Ukweli kuhusu Vita vya Majimaji

Ukweli kuhusu Vita vya Majimaji

Kilwa
kipindi cha banu Umayya
huu ni utawala wa kwanza katika kipindi hichi baada ya makhalifa wanne utawala wa banu Ummayya ulianza na Muawiya bin Abuu sufiyan ulifuatiwa na yazid bin muawiyya 61-64 Hijiria sawa na mwaka 680-685 A.D, utawala huu haukuwa mzuri, kwani ulikuwa na upungufu mwingi;'
baadaye ulifuatiwa na uongozi wa Umar ibn Abdul-Aziz, ambaye alijaribu kurudisha hali ya kawaida katika katika dola yake na zile za mashariki ya kati na mashariki ya Mbali
Marwan wa pili au Abdul malik marwan, alikuwa ni mmoja katika utawala huu yeye ndiye aliyefanikiwa kuufikisha Uislam Hispania miaka ya 86-96 hijiria (705-715 A.D)
Hispamia ilipokuwa chini ya utawala wake, wakati huo ikiitwa Andalus, kulikuwa na migogoro mingi iliyosababisha ukoo wa Abbas kujitenga, Abuu Muslim alllifanikiwa kupata wafuasi wengi ambao walimuunga mkoono kwa kuwahamasisha juu ya kile kilichofahamika (Ahlul Bayt.) ukoo unaotokana na Mtume ndio bora katika uongozi Mwishowe walipigana kati ya banu Umayya na Banu Abbas
banu Umayya wakashindwa watu wakamchoguwa Abuu abbas kuwa ni kiongozi wao na huo ndio ukawa Mwanzo wa utawala wa banu Abbas Mnamo mwaka 750 A.D
Kutokana na migogoro ya banu Abbas na Umayya Waislam wengi walimiminika kuingia Pwani ya Azania Mgogoro wa mwaka 750 ndio uliomsukuma Mtoto wa aliyekuwa Mtawala wa tatu, Marwan wa pili au Abdulmaliki ibn marwan akiitwa Hamza ibn abdul maliki ibn Marwan, afike katika visiwa vya Kilwa,;
Maelezo yanasema
Mtu mmoja jina lake Hamza alikuwa katika hao wa kwanza waliofika wakati huo hamza alikuwa mwanawe Abdul maliki aliyekuwa Khalifa aliyetawala kutoka Mwaka 65 Hijiria hadi 86 Hijiria Hamza ndiye aliyeleta Ustarabu
katika mwaka 755, kundi la Amu said, kizazi chenye mnasaba na sayyidna Ally kiliingia Somalia Mwaka 120 Hijiria (740 A.D), Zaid mjukuu wa hussein bin ali bin Abuu talib (r,a), aliingia katika mgogoro wa Uongozi na baadaye kuuwawa katika ya mwaka 724 hadi 743.)
Wafuasi wa Zaid Amu said wanaotoka kusini mwa Arabu, waliingia katika mwambao wa Afrika mashariki kisha wakaoleana na wasomali, wakati huo eneo la somalia linaitwa Afica ya kati kabla ya mkutano wa Berlin, wa kuligawa bara la Africa (Berlin Conference of 1884-feb 1885)
KIzazi hicho chenye nasaba moja kwa moja na Sayyid na Ally bin Abuu talib (R.A) Kilianzisha Diwani ya kwanza Ruga Vumba kuu na Vumba ndogo Wasin ikiongozwa na Ahmed bin hussein wa ukoo wa ba-Alui pia kizazi cha Abuubbbbakar bin Sheikh, ambaye alikuwa Mtawala wa vumba kubwa na vumba ndogo
kwa mujibu wa silsila ya viongozi wa mwambao huu utaona imeanzia kwa Ally bin Abuu Twalib na bibi Fatma (r.a) Sayyid hussein sayyid zeina el-Abidina ali, sayyid muhammad el-bakir,sayyid jafir sadiq,sayyid ali al harith, sayyid muhammad, sayyid issa, sayyid AHMED NA SAYYID Abdullah.
Silsila HIYO INAENDELEA KWA SAYYID Alui, ambaye kwake yeye huyu Bwana ukoo wa bani Alawi au Ba Alawi unapata mzizi wake
Ukoo huo umekwenda moja kwa moja mpaka kwa sayyid ABUUBAKAR MASELA el- Ba-alawi., ambaye ni mmoja katika ya hao ndugu wa mwanzo kuja Africa ya mashariki na kutoka kwa huyu kizazi kiliendelea mpaka kwa Shekh Abuubakar DIwani wa Ruga
Utaona kwemba katika mwambao wote wa somali mombasa Zanzibar pate, lamu na sofala zipo koo hizi za Ba-Alawi ba -Urri, na ba- Amir,
pamoja na makundi mengine ndugu saba wa Al-haswa wakaingia ndani ya Somalia katika mwaka 295 Hijiria (908 AD), Wakati wa mtawala wa Oman aitwaye El- wawari Bin matrash Ndugu hawa saba wakiwa na majahazi matatu walifika Mogadishu wakitokea Al-Haswa katika Pwani ya Oman katika kabila la El Azd
Mnamo mwaka 975 A.D, hassan bin Ally akiwa na majahazi saba kutoka Shirazi aliingia Kilwa yeye mweenyewe akabaki Kilwa kisiwani kisha jahazi lingine likiongozwa na mwanae aitwae Muhammad lilielekezwa Mombasa ' Mwingine aitwae Bashati alilielekeza jahazi lake nchi ya kua (Mafia) na aliyeitwa suleyman yeye alielekea pate na aliyeitwa Hussain alielekea Zanzibar, wakati watoto wake Daudi na Ali mmoja alikwenda Kismayu Somalia na mwingine akaenda (Visiwa vya Qamar Comoro)
