Ukizaa na mume wa mtu, jukumu la kulea mtoto ni lako mwenyewe!

Ukizaa na mume wa mtu, jukumu la kulea mtoto ni lako mwenyewe!

Kuna Watu watasema nawachukia ninyi kinadada.😂
Wanafikiri ninaishi bila Mama, shangazi, Dada au mke🤣🤣

Yaani mtu ukanisukumize kwa mume wa mtu mwenye mkataba wake halafu utake akupe nafasi ya mke na watoto kama mume wako!?
Ni sawa na kuiba Mali ya mtu halafu uende kuwaomba police wailinde ili mwenyewe asiichukue😅😅
 
Yaani sop itabidi, Jambo Hilo lipo automatically.
Hata iwekwe sheria ipi, Jambo Hilo lipo hivyohivyo.

Ni vizuri Tuwafundishe mabinti zetu maadili maana wao ndio wahanga wakubwa.
Hatuwezi kujidanganya kisa tumetunga visheria ndio tukadhani madhara yatokanayo na mmomonyoko wa maidili yatawakuta kijana na Binti Kwa kiwango sawa
Mimi huwa naamini wanaume wengi akikataa kulea au kuhudumia ujue behind ze sini kuna kitu tu.

Ila yote kwa yote endelea kuhubiri brother wenye wana masikio watajifunza .
 
Yaani mtu ukanisukumize kwa mume wa mtu mwenye mkataba wake halafu utake akupe nafasi ya mke na watoto kama mume wako!?
Ni sawa na kuiba Mali ya mtu halafu uende kuwaomba police wailinde ili mwenyewe asiichukue😅😅

Watu wajifunze kwenye kisa cha Ibrahim, Sarah na Hajiri.
Hapo watajua jinsi wanaojenga mataifa makubwa jinsi wanavyofanya mambo Yao.
Pale ilikuwa aidha Ibrahimu akatae ili Sarah avunje ndoa Jambo ambalo Ibrahim asingekubali, au amkubalie Sarah ili mipango iende kama ilivyoenda.
 
Mimi nawashtua Kwa sababu nawapenda.
Ila wao wenyewe wataona ninachuki nao Kwa kuwaambia ukweli.

Sifurahii ongezeko la single mother kwani sio tuu linawatesa Dada zetu Bali pia linaumiza Watoto.

Watoto wanakua pasipo ulinzi na upendo wa Baba
Wanawake hawashauriki hawa viumbe wengi wao wamejaa tamaa hawako tayari kumvumilia mwanaume ambae bado anajitafuta wao wanapenda shortcut apate mwanaume mwenye mali bila kujua zimetoka wapi
 
Wanawake hawashauriki hawa viumbe wengi wao wamejaa tamaa hawako tayari kumvumilia mwanaume ambae bado anajitafuta wao wanapenda shortcut apate mwanaume mwenye mali bila kujua zimetoka wapi

😀😀😀
Acha mambo yakae vivihivi tuone mwisho wake na mwisho wetu utakavyokuwa
 
°kama DNA test zinakuonyesha ni ww utawajibika
° Hakuna Sheria iliyosema mwanaume akizaa na nje ya Ndoa asitunze huyo Mtoto wa nje ya Ndoa, kama hiyo sheria ipo itaje na utaje kifungu hicho.
Waache kugawa gawa bila mpango kwani alikwambia anahitaji mtoto? Kujidhalilisha tu kudai matunzo wapambane na hali zao
 
Ulichosema ni ukweli mtupu,,japobaadhi hawataelewa. Kwenye suala zima la kuzaa mwanamke ndio mwenye maamuzi.
Ukienda Ustawi wa Jamii kesi nyingi za matunzo ni za wanawake nyumba ndogo. Mapenzi yakiisha basi mwanaume haangaiki na kulea mtoto. Na wengi wanaingia kwa madai kuwa wanapendwa.Na wanawake wengi wanajua kuzaa ndio garantee yabkupata fedha au ndoa kwa mwanaume kiti ambacho wala hakina ukweli kwani mwanaume akikupenda hata kama huna kizazi ata stiki na wewe.

Wanawake wengi wanakuwa wahanga sababu ya kujipa upofu wa maneno mazuri wanayopewa wakati mapenzi yapo moto moto. Wanawake wenyewe ndo tunaweza kujikomboa katika hili. Tufanye maamuzi ya kuzaa kwa sababu tunahifaji lkn sio kwa sababi ya tamaa,, fedha au ndoa kutoka kwa mwanaume.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukizaa na mume wa mtu wewe ni mkwepa majukumu kama walivyo wakwepa majukumu wengine. Umekwepa jukumu la kuanzisha maisha ya malezi na kijana mwenzio kwa kukimbilia mtu ambaye ameshajiestablish na mtu mwingine tayari, maana yake unaenda kumega kipande cha cake cha familia nyingine wakati ungeweza kuanza ku bake ya kwako uile nzima. Huu ni ukwepaji wa majukumu.

