Wafugaji mje huku mtupe visa vya visirani vya mbuzi wa kienyeji
Nakumbuka vituko vyao vingi sana maana tuliwahi kuwa nao tulipokuwa kijijin wakati huo nikiwa mdogo
Mbuzi ni kama binadamu ambavyo wapo wenye tabia mbali mbali na mbuzi ni hvyo hvyo kuna vimalaya humo kwenye kundi la mbuzi,kuna wezi,kuna wambeya,pia kuna vihele hele
Mbuzi anatakiwa achungwe na watoto maana mtu mzima hzo jogging hutaziweza
Mbuzi vihele hele,nakumbuka tulikuwa na mbuzi wengi lakin ukichelewa kuwapeleka machungani kuna wale mbuzi wachache katika kundi watalia na kupiga kelele ili wazazi wawasikie ili wawaambie muwapeleke machungani
Mbuzi malaya,kuna vile vidume vidogo huwa vinatabia ya kupiga kelele ya kupanda jike usiku kucha na wakati hata vikipewa mbususu haviwezi kuifikia,pia wapo majike ambao wao kila mara utakuwa unawaona wanayapanda madume(ila baada ya kupata elimu niligundua kumbe huwa wanakuwa kwenye heat)
Mbuzi wezi,hawa huwa ni wajanja wajanja sana muda wote hawawazi kula nyasi wanataka kula vya kuiba mashambani,huwa na tabia ya kuwapiga pembe wenzao kama wakiwa karibu na mazao ili wakimbilie kwenye mazao,kipindi hicho nakumbuka tulikuwa tusipofunga vizur mlango wa banda basi usiku wanatoka,tulikuwa tukiwakamata tunawapanda kama farasi,na unapompanda inabid kuwa makin sana maana anakimbia sana na anakuwa na tabia ya kupita karibu na visiki au ukuta ili ujipige pale uumie,
bAada ya kuwajulia wakati wa kwenda kuwachunga ili wasisumbue sana tulikuwa tunaenda na kamba,wale wasumbufu tunawatia kamba
Nakumbuka nilkuwa nikiwapeleka machungani lazima nipoteze mbuzi,inabid niwarudishe nyumban ili nikamsake huyo/hao waliopotea
Katika story za wana jamaa mmoja aliwah niambia kuwa wao walikuwa wanawang'oa meno baadhi ya mbuzi wasumbufu,wakiwapeleka kunywa maji wanaanza kumshika mmoja mmoja wanamgonga na jiwe mpaka jino linatoka au wanamkamata wanamzamisha kichwa kwenye maji kwa muda ndo wanamtoa,hao waliokuwa wanatolewa meno itamchukua siku hata tatu atakuwa ametulia sana na hali majani sana kama siku zingine
TUlikuwa tusipowapatia maji ya kutosha,ile jioni wakati wa kuwarudisha walikuwa wakifika nyumban wanakuwa na fujo balaa watalazimisha mpaka waingie ndani,na wataangusha viti na kumwaga maji
Mbuzi sina hamu nao,nimechapwa sana enzi hzo kwasababu ya hawa wapuuzi pamoja na kwamba mimi nilikuwa mtoto mpole sana
wAlinifanya hata nisipate muda wa kucheza mpira hadi leo nikiambiwa nipige mpira naanguka tu mwenyewe