hata hivyo G.S.P.Feeman Grenville akimnukuu Shekh Muhyidiin anasemakuwa yalikuwa majahazi saba jahazi la kwanza lilikwenda mandakh la pili lilikwenda Shungu la tatu lilikwenda katika mji uliitwa yanbu la nne lilikwenda mombasa na la tano lilikwenda katika kisiwa cha Kijani Pemba ) jahazi la sita lilikwenda katika nchi ya kilwa na la saba Hanzuani (morocco)
kwa upande wake Hassan bin Ally alipofika kilwa aliitamani sana sehemu hiyo na kuone pana manzari nzuri hapaja jengwa akaenda kumuona mtu mmaja aliyeitwa Muriri wa bari Ambaye alikuwa ni Muislam'
Huyo akampeleka kwa kiongozi wa eneo hilo la Mrima ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Bwana Kilwa Abdallah ibin Kilwa ambaye jina lake limenasibiswa na jina la mji wa KiLWA 'Hassan bin Ally alipewa sehemu ya Ardhi ya KIsiwa na huyu bwana kilwa baadaye alikuja kuwa kiongozi wa hapo
baada ya utawala wa Hassan bin ally baadaye aliitawala kilwa mwanaye ally bin hassan, amdaye yeye ndiye aliyeitanuwa dola ya Kilwa na kuwa kubwa na yenye umaarufu mkubwa katika pembe zote za Dunia wakati huo
......Ndipo sultan Ally alipoanza kueneza utawala wake tena alijitahidi akatanua biashara ya dhahabu iliyokuwa ikitoka sofala kwenda Mogadishu'
kwa ufupi wa maneno Utawala huu wa dola ya kilwa ukawa wa kitajiri na kutikisha dunia kwa wakati huo''
Walter rodney mwanahistoria mashuhuri anasema Africa ilistaarabika kupitia Uislam kabla Mzungu wa kwanza hajakanyaga mguu wake barani Africa
mataifa mbalimbali yalishuhudia maendeleo makubwa ya kilwa kupitia harakati mbalimbali za kimaendeleo hasa kuwanzia mwaka 1300 A.D, WAKATI HUO IKIWA CHANI YA ABDUL muzhafar hassan mjukuu wa mtawala wa mwanzo hassan bin ally ibin batuta anasema-
wakati nilipofika kilwa nilimkuta mtawala wake aliyekuwa anaitwa abu mudhaffar hassan akiifahamika kwa jina na Abul mawahib,
na hii ilitokana na wingi wa maajabu na ukarimu usio kifani
HiSTORIA inazidi kufichuwa zaidi kuwa Waislam wa kilwa walitumia baadhi ya nali zao kuimarisha miji yao badala ya ujenzi wa matope na miti waislamu hao ndio waliokuwa wa mwanzo kutumia mawe yaliyochanganywa na saruji na chokaa iliyotokana na matumbawe
kazi hiyo ya ujenzi ilikuwa bora kuliko ujenzi ule wa matope uliotumika hapo kabla ambayo majengo yake yame sababisha kupotea'
Dola ya kilwa ilikuwa na muundo wa kikee ulioendana na hali halisi ya wakati huo Kimaendeleo kiuchumi kitaaluma na kijaografia makao makuu ya dola hii yalikuwa kaole Bagamoyo lakini Ofisi zake kuu za utendaji zilikuwa Kilwa Kisiwani katika Ikulu ndogo na kubwa zikifahaamika kwa jina la Husuni kubwa na ndogo husuni kubwa ilijengwa karne ya 14, chini ya utawala wa Al hassan ibn suleyman ndani ya jiji la kilwa Kisiwani Jengo hili lilitumika mpaka mwaka 1843 baada ya mtawala wa mwisho kukimbilia Muscat nchini Oman
ikulu hiyo limetuama katika sehemu ya muinuko ikiitazama bahari ya hindi kwa upande wa mashariki mlango wa kilwa ulielekea upande wa kaskazini na jiji lenyewe la kilwa likibaki upande wa magharibi''
jengo hilo la kuvutia ambalo halijawahi kujengwa mfano wake kusini mwa jangwa kuu la sahara kabla ya karne ya 18 kipindi hicho jengo linakusanya zaidi ya vyomba 100, ambavyo vilitumika kama ofisi mbalimbali za ikulu kama taasisi
Eneo la kusini la jengo hili limegawanyika katika sehemu 'mbili yaani ile ya chini ya juu
sehemu ya chini ina ukubwa wa mita za mraba 2,116 na ina vyumba vya ofisi 38 kila upande ulikuwa na vyumba viwili katika ya vinne vyaenye kufanana
sehemu ya juu ya jengo hili ni enneo lenye vyumba vya ofisi na naeneo maalum kwa ajili ya wageni na wanadiplomasia
kusini magharibi ya eneo hili kulitengwa kwa ajili ya shughuli mbali muhimu kwanza zilijengwa nyumba za viongozi pili zilijengwa ofisi za kodi ya mapato na jirani na nyumba hiyo kulikuwa na kisima kirefu cha ukubwa wa mita 4.6 cha maji kileo leta maji ya kutosha
Upande wa maghribi ya ikulu hii ulikuwa na ukumbi mkubwa wa mkutano wenye mita za mraba 195.pia kulikuwa na ukumbi wa pili mdogo wa mikutano kwa ajili ya wageni maalum Upande wa kaskazini mashariki ya ukumbi huu kuna mabafu ya kuogea eneo hili lina ukubwa wa mita 13 lenye pembe sita kona zake za pembe tatu zina viti maalum vya kukalia muogaji na ngazi za kushukia !
kweli uongozi wa kiadilifu uliweza kuibadilisha africa na ikawa nchi tajiri duniani na kutajika' kote ulimwenguni)
........Inshaallah Tutaendelea.
 
