DOKEZO Ukatili unaofanyika kwa watoto wa shule binafsi ya EXPERANCIA (Sengerema)

DOKEZO Ukatili unaofanyika kwa watoto wa shule binafsi ya EXPERANCIA (Sengerema)

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Awali ya yote napenda kuushukuru uongozi wa Jamii Forum kwa kuendelea kuruhusu kufichua maovu yanayoendelea kutendeka katika jamii zetu.

Kuna ukatili wa watoto (wanafunzi unaoendelea katika shule ya binafsi (Experancia) iliyoko wilaya ya Sengerema.
1. Watoto wanapatiwa adhabu zenye kuwazidi uwezo ikiwa ni pamoja na bakora maeneo yasiyo sahihi na zenye kuwazidi uwezo kulingana na umri wao.

2. Watoto wa kike kuingiliwa na Mkurugenzi wa shule husika kwa zamu na baada ya hapo kuwapatia vidonge vya kuzuia ujauzito (P2), na inasemekana kwa bahati mbaya kuna mwanafunzi aliwahi ingiliwa na kusababishiwa ujauzito na baada ya hapo zikafanyika jitihada za kuutoa huo ujauzito 😭💔.

Ninaomba uongozi wa Jamii forum tuwasaidie watoto wetu jamani, dunia sio mbaya ila Binadamu tumegeuka wabaya kuliko hata wanyama wenyewe😭😭. Dunia imekuwa sio mahala salama tena.

Dkt. Gwajima D tusaidie kuwaokoa watoto wetu.

Hizi ni picha zilizotumwa na mzazi baada ya kwenda kumsalimu mwanae na kukuta khali isiyo ya kawaida kwa watoto.

View attachment 3125656View attachment 3125657View attachment 3125658View attachment 3125659
Mzazi aliuliza walimu huyo kijana alifanya kosa gani?

Isijekuwa mnasagiana kunguni na kuwekeana mizengwe ya kibiashara hapa.

Mwanafunzi akilambwa mboko, siwezi simama moja kwa moja na kulaumu, lazima niuchimbue undani wa kisababishi kwanza.

Mbona hatujaona foleni ya picha ya pamoja ya waathirika walalamikaji kama jambo hilo linatendeka kwa wanafunzi wengi/wote.

Na kwa nini uoneshe mgongo bila sura yake kama jambo hilo ni la kiuonevu?

Je kama picha ni ya kuokoteza ili itumike kutengenezea fitina hapa?

Toa maelezo ya kina pamoja na picha zenye kueleweka ili tuweze kulipima jambo hili.
 
Huyu ni mwanafunzi wa kawaida!? Mbona Kama kakomaa Sana!!?
 
Hizi tuhuma ni za kweli Kuna wadogo zangu wawili wapo hii shule,mmoja ni form three na mwingine form one asee wanasema ni hatari Sana wanapigwa vibaya Sana Kuna ukatili usio na vipimo.

Juzi ilikuwa ni visiting day alienda mdogo wangu wa like kuwaona shuleni ajabu amewakuta na wakovu ya kudumu na wote wanasema wanaumwa kwahy wamerudi nyumbani.

Chanzo cha yote hayo ni huyo mama mhaya aliyewaleta wahaya wenzake waliofail form four na wasio walimu kuja kuwa walimu wa shule hii,katika upelelezi wangu mtoto wa kiume wa mmiliki wa shule ambaye nae asiye na taaluma ya ualimu ndo kila kitu hapo shuleni na ndo huyo anabaka watoto.

Nipo tiari kutoa ushirikiano kama mamlaka zitahitaji ushahidi maana Kuna hawa wadogo zangu wanaweza kusema yote wanayofanyiwa.
Okay..Basi nenda pm kwa Dkt. Gwajima D
 
Uliza kwanza alifanya nini hadi kupewa adhabu ya namna hiyo.
Kabisa..
Kwa private unaweza kuta dogo alimshika tackle madam..

Hao madogo siku hizi mabegi yao yamejaa vileo...visungura, banger... 24/7 wako high.
 
