UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Mkandara;9406994]Tukiendekeza fikra hizi hapa hapatakuwa na Muungano kabisa na mtakuja nambia maana nashukuru Mungu kanijaalia kuona mbali.
Zanzibar waliojiondoa katika muungano kwa katiba ya 2010 hukusema lolote na hata sasa huoni kama ni tatizo.
Nyerere alisema kama wznz hawataki muungano hatawapiga mabomu. Wewe unasemaje, wapigwe?

Ni wewe uliyesema takwimu za Warioba zina matatizo kwasababu wznz walitaka mkataba(kumbu kumbu zipo JF) vipi leo useme msimamo wa wznz wengi ni serikali 2.
 
Haya ungeyasema wakati JK na Karume wanaruhusu katiba ya znz kuwa juu ya JMT tungekuelewa. Leo muungano ushavunjwa kwa kuanza na katiba, halafu unatisha watu kuwa nchi itasambaratika. Mbona haijasambaratika wakati katiba inavunjwa.
Unachotaka ni ukondoo wa Tanganyika, kwamba ifike mahali wznz wanalala Watanganyika tunatandika vitanda vyao kwasababu tunataka muungano. Wao wanasema hawataki muungano, wewe unapata hoja wapi kuwatisha kwa mifano hiyo. Wamejiandaa kukabiliana na changamoto kwanini wewe uwe na hofu.
Kwetu watanganganyika, hebu tuambie nini unadhani tuna umuhimu nacho kwa kuungana na znz zaidi ya kutoa misaaada.
 
Hebu eleza vita itatokeaje, maana sioni vita labda mwenzetu unaiona.
Kama wznz hawataki muungano sitawapiga mabo,u-Nyerere
 
Una maana katika makundi CCM nayo ni kundi na inapaswa kutetewa kama makundi ya akina mama na walemavu.

Ukawa imeanza lini? Siyo baada ya NEC ya CCM na msimamo wao wa kuchakachua.
Umesema unakubaliana na CCM, hili nalo unakubaliana nao?
 
Mkandara: mbona Muungano wa Marekani una miaka zaidi ya 200 na wameendelea kutushinda sisi kwa kila kitu..Hadi sasa hivi sijaona hoja ya maana kabisa zaidi ya wajumbe wote kupingana kwa jina la chama.
Muungano wetu na Marekani una historia iliyolingana? Katiba za Marekani na Tanzania zimeandikwa katika muundo sawa.
Kama Marekani hawana tatizo ya Puerto Rico yametokeaje?
Kwavile Marekani waliandika katiba ya wananchi, na sisi tunaandika kwa vyama, hivi huoni kuna tofauti ya miungano hiyo miwili? Je, unadhani ni sawa kulinganisha chungwa na Fenesi kwasababu tu yote yanaitwa Matunda




U
 
Marekani ina kiti kimoja UN. Canada ina kiti kimoja UN.
 
ZNZ wanatuchukia kwa sheria za uhamiaji, ukaazi na ajira. Hilo hulizungumzii unachoona ni tatizo ni pale Tanganyika inapotajwa. Wanajamvi wangekuelewa kwanza kwa kukemea uchafu wa znz halafu ueleze point.

Kama hutakemea ubaguzi wa kizanzibar huna moral authority ya kukemea ya EU. Ubaguzi tayari upo hapa.
Akifanyiwa Mtanganyika huo ni muungano, akifanyiwa mznz ni matatizo kama ya EU

Hiyo model ya EU ndio wznz wanaitaka sasa wewe ambaye huna nchi kama wao machungu yanakupata wapi.
ZNZ iliposema ni nchi na kuwachoma moto Watanganyika Mkandara anaona hewalaa hilo sawa.
Mtanganyika akisema amechoka kubeba furushi la samadi Mkandara anakuja juu.

Ndiyo maana tunasema ukondoo basi tunataka Tanganyika kama haiji tuvunje jahazi tugawane mbao.
Hata wakilazimisha, tayari mbegu ya chuki alityopanda mznz itamea ukumbini kwakwe.
 
Imeripotiwa kwamba Rais Kikwete katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi, amesema kwamba "ukawa wameenda tu likizo, likizo ikiisha, watarudi bungeni". Je hii ni dalili ya historia ya juisi na maembe kujirudia?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Ni nyie mnao amini Zanzibar hawataki Muungano wakati tunayaona Bungeni ni kina Jussa na rasimu nzima imeandikwa kwa kuchukua mawazo ya kina Jussa. Mara zote ktk maandishi yangu nimekuwa nikitenganisha kundi la Maalim Seif/Jussa na lile la Wazanzibarkwa sababu nawajua tofauti zao. Wewe usojua ndio unachanganya madawa sana.