Morogoro
Tunapozungumzia Ujenzi wa Miji na harakati za Waislamu chani ya Dola ya Zanzibar nguvu Kutoka Zanzibar kwenda Pwani ya Tanganzika ndizo zilizokuwa zinasukuma harakati hizo katika Miji ya Bara kwa kupitia Machifu wao wakishirikiana na Maliwali
hapa tena inatubidi turudi bagamoyo na Kilosa Ambayo ndio Mji wa mwanzo kuongoza harakati hizo kwa kupitia hawa Wabarawa yaani Wamashomvi na wapazi wakishirikiana na Wazigua kwa kipindi hicho wakiiwakilisha Dola ya Zanzibar waliutleta Ustarabu Morogoro
Chimbuko la harakati za Mwanzo katika Mji wa Morogoro ni katika kijiji cha Kinoole hapo ndipo Wabarawa wa mwanzo wa Twariqa Qadiriya chini ya Uwesu ilipokwenda kufanya kituo cha kufundisha maarifa ya Ustarabu.'
Utakuta mbaka leo watu wa kinole morogoro kisomo Qiraa' chao cha Qur-an ni cha kisomali kibarawa lakini pia dola ya Zanzibar ilimpeleka Liwali wa Zanzibar katika kinole hiyo hiyo Thne Bin Mohammed ambaye ni matunda ya madrasat bakathir ya Ukutani Zanzibar, mwanaye aitwaye muhammed Thnei aliushika Ukadhi baada yake,'
kingo Luwira kabla ya kujengwa kwa Mji huu wa Morogoro ya sasa Waluguru wenyewe waliishi juu ya milima yaani Uluguruni Mpaka kipindi cha Utawala wa Sayyid barghashi ndio Mji huu wa morogoro ulipojengwa na kuimarishwa, kisabengo bin Aus Mziguwa kutoka bagamoyo ndio aliwakilisha Bendera ya Zanzibar hapo morogoro
Kutokana na masimulizi ya Stanley kisabengo alikuwa ni Mziguwa wa kizazi cha wawindaji ambaye aliishi pwani ya karibu ya Bagamoyo'
mwanzoni alikwenda kuishi eneo la Simba weni sasa kingoluwira lakini baadaye mfalme wa Zanzibar alifunguwa mahusiano mazuri na Viongozi wakuu wa Uluguru hivyo Chifu kingo alitumia vizuri hapo morogoro chini ya mahusiano hayo
Katika kipindi cha Sayyid baraghashi mfalme wa Zanzibar Mwaka 1870-1888 alianzisha mahusiano ya kisiasa na Viongozi wa kiluguru''
wakati huo Chifu Mwande aliishi juu kabisa ya Mlima Chifu Mdeng'o aliishi katikati ya Mlima na Bwakila wao walikuwa upande wa chini ya Mlima
lakini kwa upande wa kusini yaani Mkuyuni alikuwa Chifu kingalu ambaye yeye aliupokea ujumbe kutoka Zanzibar Mwanzoni kabisa na Chifu Hega pia alikuwa maeneo hayo hayo ya Upande wa kusini''
wakati upande wa Magharibi yaani Mgeta alikuwa Chifu Mbago bin Ngwasa na huko matombo alikuwa bambalawe machifu hao wakaupokea ujumbe kutoka Zanzibar
wakakubaliana kuwa mfalme wa Zanzibar atashirikiana nao katika Ujenzi wa Mji wao pamoja na ulinzi ambapo ndani ya mji huo kutakuwa na kambi za jeshi la usalama na Ngome kubwa yaani uzio wa kuilinda milima ya Uluguru
kambi ya jeshi la usalama ilijengwa katika eneo la simba weni waliletwa Askari wa kibaluchi kutoka Zanzibar Chini ya kisabengo bin Aus.
Ulijengwa mnara wa jiwe vizuri unaozua kila pemmbe ya kuingilia Uluguruni ikiwekwa Milango kikuu minne kila mmoja unaukabili upande na iliwekwe njia ndogo ndogo katika minara mingi.....'