Hata hivyo hawa wazinzi wawili wakishafanikiwa kupata tokeo la walichokifanya busara itumike ili mtoto alelewe tena kama uwezo upo alelewe vizuri, Baba ahakikishe anatengeneza extra income kwa ajili ya mtoto aliyeongezeka, kinyume na hapo mtamuathiri mtoto kisaikolojia sababu ya ujinga wenu.

Imagine mtoto alinayekua kwa kushuhudia mama yake anapelekana ustawi wa jamii na baba yake juu ya malezi yake, no wonders tuna vijana wa hovyo wa kike na kiume kwa sasa, matokeo ya malezi waliyopokea.
 
Haya mambo acha tu,
Mzazi mkanye mwanao asiingie Katu kwenye mahusiano na mme wa mtu.

Ikishatokea mnajikuta mnachukiana tu, mwanaume ukijitahidi kutaka kumjali mtoto pesa zinapotea,hazionekani.

Unabaki kulaumiwa bure na kujilaumu kutelekeza mtoto!!
Nahisi asili inakuwa inawaadhibu bila kufahamu.
 
Ulichosema ni ukweli mtupu,,japobaadhi hawataelewa. Kwenye suala zima la kuzaa mwanamke ndio mwenye maamuzi.
Ukienda Ustawi wa Jamii kesi nyingi za matunzo ni za wanawake nyumba ndogo. Mapenzi yakiisha basi mwanaume haangaiki na kulea mtoto. Na wengi wanaingia kwa madai kuwa wanapendwa.Na wanawake wengi wanajua kuzaa ndio garantee yabkupata fedha au ndoa kwa mwanaume kiti ambacho wala hakina ukweli kwani mwanaume akikupenda hata kama huna kizazi ata stiki na wewe.

Wanawake wengi wanakuwa wahanga sababu ya kujipa upofu wa maneno mazuri wanayopewa wakati mapenzi yapo moto moto. Wanawake wenyewe ndo tunaweza kujikomboa katika hili. Tufanye maamuzi ya kuzaa kwa sababu tunahifaji lkn sio kwa sababi ya tamaa,, fedha au ndoa kutoka kwa mwanaume.



Sent using Jamii Forums mobile app

Nikisema kuna Watu wanasema ninachuki.
Wakati Mimi natoa way-foward ya kuondokana na matatizo hayo.

Wewe ushajua mwanaume kaoa, alafu anakutongoza huoni kama anakuchezea Akili, amekuona hamnazo.
Sawa basi mwambie akuoe hata kama anamke mwingine, najua hili wanaume wengi tutapiga Chenga Kwa sababu tunajua tamaa zetu ndio zimetufanya tutongoze.

Lakini unang'ang'ania ananipenda ndio maana ananipa Pesa😀😀 au amekupangishia nyumba, hayo ni mapenzi ya awali, Baada ya miaka mitano ndio utajua ukweli ni you.
Sasa kuliko kusubiri hiyo miaka mitano ni Bora umdhibiti mwanaume Kwa kumuambia nenda kwetu ukajitokeze unioe ili uwe na Haki zote juu yangu na watoto watakaozaliwa.
Hutaki.

Haya Kabla hujaingia kwenye Ndoa za Watu, jiulize wewe ndio ungekuwa umeolewa alafu akatokea Mwanamke mwingine anataka kudokoa mume wako ungejisikia na kumfanyaje huyo Mwanamke?

Elewa kabisa, MKE hawezi mpenda mtoto wako Kwa sababu huyo mtoto Mama yake ni mwizi wa mume wa wenyewe. Na hapo ndio inatokea Ile ya Mama wakambo wabaya.
Bora Watoto waliokutwa Kabla ya ndoa kuliko wanaozaliwa nje Baada ya ndoa
 
Ukizaa na mume wa mtu wewe ni mkwepa majukumu kama walivyo wakwepa majukumu wengine. Umekwepa jukumu la kuanzisha maisha ya malezi na kijana mwenzio kwa kukimbilia mtu ambaye ameshajiestablish na mtu mwingine tayari, maana yake unaenda kumega kipande cha cake cha familia nyingine wakati ungeweza kuanza ku bake ya kwako uile nzima. Huu ni ukwepaji wa majukumu.