Kabla ya bunge la katiba kuanza mlituambia CCM wote wa Zanzibar na BLW wanataka serikali 3 ila CCM ndio hawataki sasa tunaona tofauti kabisa na hoja zao ni nzito na kali zaidi ya viongozi wa Bara. Katiba ya mwaka 2010 haikuandikwa na Wazanzibar bali iliandikwa na viongozi wa CCM na CUF. Katiba ya sasa ya JMT- 1977 iliandikwa na viongozi wa CCM TANU/ASP/UMMA wakichukua mrngi toka ile ile ya CCM na Tanganyika haina maana Watanganyika ndivyo walivyotaka.

Kama una kumbukumbu nzuri ama kuna record humu JF tafuta mada iliyozungumzia katiba ya Zanziba ya mwaka 2010 Nani alikuwa mtu wa kwanza kupinga na kukashifu hujuma ile ilofanyika pasipo kuvihusisha vyama vingine vya kisiasa. Wewe unayazungumzia leo wakati mimi nimeyasema toka mwaka 2010 humu humu JFbila shaka wengine watakuhakikishia hilo. Tatizo lenu wapenda S3 hamtaki kulivua koti la Muungano kama mlivyo iga wazungu japo kuna hatari kubwa ya kumfukuza kichaa (CCM) mkiwa uchi wa nyama.

Leo hii mnataka kutuandikia katiba ya Muungano mnataka kwanza muundo wa serikali, haya sii mawazo ya wananchi hivyo huwezi kusema Wabara wanataka serikali 3. Mnataka muungano wa shirikisho haina maana Wabara wamechagua serikali ya shirikisho. Mnataka serikali kuu iwe na wizara chache, mambo mengi yasiwe ya Muungano tena mkiamini haitakuwa na gharama kubwa!

Haya yote ni mawazo yenu sii ya Watanganyika wala Wazanzibar kwa sababu mtu kama mimi najua fika mfumo wa serikali 3 na gharama zake kwa sababu naishi ktk mfumo huo, nyie mnaosoma vitabu tu academics mkitegemea mnaweza kurusha ndege. Hivyo mtakachopitisha huko haitakuwa mawazo ya wananchi kwa sababu wajumbe wenyewe wanasema wazi kwamba wapo pale kuwakilisha mawazo yao wenyewe (mawazo binafsi) na ati hawawaklilishi kundi ama kundi lolote kwani JK kawachagua wao kama waona kuwataka wajumbe wengine wafanye hivyo.

Hizi fikra za kibinafsi ndizo zimefikia hata kusema Rasimu hii ni ya Warioba, mnataka aheshimiwe yeye na uwezo wake wakati huo huo mnadai ni mawazo ya wananchi wengi, sasa cha kujiuliza hii rasimu ni ya Warioba ama ya wananchi? Hawa UKAWA wenye mawazo binafsi na walokimbilia Zanzibar kuwashawishi wananchi huoni kama ni wao wanaowakilisha mawazo ya kina Jussa huku wakidai kuitaka Tanganyika? kama kweli wanaitaka Tanganyika kwa nini hiyo mikutano yao isiwe Tanganyika kwa wenye ridhaa ya kidai nchi yao ila wamekwenda Znz!

Hawa ndio mnawaamini na kuwaita wajumba wa baraza maalum la kutunga KATIBA. Nilisha sema wazi kuwa Katiba haitungwi na wanasiasa wala vichwa vya wasomi njaa ili mradi kujaza bunge bali hutungwa na - WATAALAM WA MAMBO YA kATIBA (INTELLECTUALS)
 
Wewe mgumu sana kuelewa mkuu wangu. Purto Rico kuna tatizo gani? wao sio state ya Marekani hadi sasa, ni kama koloni tu au territory kama ilivyo Yukon kwa Canada, Falkland kwa UK. Hivyo huwezi kuifananisha na Zanzibar ambayo ni state ilounda mungano wetu. Kifupi Zanzibar kwa Marekani inakuwa ktk zile states 13 za mwanzo kuunda USA acha hata hizo 37 zilizofuatia.

