Ukraine sasa iko katika vita kamili vya kujikomboa

Ukraine sasa iko katika vita kamili vya kujikomboa

Unafuatilia huu mpambano unavyokwenda au unakielezea kile unachokielewa kwa kile unachokiona kuhusu huu mpambano?

Kwa ufupi umeachwa nyuma kwa taarifa nyingi sana! Au pengine uruhusu kuwasikiliza wajuzi wa mbinu za kivita kama wengine tunavyofanya, na hili ni bora zaidi kwako na kwa wengineo wenye mfano wa kwako.

Kuizingira miji mfano wa Kieve ni mbinu ya kivita ndivyo wataalamu wanavyosema. Huo ni mji mkuu wa nchi hivyo utalindwa kwa gharama yoyote ili usianguke. Msafara wa jeshi la Russia kuonekana unaelekea Kieve ukawafanya sehemu kubwa ya jeshi la ukraine kuuhami mji wao kwa gharama ya namna yoyote. Sehemu nyengine za nchi zikabakiwa na idadi ndogo ya jeshi kukabiliana na Russia.

Alichokifanya Russia ni kuuzunguka mji wote. Mianya yote akaiziba. Hii ikawa ni faida kwa sehemu nyengine za Ukraine zenye majeshi kuteketezwa kwa urahisi kwa sababu upinzani ulikuwa mdogo.

-Nukta nyengine ni kwamba mkutano wa uliyofanyika baina ya Russia na Ukraine ya amani uliyofanyika nchini Turkey moja miongoni mwa guarantee walizokubaliana nazo kwa kukubaliana baadhi ya matakwa ili kuiendea amani kwa mustakabali wa pande zote mbili ni Russia kuondosha sehemu za majeshi yake baadhi ya sehemu za Ukraine. Ndiyo maana Russia akaondoa majeshi yake Kieve na kwengineko ili kuonyesha kuwa yupo serious na anaheshimu makubaliano.

Hotuba ya rais wa Russia ipo wazi na kama mdau wa juu Mokaze alivyowasilisha huu mgogoro una historia. Naam, tutamlaumu Putin kwa alichokifanya ila kuulewa huu mgogoro zaidi inakubidi uutumie muda wako kusoma majarida mbalimbali ya uhasama baina ya NATO na Russia(Soviet).

Maazimio ya kile Rais wa Russia alichokiita Special military operation ni yaliyojikita kwa usalama wa Russia na usalama wa raia wa majimbo yaliyojtangaza kujitenga Ukraine ambayo ni:

1)Kupunguza nguvu jeshi la Ukraine na kuondoa NAZI.
2)Kuyakomboa majimbo yaliyojitenga nchini Ukraine dhidi ya uonevu wa jeshi la Ukraine.

-Nukta ya kwanza ambayo kwa mujibu wa Russia tayari wameshaitekeleza. Ikiwa kama kweli unafuatilia hii vita utaona tangu siku ya kwanza jeshi la Russia lilikuwa likilenga kambi za jeshi, maghala ya kuhifadhia silaha, maghala ya kuhifadhia mafuta, yaani miundombinu yote ya kijeshi kwa ujumla. Hii ndiyo demilitarization. 90% ya jeshi la Ukraine limeharibiwa na hili limethibitishwa na msemaji wa Ikulu ya Ukraine.

-Phase 2 ambayo Russia wameitangaza ndiyo hiyo ya kuikomboa hiyo miji kutoka mikononi mwa jeshi la Ukraine ambapo mpaka jana taarifa zinasema kulikuwa na idadi ya 6000 ya wanajeshi wa Ukraine.

Mpaka sasa taarifa ni kuwa: "The cleanup of Mariupol continues. As of April 7,2022, the allied army of the DPR and Russia liberated Novogrigorovka (Volodarsky district), Pannovka, Suzhenka, Lugovoye, Sadovoye, Fedorovka, Kalchinovka, Nazarovka, Ukrainka, Republic, Ksenovka, Novoromanovka, Sergeevka, Starchenkovo, Peremoga, Priazovskoye, Shevchenko (Pershotravnevy district), Ilyichovskoye, Rybatskoye, Chervonoye..."


Short situation report: Mwendo huo huo ndiyo wanaokwenda nao:•
-Kherson-Nikolaev.
-Odessa.
-Zaporozhye.
-Ugledar-Velika Novoselka
-Maryinka.
-Avdiivka.
-Izyum.
-Kharkiv—Sumy.