Hii Hali haikubaliki kabisa. Nasikitika binafsi nimechelewa kuona ila tayari timu yangu ya Mwanza ilishaona na ilishaanza kufanyia kazi. Ngoja tusubiri mrejesho. Ahsanteni sana kwa kuendelea kushirikiana nasi kwenye kufuatilia na kuibua taarifa ambazo huenda tusingezipata. 🙏🏽
tupo pamoja mheshimiwa. Tunakukubali mnoo. Mungu aendelee kukujalia hekima na busara
 
Lazima na voodoo inahusika na Mkurugenzi.

Uliyeandika voodoo haija kunyamazisha

Tupe habari zaid, tangu uandike hapa huko imekuwaje
 
Hii Hali haikubaliki kabisa. Nasikitika binafsi nimechelewa kuona ila tayari timu yangu ya Mwanza ilishaona na ilishaanza kufanyia kazi. Ngoja tusubiri mrejesho. Ahsanteni sana kwa kuendelea kushirikiana nasi kwenye kufuatilia na kuibua taarifa ambazo huenda tusingezipata. 🙏🏽
Jembe langu hili hapa tayari! Asante Mheshimiwa. Itapendeza tukipata na mrejesho!
 
Duh nikikuta mtoto wangu kafanywa hvi nitamalizana na hao waalimu atakalia mtu ukuni
Hiv kwel mtoto mpaka apogwe kiasi hicho na mzazi achukulie poa tu, inawezekana kweli????

Yan mtoto apewe mimba na mwalimi mpala waitoe bado mzazi awe hajachoma moto hiyo shule???

Mkuu, naulizankwa nia njema, unayosema ni ya kwel au umezidisha chumvi au una jambo lako ninafsi na wenye shule???
 
Lazima na voodoo inahusika na Mkurugenzi.

Unayeandika voodoo haija kunyamazisha

Tupe habari zaidi, tangu uandike hapa huko shuleni imekuwaje?
 
Walahi Mimi hakuna atakaeamua Ilo balaa lake
Ila wananchi wa Tanzania tumezidi uzwazwa. Haya yote yanatokea na wazazi wako kimya? Huwa hawawasiliani na watoto wao? Wanashindwa kujipanga wavamie shule kwa pamoja wamshikishe adabu huyo hayawani? Ndiyo, mambo mengine ni ya ku deal nayo kihuni... Unalipa fedha ili mtoto aende kuteswa? Hakuna shule nyingine?
 
Wenyewe wanakuambia viboko vinaleta nidhamu na maadili.

Lakini tujipime nani anaongoza kwa maadili na nidhamu mbovu kati yetu na watu wa Ulaya?

Wapi wanaongoza kwa wizi, ufisadi, ubakaji, rushwa, ujambazi? Wapi wanaua albino? Wapi wanawaibia majeruhi wa ajali na kuwamaliza kabisa?

Viboko vipo kwa ajili ya kutengeneza nidhamu ya woga na kuandaa machawa wa baadae.
Viboko ndiyyo vinafanya waafrika tunakuwa makatili sana. Ona mtu kama Magufuli inaonekana alikuwa kwenye mazingira ya kupigwa na ukatili mkubwa ndiyo maana na yeye aligeuka kuwa katili.
 
Halafu utashangaa kuna wazazi bado wanaacha watoto wao hapo kisa bado hayajawakuta matatizo na wengine bado wanawapeleka shule hiyohiyo.
 
Hii Hali haikubaliki kabisa. Nasikitika binafsi nimechelewa kuona ila tayari timu yangu ya Mwanza ilishaona na ilishaanza kufanyia kazi. Ngoja tusubiri mrejesho. Ahsanteni sana kwa kuendelea kushirikiana nasi kwenye kufuatilia na kuibua taarifa ambazo huenda tusingezipata. 🙏🏽
Sawa docta...ila hapo Sasa lazima wawe na jicho la tatu vile vile maana katika shule zinazofanya vizuri wilayan sengerema ni hiyo..na washindani wake watakuwa wamepita humo humo
...maana sisi wabongo kwa fitina na kuharibu taswira ya mtu/taasisi tupo vizuri sana..
 
Back
Top Bottom