Ukitaka kuwatesa warembo wakali wa mjini, wakutafute kwa udi na uvumba, fanya hivi wewe mwanaume

Ukitaka kuwatesa warembo wakali wa mjini, wakutafute kwa udi na uvumba, fanya hivi wewe mwanaume

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
  • Hakikisha ngozi yako inanukia pesa (imenawiri, na vinyweleo vimesimama na kutoa jasho)​
  • Mwili wako unukie vizuri, sio ile harufu kali ya kutisha​
  • Uwe na biashara yako/ofisi yako inayoeleweka.​
  • Uwe ni mtu wa kuongea maneno machache ila vitendo viwe vingi​
  • Usiwe mtu wa makundi, ishi mwenyewe mwenyewe, mfano ukienda sehemu, nenda mwenyewe.​
  • Uwe ni mtu wa kusaidia wahitaji kwa wanaohitaji msaada wako.​
  • Ukiwa na gari kubwa kama land cruiser hivi, itapendeza zaidi​
  • Piga viatu vya ngozi rangi nyeusi, ikiwa travolta itakuwa powa zaidi.​
  • Vaa suruali ya jinsi ya kijani na shati jeupe linaloonyesha vest uliovaa ndani. Kama utakosa jinsi ya kijani, unaweza kuvaa zilizopo.​
  • Ndevu ziwe fupi za kuchana na brashi, ikiwezekana uzitoe kabisa; usifuge mzuzu kama beberu.​
  • Kichwani unaweza kunyoa kipara, au staili ya box​
  • Kichwani, paka mafuta yatakayoonyesha mpaka shina la nywele, ngozi ya kichwa ing'ae.​
  • Usihonge mwanamke yeyote, waache wao wakuhonge kwa sababu watakuwa wanakutafuta kama utitiri kwenye nyumba za ibada, waganga n.k​
  • Achana na wanawake wanao omba omba hela.​
  • Baada ya hapo, kula maisha kama mwanaume halisi anavyotakiwa kuishi.​
 
images (16).jpeg
 
Naona suruali za kijani wewe mwana ccm Ebu acha upumbafu basi bwana mkubwa😅(jokes)
Unajua mkuu, hizi jinsi za kijani kitambaa kigumu ni vigumu sana kuzipata kwa sasa, ukionekana umeivaa unaweza kujikuta uko mwenyewe tu
 
Back
Top Bottom