Ukraine ameshapoteza kwenye huu mpambano pakubwa sana!
Mkuu wanapambana au Ukraine anajihami tu?
 
Russia anayo jeuri ya Hypersonics kitu ambacho hata America hana na ndio maana akataka kufanya njama kwa Ukraine ajiunge na NATO ili aweke base ya kijeshi ili iwe kwake ni rahisi kupunguza muda wa kumvurumishia Russia Makombora pindi kama vita vitaibuka.
Samahani Broh, hivi hii inaweza kuwa sababu ya kutosha kujustify uvamizi wa Russia? Marekani hawezi kufanya hivyo kupitia Estonia, Latvia au Turkey? Maana hao wote ni wanachama wa NATO wanalio karibu kabisa na Russia.
Nahitaji kujua Broh, sipo vizuri kwenye masuala haya ya siasa na migogoro ya kimataifa.
 
Ukraine apigane kivyovyote vile Putin na nchi nyingine zinazodharau wenzao zijifunze.Putin pamoja na kuipiga Ukraine,nadhani hakutegemea kama atakutana na anayokutana nayo.Ukraine agharamike ila na Putin pia imgharimu sana.Ukraine atasaidiwa kujijenga,Putin atapambana na protest ndani na nje ya nchi na hatimaye anaweza akafa au kuuawa siku za mbeleni.
Mimi napenda sana nchi ikiongozwa na jasusi mzalendo kama Putin. Putin kiapo chake ni kufa kwa kuitetea nchi yake, kwahiyo usitegemee Putin kama jasusi atakubali kirahisi rahisi kutoka Ukraine. Akiona analemewa sana ataomba meza ya majadiliano lakini Hilo pia sitegemei kama litatokea maana ninavyowajua majasusi wazalendo hawanaga simile..!

Hawa jamaa wapo tayari hata kudondosha Nuclear weapon popote duniani ndiyo akubali afe au auwawe na warusi na KGB Yao watamficha sehemu huku akiendelea kula kuku kwa mrija na wanaweza hata kumfanyia plastic surgery akaja Tanzania kama Mwekezaji akaendelea kula bata
 
Mimi napenda sana nchi ikiongozwa na jasusi mzalendo kama Putin. Putin kiapo chake ni kufa kwa kuitetea nchi yake, kwahiyo usitegemee Putin kama jasusi atakubali kirahisi rahisi kutoka Ukraine. Akiona analemewa sana ataomba meza ya majadiliano lakini Hilo pia sitegemei kama litatokea maana ninavyowajua majasusi wazalendo hawanaga simile..!

Hawa jamaa wapo tayari hata kudondosha Nuclear weapon popote duniani ndiyo akubali afe au auwawe na warusi na KGB Yao watamficha sehemu huku akiendelea kula kuku kwa mrija na wanaweza hata kumfanyia plastic surgery akaja Tanzania kama Mwekezaji akaendelea kula bata
Yaani Putin ahangaike mpk na ma plastic surgery kisa hao mashoga?Never
 
Mpuuzi ni wewe na nchi yako mzee sio putin!
Wewe mweusi wa afrika putini anakuhusu nini, tuanzie hapo....au jini mahaba amekukamata?
hata nikimbabatiza putini na kumuuliza raisi wa tanzania ni nani atajing'atang'ata.....
 
Ww ndio mpumbavu kwa sababu umeshindwa kujua ya kwamba kila mtu hapa duniani huwa anajiangalia yeye kwanza na simwingine .

Na hii ndio kanuni ya maisha.

Kwa hiyo Putin anacho kiangalia ni taifa lake kwanza na si ww au taifa lako maana ww hujamuweka Madarakani.

Hata ww katika maisha yako ya kila siku unacho kiangalia ni maslahi ya yako na familia yako kwanza, huwezi kuacha kufanya kitu chenye manufaa kwa familia yako eti kisa mwingine hapendi labda uwe mpumbavu kama ww.
Tafuta hela wewe njaa kali....na hii ndio kanuni ya maisha....
unaleta mahaba kwa putini wakati unaishi ileje....zwazwa kabisa...
 
