Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Labda hii watu hawajui. Leo si tunazungumzia dini zetu, let's go.

Kuna tofauti ya watu walioandikwa kwenye Biblia na Koran, hilo kwanza ulijue. Ibrahim unayemsoma kwenye Biblia si Ibrahim unayemsoma kwenye Koran.

Ibrahim wa kwenye Biblia baba yake anaitwa Terah ila wa kwenye Koran anaitwa Azar. Kasome Quran 6:74.

Kwenye Biblia wana Yesu, kwenye Koran wana Issa. Huyu Issa hakusulubiwa msalabani, ila Yesu alisulubiwa. Ndugu zangu, hawa ni watu wawili tofauti.

Kuna MUNGU (Almighty GOD) kwenye Biblia na kuna Allah kwenye Koran

So watu wa huku ni tofauti na wa kule. Kwa Biblia, Ishmael anajulikana kama mtoto wa kijakazi, ila kwa Kuran ni tofauti.

So mkikaa na kuzungumza, cha kwanza jueni mnawazungumzia watu wa sehemu tofautitifauti.

Mfalme Suleiman wa Bible alikuwa holy na baadaye akaanguka dhambini ila wa kwenye Kuran alikuwa anaongea mpaka na majini. So mkiwa mnawasoma watu wa kwenye Bible, msije kufikiri ni watu walewale wa kwenye Kuran, sio hivyo.

Musa wa kwenye Biblia alipewa Amri 10 za MUNGU, Musa wa kwenye Koran hakupewa amri 10 zozote.

Biblia inamtambua Samson kama jamaa aliyebarikiwa nguvu na uwezo wa kupambana na udhaifu wake ni kukata nywele zake, ila hakuna kisa cha namna hiyo kwenye Quran.

Biblia imeorodhesha mitume na manabii wengi wakitoka katika chimbuko la wayahudi, wakati Quran haiwazungumzii wayahudi katika chimbuko la unabii.

Ndio maana ukimsoma mtu wa huku, unaona tofauti kubwa na mtu wa kule.

Kuran imemtambua Adam kama mtume, ila kwa Biblia imemtambua kama mtu wa kawaida tu, mtu aliyeumbwa mwanzoni kabisa.

So mlifahamu hilo, sio mnakaa kwenye vijiwe vya kahawa mnabishana weeee meaningwhile watu mnaowazungumzia ni tofauti.

Historia ya Matukio ikitofautiana basi jua kabisa hao ni watu tofauti kabisa.

Hivyo ni vyema kila mtu abaki na anachokiamini, muda au siku ya kiama ndio ukweli utadhihirika nani alikuwa sahihi na nani alikuwa muongo.
Wewe dogo unajifanya mjuaji sana wa haya mambo wakati ukweli huujui. Na unapenda ligi za kidini ukitetea ukristo wako wakati huna elimu and so unakosa moral authority to establish this type of discussions.

Naomba nikujibu point yako ya kwanza ya Ibrahim.
Kiarabu kina wenyewe sio mnatafsiri mnavyotaka nyinyi. Hiyo aya ya Surat An'aam (6:74) Quran imetumia neno Abi kudenote baba (kama ambavyo wewe umetafsiri)......lakini katika ufasaha wa lugha, Abi haitumiki tu kudenote baba mzazi. Hata baba mdogo/mkubwa inatumika pia yaani uncles au mababu zako waliotangulia (ancestors). Nitakupa ushahidi juu ya hili:-
1. Ukisoma Quran 2:133 wakati Yaqub (Jacob) umemjia umauti akawauliza wanawe watamwabudu nani baada ya kufa kwake? Wakamjibu tutamwabudu Mungu wa baba zako Ibrahim, Ismael na Isihaka. Hapa Ismael naye kaitwa Abi wakati si baba yake mzazi.
2. Kwanza baba yake Ibrahim hakuwa mwabudu sanamu. Ukisoma Quran 14:41 Ibra anaomba yeye na baba yake na waumini wengine waingizwe peponi. So hii ni evidence aliyetajwa pale 6:74 si baba yake mzazi.

Baba yake Ibrahim kwa mujibu wa Uislam anaitwa Tarah, kasome kitabu cha Ibn Katheer, kinaitwa Al bidaya wa Nahaya volume 1 page 139.
Pia nenda usome Tafsiri ya Quran ya Tabari by Ibn Jarir volume 7 page 158 na Historia ya Tabari volume 1 pg 119.