Stanley anasema aliikagua milango hiyo na kuona kuwa ilitengenezwa Zanzibar jinsi ilivyo sanifiwa
baada ya kujengwa uzio huo waluguru wakamuita kisabengo kuwa ni Kingo''yaani Uzio kwa kuwa yeye ndio aliyeuwekaa uzio huo,lakini kwa kuwa alikuwa mgeni muhamiaji wakamuita Luwira maana yake muhamiaji Mlowezi hivyo basi kisabego bin Aus''alijulikana kuwa ni kingo Luwira hata hilo eneo la simbaweni limekuwa Kingo Luwira Mpaka hivi sasa,ingawa wengi hupaita mahala hapo''Kinguluwira''
kutoka Simba weni Kingo luwira ya sasa ndipo kisabengo alipoanza kuujenga zaidi Mji huo wa morogoro alianza kuchimba mabwawa katika eneo la Ngarengere na kuutanua mji mpaka Mlali'.
hapo ndipo walipoletwa Wabaluchi na Wahindi wengine waliokuwa wanalima miwa na kuzalisha Sukari kisaki-kilosa Wabaluchi wa kiwa pamoja na wahindi(waislamu wa ismailiya)wakaanza kuingia katika Mji Mpya Uliojengwa na kisabengo wahindi waliifananisha hali ya Morogoro na kashmir yaani, milima.mabonde Mito na Ardhi yenye Rutuba.
kuna jammii nyingi ndogo ndogo ndani ya morogoro ..kuna jamii zenye nguvu za Waislamu wa Agakhan wa Dhehebu la ismaailia ambao wanatoa mafunzo yao kwa jamii yao wenyewe
mashek wa kihindu kiarabu na wakiswahili iliwezekana kuishi morogoro kwa njia ya mashirikiano ya Urafiki na amani na upendo kama Nymbani kwao''
wahindi na wabaluchi hawa walikuwa na uhodari wa kuzalisha sukari Nyeusi walioiita sukari Guru,Kibaluchi Guru (Nyeusi) na Kihindi-Golo au Goro (Nyeusi) walipokuja huku waliwaita wenyeji wao hivyo hivyo Goro au Guru yaani weusi wahindi hawa waliwaita wenyeji waislamu weusi wakawaona Moor'(matamshi moro) yaani waislamu
hilo moor''ni neno lililotolewa kutoka lugha ya kireno mara wareno walipokuja Africa ya Mashariki waliwaita Waislamu hivyo walivyokuwa wakiwaita Moor''yaani waislamu wa pwani ya Africa mashariki kama walivyonukuliwa na Freeman Grenvile
These Moors have some commerce with the island Commoro'''
yaani hawa moro(waislamu walikuwa wakifanya biashara na watu wa kisiwa cha Comoro
Hivyo Moor''(matamshi Moro) Waislamu na hiyo Goro au Guru (weusi) ikafanya neno Moroggoro'' ni Nchi ya waislamu Weusi''
ingawa kuna baadhi ya vyonzo vingine vya kihistoria vinassema kwamba morogoro limetoholewa kutokana na wenyeji wa mji huo yaani waluguru na pia kutoka katika Mlima maarufu wa Uluguru ikaitwa Morogoro''
ila inasemekana hii ni kuficha ukweli tu
Chifu kisabengo bin Aus Kino ala kulli hali, Mji huu umeanzishwa na huyo Kisabenngo bin Aus ambaye alifahamika kwa jina la Chifu Kingo au Sultan Kingo pale alipohamia yeye mwenyewe kattika huo Mtaa unaoitwa Mtaa wa sultan
na akajenga nyumba zake tatu pamoja na Msikiti kwa kushirikiana na Waumini wengine ambao ndio Chimbuko la ilmu katika morogoro kuanzia Ghorofa la Mshendwa moja kwa moja kuungana na Msikiti wa Kingo'' Morogoro
 