Mkuu kazi iliyopo hapa ubaoni ni muundo wa serikali yetu kabla ya kuandika katiba mpya. Kwa maana ya kwamba hapa tunaandaa janvi ili katiba ya TAIFA ikidhi maridhiano ya muundo wa serikali. Hivyo basi unaweza utazama muundo wa serikali ya Marekani, India Canada na hata Uingereza ukautumia kuunda serikali zetu, na kwa kufanya hivyo hututakuwa tunaiga Katiba ya nchi hizo. Muundo wa seikali kitu kingine tofauti kabisa na Kuandika Katiba! hizi ni kazi mbili tofauti na nyie kwa fiktra zenu mnataka kuzifanya kuwa kitu kimoja.
 
WAGAWE UWATAWALE

Mwanzo kabisa wa bandiko tumeeleza jinsi ambavyo mbinu zitatumika kuwagawa UKAWA.
Hii ni baada ya hoja za gharama, jeshi kushindwa.
Hizo ndizo zilizokuwa silaha za CCM walizotegemea zingeweza kuangamiza hoja za S3.

UKAWA walichukua muda mrefu kuanza mikutano. Katika muda huo CCM wamekuwa wakivuta kasi ili watoke bungeni na kuanza ksambaza hoja zao za upotoshaji.
Moja ya upotoshaji inayoonekana kutumiwa ni UKAWA kupewa fedha na mataifa ya magharibi.

Hoja hiyo ilioonekana kama laini kwasababu imetumika kila wakati serikali inapokosa hoja za kushawishi wananchi.Hoja hiyo imekuwa unafungamanishwa na amani na utulivu.
Kwamba, kupingana na serikali ya CCM ni kuvuruga amani na utulivu. Huo nao ni wimbo uliozooeleka.

Kwa bahati mbaya baadhi ya watu huvutika kirahisi na hoja ya amani na utulivu.
Hoja hiyo inapofungaminishwa na mataifa ya magharibi, huwatisha watu bila sababu yoyote.

Sasa hivi kuna mifano kwamba Tanzania itageuka kuwa somali, Ukraine au Russia.
Wananchi wanaoangalia TV wanaamini hasa wakiona nchi za magharibi zikiwa katika mvutano kama kule Ukraine,ndipo CCM wanapotumia mwanya kuwachanganya wananchi wasiobahatika kuwa na uelewa wa mambo hayo.

Hakuna mapambano hata kama muungano utavunjika leo.
Ni hisia tu zinapandwa kwasababu hazipo sababu za maana za kuthibitisha kuwa kutatokea vurugu.

ZNZ ni nchi na imejitambua hivyo, nani ataweza kwenda kuishambulia.
Na mapamabano yataanza kwa kisingizio gani hasa. Hizi ni propaganda za kuwatisha wananchi.

Hata hivyo UKAWA wasidharau propaganda za CCM.
Kwa mfano, CCM imeanza kutumia vijana wake kwenda kusambaza uongo.

Msome Paul Makonda hapa uone jinsi vijana wanavyotumika vibaya katika taifa hili....
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/647862-nje-ya-bunge-hakuna-katiba-ya-wananchi.html

Halafu soma habari hii ya gazeti la habari leo
http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/24753-ukawa-waanza-mivutano

Utakachoona ni kuwa hoja ya Makonda ya kuvuruga amani na usalama na kutumiwa na mataifa ya magharibi ndiyo ile ile iliyotumiwa na habari leo.

Tofauti ni kuwa habari leo wameitumia kuwavuruga UKAWA kwa kusema kuna pesa zinatumwa kutoka mataifa ya magharibi na zimeliwa na baadhi ya vongozi.

Hoja hiyo inatueleza mambo makubwa mawili
1. Kwamba, kuna darasa ambalo mhariri wa habari leo na Paul Makondawamehudhuria na kuondoka na somo moja.

2. Kuwa mbinu za kuwagawa UKAWA sasa zipo kazini.

UKAWA lazima waelewe kuwa njia ya kupigania wanahciokitaka haitakuwa rahisi na ina wasaliti.
Wapo watakaolipwa ili kufanikisha mipango ya CCM.

Hapa ndipo ninashawishika na hoja ya Mchambuzi kuwa kauli ya rais Kikwete ya UKAWA wapo likizo na watarudi haikutoka bila sababu.

Tayari Kikwete anajua na ana vyombo vya dola, mbinu wanazosuka huenda zimefikia hatua nzuri hata kumfanya atambe hivyo.

UKAWA lazima wachukue tahadhari zote vinginevyo mpango wa kuwavuruga utatimia muda si mrefu.
 