Dogo, ukija huku ujipange sio unakurupuka kama mlevi wa wanzuki. Hivi hujiulizi, yaani makosa uje kiyaona wewe leo wa karne hii ya dot com, huko nyuma hakukuwa na watu wanatafakari mambo haya? Hawakupata majibu?
Ni bora uulize kuliko kuconclude usichokijua.
WHEN YOU ARE NOT SURE, GUESS POSITIVELY.
Sean.
 
Mimi Naamini Sio Kila Sahihi Ni kweli!
Kwahyo Sahihi Bukhari zote na sahihi Muslimu zote sio Sahihi zote kwa 100%

Kama unabisha Ninazo Hadithi kadhaa ambazo si za kweli Zipo.kwenye Sahihi Zenu!

Hilo liko wazi kuna hadithi dhaifu kadhaa, ila katika uso wa ardhi hii ukitoa Qur'an hakuna kitabu kingine kinachozidi usahihi sahihi AL-Bukhari.

Kingine yeye Imam Bukhari kitabu chake hicho alivyokiandika hakukipa jina hilo la "Sahih al-Bukhar", bali wanazuoni walio kuja baadae, baada ya kukipitia wakakipa jina hilo. Yeye imam Bukhari kitabu chake hicho alikipa jina hili "Al-Jami'ul Musnadus Sahihul Mukhtasaru Min Umuri Rasulullillah Sallallahu 'Alayhi Wa Sallam Wa Sunanihi Wa Ayyamihi."
 
Mitume na manabii wote walikuwa na ujumbe mmoja ambao ni kumuabudu Allah na kuupiga vita ushirikina.

Tofauti ya Mtume na nabii, ni kuwa kila Mtume ni nabii lakini siyo kila nabii ni Mtume. Mtume alipopewa ujumbe alilazimishwa lazima aufikishe ujumbe huo, nabii kwake ni tofauti halazimishwi kuufikisha ujumbe huo. Mtume hupelekwa sehemu imani imetoweka kabisa na watu wanakuwa wameingia katika ushirikina ila nabii hutumwa hata kama sehemu imani ipo.

Mitume hupewa sheria kadhalika.

Kwa ufupi mitume na manabii wote wa Allah walikuwa na imani moja ya Uislamu ila walitofautiana sheria.

Hapakuwahi kuwa na mtume wala nabii wa kike. Hii ni nukta ya msingi pia chukua.
🤣🤣🤣🤣
 
Alifunuliwa na kuagizwa awaulize watu walioshushiwa kitabu ili hali wakati wake biblia haikuwepo. Huoni allah na Mohammad wote walidanganya?

Watu wa kitabu aliwauliza kwa kuonyesha ukweli wake, sababu hata wao watu wa kitabu wapo walio muamini.
 
Mitume na manabii wote walikuwa na ujumbe mmoja ambao ni kumuabudu Allah na kuupiga vita ushirikina.
Ndio maana ukaulizwa,ikiwa vitabu vingine vilikuwepo Quran ilikuja na jipya gani kutoka kwa mtume wa kiarabu???
Tofauti ya Mtume na nabii, ni kuwa kila Mtume ni nabii lakini siyo kila nabii ni Mtume. Mtume alipopewa ujumbe alilazimishwa lazima aufikishe ujumbe huo, nabii kwake ni tofauti halazimishwi kuufikisha ujumbe huo. Mtume hupelekwa sehemu imani imetoweka kabisa na watu wanakuwa wameingia katika ushirikina ila nabii hutumwa hata kama sehemu imani ipo.
Ndio tunaomba uthibitisho kwa Alitumwa na Mungu hakika.wala hakukurupuka asubuhi akaja na hekaya kama nabii tito.
Mitume hupewa sheria kadhalika.

Kwa ufupi mitume na manabii wote wa Allah walikuwa na imani moja ya Uislamu ila walitofautiana sheria.
kwahiyo sheria zilikuwa za kwao binafsi au za Allah??

Hapakuwahi kuwa na mtume wala nabii wa kike. Hii ni nukta ya msingi pia chukua.
tuna uhakika gani??kama uislam una manabii zaidi ya 200k,tuna uhakika gani kama akina mwamposa na hata wa kike hawapo ktk hii orodha??
 