slave mentality at its best,yaani badala ya kujivunia uafrika wako au utu wako au utanganyika wako unajivunia uislamu?kweli hawa slave masters wetu wametuachia maradhi mabaya sana kwa kuendelea kutawala akili zetu......
 
Kusema kweli huwa napata tabu sana kuhusu ufahamu wa kila mmoja kuhusu dini.

Nikiwa na maanisha kuwa DINI ni moja ya nyenzo ya kuendesha akili za watu..

Embu tujiulize mambo ya fuatayo

1: kama Yesu hakusema kuwa yeye ni Mkristo je huu ukristo ulitoka wapi?

2: Wakati bikira Maria anapashwa habari na Malaika kuwa atapata mtoto mwanaume atamwita Yesu hili jina la mwisho la kristo likitoka wapi au alikuja kupewa na nani na kwenye andiko lipi?

3: Naamini kabisa nyakati Yesu alikuja karne ya 4 naamini kabisa kulikuwa hakuna Alphabetic order yani [A, b, c, ...Z] sasa J yani Jesus alilipataje hili jina lenye herufi zilizopo kwenye Alphabetic order ambazo hazikuwa zina exist?

3: kama kweli serikali ya utawala wa kipindi hicho vha Yesu kuja walimuua Yesu inakuwaje leo hii wazungu wanampenda sana mtu huyu?