Kiukweli mkuu hujibu swali...
Sidhani kama hili swali la serikali 2 zitasaidiaje Tanganyika kuvua koti la muungano linajibiwa kwa sentensi 20. Unachojitahidi kueleza wewe ni kwa nini huoni umuhimu wa serikali 3.
Lakini ni kwa vipi serikali 2 zitatatua tatizo, kiukweli hata hujagusia kabisaa...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nashukuru nawe umeliona hilo.

Mkandara zaidi ya mara 16 anasema Tanganyika imevaa koti la muungano kwa jina la Tanzania na hivyo muafaka ni kulivua.

Sisi tunakubali tunasema ili kuvua koti lazima Tanganyika izunduke ili tuwe na SMZ na STG (Serikali ya Tanganyika). Hapo tutakuwa na mambo 7 tu mengine tumevua koti.

Mkandara anasema S3 hapana, kinachotakiwa ni kuwa na mambo ya znz na ya 'serikali ya bara'. Tumemuuliza hiyo ya bara ni ipi? Hakuwa na jibu ila katuambia Tanganyika ndiyo imekubali kutoa mamlaka kwa Tanzania hivyo hakuna Tanganyika.

Tukamuuliza kama ni hivyo vipi unaweza kutenga mambo ya Tanzania 'Tanzania bara ya Mkanadara' na SMZ?Hana jibu.

Alichosema ni kuwa ili kuua malalamiko ya wznz lazima tuwape miradi na mapesa meengi tu. Tuache kujenga bandari zetu ili mizigo ifikie znz.

Tena akaseam hotuba ya JK tarehe 25 April ameahidi misaada ya miradi na hiyo ni suluhu ya matatizo. Huu muungano wa Tanganyika kununua una manufaa gani. Yaani tuchukue rasilimali zetu twende kuongeza kwa wale walio nazo tena wakitubagua! kha

Nimemuuliza vipi malalamiko ya Tanganyika, hakika hana jibu. Alichojaribu ni kuhalalisha kuwa Zanzibar kuwabagua Watanganyika ni halali ili kulinda isimezwe katika muungano.

Kama ulivyosema mkuu Tuko, watetezi wa S2 hawana hoja za kutetea, walichonacho ni kukosoa S3 tena kwa hoja zisizo na mashiko.

Wznz hawataki muungano, wznz hawawataki Watanganyika bado tunalazimishwa kuwa wakipewa zaidi watatulia.

Huu uzmbe wa kuwapa kila wanachodai kama watoto wadogo sasa wameufanya mtaji.
Madeni ya michele, umeme n.k. wanasukuma Tanganyika
Imefika mahali hawana adabu wala heshima na katiba. Hili halivumiliki sasa.

Tunataka S3 ili tuwe na fiscal autonomy ya mambo yetu kama walivyo na yao.
Hatuna sababu za kuvaa koti lililojaa kupe na kunguni, etit unalaumiwa tunapotaka kulisafisha.

Tutavua koti na vilivyomo. Kama sheria na taratibu hazitafanya kazi tutailinda na kuitetea Tanganyika kama wazee wetu waliotangulia walivyofanya.
 
Kauli ya kutumiwa na watu wa nchi za magharibi imetumiwa na Paul Makonda, gazeti la habari leo na sasa Nape Nnauye

Idadi ya wanafunzi wa 'darasa ' inagongezeka. Msome Nape kama alivyobukuliwa na Habari leo
Naye Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema Ukawa ni kikundi cha wachumia tumbo ambacho kinategemea fedha za wasioitakia mema Tanzania kuvuruga amani iliyopo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu wewe unashindwa kuliona tatizo kwa sababu mnatazama KERO badala ya Mapungufu yaliyomo ktk mfumo tulokuwa nao wa kiutawala. Ni mfumo wa kiutawala ndio unaweza leta maendeleo ama kutoyaleta kwani hoja kubwa ya Wazanzibar ni MAENDELEO ktk visiwa vyake na ndipo kero zilipokuja baada ya wao kutopewa kipaumbele kwa miaka 30, japo nyie kizazi kipya mnadai miaka 50 serikali 2 imeshindwa kuondoa kero.

Kwa mwenye weredi ataelewa kwamba sii muundo wa serikali unaoweza kubadilisha maisha ya wananchi isipokuwa tu ikiwa muundo huo utagawa mamlaka ya shughuli za serikali ktk serikali za nci na majimbo. Kosa kubwa la muundo wa serikali 2 ni kulimbikiza shughuli zote za mamlaka ya serikali kuwa chini ya serikali kuu na zile za states ama majimbo wana mamlaka madogo sana ya nayo ni ahadi na kutembeza bakuli kama kanisani. They can't make any decision on behalf of their people without approved by the central government, huu mfumo wa Kiimla ndio tatizo letu na katiba mpya inaweza kabisa kubadilisha hili bila kuwa na mfumo wa S3.