  • Kicheko
Reactions: 511
Biblia inajumuisha maandiko yaliyoandikwa na waandishi mbalimbali katika kipindi tofauti cha historia ya dini ya Kiyahudi na Kikristo. Haijaandikwa moja kwa moja na nabii mmoja maalum. Badala yake, inajumuisha maandiko yaliyoandikwa na manabii, wataalamu wa dini, wanahistoria, na waandishi wengine, ambao waliandika kwa kuzingatia ufunuo, uzoefu wa kidini, na matukio ya kihistoria. Kwa mfano, katika Agano la Kale, vitabu vingi vinavyohusishwa na nabii kama vile Isaya, Yeremia, na Ezekieli, wanasemekana kuwa na sehemu ya maandiko yaliyojumuishwa katika Biblia. Katika Agano Jipya, vitabu vya Injili vilivyoandikwa na wanafunzi wa Yesu pamoja na barua za mitume ni sehemu ya maandiko yaliyojumuishwa katika Biblia.
Mwanafunzi gani wa Yesu aliandika injili? Hakuna ushahidi wowote unaoonesha Marco, Luka wala Peter waliandika injili. Hivyo vyote havijulikani alindika nani. Sasa mandishi ya watu kwa utashi wao na uzoefu wao katika dini yanakuwaje neno la Mungu?
Yaani maandishi ya Paulo yawe neno la Mungu? Kwanini Yesu mwenyewe hakuacha maneno yake yawe neno la kuishi angalu tungeyaita neno la Mungu.
 
Hilo liko wazi kuna hadithi dhaifu kadhaa, ila katika uso wa ardhi hii ukitoa Qur'an hakuna kitabu kingine kinachozidi usahihi sahihi AL-Bukhari.

Kingine yeye Imam Bukhari kitabu chake hicho alivyokiandika hakukipa jina hilo la "Sahih al-Bukhar", bali wanazuoni walio kuja baadae, baada ya kukipitia wakakipa jina hilo. Yeye imam Bukhari kitabu chake hicho alikipa jina hili "Al-Jami'ul Musnadus Sahihul Mukhtasaru Min Umuri Rasulullillah Sallallahu 'Alayhi Wa Sallam Wa Sunanihi Wa Ayyamihi."
Sasa Tofauti iko wapi Kuita Sahihi Bukhari na Kuita kwa Kirefu chake?
Hapo umeandila Kirefu cha Jina La Sahihi al Bukhari..
Na hata ukiangalia maana ya hicho ulichokiandika Ni hicho hicho..

Mkuu hakuna Hadithi Dhaifu kwenye Hadithi zilizopewa Grade ya Sahihi..

Nafahamu unajua Grade za hadithi na ndo maana Nikaandika hivyo..

Kuna Sahihi, Hassana, Dhaifu na kuna mawduʻ au Maudhu (موضوع)..

Nilichozungumzia Ni kuhusu Hadithi zilizochambuliwa na kupewa Rank ya grade ya Sahihi..
Sio zote ni Sahihi...
 
Qur'an Ina matatizo zaidi ya kiuandishi, iliandikwa au kukusanywa miaka zaidi ya 100 baada ya Mtume kufariki, wakati Biblia ilikuwa imekamilika au baadhi ya vitabu vyake viliandikwa miaka 30-40 baada ya Yesu kupaa. N walioandika waliishi naye; walimjua na kimfahamu Yesu.
Ndiyo maana Qur'an Waislamu and wengine hawaijui , kazi yao ni kufunga na kuswali na kusikiliza mawaidha tu. Hata waliotafsiri mengine wamepotosha baadhi ya maandiko. Mtu mwenybhekima atasoma na kuchambua. Mwislamunhna uhakika kam akifa atakwenda mbinguni, sababu hata Mtume mwenyewe hajui. Angalia Yesu alizungumza kwa ujasiri sana. " Nilipo Mimi nanyi mtakiwepo"
Hakuna ushahidi wowote kuwa kuna mwanafunzi wa Yesu aliandika injili. Ni stori za watu tu.
 
Mwanafunzi gani wa Yesu aliandika injili? Hakuna ushahidi wowote unaoonesha Marco, Luka wala Peter waliandika injili. Hivyo vyote havijulikani alindika nani. Sasa mandishi ya watu kwa utashi wao na uzoefu wao katika dini yanakuwaje neno la Mungu?
Yaani maandishi ya Paulo yawe neno la Mungu? Kwanini Yesu mwenyewe hakuacha maneno yake yawe neno la kuishi angalu tungeyaita neno la Mungu.
Maandishi ya Muhammad yanakuwaje neno la mungu?
Thibitisha kwamba Muhammad alishushiwa neno lolote na mungu.
 
