Ukoo wetu wote ni masikini. Naombeni ushauri Nawezaje kukata huu mnyororo wa umaskini?

Ukoo wetu wote ni masikini. Naombeni ushauri Nawezaje kukata huu mnyororo wa umaskini?

Kumcha Mungu Ni dawa kubwa Sana, hasa ukiwa na Imani thabiti, ondoa unafiki ktk kumcha Mungu, mf. Ukiwa peke yako gizani ona km Mungu anakuona
Kumjua Mungu si rahisi mtu utasikia mimi namjua Mungu sana hakuna akili ya kibinadamu hata mtu asome theolojia digrii zote duniani aweza kumjua Mungu ni kuomba tu Mungu atusaidie kumjua sababu akili zake hazichunguziki
Hebu fikiria wakati dunia ilijaa Dhambi kila kona Biblia Inasema Mungu akamtuma Yesu aje kwa ajili ya wenye dhambi sio watakatifu wawe kanisa takatifu pekee la mitume katoliki au walokole Pentecoste!!

Naungana na Mtume Paulo alienda kwa wagiriki wakamwalika kuhubiri .Jengo lao waliandika kwa Mungu asiyejulikana!! Akawasifu kuwa walionyesha wako vizuri.
Kumjua Mungu hata mimi kila siku naomba tu anisaidie kumjua zaidi naimba sana wimbo wa kitabu cha nyimbo cha KKKT cha Mwmbieni Bwana unaosema Nataka nimjue Yesu nizidi kumfahamu...huwa nauimba kwa kumaanisha sababu kwa akili zangu sidhani kama naweza mjua Mungu au Yesu au Roho Roho Mtakatifu akili yangu finyu na ya kila binadamu finyu inahitaji neema tu ya Mungu kumjua kwa sehemu ndogo
Hata Eliya Alitaka kumjua Mungu aliishia tu kamuona kasehemu kadogo sijui. mgongoni

Ayubu alihoji kitabu cha Ayubu akaulizwa utanijuaje wakati hukuwepo nilipoumba mbingu na nchi?

Sidhani kama kuna yeyote aweza kumjua Mungu kikamilifu na kumpendeza Mia kwa Mia tuombeane
Yesu pekee ndie sauti ilitoka mbinguni kusema huyu ndie mwanangu mpendwa ninayependezwa Naye!!

Tuliobaki duniani ukiwemo wewe sauti hiyo haijawahi kuja kusema huyu mwenye ID ya Twende Wote wa jamii forums ndie mwanangu mpendwa ninayependezwa naye unajigesabia haki mwenyewe !!!
 
Toa kile kitu ulichonacho chenye faida kwa wengine uanze kupata pesa.

Kama una kipaji basi tumia kipaji chako. Kama una nguvu za kazi basi tumia nguvu zako. Kama unajuana na yeyote anaeweza kukuinua kidogo ulipo basi tumia mtu huyu.

Nashauri zaidi iwapo unaweza kwenda mbali na ulipo ili kuminimize mizigo basi fanya hivyo. Itasaidia kukujenga mpaka pale utapokuwa tayari kusaidia watu kwa uwazi.

Baba yangu ni mtoto wa kiume wa kwanza katika familia ya kimasikini sana. Kimasikini as in mboga ni moja tu maharage na msosi ni ugali. Nyumba ya udongo, mazingira ya kijijini na hali mbovu haswa. Nilienda kuona sehemu aliyozaliwa na kukulia na kwakweli kama ni kutoboa ametoboa haswahaswa.

Kwa bahati nzuri babu alikuwa anasisitiza sana elimu kwake. Alihangaika na uwindaji, uchimbaji madini na kilimo ili chochote kinachopatikana kiende katika elimu yake. Hivyo akafanikiwa kwenda shule mpaka kumaliza chuo kikuu.

Harakati za baba kuinua ukoo wake alizianza toka akiwa chuo. Alifanikiwa kupata boom na boom yake ndio ilimsomesha mdogo wake wa kiume anaemfuata sekondari. Baada ya kumaliza chuo na kupata kibarua ada ya kumsomesha mdogo wao mwingine wa tatu ndio ikapatikana. Kwa kuwa ada ndio ilikuwa inapatikana kimachale machale baba mdogo zangu wamechelewa sana kumaliza chuo wakiwa baada ya 25 years of age.

Kutokana na bidii yao na kusema ukweli bahati ya kupata ajira nao wakaanza kusomesha watoto wa ndugu zao ikiwemo dada zao ambao hawakwenda shule as a sacrifice to them. Leo hii watoto hao wa mashangazi wengi wamemaliza au wanamaliza elimu zao na wengine wana ajira tayari zinazowawezesha kutunza familia zao.

