Uko tayari? Dar es Salaam mpya inakuja. Serikali kutwaa eneo la mita za mraba 233,000. Maeneo ya Sinza, jirani na Mlimani City, Boko, SIMU2000 kuguswa

Niambie no apartment ipi ya mtu binafsi ( ghorofa ) Ambayo Haina watu Dar ?
 
Nimekubali kuwa similiki chochote kwa asimilia mia. Eneo likiwa na madini ama likihitajika tu na wenye mamlaka unapisha tu. Sijui kama tathmini ya fidia itahusu mpaka hisia za wamiliki. Ewe banda langu nilikupenda sana lakini sirikali imekupenda zaidi,jiandae kupumzika kwa amani
 
Kwa manufaa ya Umma, inamaana kunufaisha wengi zaidi kuliko mmoja pekee
 
Tumechelewa sana kufanya master plan hasa kwenye majiji,
Na wanapaswa kwenda kupanga mapema mji unakoelekea na sio tena katikati ya miji
 

Hii inawezekana na ni kitu kizuri. Nina shaka na watu waliopo kama wana uwezo wa kuibeba vision kama hii mpaka ikafanikiwa, bila kuleta hadithi za mambo yasiojulikana
 
Simple? Hizo trillion of money za kulipa fidia na kuanza kujenga upya zinatoka kwa nani?
Hapo kwa individual hawezi kufanya huo uwekezaji ila inakuwa ni kampuni ya commercial real estate wanaweza kufanya hivo gradually sio kwa mkupuo.

Unajua pale buguruni nyumba hazijajengwa kwa ustaarabu sasa mfano ukinunua nyumba za chini kama 10 kwa hata milioni 300 kwasababu zile nyumba ni choka mbaya, hapo unaweza pata eneo kubwa ukapandisha apartment za kwenda juu za ghorofa 10 ambapo hapo unaweza kupata apartment za kutosha hata zaidi ya 50
 
Naona kunaangaliwa sehemu kwenye fursa za kibiashara zaidi.
 
Mitazamo inatofautiana, wengine wanabiashara zao zinawalipa kununuliwa ni pigo kubwa
 
Karakana ni sehemu ya Dar mpya, kwa nini unakuwa mgumu wa kuelewa? Kunguni mna shida sana
Huo ni mradi wa BRT inshu za sijui dar mpya mara wanapanga upya si wangechukua manzese, vingunguti au buguruni?
Mita za mraba 233,000 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa BRT unaofanywa na DART zinajumuisha maeneo yafuatayo:-
1. Makutano ya barabara ya Bagamoyo na Kunduchi (Mbuyuni) ni sqm 156,000 kwa ajili ya ujenzi wa Karakana kuu.
2. Eneo la Halmashauri ya Ubungo lililopo Simu 2000 sqm 35,000 kwa ajili ya ujenzi wa Karakarana kuu.
3. Bokobasiaya sqm 18,000 kwa ajili ya ujenzi wa kituo mrishi na maegesho ya magari.
4. Makutano ya barabara ya Sam Mujoma na Chuo Kikuu cha Ardhi mkabala na Mlimani City sqm 24,000 kwa ajili ya ujenzi wa kituo mrishi na maegesho ya magari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…