Ndio maana OIC ilipigwa vita bara kwa kutumia jina la JMT, ndio maana Chadema na CUF japo walishinda chaguzi ktk majimbo tofauti hawana mamlaka ya kuendesha shughuli za maendeleo ya majimbo hayo pasipo kuidhinishwa na kukatiwa fungu na CCM (serikali kuu)na kadhalika. Hapo walipo sii Chadema wala CUF wanaweza kuleta maendeleo kwa wananchi, tukiamini hili pasipo mabadiliko tutakuwa tunajidanganya iwe kwa serikali 1,2 au 3.

Sii Zanzibar wala Majimbo wana mfuko wao wa maendeleo kutokana na kodi za wananchi wake, pasipo kupewa toka bajeti ya serikali kuu. Hili ndilo jibu langu hivyo sitetei serikali 2 wala 3 kwa sababu najua wingi ama uchache wa serikali sio tija, huu ni mchezo wa kisiasa ambao CCM na vyama vya Upouinzani pamoja na wahaini wanautumia kupambana wao kisiasa ili kuunda katiba inayowalinda wao kama wanasiasa ama asasi na sii wananchi wa JMT. Maadam tunahitaji katiba ya wananchi swala la Muungano wetu ni la mwanzo na mwisho na halihusiani kabisa na kuandikwa kwa katiba mpya ambayo sisi wananchi tuloiomba ila limeongezwa na wanasiasa kwa sababu zao na faida zao. Sasa mkuu wangu unataka jibu lipi zaidi?

Nirudie Hakuna muarobaini wa matatizo tulokuwa nayo kupitia mabadiliko ya serikali 1, 2 wala 3 kwa sababu mapungufu yetu hayahusiani na muundo wa serikali bali mamlaka ya serikali hizo kiutawala. Badala ya kugawakna kazi (mamlaka) muundo wa serikali 2 umekuwa ukitugawa kwa mambo yasokuwa ya muungano hivyo kila nchi kuendesha wizara zake na kuusanya mapato yake.

Labda niwape tena mifano unaohusiana na maisha yetu. Mkuu mtazamo wangu ni sawa na wewe umeoa mke, lakini mkeo ana biashara zake na wewe una biashara zako, kisha kila mtu anachukua chake na kuchangia mfuko wa familia. Hii siii haba ila tatizo linakuja kuwa wewe ndiye mwenye access na account ya pamoja, fedha za chakula unamgawia mkeo kwa mahesabu makali lakini wewe unaenda nunua suti za bei mbaya toka mfuko wa familia ukidai wewe ndiye mwenye mchango mkubwa ndani ya mfuko ule na zaidi ya hapo fedha zako huzichanganya na zile za pamoja ndio kusema kwamba mkeo akitoa Tsh 200,000 kwa mwezi wakati account ina mil. 3 wewe unahesabu kati ya Mil.3 zile mil.2.8 nyingine ni zako wewe pasipo kujua ama unafanya makusudi ukijua ya kwamba unatakiwa kutenga Tsh 200,000 zenye uuwiano na mkeo kuwa za familia na sii zako. Mkeo pato lake ni Tsh laki 3, Tsh laki2 ni ni asilimia 66.7 ya pato lake hivyo nawe ktk pato lako unatakiwa kuchangia familia asilimia 66.7 ya pato lako.

Pili, katika hizo mil.2.8 unazo dai zako kuna karibu 1.2 (asilimia 40) ulikwenda kukopa fedha benki, ukaweka rehani nyumba ya familia kama dhamana, hivyo hizo Mil 1.2 ulizopewa na benki kama mkopo, sii zako bali za familia,vizuri kushauriana na mkeo jinsi ya kuzitumia kwa faida ya familia. Na hivyo basi mkeo akitaka kununua jiko jipya, shuka mpya, vikombe na vijiko na kadhalika usimnange ukamwambia hatuna fedha maana mlisha gawana, na kudai kuwa yeye ulimpa Laki 3 ni zaidi ya laki 2 alochangia mfuko kwa sababu tu naye ile laki 1 ilobakia nayo yeye pia alikwenda kununua mkoba wa Louis Vuitton badala ya nepi za watoto.