Ndio maana ukaulizwa,ikiwa vitabu vingine vilikuwepo Quran ilikuja na jipya gani kutoka kwa mtume wa kiarabu???

Ndio tunaomba uthibitisho kwa Alitumwa na Mungu hakika.wala hakukurupuka asubuhi akaja na hekaya kama nabii tito.



kwahiyo sheria zilikuwa za kwao binafsi au za Allah??


tuna uhakika gani??kama uislam una manabii zaidi ya 200k,tuna uhakika gani kama akina mwamposa na hata wa kike hawapo ktk hii orodha??
Ukisoma sahihi Bukhari Hadithi No 3..
juzuu ya kwanza..

Inasema Baada ya Waraqa ambaye alikuwa Mkristo aliyeijua Dini ya kikristo vizuri Kifariki Na Ufunuo.wahyi nao ukakoma kwa muda..

Yaani "Pause of revelation" Hujiulizi kwanini?
Kwa sababu Huenda aliyekuwa anamjuza Alifariki 😅 (natania)
But ndo.Ilivyoandikwa hivyo..

Kwahyo Baada ya kufariki Mjomba wake Khadija Mwanatheolojia wa Kikristo na Mungu naye akaamua kusimamisha Wahyi kwa muda kwanza
Screenshot_20240407_210858_Adobe Acrobat.jpg
 
Hakuna ushahidi wowote kuwa kuna mwanafunzi wa Yesu aliandika injili. Ni stori za watu tu.
Utaupata wapi ushahidi usio na shaka kwa jambo lililotokea miaka 2000 iliyopita????
Hata tungeweka maandishi bado yasingefaulu,maana yanahamishwa kutoka chanzo hiki kwenda kile kwa tech tofauti.

Miaka 2000 ijayo kuna watu watakataa wakiambiwa watu leo wanatumia siku mbili kusafiri hapa mpaka kigoma,sababu tu hakutakuwa na video ya tukio wala mtu aliyeishi leo wa kuwahakikishia.
 
  • Thanks
Reactions: 511
Ukisoma sahihi Bukhari Hadithi No 3..
juzuu ya kwanza..

Inasema Baada ya Waraqa ambaye alikuwa Mkristo aliyeijua Dini ya kikristo vizuri Kifariki Na Ufunuo.wahyi nao ukakoma kwa muda..

Yaani "Pause of revelation" Hujiulizi kwanini?
Kwa sababu Huenda aliyekuwa anamjuza Alifariki 😅 (natania)
But ndo.Ilivyoandikwa hivyo..

Kwahyo Baada ya kufariki Mjomba wake Khadija Mwanatheolojia wa Kikristo na Mungu naye akaamua kusimamisha Wahyi kwa muda kwanza
View attachment 2956878
Huwa nawaambia ndugu zangu,hizi dini zina misingi dhaifu,lakini uislam uko ktk msingi dhaifu zaidi.
Ni vile tu watu hawasomi historia zake.

Kama uthman ndiye wa kwanza kukusanya Aya kisha akazichoma alizoona yeye hazifai😁😁😁,si tatizo hili???
 
Utaupata wapi ushahidi usio na shaka kwa jambo lililotokea miaka 2000 iliyopita????
Hata tungeweka maandishi bado yasingefaulu,maana yanahamishwa kutoka chanzo hiki kwenda kile kwa tech tofauti.

Miaka 2000 ijayo kuna watu watakataa wakiambiwa watu leo wanatumia siku mbili kusafiri hapa mpaka kigoma,sababu tu hakutakuwa na video ya tukio wala mtu aliyeishi leo wa kuwahakikishia.
Mkorinto kaka Soma Comment # 201 na #166
Tupate cha Kuanzia Kujenga Hoja
 
Huwa nawaambia ndugu zangu,hizi dini zina misingi dhaifu,lakini uislam uko ktk msingi dhaifu zaidi.
Ni vile tu watu hawasomi historia zake.

Kama uthman ndiye wa kwanza kukusanya Aya kisha akazichoma alizoona yeye hazifai😁😁😁,si tatizo hili???
Sitii neno hapo
 
  • Kicheko
Reactions: 511
Maandishi ya Muhammad yanakuwaje neno la mungu?
Thibitisha kwamba Muhammad alishushiwa neno lolote na mungu.
Jibu hoja, usigeuze swali. Kwani ni wapi nimesema maneno ya Muhammad ni maneno ya Mungu?
 
Back
Top Bottom