Kutokana na haya ukoo wetu umeweza kuhamia kutoka kijijini na kuishi mjini kwenye makazi bora na matunzo bora. Hili nalishukuru sana kwani limetuwezesha hata sisi watoto kuwa na base nzuri kwa ajili ya maisha yetu.

Hii historia nimeweka hapa kuonesha kuwa inawezekana kuvunja minyororo ya umasikini. Inaweza kuchukua muda ila bidii na uchapakazi vitakuwezesha bila neno
 
Nakushauri kama ni kjijini kwenu mawili either ubuni kitu kitaleta tija na uhitaji mkubwa mfano mm rafiki yangu alikuwa ivyo ivyo alivymaliza chuo alikuwa kabana kama mil 2 na kitu karudi kijini kwao akapiga mishe mwaka sijui nyingine pesa katoa wapi akaniambia ana kama 5 mil na kitu kiutani utani kaja kugundua pale kijini kwao watu hawana mashine ya kusagia na kukoblea wanaenda mbali basi kanunua mashine anapiga hela ana pikipiki za tairi tatu mbili zakuchukua mazao shambani

pili ukiona hamna ishu nenda mbali kidogo nje ya mji wenu8
 
nawashangaa sana wabongo, yaani mtu una miguu, mikono, macho na upo energetic tena huna magonjwa sugu lakini bado unajiita 'maskini', sasa sijui tukusaidieje apo?? tuuzie figo, moyo au kongosho zako sasa kama umeshindwa kujishugulisha
Mkuu usishangae unajua Kuna mazingira fulani yanaweza kukupiga upofu kila kitu kinakuwa kigumu, hasa usipotembea ndo mbaya kuliko, kitu chochote
 
Kama ushauri wangu utakuwa na maana uchukue, kama hauna maana tupa kapuni!

✓ jitenge na mnyororo wa ukoo wenu kiroho, hapa mtafute sheikh akupigie dua, anakutenganisha! Ukoo wako unaanza rasmi kuanzia kwako! Make issue kama hii hurithishwa (sometimes) ungelikuwa Mwanza ningelikupa address ya sheikh!

✓Au, tafuta mtaji! Anza biashara yako hata kama ni ya kawaida tu, kisha njoo Kawe uchukue mafuta ya Arise and Shine! (Nimeshuhudia wengi wente situation kama yako, wengine nimekuwa majirani nao), kama huamini uko, tafuta mafuta ya masheikh sanasana ya Qudra! tumia!

✓ukifanya biashara sahau kabisa kuwa mimi nina degree, hutoendelea kamwe, ikiwezekana kaishi mkoa mwingine mbali na huo ulikosomea chuo ili kuwa huru kufanya biashara zako!
Mi nipo mwanza nipe address ya huyo sheikh

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mkuu usishangae unajua Kuna mazingira fulani yanaweza kukupiga upofu kila kitu kinakuwa kigumu, hasa usipotembea ndo mbaya kuliko, kitu chochote
Uko sahihi mfano Dar kuna akina mama wagogo ombaomba sio walemavu wala nini

Wanafanana na wanawake kibao walioko vijijini nje ya Dodoma mikoa mingine wanaojitegemea!!
 
Ushauri wako 50% foolish! Wewe ni Mchagga?
Kuna makabila kuna koo malofa yamejaa umaskini wa kutupwa unaishia kusifiwa ohh wanaoana kabila yetu na ukoo!! wetu unaishia kuendeleza kizazi cha maskini tu kwenye ukoo
Kiumeni malofa na kikeni malofa wa kutupwa nyie mliooana ndio mnaonekana mabilionea akina Bakheresa au Dangote nau Billy Gates wa kuhudumia malofa wa ukoo pande zote!! Hata muwe wazoa takataka na mkokoteni Dar es salaam
 
Maskini akili anayo yaweza kuwa ya Omba Omba nk, fukara hata akili ya kuomba au kutafuta msaada kwa wenye uwezo hana ,Tajiri ni mtu anayejitosheleza kwa mahitaji yake yote muhimu bila kutegemea mtu kuanzia chakula, mavazi Malazi nk tofauti viwango tu ya utoshelevu mfano mwingine mwanae anasomesha Ulaya mwingine English Medium. TANZANIA
Wewe u wapi katika hao?
 
Tunduliza kwenye kibubu angalau 50% ya kila pesa unayopata- Nakushauri utumie kibubu maana kwa njia hyo utasave hela yako vizuri na kufikia target uliyojiwekea bila kushawishika kuitumia .N/B- Don't save just for the sake of saving bt save for the sake of investment

Jenga kibanda ufuge kuku za kienyeji hasa jogoo.Jogoo wanatengeneza pesa haraka kuliko kuku wa kike.