Sijui unanipata? Kama mwananchi hapa ndipo tunatakiwa kukomelea, matumizi mabaya ya viongozi wetu na mamlaka makubwa walopewa hii inatuumiza sisi watoto wa familia hii. Na nimeweza kuyajua haya kwa kujiweka mimi ktk kundi la watoto wako hivyo ni rahisi mimi kuona pande zote mbili badala ya mimi kujitambua kama mtoto wa kiume ni jukumu langu kumtetea baba mwanamme mwenzangu.

Na ndio nikasema ya kwamba inabidi mkuu wangu ujitazame upya kwa sababu fedha zilizopo ktk mfuko wa familia sii zako japo unatazama tu mchango wa mkeo. Kwanza tazama mshahara wako kulinganisha na wake ili ujue ni asilimia ngapi ya mshahara wake hkachangia mfuko wa nyumbani yawezekana yeye katoa zaidi yako maaka mshahara wake ni Tsh laki 3 kutoa laki 2 ni asilimia kubwa kuzidi wewe mwenye mshahara wa laki 5 kisha familia inaendeshwa kwa mikopo ambayo unachukulia kama fedha ni zako uliomba wewe. Hivi kweli kuna kosa kwa mkeo kuhoji mapato na matumizi haya likawa swala la ndoa?

Haya madai ya mkeo yanapozidi yanakuwa KERO na hivyo kwa sababu unaona keor zinazidi ndio unafikia maamuzi ya kuomba kujadili tena ndoa yenu. Hapa ndipo mimi nakataa na mundo wa serikali ktk hoja nzima ya kuandika katiba mpya kuingia swala la muungano. Na inaposhauriwa kufanya ndoa iwe ya makubaliano (Prenuptial agreement) na wengine wakishauri separation ya kindoa kiasi kwamba kila mtu na fedha yake mkutane kitandani tu maana ndoa ni mapenzi na uzazi sii fedha!

Hapa ndipo napowakatatlia nyote iwe S2 au S3 kwa sababu nayaona matatizo yalipoanzia. Matatizo ni mgao wa pato lenu na haiwezekani kuendelea na muundo uliopo wala kugawana kazi na mapato yake kiasi kwamba inakuwa kila mtu atabeba mzigo wake, chake chake changu changu hii sii ndoa tena mkuu wangu bali mnakaribisha kuachana kabisa na umaskini utazidi baina yenu hapatakuwa na mshindi. Jiulize kwa nini CAG anashindwa kukagua mali za viongozi wetu? anashindwa kuhoji hata mishahara ya viongozi wetu? Posho zao na kadhalika hii ni kutokana na katiba iliyopo inawalinda na sio kuwepo kwa serikali 2.

Hivyo basi nimeyaona malalamiko ya Wazanzibar kama ya mkeo na kuyaelewa na nikajua wapi wewe kama mume ulikosea na unendelea kukosea unapotazama mahitaji yako binafsi ukasahau kwamba huyu ni mkeo. Anapopendeza yeye ndio unavyosifiwa wewe na nyumba yenu sii tu kwamba kuvaa suti kwako ndio sifa! Na ndio kikashauri kuwepo na miiko na maadili kujenga vipaumbele ktk kuijenga familia kwa mazuri na sii mavazi.

Namalizia kusema ya kwamba nimeandika mengi sana kuhusu Mchango wangu ktk uandishi wa katiba mpya na kama hadi sasa hivi hamunielewi na bado mnataka kuendelea na hizo serikali 3 Endeleeni siwakwazi wala sintoendelea kubishana juu ya hili. Alonielewa kanielewa na asiyetaka kukubaliana nami sawa vile vile kwa sababu ni haki yao kufikiri wanavyofikiria.
 
Mkuu Mkandara
Naona umeiga kona tena.
Wewe umesema unawaunga mkono CCM kwa S2 na bandiko la hapo juu ukasema kilichopo ni mapungufu wala siyo kero.

Kila unapoongelea mapungufu a.k.a kero mara zote unafumba macho na kudhani tatizo ni znz tu. Huongelei adha za Mtanganyika.

Umesema mfumo wa sasa haukutoa kipaumbele kwa znz kwa miaka 30.
Kwamba, pesa za kukopa zinatumika na Tanganyika tu.

Maswali hayo unashindwa kuyajibu au kuyatolea ufafanuzi kwasababu hujaweza, hujaweza kueleza ni vipi tunaweza kuwa na muungano wa S2 ambao mchangiaji pekee ni Tanganyika halafu tukaweza kugawana mapato, misaada na mikopo kwa uwiano sawa bila pesa hizo kuwa za Tanganyika kwa muungano wa koti.

Jibu la haraka ni kuwa muundo wa S2 hautoi jibu.
Unachoogopa kusema ni kuwa S3 itawajibisha znz ambayo wewe unadhani inapaswa kupokea tuu bila kutoa.

