Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Unajua hivi viumbe vinaakili kinoma,itakuwa vinakuona huyu fala atatuambia nn,zimepita pasaka 4 mjini Bado tupo.
Fanya hivi:akikata kamba akikimbia we mkimbize kimya kimya ukimshika muonyesheee bisu a.k.a mkameme huku umekunja uso huku unamwambia sio mda utamla kisusio,hata rudia upuuzi wake.
 
Wanapenda mazao ya watu utasema wanajua kulima. Niliwahi kumpiga mmoja ñusura nimuue baada ya kuwaongoza wenzake kula mazao nikapigwa halafu ile nimekaa nasikilizia maumivu kakaja kakanipigia chafya usoni
Ukiona mpaka mbuzi anakupigia chafya usoni ujue kwenye hii dunia wewe ni looser tu. Sisi wenyeji wa Iringa ni kuanza kufanya urafiki na kamba tu.
 
Bwana babu alikuwa na mazoea ya kuwatukana mbuzi
Kutokana na kero zao
Siku beberu likamvizia anakusanya majani awape mbuzi wengine
Babu wa watu kainama
Sie tupo jiko la nje na mahindi yetu ya kuchoma tunausoma mchezo
Hatukumshtua maaan alikuwa anatupa kipigo baada ya kuwapa pilipili kwa kelele zao
Beberu karudi nyuma hatua kadhaa kama kawaida yao wanapo taka ku attack
Huyo Mbio kampa babu kichwa cha makalio babu biduuu miguu juu na majan yake
Huku sisi tumeziba midomo kwa vicheko ikatokea mmoja kaangua kicheko kwa nguvu wewe lilirushwa panga wote tulisambaratika
Tunasikia tu kmnna zenu nisiwaone hapa kwangu mwuishie huko kwa wazaz wenu tulikaa wiki hatukukanyaga kwake
 
Mi nakumbuka Kuna wakati mbuzi mmoja wa dingi yangu alinizingua nikamkamata nikamfunga vizuri nikacharaza mafimbo mpaka akafa.

Hawa viumbe wadogo kuanzia mbuzi,kondoo na nguruwe Ni miyeyusho Sana.
 
Kuna siku nlikanyagaga kba ya mbuzi alifungwa njiani wee akajivuta bana we ilikuwa kiliman nlijikuta npo chini asee na kidonda juu mbuzi n nyoko asee kweli wana visiran
 
Duh! Leo ndo nimeelewa, kipindi nakua kulikuwa na mzee anafuga mbuzi aisee akili zake zilikuwa za kikwake kwake tu manake yale mambuzi yalikuwa yanamsumbua mara yakimbilie milimani kulala huko, kesi mtaani kila kukicha.

Ninapenda sana ufugaji lakini sikuwahi kuwaza kufuga hawa viumbe baada ya kuona zile taabu alizokuwa akizipata yule mzee.
 
Kuna bibi alikua jirani yetu anambuzi wake kama 6 au nane hivi basi huko bandani anawapiga anawatukana kuna siku beberu likampuha kichwa Alipiga ukunga akasema lichinjwe litamuua 😂😂😂😂😂😂 nilicheka sana maana alibananishwa bandani akapewa dozi 😂😂😂 ikawa mwisho wa beberu yule
 
Back
Top Bottom