4: Je unafikiri
waliomuua Yesu waliacha historia yake vilevile bila kuibadilisha? Nikiwa na maana kama walimuua haita wezekana waziache story zake vilevile pasina kuibadilisha na wakati alikuwa chukizo kwao..

4: Kwa nini tunamachapisho ya bibilia tofauti tofauti?
 

Attachments

  • 1433924143391.jpg
    1433924143391.jpg
    31.9 KB · Views: 145
Papyrus of kemet..[ Egypt book of dead]

Inasemekana kuwa story ya yesu zineibwa kwenye kitabu kifaamikacho kama Egypt book of dead ambacho ni cha kale zaidi yani kabla ya kuja Yesu.. Kwa unayetaka kujifunza fuatilia ujajua kuna giza kubwa sana ambalo leo hii linatifanya tusijitambue tuko wakati gani..

Tafadhali msiache mambo haya hivi hivi do your own research and come into your own conclusion..
 

Attachments

  • 1433924723623.jpg
    1433924723623.jpg
    24.1 KB · Views: 114
Huyu father Christ Mass ameelezewa katika bibilia sehemu gani? Mstari wa ngapi? Bibilia ipi?.. Utaona kabisa jinsi wazungu wanavyofanya kazi kubwa yakuingiza Dunia hii kwenye kiza.
Televison[ Tell lie vision]
Radi
Magazeti
Clubs
Michezo ya aina yote[soka, n.k] ni vyomba mahususi vya kuuwa uwezo ya kila mmoja wetu asione mambo jinsi ya livyo.. Wakuuwa kabisa uwezo wako wakuconnect with your inner self . Angalia oparation za Vyombo vya habari, taarifa tunazozisoma kwenye magazeti ila sio magazeti yote ila mengi ni yanafanya kazi ile ile yakukusahaulisha..
 

Attachments

  • 1433924788094.jpg
    1433924788094.jpg
    26.4 KB · Views: 132
Kusema kweli huwa napata tabu sana kuhusu ufahamu wa kila mmoja kuhusu dini.

Nikiwa na maanisha kuwa DINI ni moja ya nyenzo ya kuendesha akili za watu..

Embu tujiulize mambo ya fuatayo

1: kama Yesu hakusema kuwa yeye ni Mkristo je huu ukristo ulitoka wapi?

2: Wakati bikira Maria anapashwa habari na Malaika kuwa atapata mtoto mwanaume atamwita Yesu hili jina la mwisho la kristo likitoka wapi au alikuja kupewa na nani na kwenye andiko lipi?

3: Naamini kabisa nyakati Yesu alikuja karne ya 4 naamini kabisa kulikuwa hakuna Alphabetic order yani [A, b, c, ...Z] sasa J yani Jesus alilipataje hili jina lenye herufi zilizopo kwenye Alphabetic order ambazo hazikuwa zina exist?

3: kama kweli serikali ya utawala wa kipindi hicho vha Yesu kuja walimuua Yesu inakuwaje leo hii wazungu wanampenda sana mtu huyu?

4: Je unafikiri
waliomuua Yesu waliacha historia yake vilevile bila kuibadilisha? Nikiwa na maana kama walimuua haita wezekana waziache story zake vilevile pasina kuibadilisha na wakati alikuwa chukizo kwao..

4: Kwa nini tunamachapisho ya bibilia tofauti tofauti?

Sijasoma mjadala tangu mwanzo lakini kwa ulichoandika hapa, licha ya kujiita "... Smart mind", ninamashaka na mind yako!! Unauliza maswali ambayo ni obvious and trivial!!! Eti habari za alphabet!!! Ulishawahi kujiuliza maswali kama hayo kwa manabii na watangulizi wengine kabla yake kama akina Moses, Ibrahim na wengine?!

Yesu sio Mkristo ila ni Kristo ( he is not a Christian but he's a Christ)

Machapisho yanaendana na lugha na mahala inapotumika!! Kama umesoma lugha utakumbuka moja ya tabia ya lugha ni " kuzaliwa, kujua na kufa" sasa ulitaka lugha iliyotumika mwaka 1000 itumike mwaka 2010?!
 