Mkandara na CCM na serikali yao wanaamini kwa dhati kabisa kuwa ni sawa Mtanganyika alipe kodi, achukue misaada na mikopo na nusu awape wznz kwasbabu wao ni bora
Ndiyo maana Mkandara anasema kuvunja muungano ni kugawana umasikini.

Mkandara deni la taifa la sasa la ndani na nje znz haihusiki. Vipi uongelee kupokea tu na siyo kutoa.
Matokeo yake znz wanakopa michele Kenya halafu bili wanaleta Tanzania.

Wanasajili meli zingine za kihuni wanachukua pesa, ada za shirika la kimataifa analipa Mtanganyika.
Hii free ride ndiyo Mkandara anaita Kipaumbele.

Nakuhakikishia kuwa umasikini wa Tanganyika utabaki ule ule hata muungano ukivunjika.
Hatuna umasikini wa kugawana na znz kwasababu hadi sasa sisi ni masikini tunawowalea znz kwa kodi zetu.

Hatuwezi kukubali kubeba zigo la samadi na kupe huku wakiendelea kupiga kelele kila siku tena zisizo na maana ili mradi tu wafungue vniywa.Hatuna umasikini wa kugawana na znz, Tanganyika ni taifa kubwa mbele ya znz.period.

Maelezo yako kama ya wana CCM wengine hawajibu hoja ya kwavipi tuvue koti.
Unachotaka kusema ni tuwape znz kipaumbele na si Tanga au Mtwara wanachongaia kodi na pato la taifa.

Tuwape kipaumbele kwa mchango gani?
Kwamba, walale na wake zao wakitumia umeme wa bure mkulima wa Mtimbira alipe kodi ya kuwapa kipaumbele!
tafadhali bwana.

Kama znz wanadhani wanaonewa, hakuna sababu ya wao kuendelea na uonevu. Njia nyeupee waondoke.

Huu muungano ni kwa ajili yao si yetu na wala hatuwahitaji.
Muda wa miaka 50 kupigizana kelele na watu hawa unatupotezea muda.

Hatutaki kunyonya ndama asiye na kiwele. Tunyonye znz kwa kitu gani hasa, Uchumi wake ni mdogo kuliko asilimia 90 ya wilaya za Tanganyika. Kwanini tusiende kwenye nundu tukae tunakamua ng'ombe asiye na kiwele.

Mkuu bado hujajibu swali la Tuko. Unakwepa sana kwa utetezi wa znz.

Ukweli ni kuwa znz ni kupe ambao sasa ni tatizo kwa ng'ombe. Ni ima wang'olewe au wakae mgongoni kwa adabu. Tumechoka kutumia muda wetu kujadili watui laki 5 na siyo milioni 41.
 

Thread za kisayansi kama hizi mimi huwa nachagua kuwa msomaji tu.
 
Last edited by a moderator:
Nionyeshe mahala nilipoandika kwamba mimi Mkandara nawaunga mkono CCM na S2. Mkuu vipi lakini uko sawa kweli au ushabiki huu unakuipelekesha!

Lakini sitoshangaa maana kila hoja yako nikiisoma unakwenda pengine kabisaaa kwa sababu huelewi huo mfumo hufanya kazi gani na kwa minajiri gani. Ndio maana hunielewi na hutanielewa kutokana na ushabiki kama washabiki wa mpira ambao hawajui kuucheza hata danadana lakini maneno mengi sana na kila siku kulaumu na kulaani upande wa pili kama vile mpira huchezwa na timu moja pasipo ushindani. Madam mtu hakubaliani na S3 basi ni lazima awe anawaunga mkono CCM.

1. Sikubaliani na mabadiliko yoyote ndani ya Muungano iwe ya Muundo wa serikali ama muungano wenyewe kwa sababu kazi tulowatuma wajumbe hao ni kuandika katiba mpya ya JMT. na hakuna sababu wala hawawezi kufanya mabadiliko ya Muungano wenyewe ili kupata katiba mpya.

Ukifanya hivyo unaharibu taratibu zote za uandishi wa katiba mpya kwa sababu ni lazima izaliwe Tanganyika kwanza yenye serikali, bunge na Mahakama zake (uchaguzi mpya wa wawakilishi wa Tanganyika) hii itachukua miaka zaidi ya mmojaa na baada ya hapo ndipo wawakilishi wa serikali zoye 2 (Tanganyika na Zanzibar) wakutane na kujadili muungano ifikie maafikiano na kisha ndio tuipate katiba ya JMT. Hivyo kinachofanyika hapo Dodoma ni Uhuni na Uhaini wa kalamu kwa sababu hawa wajumbe walochaguliwa kutunga katiba mpya ya JMT hawana dhamana ya mtu yeyote wala wananchi kujadili wala kutunga Muundo wa muungano wa nchi yetu - HAWANA.

