia alipovunja miungu ya jamii yake. WAAMUZI 6:28-32

Watu open minded kama wewe ndo watamuelewa afande sele. Wengi wao vichwa panzi akili mgando wanashindwa kuelewa kuwa hii nchi haina dini kila mtanzania ana haki ya kuabudu na kuongea anachokiamini.
 
Kama ulismkia mama samia suluhu ametamka wazi kuwa alikua anaumwa moyo kwa miaka 10 so it means kabla hata hajawa rais alikua mgonjwa tusiwasingizie wazungu tujifakari kali sana kumbuka lowasa aliambiwa ni mgonjwa atatufikia madarakan lakn tunaona wale waliotmka hayo wanaondoka mmoja mmoja
mzee achana na kitu kinaitwa system ni hatari sana....hivi ile series ya 24 hrs mlikua mnaangalia kujifurahisha? nakushauri karudie ile series utajifunza kitu....
 
Empty Brain.Ikifika siku,saa,dakika,sekunde lazima uondoke kama alivyoondoka.Ukitaka kuthibitisha rejea walivyommiminia risasi kule Dodoma,lakini wapi,anadunda na anawasumbua ile mbaya.Siku yake ilikuwa bado.Acha ujinga wazungu watahangaika naye wa nini,kwani ana nini cha kutisha.Andika kwa kutumia akili na sio kwa kutumia.....................yako.

Hizi ndo akili za kiafrika siku zote wao ni kuwaza tu kwamba wazungu wanawaua!! This is a mental slave, uzembe afanye mwingine na yakimpata eti utasikia Mzungu kahusika! Ni ujinga sana watu kufikiria huo upuuzi.
 
Sherehe ya wajinga ni kushangilia tu na kutukana badala ya kutafakari Mafundisho ya nyakati hizi..
Watu wanatuhumiana kuhusu Uchumi na Covid wakiwa na nia ya kupata fursa za Siasa na Madaraka badala ya kufikiria Maendeleo ya nchi kama BABA WA TAIFA alivyoasisi na kuelekeza.
Hii ni aibu kubwa kwa Taifa watu kupungua Hekima.. Baadhi ya watamani madaraka wanatafuta jinsi yoyote watu wawaone kuwa wanastahili kuongoza Nchi.
Kwakweli binadamu alipofikia ni hatua mbaya Sana Mungu atulehemu
 
Afande amemlaumu sana Mungu kwa kutuonea waAfrica.

Ameshauri watanzania na waAfrica kuachana na dini za wazungu tuamini mizimu yetu na jua.

Amesema hayo akishangaa kwa nini Mungu aliyepewa kipaumbele na JPM ameshindwa kumlinda na husda za wazungu mpaka wakafanikiwa kumuondoa.
Afande lazima anapakuliwa pilau akivuta msuba,kaanza tabia za vidole juu
 
Back
Top Bottom