Fikiria kama Alphabetic order zilikuwa zinaexist kipindi alichokuja Yesu... Think about it
 

Attachments

  • 1433925241185.jpg
    1433925241185.jpg
    14.7 KB · Views: 186
Jambo la mwisho la msingi sana

Ukiangalia kwa vizuri kabisa ramani ya Africa unaiona Suez Canal..

Hii Suez Canal haikuwepo kipindi cha karne za Musa or Moses kuja.. Hata Abraham baba wa Imani alipewa arthi na Mungu haikujulikana ilikuwa ni sehemu gani ila kwa ufahamu wetu sisi tunajua Abraham alipewa ardhi yani kama uwanja wa mpira ndo dunia ilikuwa hivyo nikimaanisha Dunia ilikuwa kama uwanja.

Tunaporudi katika historia ya darasani tunaeleza kuwa Suez Canal iliyokea baada ya tetemeko kubwa ambalo iliachanisha barara ndo mana leo hii kuna Mabara 7 [Africa, America, n.k]

Sasa kama Suez Canal ilitokea baada ya mabadiliko ya kidunia hawa watu waliovushwa na Musa alivuka maji ya mto au bahari gani na wakati kwa kipindi alichokuja Musa Dunia ilikuwa kama uwanja wa mpira?..

Mzungu anakazi kubwa yakutueleza hili
 

Attachments

  • 1433926488575.jpg
    1433926488575.jpg
    45 KB · Views: 196
Hili ni swaki makini sababu kama ni Kweli waarabu walitengeneza uswahiba na waafrika kiasi hicho ni dhahiri kwamba maelfu kwa maelfu ya waafrika waliochukuliwa kama maswahiba a.k.a watumwa wangekuwa wengi sana huko uarabuni.

Wazungu ni makatili lakini waafrika wapo wengi mpaka wana mataifa yao huko latin America yenye dola kamili ya watu weusi Caribbean islands mataifa kama Haiti Trinidad and Tobago Jamaica etc.
Huo ndio ushahidi tosha wa kuonyesha,walionunuwa watu weusi ni wazungu.Arabuni ilikuwa ni jangwa,watumwa wachukuliwe kule wakafanye kazi gani.
Wazungu walichukuwa watumwa kwa ajili ya Mashamba yao,kabla ya kuanza kutumika machine.
Nchi za arabuni watu weusi walikuwapo,kabla hata utumwa kuwepo,na asili ya muarabu sio mtu mweupe,ni kutokana na waarabu kuona na wahindi,wabulushi,wairani,wazungu,ndio waakanza kubadilika rangi,kwa mchanganyiko wa makabila.
 
umefanya vizuri kutuletea hii historia lakin hauko fair ingebidi utuletee na jinsi waarabu walivyoanza kuingia kwetu na kuteka maeneo ya kilwa nk. kumbuka waarabu, wajerumani nk wote ni wavamizi. mm nawakubali wajerumani kwa sababu walikuwa wachapakaz na wametuachia reli, bandari nk. ila sioni tunachoweza kujivunia toka kwa waarabu zaidi ya utamaduni wao na utumwa. samahan kama nimekukwaza
Waarabu ndio wametuachia utajiri mkubwa,watalii wengi wanakuja,kwa kulipa kwa pesa za kigeni,kuangalia magofu ya kale na historia,mbali mbali,
1.Bagamoyo
2.Kilwa
3.Pangani
4.Tongoni
5.Zanzibar nk
Sehemu zote hizo zinaingiza pesa za kigeni kwa kuja watalii.
 
Swali chokonozi....

Kwa nini hakuna "Black Arabs"
Waarabu ni weusi,mtu mweupe kwa kuishi kwenye jangwa na joto kali ni ngumu kwa maisha kale,sasa hivi ndio kuna A/C,Magari,majumba yenye A/C.1434003458386.jpgbibi wa kiarabu amempakata mjukuu,aliyepatikana katika kizazi cha makabila ya watu weupe.1434003659385.jpg1434003659385.jpg1434003659385.jpg
 

Attachments

  • 1434003416738.jpg
    1434003416738.jpg
    2.3 KB · Views: 875
  • 1434003430790.jpg
    1434003430790.jpg
    66.7 KB · Views: 170
  • 1434003565567.jpg
    1434003565567.jpg
    3.5 KB · Views: 683
  • 1434003581366.jpg
    1434003581366.jpg
    107.2 KB · Views: 203
Mbona black arabs wapo mkuu, kama una azam tv anagalia wanasah tv utawaona
Mwarabu mweusi anathaminika katika nchi yake aliyozaliwa,kuliko hata mweupe aliyezaliwa nje ya nchi ya kiarabu husika.
 