2. Matatizo tulokuwa nayo hayahusiani na muundo wa Muungano kama ingekuwa hivyo tungeujadili Muungano wenyewe kwanza kabla ya utunzi wa Katiba ya JMT.

Matatizo yaliyopo yanatokana na MFUMO wa UTAWALA ambao bado ni wa KIJAMAA japo tupo ktk Demokrasia ya vyama vingi na Uchumi wa soko huria. Kuna mazuri ya Ujamaa tuliyaacha na kuna mabaya ya Ubepari tuloyachukua kwa mfano leo hii tuna Waheshimiwa sii viongozi. Matumizi ya nenio hili WAHESHIMIWA tayari linawafanya wananchi wajenge nidhamu ya woga na kutokuwa sauti kama waajiri. Kuondolewaa kwa miiko na maadili kwa viongozi na kikubwa zaidi Central Government kusimamia shughuli zote za uchumi wa nchi.

N:B Mkuu hayo mengine twende Taratibu maana unachanganya mambo 100 kwa wakati mmoja. Umesoma wapi kwamba deni la TAIFA haliwahusu Zanzibar? keshi utakuja sema hata Benki Kuu ni ya Bara haiwahusu Zanzibar! halafu wao wakiuliza mnakuwa wepesi wa kutangaza talaka. Wenyewe mnasema hakuna nchi Tanganyika na ndio mnayoidai hivo huwezi kusema deni la Taifa ni deni la Tanganyika wakati haipo na deni lenyewe linaihusu seriikali ya JMT na rais wake. Mkiambiwa mnavaa koti la Muungano mnachukia sasa haya madudu uloandika yana maana gani kama sii kuvaa koti?

Yaonyesha wazi kwanza hamuufahamu kabisa muundo wa S2 kama msivyofahamu Uislaam hivyo kila mnachoandika ni vichekesho tu kama vile Mkristu akitaka hukumu ndoa ya Kiislaam (Na swala la mahakama ya Kadhi) kwa sababu mnataka waislaam nao wawe na mfumo kama wa Wakristu! Kwa upande mwingine mimi napingana na Mahakama ya kadhi kwa sababu naufahamu Uislaam!
 
Inawezakana kabisa hatufahamu na kwa vile unafahamu muundo wa S2 tunaomba utusaidie kidogo pengine tutabadili mawazo.

1. Kuna S2 za nchi gani?
Je JMT na ZNZ zinaweza kutengeneza serikali 2? Hii JMT ni serikali inayowakilisha nchi gani?

2. Mkataba unasema ni muungano wa Tanganyika na znz, vipi leo Mkandara utuambie ni JMT na SMZ?

3. S2 zina Mamir jeshi wakuu 2, wa JMT na SMZ. Yupi ni mkubwa kati yao?

4. Rais wa JMT akiwa znz ana mamlaka gani?

5. Waziri mkuu wa Tanzania wigo wake wa madaraka kwanini unaishia bara na hauvuki bahari?

6. Deni la znz nje linaitwaje, kama ni la Tanzania kwanini znz iwe ni nchi kamili?
Wataliapaje deni wakiwa nchi ya jirani?

Kwa muundo wa S2 unaoutetea katika nukuu hapo hapo juu
1. Tanganyika itajivuaje koti ili iwe na mambo yasiyo ya muungano?
2. Tutashughulikiaje kero za znz kuhusu mamlaka kamili ya kukopa na misaada ikiwa ni sehemu ya Tanzania
3. Nani anasimamia masilahi ya mshirika wa muungano ikiwa Tanganyika ndiyo Tanzania

Miaka 50
1. Ni kwanini kero zinaongezeka na si kupungua?
2. Ni kipi kipya kitakachofanyika kilichoshindikana huko nyuma?

Kuvunjika muungano
1. Nini madhara yake kwa Tanganyika

Gharama za muungano
1. Kwanini znz haichangii na nani wa kuiwajibisha kama znz ndiyo Tanzania
2. Kamati ya kushughulikia kero ilimshirikisha Gahribu Bilal, Seif Idd na Samia Suluhu,. hawa ni wznz.
Nani amewakilisha upande wa pili wa muungano?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…