Maisha yako ww yana mhusu nn yeye?
Kinacho angaliwa ni maslahi ya taifa lake na sio mlala njaa kama ww.
Nikuonee huruma wewe ...pole sana....
Ningekuwa naishi kwa shemeji kama wewe lazima ningemshabikia putini ......shauri yako....yakibuma atakurudisha kijijini
 
Ujinga ni kuamini kwamba hizo Hypersonic sijui Nuclear weapons anazo Russia pekee, NATO na Russia wakiingia vitamin hawachukui hata mwezi.. Russia haitabaki kitu. Russia hata kwa Germany hachomoki. Hapo tu Ukraine kapewa support ya vifaa sio ya Kijeshi na Russia kambwela.. akipata support ya kijeshi itakuwaje?

Kuwa na common sense kijana.
Mahaba haya, eti Russia hata kwa Germany hachomoi. Haya endelea kuota
 
Ni hivi huyo Ukraine apigwe na Russia au asiaidiwe na NATO hainuhusu
Kinachonihusu ni huyu mpumbavu putin anavuruga utaratibu wangu wa maisha ya kila siku na tena hata siishi Ukraine,
Hili ndio tatizo kwangu ambalo linanihusu, lakini vichwa mavi vya kibongo wanaomshabikia putin, labda sababu maisha yenyewe kwao ni kubabatiza(choka mbaya) na ameshazoea umasikini kwa hiyo hata haoni gharama za maisha kupanda kutokana na sababu za kijinga za huyu mpuuzi putin.
Aliyesababisha haya ni US and NATO. Kuna haja gani ya kutaka kwenda kuweka missile zake Ukraine??
Hata ingekuwa mimi adui yangu mkubwa aje apange chumba cha jirani nitafanya figisu hadi atoke hapo.
 
Tukaaminishwa ndani ya siku tatu Ukraine itakua chali.

Ikaja wiki.

Wakasema kesho tu Putin anamaliza kazi.

Moto unazidi kuwaka.

Bei za vitu zinapaa.

Raia wamekomaa kusema vita iendelee
Kama hatukuwaambia wapigane na bado wakaamua kupigana
Unahisi kama tukiwaambia wasipigane wataacha kwakua tumewaambia wasipigane
Acha UKRAINE aendelee kula kipigo mpaka anyooke
RUSSIA sio ZIMBABWE
 
Kuvamia kwa kujilinda ni haki.

That’s a very loose angle. Hiyo ni kuzipa ruhusa (blank check) nchi zenye nguvu na viongozi wakorofi kunyanyasa nchi nyonge.

Ni kama US ilipovamia Iraq 2003 bila kibali (sanction) ya UN. Au Germany ilipovamia Poland 1939 kwa kisingizio cha kujilinda kumbe tayari wana mipango ya kufagia hadi Moscow na London!
 
zelensk hakuwa rais aliyechaguliwa na wa Ukraine wenyewe,NI pandikizi la USA &NATO ,alipandikizwa ili a push ku accomplish the mission dhidi ya russia. Thus why haoni hasara yeyote kwa dhiki wanayopitia waukraine .since when US & NATO become a truely friend!!?? Since when !!!???, if you see Americans are close to u ,there something paratable for their stomach!!!
 
UKRAINE imebakia majivu jamaa anaomba msaada kila leo na bado anapigika
RUSSIA sio ZIMBABWE

Huyo jamaa haombi misaada ila anapewa misaada yote inayohitajika ili vita ipiganiwe Ukraine.

NATO ni sehemu katika vita hivi. Kila mtu anajua hivyo isiyokuwa wewe uliye kenua sawa sawa hapo:

IMG_20220302_122620_294.jpg
 
Wote Wamepoteza na hasa Ukraine kapoteza zaidi, Mrusi kapoteza kinyume na matarajio yake kwamba vita ile ingekuwa kitu rahisi kwake.

Kijeshi au kivita, Mrusi kapoteza zaidi kwa askari wengi na vifaa vingi (vifaru + ndege) kuangamizwa.

Ukraine imepoteza zaidi kwa miundombinu, majengo mengi kubomolewa, raia wengi kuuawa na kukimbilia uhamishoni.
 
zelensk hakuwa rais aliyechaguliwa na wa Ukraine wenyewe,NI pandikizi la USA &NATO ,alipandikizwa ili a push ku accomplish the mission dhidi ya russia. Thus why haoni hasara yeyote kwa dhiki wanayopitia waukraine .since when US & NATO become a truely friend!!?? Since when !!!???, if you see Americans are close to u ,there something paratable for their stomach!!!

Kwanini wa Ukraine wameshindwa kumwondoa madarakani Russia war machine ikiwa 20km tu kutokea Kyiv city centre?

Umbali huo ni Kimara magogoni mkuu.
 
Back
Top Bottom