Attachments

  • 1434004168188.jpg
    1434004168188.jpg
    63.2 KB · Views: 140
Original Arab.. Wapenzi wadau kuna kazi naiandaa endeleeni kupost nipate mda vizuri ya kuiandaa mana naona watu hawajui au maeiisahau historia ya kweli. Hii picha ya jamaa huyu hapo chini ni Original Arab acha nimalizie kuiandaa halafu wadau tufaelekezana hatua moja Kwa nyingine
 

Attachments

  • 1434004864847.jpg
    1434004864847.jpg
    25.2 KB · Views: 167
udinii huu ulio dhahiri, na chuki hizi za wazi zinazopandikizwa hazitatuacha kamwee...mtoa maada lengo lako ni lipi hasa???
 
Mkuu unazidiwa na propaganda za udini kiasi cha kupofua ufahamu wako kabisa. Ungeongea historia ya Kilwa kisiwani sawa lakini makabila uliyoyataja kusini hayakuwa na machifu wa kiislamu kiasi hicho unataka kutuaminisha.

Nakupa taarifa kidogo tu....

Wakoloni mbona walipovamia dola za Mwanamutapa (Zimbabwe) pia walipigana vita?? Nazo zilikuwa Kiislamu?

Unachopotosha ni kuwa wakoloni walikuja kupambana na Uislamu, si kweli walikuja kutunyonya waafrika na kutukandamiza regardless dini au kabila letu, hivyo waafrika kwa kuamua kulinda heshima yao (kumbuka baadhi ya dola zilikuwa za kiislamu, baadhi za kipagani) wote walipambana, tena kwa asilimia kubwa maybe 90% ya chiefdoms zilikuwa za dini za asili (tunaita pagan)
hizo stori za kuokoteza kwenye kahawa humu JF utaishia kuumbuka tu mkuu, waachie wale ndio level zao.
Waarabu wametenda madhila makubwa mno kwa karne nyingi kwa waafrika kuliko hao wakoloni kama hujui.

Hitimisho... Vita zote za kupambana na ukoloni zilikuwa katika mrengo wa Pan African Movement sio Jihadi mkuu.
 
Fikiria kama Alphabetic order zilikuwa zinaexist kipindi alichokuja Yesu... Think about it

What about Joshua? John?, James.....

Kwa taarifa yao Kiyahudi huwa na Y instead of J so Jesus si kiyahudi bali ni Kiingereza (this is very basic info)
According to bible Jesus anaitwa Emmanuel
 
Jambo la mwisho la msingi sana

Ukiangalia kwa vizuri kabisa ramani ya Africa unaiona Suez Canal..

Hii Suez Canal haikuwepo kipindi cha karne za Musa or Moses kuja.. Hata Abraham baba wa Imani alipewa arthi na Mungu haikujulikana ilikuwa ni sehemu gani ila kwa ufahamu wetu sisi tunajua Abraham alipewa ardhi yani kama uwanja wa mpira ndo dunia ilikuwa hivyo nikimaanisha Dunia ilikuwa kama uwanja.

Tunaporudi katika historia ya darasani tunaeleza kuwa Suez Canal iliyokea baada ya tetemeko kubwa ambalo iliachanisha barara ndo mana leo hii kuna Mabara 7 [Africa, America, n.k]

Sasa kama Suez Canal ilitokea baada ya mabadiliko ya kidunia hawa watu waliovushwa na Musa alivuka maji ya mto au bahari gani na wakati kwa kipindi alichokuja Musa Dunia ilikuwa kama uwanja wa mpira?..

Mzungu anakazi kubwa yakutueleza hili

mkuu
Suez canal haikutokana na tetemeko la ardhi Bali ulichimbwa na watu
rejea historia vizuri
 
Back
Top Bottom