Jiunge kwenye vikoba hata kama Ni Cha sh' 2500/- kwa wiki- Hii Ni njia mojawapo ya kusave hela zako.

Usiendekeze mademu wengi mkuu,tafuta mwanamke mmoja aliye serious na anayejua kutafuta pesa.
 
Familia yetu yote hakuna mwenye unafuu wa kiuchumi. Nikaangazia macho ndugu wa baba na mama, na wao wote ni masikini sana. Nikafuatilia historia ya mababu na wao walikuwa mafukara kabisa.

Nina shahada ya kwanza ila ninakaribia kumaliza mwaka tangu nimalize chuo lakini sijawahi kuifanyia kazi. Nafanya vibarua vya kupalilia mashamba ya watu na za zege.

Najua hapa kuna watu wa namna mbalimbali. Naombeni msaada wa kujinasua katika hili wimbi la ufukara angalau niwe na unafuu wa maisha. Niweze kujikimu kwa uhakika wa chakula na malazi tu.

NB: siombi msaada wa pesa, naomba msaada wa Mawazo.

Ahsanteni.
Unachopata, jaribu kudunduluza iweke akiba, na upate mtaji wa kuanzusha shughuli ya kukuinua taratibu. Hivyo Anza kwa kuwa na akiba ya fedha.
 
Una degree moja unafanya kazi ya saidia fundi, sawa, je hiyo ipo siku itakutoa ?

Ajira hakuna ila ukipambana ajira utapata.

Pia angalia utakavyoweza kuukata huo mnyororo wa umaskini, wewe umesoma japo elimu yetu haisaidii sana.
 
Una degree moja unafanya kazi ya saidia fundi, sawa, je hiyo ipo siku itakutoa ?

Ajira hakuna ila ukipambana ajira utapata.

Pia angalia utakavyoweza kuukata huo mnyororo wa umaskini, wewe umesoma japo elimu yetu haisaidii sana.
Ushauri rahisi kwa tatizo gumu.

We' mama huwa unashauri simply sana
 
Habari na Amani ya Mungu iwe juu yako;
wengi wamesema mengi lakini sio wote wamegusa sababu hasa ni nini na nn chakufanya.

nitakueleza ukweli ingawa sio wote watanielewa na kukubali kwasababu asiyejua na hajui hajui kama hajui mpaka atakapojua ( samahani kwa lugha ngumu)

Maisha ni rohoni na yanadhihirka (yanatokea) mwilini. namaanisha kila kitu kinaanza katika ulimwengu wa roho kwanza kabla hujaona yakitukia katika ulimwengu tunao ouna. Ulimwengu wa roho una miaka mingi mno kuliko maisha tunayo ishi, pia unasiri za kutosha.
kabla chochote hakijafanyika kinaaza rohoni kwanza, mfano unaposema kwenu wote ni masikini na mnapitia mambo magumu... hiyo ni tendo liko katika ulimwengu wa roho. hata mmoja wenu akijitahidi anaweza enda juu kidogo na akaanguka chini kwa nguvu sana.

kinachosababisha ni nguvu ya giza/ shetani/ kupitia ama uchawi ama mizimu ambayo wamefanya maagano fulani na kuweka mipaka fulanifulani. Ukifuatilia ukoo wenu utagundua, kwamba wazee walitumikia na kujihusisha na miungu na waliweka maagano fulanifulani, wakitoa sadaka na matambiko.na waliishi maisha fulani ambapo inawalazimisha ukoo wote waishi maisha hayohayo. waliweka madhabahu pia, ama kwenye miti ama milima ama sehemu nyinginezo.

Namna ya kutoka katika mnyororo huo ni kuvunja maagano na kuangusha hizo madhabahu, vingenevyo hamna namna. Kulipa sadaka ambazo zilitolewa ni kwa kutoa sadaka kubwa zaidi ya zile zilitolea. Habari njema ni kwamba DAMU YA YESU ni SADAKA iliyo kubwa kuliko sadaka zote na popote na kwa wakati wowote. kwa hiyo njia pekee ya kupoke auponyaji wako ni kukutana na YESU atakutoa wewe na ndugu zako na ukoo wako.

inasomeka kama ni rahisi, ni kweli - rahisi lakini ina gharama ya IMANI na UVUMILIVU kwa maana ya muda na BIDII, UTII na SHAUKU.

nakazi tu kwamba, hata kama utaweka juhudi kaktka mikakati ye yote ile, huwezi toboa mpaka utengeneze hapo kwanza. haimaanishi uache fanya kazi kabisa ila elekeza nguvu kufunguluwa kwanza, baada ya hapo utafanikiwa

naamini nimesaidia kwa sehemu;
Nakazia hapa apitie hapa vizuri atengeneze avunje maagano yote akimtumainia Mungu atafanikiwa
 
Back
Top Bottom