Hata hivyo hawa wazinzi wawili wakishafanikiwa kupata tokeo la walichokifanya busara itumike ili mtoto alelewe tena kama uwezo upo alelewe vizuri, Baba ahakikishe anatengeneza extra income kwa ajili ya mtoto aliyeongezeka, kinyume na hapo mtamuathiri mtoto kisaikolojia sababu ya ujinga wenu.

Imagine mtoto alinayekua kwa kushuhudia mama yake anapelekana ustawi wa jamii na baba yake juu ya malezi yake, no wonders tuna vijana wa hovyo wa kike na kiume kwa sasa, matokeo ya malezi waliyopokea.

Tatizo la ukifanya Makosa kulipia ni lazima Kwa namna moja ama nyingine.
Mtoto kivyovyote lazima aathirike kwani hatalelewa na Mama na Baba yake OG. Hiyo tosha ni hasara kubwa.

Umesema kweli.
Baadhi ya Wanawake hasa WA mjini siku hizi wamejikuta destroyers Kwa kuvamia Maisha ya familia za Watu.
Tena Wakati mwingine unakuta mwanaume hata hakuwa na time na huyo bibie Ila bibie akatumia nguvu aidha ya mwili au nguvu ya ziada kumshawishi Mwanaume Kwa lengo la kujipatia kipato au kutengeneza mfereji mdogo wa Ulaji.

Watu wa hivi lazima wagharamike wao na watoto wao.

Kusema busara itumike ni kuruhusu ongezeko kubwa zaidi la Watu wenye Tabia hizo kufanya uharamia huo.
Dawa ni kufanya mambo yawe magumu ili kutoa fundisho Kwa ambao wanataka kujaribu.

Huruma na busara inatakiwa kutumika Kabla tukio halijatokea, lakini kama limetokea madhara hayataepukika.
 
Haya mambo acha tu,
Mzazi mkanye mwanao asiingie Katu kwenye mahusiano na mme wa mtu.

Ikishatokea mnajikuta mnachukiana tu, mwanaume ukijitahidi kutaka kumjali mtoto pesa zinapotea,hazionekani.

Unabaki kulaumiwa bure na kujilaumu kutelekeza mtoto!!
Nahisi asili inakuwa inawaadhibu bila kufahamu.

Hapo ni Bora mtoto aje kuishi ndani ya familia.
Lakini Hilo Wanawake wengi wanalipinga Kwa kisingizio cha Mama wakambo
 
Ukweli siku zote huwa unakua mchungu. Na ukweli siku zote huwa unauma. Wenye kuelewa wataelewa na wasiotaka kuelewa ipo siku wataelewa.

Mi mwenyewe ni mwanamke na ni mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake lkn sisi wenyewe hatujui tunachotaka na hatupendani na ndo maana tunakuwa wahanga wa kila kitu.

Wanawake tunapaswa kusimama kwenye ndoto zetu. Ishawahi kutokea kesi moja mke mdogo ameenda kumshtaki mke mkubwa eti amemnyima urithi mtoto wake.

Huyo baba alikuwa na familia yake na alikuwa na mali nyingi tu alizochuma na mke wake ikiwemo mifugo. Alipata nyumba ndogo akazaa naye baada ya miaka 3 yule baba akafariki akaacha mtoto wa bi mdogo akiwa na miaka. Sasa yule mama amabye ni mke mdogo akaanza kudai haki eti bi mkubwa ampe urithi wa mtoto wake maana yule bwana kaacha mali nyingi. Nikasema wanawake ki ukweli tumrogwa. Nikamuuliza ulikuwa hujui kama alikuwa na mke nilikua najua ,,eeeh mara oooh alikuwa anagombana na mke wake. Eeeh kisha sasa wakati upo na huyo bwana alishakupa hata ngo'mbe hapo wawili ufuge tu kwa ajili ya watoto wako,,,jibu hapana. Haya umesema anamaeneo mengi je alishawahi kukupa hata kajieneo tu kwa ajili ya mtoto wako hapana. Sasa leo hii yule bi mkubwa akupe wewe urithi kama nani? kama huyo bwana tu uliyesema anakupenda alishindwa kukupa? Nikamwambia tu nenda kajifikirie ungekuwa ndo wewe upo kwenye nafasi ya yule bi mkubwa ungechukua maamuzi gani? Huyo akaondoka zake

Ni visa vingi ambavyo ki ukweli ambavyo nikisema humu sidhani kama kuna watu watatetea. Ki ukweli wanawake tunafeli sana tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa Robert Heriel
... na hao mashoga mnawakaribisha kupiga umbea nyumbani ni hatari sana kwa ndoa zenu! Unakuta lishankupe na dera lake ndani liko tupu unalileta nyumbani Jpili kupiga stori; hatari sana.
 
Back
Top Bottom